Wana JF
Kwenye Bunge la Mwaka jana Mh. Anna Kilango Malecela alilalamika sana kuhusu miradi ya umeme vijijini (REA) kupelekwa Sengerema wakati kuna baadhi ya wilaya hazina umeme! Kinachoendelea hivi sasa kuna mradi wa MCC umeanzia tena Sengerema na baadae ndio makandarasi hao ndio wahamie Mwanza, ambapo dhana inayonekana kwa watu wasio wa Sengerema kuwa ni upendeleo au kampeni za chinichini. Hoja yangu ni kwa nini huu mradi wa MCC usianzie Mwanza kwenye sehemu ambazo zimejengwa muda mrefu na zimesubiri umeme huu kwa zaidi ya miaka mitatu sasa!!! Sikatai wananchi wa Sengerema kupata umeme kwani ni haki yao ya msingi kuwa na umeme, lakini kwa hili wizara na Tanesco walitakiwa kufanya checks and balance na kuangalia ni sehemu gani ina tija hasa kwa Tanesco ambayo inahitaji fedha zaidi kujiendesha kibiashara. Na hili la kuhamisha miradi ya umeme kwenda sehemu nyingine kiupendeleo hapa Mwanza sio geni kwani mradi wa umeme wa Nyamuhongolo umefanikishwa na kigogo mmoja wa Tanesco mkoani Mwanza anayeishi huko, mradi huo ulikuwa uende Buswelu. Wizara/Tanesco jaribuni kuangalia sehemu kama Buswelu, Nyegezi, Bugarika, Luchelele etc wananchi wanaoishi huko wana shida sana ya umeme!
Kwenye Bunge la Mwaka jana Mh. Anna Kilango Malecela alilalamika sana kuhusu miradi ya umeme vijijini (REA) kupelekwa Sengerema wakati kuna baadhi ya wilaya hazina umeme! Kinachoendelea hivi sasa kuna mradi wa MCC umeanzia tena Sengerema na baadae ndio makandarasi hao ndio wahamie Mwanza, ambapo dhana inayonekana kwa watu wasio wa Sengerema kuwa ni upendeleo au kampeni za chinichini. Hoja yangu ni kwa nini huu mradi wa MCC usianzie Mwanza kwenye sehemu ambazo zimejengwa muda mrefu na zimesubiri umeme huu kwa zaidi ya miaka mitatu sasa!!! Sikatai wananchi wa Sengerema kupata umeme kwani ni haki yao ya msingi kuwa na umeme, lakini kwa hili wizara na Tanesco walitakiwa kufanya checks and balance na kuangalia ni sehemu gani ina tija hasa kwa Tanesco ambayo inahitaji fedha zaidi kujiendesha kibiashara. Na hili la kuhamisha miradi ya umeme kwenda sehemu nyingine kiupendeleo hapa Mwanza sio geni kwani mradi wa umeme wa Nyamuhongolo umefanikishwa na kigogo mmoja wa Tanesco mkoani Mwanza anayeishi huko, mradi huo ulikuwa uende Buswelu. Wizara/Tanesco jaribuni kuangalia sehemu kama Buswelu, Nyegezi, Bugarika, Luchelele etc wananchi wanaoishi huko wana shida sana ya umeme!