Michezo magazetini leo...

Status
Not open for further replies.
Bure kuendelea Chalenji
Imeandikwa na Evance Ng'ingo; Tarehe: 2nd December 2010

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema mashabiki wataendelea kuona bure mechi za Kombe la Chalenji mpaka Jumapili wiki hii.

Jumatatu iliyopita TFF ilitangaza kuwa mashabiki wataona bure michuano hiyo ya Chalenji inayoendelea Uwanja wa Taifa Dar es Salaam hadi leo na kuwa kesho wangeanza kulipa.

Lakini akizungumza jana Rais wa TFF Leodegar Tenga alisema wameamua kuongeza muda huo kwa mechi za kesho na Jumapili na kuwa kuanzia hatua ya robo fainali ndipo wataanza kulipa.

Alisema kipindi ambacho wameruhusu watazamaji kuingia bure kumekuwa na hamasa ambayo imefanya wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars' kucheza vizuri zaidi pamoja na ile ya Zanzibar ‘Zanzibar Heroes'.

Wakati huo huo, Kenya imejiweka kwenye nafasi mbaya ya kufuzu robo fainali baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Ethiopia.

Hicho ni kipigo cha pili mfululizo, ambapo katika mchezo wa kwanza ilifungwa mabao 3-2 na Malawi, hivyo imebakisha mchezo wa mwisho Jumapili itakapocheza na Uganda.

Kama Kenya itashinda mchezo huo, itabidi iangalie na matokeo ya makundi mengine ili iweze kuingia robo fainali kwa mgongo wa timu zenye uwiano mzuri wa pointi.

Uganda na Malawi kila moja ina pointi nne, wakati Ethiopia ina pointi tatu, hivyo nafasi ya Kenya ni finyu.

Kulingana na taratibu za mashindano hayo kwa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), timu mbili za juu kutoka kila kundi kati ya makundi matatu ya michuano hiyo zitafuzu robo fainali, ambapo pia kutakuwa na timu mbili zenye uwiano mzuri wa pointi nazo zitafuzu.

Katika mchezo wa Uganda na Malawi uliofanyika mapema jana kwenye Uwanja huo huo wa Taifa, timu hizo zilifungana bao 1-1, huku Uganda ikisawazisha dakika ya 80 mfungaji akiwa Emannuel Okwi kwa shuti.

Malawi ilikuwa ya kwanza kuziona nyavu za Uganda dakika ya pili ya mchezo kupitia kwa Victor Nyilanda aliyefunga kwa kichwa kufuatia pasi ya Henry Thabit.
 
1994 Mara ya mwisho Tanzania kutwaa Kombe la Chalenji
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 3rd December 2010 @ 23:59 Imesomwa na watu: 55; Jumla ya maoni: 0


12_10_f9xr9w.jpg






MICHUANO ya Chalenji ilianza Jumamosi iliyopita jijini Dar es Salaam na inashirikisha nchi 12.

Michuano hiyo inashirikisha nchi wanachama wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (Cecafa). Lakini mwaka huu kuna nchi tatu zimealikwa ambazo si wanachama wa Cecafa, ambazo ni Ivory Coast, Zambia na Malawi.

Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars' ipo Kundi A pamoja na Zambia, Somalia na Burundi, wakati Kundi B linaundwa na timu za Rwanda, Ivory Coast, Sudan na Zanzibar, huku Kundi C likiwa na nchi za Uganda, Malawi na Ethiopia.

Katika mchezo wa ufunguzi Jumamosi Kilimanjaro Stars ilifungwa bao 1-0 na Zambia, wakati siku iliyofuata Zanzibar iliifunga Sudan mabao 2-0. Waamuzi wanaochezesha michuano hiyo na nchi wanazotoka kwenye mabano kuwa ni Issa Kagabo (Rwanda), Rassas Librato Sabit (Sudan), Israel Mujuni (Tanzania Bara), Dennis Bate (Uganda), Ramadhan Kibo (Zanzibar) na Bamlak Weyesa Tessema (Ethiopia).

Waamuzi wasaidizi ni Charles Nizigiyimana wa Burundi, Gebre Silassie Solomon (Ethiopia), Wamalwa Elias Kuloba (Kenya), Theogene Ndagijimana (Rwanda), Hamis Chang'walu (Tanzania Bara), Bugembe Hussein (Uganda), Medany Mustafa (Sudan) na Bashir Arab (Somalia).

Kipigo ilichokipata Stars Jumamosi kiliwashtua wadau wa soka kwa kiasi kikubwa, lakini Kocha Mkuu wa timu hiyo Jan Poulsen kidogo alirekebisha mambo hivyo Jumanne Stars ikaifunga Somalia mabao 3-0, angalau ikawapa matumaini mashabiki.

