Michezo Yetu Ya Utotoni Imepotea!

Michezo Yetu Ya Utotoni Imepotea!

Mwanza unaitwa Dama sijui maeneo mengine wanauitaje,baadhi yakanuni kigae kikikaa mstarini umebau(kushindwa)au ukikanyaga mstari,pia kunamuda unatakiwa kuweka kigae mguu moja huku mwingine ukitumika kuruka vyumba...nice tulienjoy sana kipindi hicho
palikuwepo mchezo ambao unachora chini vyumba vyumba halafu unarusha kipande cha kigae na kisha unakisukuma kwa mguu toka chumba kimoja hadi kingine. Halafu unatembea katika hivyo vyumba huku umefumba macho na kila hatua moja unauliza wenzako "Am I right?" ingawa kwakweli tulikuwa tukisema "Marait?". Ulikuwa ni mchezo unaompa mtoto changamoto na pia ni mazoezi mazuri sana. Sijawahi kuuona sasa miaka mingi kabisa.
 
Mwanza unaitwa Dama sijui maeneo mengine wanauitaje,baadhi yakanuni kigae kikikaa mstarini umebau(kushindwa)au ukikanyaga mstari,pia kunamuda unatakiwa kuweka kigae mguu moja huku mwingine ukitumika kuruka vyumba...nice tulienjoy sana kipindi hicho
Kilimanjaro tuliuita au tikri. Nimchezo nilio umudu sana kuliko mingine nliwekwa wa mwisho kira mara sababu nliweza kucheza bila kukosa mpaka mwisho. Nlifinywa sana na mama mpaka nlimchukia kisa michezo. Watoto wa sasa zzzzro kabisa. Wanajua wasap,twta,facebook. Basi daah shule ubunifu ushindani ujanja hakuna kitu
 
Wadau, mnaweza kuona ni kwa jinsi gani tunapoteza asili yetu! Leo hii, watoto hawachezi dama (kiboleni), hawachezi golori, hawafinyangi wadoli wala hawaokoti makaratasi ya kutengeneza mipira! Tunaelekea wapi?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
kweli utoto raha sana ila siku hizi mtoto anazaliwa na kuwekewa midoli yote ndani wala hakuna raha yoyote.Enzi zile watu mnatengenaza manati halafu mnaenda porini kuwinda ndege
 
magari ya ma box na waya jamani sioni ubunifu tulokuwa nao ukiwepo leo hii
 
Chezo langu pendwa vita vya bunduki zenye risasi vizibo vya soda!mabomu machungwa ,maembe mabovu tunaokota sokoni(wakati wa msimu wa mtunda hayo) mchezo ule umetuathiri sana kwani wengi wetu tukawa majambazi na askari ukubwani!wahuni wa kiboko msheri,komando yosso,orlando kaya ni mazo ya mchezo huu-maeneo ya magomeni,mburahati hadi manzese ndio uwanja wa vita!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom