Hata mwalimu nyerere alishawahi kuulizwa kuhusu Tanganyika nakusema hata yeye hajui ilitokea wapi,akimanisha wakati wadhungu wakigawa bara letu ndio waliitupatuia jina hilo,hata hivyo kama unapenda nchi yako irudi katika uasilia wake basi wazee wanatuhadithia nchii hii ilikuwa ikiitwa MRIMA,cha msingi kama nilimuelewa prof shivji anatutaka tujikite zaidi katika mambo ya msingi kuliko kuanza kufikiria upuuzi wa jina la nchi maana hilo jina halikupi mustakabali wa maisha yako,na alieleza nyakati kama huzi ni nadra kuzipata hivyo tutumie vizuri kwa ustawi wa taifa letu.
sio kila jambo kulitizama kiitikadi zaidi,kama zanzibar tatizo lao ni utaifa wao,sie tunamambo mengi zaidi ya kutafakari zaidi ya huo utaifa wa tanzania au tanganyika.nampa pongezi kubwa sana prof kwa uchambuzi wake hasa katika suala muhimu na nyeti la ardhi.