Mikoa ya kuanzia maisha

Bonge ya Point Mkuu
 
kigoma
 
Popote misha yapo mradi 2 kazi iwe na maslahi mazuri.
 
kukutajia tu mikoa sidhani kama itakussidia ila maisha ni popote ndgu we jipange tu kuyakabiri sehemu yoyote.
 
Mind u guy,maisha popote pale!kuna wa2 wapo interior lkn wanaingiza pesa ndefu kuliko hao w mjini!so income matterz than location!alaf rural areas ndo kuna investments opportunities nyng compared to urban areas!kuna wa2 wapo rukwa na katavi lkn kipato chao ucpime ungetaman uwe wew!
 
kama wewe ni mtu unaetaka maendeleo kwa kujituma, mikoa hii ni wewe kwenda, !. Rukwa, Katavi, Shinyanga na miko mipya iliyoanzishwa.
note, endapo hutoki katika moja ya mikoa hiyo.

Nashukuru kwa ujumbe mzuri kwa msomi huyo, mimi mwenyewe ni mzaliwa wa jiji la Dar, lakini ilifika hatua hapo Dar nilipaona pachungu, na wala sikutegemea maishani mwangu kama siku moja ningekuwa naishi mikoani hasa hapa nilipo mkoa wa Mara, wilwyani Tarime. lakini sasa hakuna wa kunieleza kuhusu kurudi tena bongo, kwani sasa nina uwezo wa kwenda bongo hata kwa ndege. kwa hiyo bwana nami nasisitiza kuwa maisha ni popote pale.
 

Acha ubwege wewe..yaani bado una mawazo mgando kwa elimu yako au ulichakachua aahhhh..jokes:crazy:..Maisha unaweza ukaanzia popote ..Vitu common sense vya kuzingatia kwa kukusaidia ni..1-urahisi wa kupata huduma za kijamii kama hosptali, shule, sokoni, nyumba, roads, nyumba za ibada nk., 2-Mshahara wako unaendana na maisha halisi ya pale ulipopangiwa Mfano ukiwa unapata M1 Mpwapwa,Doms unaweza kutengeneza laki 8 kwa mwezi ukiwa alone as you compared to DSM and Atown kwasababu Mpwapwa vyakula bei chini, hosptali zko nyingi, shule zko nyingi, vyuo kibao, vyanzo vya maji vya kumwaga sio kama kimara maji ya chumvi na nyumba ni sawa na bure pango..matofali ya kuchoma 500shilingi, viwanja bei chee n.k so fanya survey kwanza ya eneo husika kwa kuzingatia hayo juu..Cheers
 
mbeya(tukuyu), iringa(wilaya ya kilolo), njombe, morogoro(kilombero) km unapenda kilimo utatoka.
 
Maisha ni kokote mdogo wangu,mimi nilianzia ajira dar nikaenda Mtwara na sasa nipo Kagera.
Ushauri wangu ukipata ajira kokote nenda alimradi mkono uende kinywani.
 
kwa ushuri wangu anzia wilaya mpya ya katavi wewe ndio utaonekana mjanja kule maana sehemu nyingine watu wana degree tatu tatu wewe utakuwa kama makamu wa rais maana rais kule ni pinda.

Ha ha ha hah
 

Ondoa uoga wa maisha, kwa mtindo huu hutafanikiwa popote utakapoishi. Ningekushauri uwe tayari kuishi popote. Jiamini hukuna haja ya kujijengea woga usio na maana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…