Gota8s
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 203
- 189
Habari zenu wana jamvi. heshima kwenu wote
Kuna suala hili huwa linanifanya nijione mimi ni wa tofauti sana. yani huwa sijawahi kukutana na aina hata moja ya watu ambao nimeendana nao. jambo moja la msingi ni kwamba siwezi ku-fit in kwenye demo'
hebu ngoja nieleze zaidi. kwanza mimi huwa sina Hobby. kila jambo ambalo yeyote huwa analifanya kama hobby mimi kwangu ninapolifanya huwa ni kama activity tu. yaani sina kitu hata kimoja ambacho naweza kusema nisipokifanya sijiskii amani, au sijiskii furaha.
Mimi ni mtoto wa kiume, kijana kabisa wa early 20s, sasa mimi sio shabiki wa mpira, sio mlevi wa pombe, sio mtu wa viwanja, sio mtu wa starehe hata kidogo, sipendelei sana wanawake (najua naeleweka hapa), mziki, movies vyote huwa navifuatilia pale napoamua tu, ila hata ninapoacha kufuatilia, sipati ile 'alosto' kama namna ninavyoona wenzangu wanakuwa.
sasa tukienda kwenye masuala ya kielimu, sijawahi kuelewa kabisa mimi napenda nini na kipi sipendi. kwanza mimi sio 'jiniaz' no, ila namudu chochote nikiamua kukifanya. kwa nfano, nilipokuwa nasoma O-level nilikuwa namudu masomo yote. biashara, sanaa na sayansi kwa kiwango sawasawa. yaani ukiona nimefail somo fulani ilikuwa kwa sababu sijaamua kujisomea tu. ilikuwa inafika wakati nazigawa Terms, nasema labda Muhula wa kwanza nitakaza kwenye sanaa, na wa pili ntakaza sayansi. hata matokeo ya mwisho CSS yalipotoka ilikuwa inconclusive. yale niliyonuia kufanya vizuri nilifanya hivyohivyo nilivyotaka.
A level nilisoma combination nisiyoitaka (kuna situation zilipelekea) nikasusia kuisoma mpaka mwezi October tangu June. Muda wote tangu naripoti nilisusia kusoma sanaa, nikawa niko PCM, mwalimu wa darasa akanitimua kuwa hanitambui, nikahamia PCB nikakaa wiki mbili ikaja ile mid-term ya September, nikapata Div II. ikaja mikanganyiko, nikaondolewa PCB nikaambiwa niende HKL ambayo ndio niliyokuwa Allocated. mpaka November 17 ndo nikaenda HKL kuanza kujiandaa na mtihani wa November. Guys, nilikaa kidogo matokeo ya mtihani yalipotoka nikaongoza Combination zote za Arts ujue kila mtu alikuwa ananiona wa ajabu ila mm nikawa naona kawaida tu. nilikuwa sio mtu wa msuli hata kidogo ila ndo nilikuwa tu wa aina hiyo.
sasa hilo lisikushangaze, kwenye suala la dini sijawahi kujua nifuate imani gani. mimi najua misingi ya dini zote. ukristo na uislamu. nasoma Qur'an na nasoma Biblia. nimesoma vitabu vingi sana vya imani zote mbili, vya unabii na vya theolojia. linapokuja suala la kusema nichague imani napata wakati mgumu achilia mbali kuchagua dhehebu. yaani mimi najikuta niko tofauti mno mpaka najiskia vibaya.
zamani nilikuwa mcheshi sana na mzungumzaji lakini saivi imenibidi niachane na hiyo attitude. kwa sababu sasa naonekana 'Much know' kwa kila nachokizungumzia. sasa tatizo jingine kubwa ni kuwa naweza ku control attitudes na feelings zozote. mimi naweza kuzimudu hisia na mihemko ya aina zote, iwe hasira, furaha, huzuni yaani hali yoyote. sio kwamba sipati hizo, no. ila naweza kuzi control. kwa mfano nikipata msiba, huwa naumia ndio hata nikimpoteza mtu wa karibu mno basi nahuzunika sana ila akili yangu inaniambia kuwa ninfahamu ninachotakiwa kukiwaza, akili inaniaminisha kuwa hisia hazipiti maarifa na uelewa, basi hapohapo kimoyomoyo najiambia imetokea na yeyote itamkuta, kwa hiyo ni kawaida. ndugu zangu mimi huwa siwezi kabisa kuwa kama wale wenzangu huwa wanagalagala na kupoteza fahamu. ikitokea hivo ujue nafanya huku najielewa, na nafanya kama kuigiza tu. huwa najishtukia.