Kwa ujumla matokeo ya mchezo wa kwanza kwa Zanzibar Heroes nayo yaliwapa matumaini mashabiki ingawa nayo Jumatano iliwaudhi baada ya kukubali kipigo cha bao 1-0 kutoka
kwa Ivory Coast.

Ni miaka 15 sasa imepita, Tanzania ikiwa inafanya kazi ngumu na isiyo na mshahara katika soka kwenye michuano hiyo kwa maana ya kuwa msindikizaji. Ni kazi ngumu kwa kweli, kuwa msindikizaji tu kila mwaka, huku ukishuhudia wenzio wakibeba vikombe na mamilioni ya pesa.

Inauma na pengine inasikitisha na kushangaza pia hasa kutokana na tathmini za makocha mbalimbali wa ukanda huu kuwa Tanzania imebarikiwa kuwa na wachezaji wengi wenye
vipaji.

Pande zote yaani Tanzania Bara na visiwani ambazo hushiriki kama nchi mbili tofauti kwenye michuano hiyo, zimeshindwa kufanya lolote kwenye michuano hiyo inayofanyika kila mwaka katika nchi inayokubaliwa kuandaa.

Mara ya mwisho Tanzania Bara kufurahia michuano hiyo ni mwaka 1994 pale Kilimanjaro Stars ilipoutwaa ubingwa huo, baada ya hapo imekuwa hadithi mpaka leo.

Kabla ya hapo, Kilimanjaro Stars imewahi kuwa bingwa wa michuano hiyo mwaka 1974, huku Zanzibar Heroes ikijitutumua na kutwaa ubingwa mwaka 1995.

Tanzania ilionekana kupata ahueni kidogo ilipofuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani michuano iliyofanyika Ivory Coast mwanzoni mwa mwaka jana.

Lakini pamoja na Tanzania kuonekana ndio timu iliyokuwa pamoja muda mrefu na kucheza mechi nyingi za kimataifa, lakini iliishia hatua ya makundi na kurudi zake nyumbani.

Nasema hivyo kwa sababu michuano hiyo ilikuwa ikishirikisha wachezaji wanaocheza ligi
ya ndani, lakini kwa upande wa Stars haikuwa na wachezaji wanaocheza ligi za nje, hivyo walikuwa na uzoefu na michuano ya kimataifa, kwani kikosi kilichoenda Ivory Coast karibu
chote ndicho kilichokuwa kikicheza mechi za awali kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika zilizofanyika Ghana.

Sasa huu ndio wakati kwa timu ya Tanzania Bara na Zanzibar kuleta sherehe nyumbani, Watanzania wamechoka kulalama kila kukicha. Kocha Mkuu wa Tanzania Bara, Jan Poulsen
anaiongoza nchi kwa mara ya kwanza kwenye michuano hiyo tangu alipowasili Agosti mwaka
huu.


Watanzania bado wana mapenzi na timu yao ni vile tu imekuwa ikiwakatisha tamaa kila inapodhaniwa kwamba inafanya vizuri kumbe ndio huvurunda hapo ndipo kila mmoja
anapoona uchungu.

Aidha Zanzibar Heroes ipo kwenye michuano ya mwaka huu ikiwa chini ya kocha Stewart Hall ambaye pia ni mara ya kwanza kukiongoza kikosi cha timu hiyo.

Kama nilivyosema Zambia, Malawi na Ivory Coast zinashiriki michuano hiyo kama timu mualikwa ili kutoa changamoto kwa timu mwanachama wa CECAFA. Hata hivyo mwaka 1981
Zambia na Malawi zilikuwa miongoni mwa wanachama wa CECAFA kabla ya kujitoa mwaka 1994.

Nchi hizo zilijitoa baada ya kuundwa kwa Shirikisho la Soka kwa nchi za Kusini mwa Afrika (COSAFA). Baadaye Rwanda, Burundi, Eritrea na Djibouti zilijiunga na CECAFA mwaka 1995 na kufanya idadi ya wanachama wake kufikia 11.

Nawaombea heri wachezaji wa Kilimanjaro Stars na Zanzibar Heroes wajue Watanzania wapo
nyuma yao, hakuna lisilowezekana panapokuwa na juhudi za kutosha. Wafanye kile ambacho
Watanzania wengi wanataka wakifanye, nacho ni ushindi na kuhakikisha kombe haliondoki.

Kikubwa ni kwamba Stars na Zanzibar Heroes zinakutana na nchi ambazo inazifahamu vyema, hivyo hazitawasumbua sana. Ingawa soka huwa halitabiriki, lakini kwa kiwango
kilichooneshwa na wachezaji wa timu hizo kama watabadilika kidogo basi kombe halitaondoka.

