NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,288
- 12,789
Ifikie hatua serikali yetu iweke sheria kali dhidi hawa manabii na mamungu makanjanja katika nchi yetu hii.
Kiukweli ulichokifanya milard Ayo siyo haki kabisa kusambaza upuuzi Kama huo aliouzungumza huyo anayejiita mungu Zumaridi.
Kupitia hiyo interview hakika Kuna watanzania wameendelea kumuamini na kanisani kwake jumapili ataongeza waumini wakutosha na pesa za kutosha kwenye kibindo chake.
Nachosikitika zaidi na zaidi waumini au wafuasi wakubwa ni watoto na wanawake, ni mashaka na wasiwasi wangu kuwa yasije yakatokea ya mchungaji Kibwetere aliyechoma kanisa na waumini ndani Kisha alitokomea kusikojulikana mpaka Sasa.
Hiyo ilitokea baada yakuwaambia waumini wake kuwa mwisho wa dunia umefika nakuwasihi waumini wauze mali waje wakeshe kanisani wakisubiri mwisho wa dunia.
Kilichotokea hapo ni historia mpaka Sasa hafahamiki alipo baada yakuwachoma waumini wake.
Sasa Tanzania tunajanga la ongezeko la ushoga, madawa ya kulevya pamoja na vifo vyenye utata nk.
Media zetu kwa Nini hamjikiti huko kwenye matatizo makubwa kuliko kuanza kutusimulia Mambo ya mtu alikwenda mbinguni akakutana na jua!
Mtu anajita mungu si inabidi awe na mbingu yake na inakuaje anatokewa na mungu wakati yeye ni mungu??
Millard ulichotufanyia watanzania hakika umetukosea sana kwa kutuletea stori za huyo mungu Zumaridi wa Mwanza.
Natoa tamko kwa Serikali yetu sikivu iingilie Kati dhidi ya hawa manabii, watakuja kutumbukiza familia zetu katika shimo la hewa.
Kiukweli ulichokifanya milard Ayo siyo haki kabisa kusambaza upuuzi Kama huo aliouzungumza huyo anayejiita mungu Zumaridi.
Kupitia hiyo interview hakika Kuna watanzania wameendelea kumuamini na kanisani kwake jumapili ataongeza waumini wakutosha na pesa za kutosha kwenye kibindo chake.
Nachosikitika zaidi na zaidi waumini au wafuasi wakubwa ni watoto na wanawake, ni mashaka na wasiwasi wangu kuwa yasije yakatokea ya mchungaji Kibwetere aliyechoma kanisa na waumini ndani Kisha alitokomea kusikojulikana mpaka Sasa.
Hiyo ilitokea baada yakuwaambia waumini wake kuwa mwisho wa dunia umefika nakuwasihi waumini wauze mali waje wakeshe kanisani wakisubiri mwisho wa dunia.
Kilichotokea hapo ni historia mpaka Sasa hafahamiki alipo baada yakuwachoma waumini wake.
Sasa Tanzania tunajanga la ongezeko la ushoga, madawa ya kulevya pamoja na vifo vyenye utata nk.
Media zetu kwa Nini hamjikiti huko kwenye matatizo makubwa kuliko kuanza kutusimulia Mambo ya mtu alikwenda mbinguni akakutana na jua!
Mtu anajita mungu si inabidi awe na mbingu yake na inakuaje anatokewa na mungu wakati yeye ni mungu??
Millard ulichotufanyia watanzania hakika umetukosea sana kwa kutuletea stori za huyo mungu Zumaridi wa Mwanza.
Natoa tamko kwa Serikali yetu sikivu iingilie Kati dhidi ya hawa manabii, watakuja kutumbukiza familia zetu katika shimo la hewa.