tensor analysis
Member
- Dec 16, 2016
- 18
- 48
[HASHTAG]#Andiko[/HASHTAG]
'Basi vikashushwa vichwa vya Treni toka mbinguni kupitia baharini, mfalme akataajabu kwa baraka za mungu' Watanzania 6:18 = Bafaraj
nao makada na wapambe wakararua mavazi yao kwa Shangwe wakisema "utukufu huu uwe wa milele" Kupagawa 2 23-26!
"Watu wakasujudu na wakasema Mfalme umenena.Neno lako ndio letu, matakwa yako ndio yetu...tupeleke tunatii..bila ya pingamizi"...Wapofu 23:3
Nao mafarisayo walipoishaisikia amri Kuu ya kusulubu, wakajawa kiburi wakipiga na kukamata wenye akili timamu wasiosujudu Hatamu 4:26
"Nami nikaiangalia Kolomije, palipo njia Kuu kwenda Chato nikamuona yule aliye mwana wa mfalme akiamrisha kusulubu Wahangaika" Kilio 1:1
"Tukaitizama nchi kwa juu, busara ikasema tuingie ndani na kuona mchwa wamekula kila kitu...Kolomije ituokoe sote. Tuombe" ...Ufunuzi 43:5
"Mimi na Utawala wangu tutawanyoosha mnyooke" asema Bwana. Nalo neno hili likawaogopesha sana wadanganyika unyonge ukawajaa. Utumwa 15:20
Mfalme akatamalaki woga ukawajaa watawaliwa siku zile. Nao walionywa ole wake athubutuye kufumbua makanwa yake lisije mkuta jambo. Utumwa 16