Mimi ni member mkongwe humu. Ninaishi Sweden na nina passport kwa sasa.
Nilikutana na kijana Mtanzania aliyekuwa na viza ya uanafunzi 2007 kumbe alikuwa muathirika. Nilimkaribisha nyumbani kwa chakula bila kufahamu lengo lake.
Kawakuwa nilikuwa mpweke sana alijenga mazoea ya kuja kwangu hasa weekends.
Alionyesha dalili zote za mapenzi, nilimuambia tukapime kwanza. Siku moja alijiforce kwangu na ukawa mwanzo wa mapenzi bila kupima.
Yule kijana alirudi Tanzania, niliendelea na maisha. Nilimsahau kabisa. Mwaka 2017 nilipata kazi wizara ya afya Sweden, occupation health walinipa form ya kujaza. Nilikwenda kwa daktari na kumwambia sitajali kama atatick box zote. Aliniuliza una uhakika unataka kupima HIV? Nikasema ndiyo.
Alinipa karatasi niende nayo lab. Baada ya wiki moja nilipigiwa simu nirudie vipimo. Sikuwa na wasiwasi. Baada ya wiki nilirudi kwa daktari. Aliniambia Protein una HIV. Nilidhami anaongelea mtu mwingine.
Alianza kunieleza kuwa matibabu sikuhizi yameboreshwa sana. Nenda kwenye kitengo.
Nimefika kwenye kitengo walikuwa wanafunga kwa chakula cha mchana. Ilibidi niende nyumbani. Nilisali sana kuomba huruma ya Mungu.
Saa nane nilirudi kwenye kitengo. Walichukua vipimo upya. Majibu kutoka HIV+. Nilipewa nurse alinipa counselling kuanzia saa tisa mchana mpaka 11:00 wakati wanafunga ofisi. Safari yangu kama muathirika ilianzia hapo.
Nyumbani kwetu hawafahamu zaidi ya kaka yangu ambae aliumia sana. Alisema tulikupeleka Ulaya upate maisha bora leo hii unapata HIV Ulaya?
Haya ndiyo maisha yangu mapya kama muathirika.
Baada ya maambukizi nilikaa miaka 10 bila kujijua. Nilikuja kumjua aliyeniambukiza baada ya kupata list ya wa Tanzania aliowaambukiza. Kuna uwezekano niliwaambukiza watu wawili au watatu kwani nilikuwa single nikijaribu bahati ya relationship.
Nilikutana na kijana Mtanzania aliyekuwa na viza ya uanafunzi 2007 kumbe alikuwa muathirika. Nilimkaribisha nyumbani kwa chakula bila kufahamu lengo lake.
Kawakuwa nilikuwa mpweke sana alijenga mazoea ya kuja kwangu hasa weekends.
Alionyesha dalili zote za mapenzi, nilimuambia tukapime kwanza. Siku moja alijiforce kwangu na ukawa mwanzo wa mapenzi bila kupima.
Yule kijana alirudi Tanzania, niliendelea na maisha. Nilimsahau kabisa. Mwaka 2017 nilipata kazi wizara ya afya Sweden, occupation health walinipa form ya kujaza. Nilikwenda kwa daktari na kumwambia sitajali kama atatick box zote. Aliniuliza una uhakika unataka kupima HIV? Nikasema ndiyo.
Alinipa karatasi niende nayo lab. Baada ya wiki moja nilipigiwa simu nirudie vipimo. Sikuwa na wasiwasi. Baada ya wiki nilirudi kwa daktari. Aliniambia Protein una HIV. Nilidhami anaongelea mtu mwingine.
Alianza kunieleza kuwa matibabu sikuhizi yameboreshwa sana. Nenda kwenye kitengo.
Nimefika kwenye kitengo walikuwa wanafunga kwa chakula cha mchana. Ilibidi niende nyumbani. Nilisali sana kuomba huruma ya Mungu.
Saa nane nilirudi kwenye kitengo. Walichukua vipimo upya. Majibu kutoka HIV+. Nilipewa nurse alinipa counselling kuanzia saa tisa mchana mpaka 11:00 wakati wanafunga ofisi. Safari yangu kama muathirika ilianzia hapo.
Nyumbani kwetu hawafahamu zaidi ya kaka yangu ambae aliumia sana. Alisema tulikupeleka Ulaya upate maisha bora leo hii unapata HIV Ulaya?
Haya ndiyo maisha yangu mapya kama muathirika.
Baada ya maambukizi nilikaa miaka 10 bila kujijua. Nilikuja kumjua aliyeniambukiza baada ya kupata list ya wa Tanzania aliowaambukiza. Kuna uwezekano niliwaambukiza watu wawili au watatu kwani nilikuwa single nikijaribu bahati ya relationship.