Wachezaji watambue Watanzania nia yao ni kubakisha kombe nyumbani, ili walishike na si kuliona likipandishwa kwenye ndege na kuondoka. Ifuatayo ni orodha ya mabingwa wa Kombe la Chalenji tangu mwaka 1973.

Mwaka Mshindi 2010 ?
2009 Uganda
2008 Uganda
2007 Sudan
2006 Zambia
2005 Ethiopia
2004 Ethiopia
2003 Uganda
2002 Kenya
2001 Ethiopia
2000 Uganda
1999 Rwanda B
1997 Uganda
1996 Uganda
1995 Zanzibar
1994 Tanzania
1992 Uganda
1991 Zambia
1990 Uganda
1989 Uganda
1988 Malawi
1987 Ethiopia
1985 Zimbabwe
1984 Zambia
1983 Kenya
1982 Kenya
1981 Kenya
1980 Sudan
1979 Malawi
1978 Malawi
1977 Uganda
1976 Uganda
1975 Kenya
1974 Tanzania
1973 Uganda
 
Mashindano ya baiskeli yalinoga Mwanza
Imeandikwa na Grace Chilongola, Mwanza; Tarehe: 3rd December 2010 @ 23:00 Imesomwa na watu: 32; Jumla ya maoni: 0


12_10_b1h8p3.jpg

Baadhi ya washiriki wa mashindano ya baiskeli Mwanza.





MASHINDANO ya mbio za baiskeli maarufu kama Vodacom Mwanza Cycle Challenge mwaka huu yalilipamba jiji la Mwanza baada ya idadi kubwa ya walemavu wa viungo kujitokeza kushiriki.

Yalishirikisha walemavu 30 wanawake kwa wanaume ambapo walikimbia umbali wa kilometa 10 kwa kilometa 16 kwenda na kurudi. Aliyeibuka kidedea kwa upande wa wanawake ni Helena Mwendesha (48) baada ya kukimbia kwa dakika 40 na sekunde 27 kisha kujinyakulia kitita cha Sh 400,000.

Helena anaeleza jinsi alivyofanikiwa kupata ushindi huo huku akitoa wito kwa Watanzania kuwa hata wao walemavu wakishirikishwa katika shughuli mbalimbali za wanaweza.

"Nimefurahi kushirikishwa katika mashindano ya kukimbia na baiskeli na sasa nimewadhihirishia Watanzania pamoja na wanawake wenzangu wenye ulemavu kuwa
sisi walemavu tunaweza, tupewe nafasi," anasema.

Helena anasema ushindi wake umetokana na mazoezi aliyokuwa akiyafanya kabla ya mashindano hayo sambamba na moyo wa kujituma.

Kila anayefanya bidii na kuamini kuwa mafanikio yanaletwa kutokana na bidii hiyo, ukweli matunda ya bidii zake lazima yaonekana katika jamii hata kama ni kidogo.

"Matokeo ya mashindano haya ni sehemu ya nia niliyoiweka ambayo ilikuwa ni lazima
nichukue ushindi wa kwanza".

Mahitaji ya fedha za kujikimu pamoja na kumsaidia mumewe kutunza familia yao yenye watoto sita ambao wanahitaji msaada wa wazazi wao pia yalimsukuma kushiriki kwenye mashindano hayo.

Helena anasema hali ya ulemavu aliona siyo sababu ya yeye kushindwa kufanya kile anachoamini kuwa kitamletea mafanikio katika maisha yake na kudai kuwa ana uwezo wa kufanya kazi yeyote ambayo itamuingizia kipato.

Mbio za baiskeli ni sehemu ya kuwaonyesha Watanzania kuwa anao uwezo wa kufanya kazi licha ya kuwa na ulemavu hivyo kuiomba jamii kutowatenga na kuwashirikisha katika shughuli mbalimbali za kijamii ambazo zitamsaidia kuinua kipato chake.

Kutokana na ulemavu alionao ambao aliupata mara baada ya kuzaliwa na kuugua ugonjwa wa uti wa mgongo hakuweza kwenda shule, lakini pamoja na hali hiyo bado anaweza kufanya biashara ambayo inaweza kumuingia fedha na kuiendeleza familia yake.

Watanzania ambao wanaona juhudi zake wamsaidie ili aweze kufanya shughuli nyingine ambazo hazihitaji nguvu zaidi kama mashindano haya. "Umri wangu sasa ni mkubwa, muda si mrefu naweza kushindwa kushiriki katika mashindano haya ukizingatia kuwa vifaa tunavyotumia siyo maalum kwa ajili ya mashindano," anasema.

