Halafu baada ya kituo cha radio kukusanya ml100 kutoka kwa wajinga au mabwege 1000 wanamchagua mjinga mmoja labda aliyecheza mara nyingi zaidi na kumpa ml 1.
Siku zote michezo ya bahati nasibu inatakiwa iendeshwe na sekta za umma, kama jiji, serikali kuu, halmashauri n.k. Hii ni kwa sababu fedha zinazobaki baada ya kulipa washindi zinaweza kutumika kufanya mambo ya umma. Kwa kutumia michezo ya kamari kuna nchi zinafanya mambo makubwa. Kwa mfano hapa kwetu tungeweza kujenga madarasa, kufidia gharama za masomo ziwe chini, kujenga wodi za hospital au kununulia dawa
Tofauti ni kuwa za majuu zinafanyika kwa uwazi na kihalali halafu ni sekta za umma zinafanya ili faida inayopitakana inakwenda kwenye shughuli za umma. Ni hatari sana kuachia watu binafsi kumiliki michezo ya kubahatisha kwa asilimia mia moja.
ukiwa kwenye kundi la wajinga, mazuzu mapumbavu alafu kama unahisi wewe ni timamu basi tumia utimamu kumnyonya huyo mjinga, zuzu na mpumbavu utoboe kwenye maisha ndo uje useme hivi... lah sivyo na wewe unakuwa zoba, au pimbi mmoja.
Sijafanya utafiti ila naamini, ukiongea jambo la msingi kwa wajinga watishia kutukana, kusengenya au kupuuza. Waambie kuhusu "connection, umbea, uchawa na ngono" hapo utawachukua wengi.
Yaani inashangaza kwa kweli mzee hiwezi amini kama hii nchi ina serikali na vyombo vyake vyote vya dola!! Kwa sasa apa tz kila mtu anatafuta njia ya kuwaibia wajinga