Kayenga jr
JF-Expert Member
- Feb 16, 2016
- 443
- 348
- Thread starter
- #21
Asante sana kwa ushauri tatizo ni hizo gharama nachosubiria kwa sasa ni kufanya hicho kipimo cha HSG tena ili kuona je huo mrija bado umeziba? Na kitu ambacho sikielewi mwanamke mirija ikiziba mzunguko wake (kwa maana ya period) anapata kama kawaida?Tatizo lako limeshagundulika huna haja ya kuhangaika. Mini Mke Wangu anatatizo kama la Mke wako mrija mmoja umeziba. Alikuwa na tatizo la kuugua kwa masaa yasiyopungua kumi mfululizo anapokuwa mwezini Ila tatizo la maumivu liliisha baada ya kufanyiwa operation ya kuzibua mirija kwa kukata na kuunga tena Ingawa operation hiyo haikufanikiwa. Nyama kubwa ilitolewa wakati wa operation ndio iliyokuwa ikimuumiza. Suala la kushika mimba mwanamke akiwa na mrija mmoja inawezekana Ila ni mtihani sana. Suluhisho la tatizo lako ni kufanya invetro fertilization hii ni kutunga mimba nje na kupandikiza ndani ya mfuko wa uzazi. Mimi Nimepata mtoto baada ya miaka kumi na tano ya ndoa kwa njia nilivyokuambia. Njia hii ni Gharama na Mimi nilifanyia nje ya nchi. Ila kwa uwezo wa Mungu Mke Wangu Alipata ujauzito kwa njia ya kawaida na kupata mtoto baada ya miaka 18 ya ndoa. Kwahiyo usihangaike hiyo ndio hali halisi ni mtihani unaohitaji subira ya Mungu kama huna uwezo wa kufanya IVF kama nilivyofanya Mimi. Ila siku hizi unaweza jaribu hata hapo Kenya kwa Gharama nafuu kati ya Dola elfu sita hadi nane Ila hii nayo ni kujaribu tu unaweza pata au kukosa Mimi nilijaribu mara tano mfululuzo hadi kuja kufanikiwa. Mungu yupo na anatenda mtegemee Yeye.