Nitaendelea baadae kisha mtanipa ushauri nifanyeje
Kuna suala hili huwa linanifanya nijione mimi ni wa tofauti sana. yani huwa sijawahi kukutana na aina hata moja ya watu ambao nimeendana nao. jambo moja la msingi ni kwamba siwezi ku-fit in kwenye demo'
hebu ngoja nieleze zaidi. kwanza mimi huwa sina Hobby. kila jambo ambalo yeyote huwa analifanya kama hobby mimi kwangu ninapolifanya huwa ni kama activity tu. yaani sina kitu hata kimoja ambacho naweza kusema nisipokifanya sijiskii amani, au sijiskii furaha.
Mimi ni mtoto wa kiume, kijana kabisa wa early 20s, sasa mimi sio shabiki wa mpira, sio mlevi wa pombe, sio mtu wa viwanja, sio mtu wa starehe hata kidogo, sipendelei sana wanawake (najua naeleweka hapa), mziki, movies vyote huwa navifuatilia pale napoamua tu, ila hata ninapoacha kufuatilia, sipati ile 'alosto' kama namna ninavyoona wenzangu wanakuwa.
sasa tukienda kwenye masuala ya kielimu, sijawahi kuelewa kabisa mimi napenda nini na kipi sipendi. kwanza mimi sio 'jiniaz' no, ila namudu chochote nikiamua kukifanya. kwa nfano, nilipokuwa nasoma O-level nilikuwa namudu masomo yote. biashara, sanaa na sayansi kwa kiwango sawasawa. yaani ukiona nimefail somo fulani ilikuwa kwa sababu sijaamua kujisomea tu. ilikuwa inafika wakati nazigawa Terms, nasema labda Muhula wa kwanza nitakaza kwenye sanaa, na wa pili ntakaza sayansi. hata matokeo ya mwisho CSS yalipotoka ilikuwa inconclusive. yale niliyonuia kufanya vizuri nilifanya hivyohivyo nilivyotaka.
A level nilisoma combination nisiyoitaka (kuna situation zilipelekea) nikasusia kuisoma mpaka mwezi October tangu June. Muda wote tangu naripoti nilisusia kusoma sanaa, nikawa niko PCM, mwalimu wa darasa akanitimua kuwa hanitambui, nikahamia PCB nikakaa wiki mbili ikaja ile mid-term ya September, nikapata Div II. ikaja mikanganyiko, nikaondolewa PCB nikaambiwa niende HKL ambayo ndio niliyokuwa Allocated. mpaka November 17 ndo nikaenda HKL kuanza kujiandaa na mtihani wa November. Guys, nilikaa kidogo matokeo ya mtihani yalipotoka nikaongoza Combination zote za Arts ujue kila mtu alikuwa ananiona wa ajabu ila mm nikawa naona kawaida tu. nilikuwa sio mtu wa msuli hata kidogo ila ndo nilikuwa tu wa aina hiyo.
sasa hilo lisikushangaze, kwenye suala la dini sijawahi kujua nifuate imani gani. mimi najua misingi ya dini zote. ukristo na uislamu. nasoma Qur'an na nasoma Biblia. nimesoma vitabu vingi sana vya imani zote mbili, vya unabii na vya theolojia. linapokuja suala la kusema nichague imani napata wakati mgumu achilia mbali kuchagua dhehebu. yaani mimi najikuta niko tofauti mno mpaka najiskia vibaya.
zamani nilikuwa mcheshi sana na mzungumzaji lakini saivi imenibidi niachane na hiyo attitude. kwa sababu sasa naonekana 'Much know' kwa kila nachokizungumzia. sasa tatizo jingine kubwa ni kuwa naweza ku control attitudes na feelings zozote. mimi naweza kuzimudu hisia na mihemko ya aina zote, iwe hasira, furaha, huzuni yaani hali yoyote. sio kwamba sipati hizo, no. ila naweza kuzi control. kwa mfano nikipata msiba, huwa naumia ndio hata nikimpoteza mtu wa karibu mno basi nahuzunika sana ila akili yangu inaniambia kuwa ninfahamu ninachotakiwa kukiwaza, akili inaniaminisha kuwa hisia hazipiti maarifa na uelewa, basi hapohapo kimoyomoyo najiambia imetokea na yeyote itamkuta, kwa hiyo ni kawaida. ndugu zangu mimi huwa siwezi kabisa kuwa kama wale wenzangu huwa wanagalagala na kupoteza fahamu. ikitokea hivo ujue nafanya huku najielewa, na nafanya kama kuigiza tu. huwa najishtukia.
Nitaendelea baadae kisha mtanipa ushauri nifanyeje