Anafafanua kuwa baiskeli anayotumia ni ngumu sana hasa wakati wa kupandisha mlima hali inayomfanya apate shida na kusikia maumivu makali kifuani. Ametoa ombi kwa waandaaji
kuwasaidia washiriki ambao hawa uwezo wa kuendelea na mashindano kwa kuwapatia mitaji ili waweze kuwa kumbukumbu ya Vodacom Cycle Challenge.

Wapo wanamichezo wengi ambao waliweza kung'ara katika mbio hizo na kupata umaarufu katika kipindi cha nyuma lakini wametupwa na Serikali yao na hata vilabu vyao hivyo kubaki wakihangaika na kuwa ombaomba.

"Hii siyo picha nzuri kwa nchi ambayo inathamini michezo na inaposhindwa kuwasaidia walemavu wanaoonyesha jitihada zao za kujitafutia kipato," anasema.

Mwanza Cycle Challenge iwe mfano kwa jamii kwa kuwa waanzilishi wa mchezo huo pamoja na kuwa wadhamini wakuu kwa kuwaangalia vinara wa mashindano hayo na kuwasidia katika Nyanja mbalimbali hivyo kujiwekea kumbukumbu nzuri kwa siku za baadae.

Kuwathamini wanamichezo waliostaafu kutawatia nguvu wanamichezo wachanga kushiriki na kuwekeza katika michezo kwa bidii kwa kuwa watakuwa wanajaliwa na kupewa thamani ya hali ya juu.
 
Jumamosi Desemba 04, 2010 Makala

Kamati ya mapato TFF bado kimyati
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 3rd December 2010 @ 22:00 Imesomwa na watu: 29; Jumla ya maoni: 0


12_10_01gu9n.jpg

Rais wa TFF, Leodegar Tenga



MEI mwaka jana Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), liliunda kamati maalumu kwa ajili ya Udhibiti na Uboreshaji wa Mapato yatokanayo na viingilio vya milangoni.

Kamati hiyo iliyofanya kazi chini ya uenyekiti wa Rais wa TFF Leodegar Tenga na Katibu wake Deo Lyatto, ilipewa muda hadi Julai 31 kukamilisha mchakato huo na kutoa ripoti ambayo ingekuwa suluhisho la tatizo hilo, baada ya kupokea maoni kwa wadau kulingana na
utaratibu maalumu.

Wajumbe wengine waliokuwa wametangazwa kwenye kamati hiyo ni Idd Kipingu, Dk. Mohamed Chicco, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, Yusufu Nzowa, Makamu wa Pili wa Rais wa TFF, Ramadhan Nassib na Ofisa kutoka Taasisi ya
Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru).

Kamati hiyo ilipewa hadidu mbalimbali za rejea, ambazo ilitakiwa izifanyie kazi kwa kupata taarifa na maoni kutoka kwa wadau wa soka juu ya nini kifanyike kupambana na hujuma ya mapato milangoni.

Ilipewa kazi ya kuangalia suala la miundombinu ya viwanja kama vina mashine za kutambua
tiketi na je, kuna uwezo wa kuzipata na nini kifanyike kwa wakati huu.

Pia suala la rasilimali watu inayohusika na usimamizi wa mapato ya milangoni ni suala lingine ambalo ilipewa kamati hiyo kwa kuangalia kama watu wanaowatumiwa kudhibiti mapato wana uwezo huo na wameonekana katika jamii kama ni waaminifu.

Eneo lingine ambalo kamati hiyo ilitakiwa kutilia mkazo ni suala la kuangalia mchakato wa
upatikanaji, usambazi, uuzaji na uhakiki wa tiketi na utaratibu wa ukusanyaji na uhakiki wa mapato.

Hayo ni baadhi ya mambo ambayo kamati hiyo ilipewa iyafanyie kazi kutokana na kuwepo
malalamiko mbalimbali kuhusiana na kudaiwa kuwepo hujuma kwenye mapato yatokanayo na viingilio.

Hakuna kificho kwamba mapato ya michezo mikubwa ya soka yamekuwa yakiwapa hofu
kubwa mashabiki kila yanapotangazwa. Kuna hofu kwamba upo udanganyifu katika mambo haya kwa manufaa ya wachache, au kuna udhaifu katika kudhibiti mapato kwa maana ya watu wanaoingia uwanjani kushuhudia mpira.

Huwa haihitaji uwe na elimu kubwa ukitazama umati unaokuwepo uwanjani, halafu useme mapato ni kidogo wakati uwanja umejaa na idadi ya viti inajulikana. Kuundwa kwa kamati
hiyo na jinsi ilivyokuwa ikifanya kazi ya kupokea maoni kutoka kwa wadau wa soka, ilijaa imani kwamba ufumbuzi utapatikana.

Lakini sasa ni zaidi ya mwaka mmoja tangu muda uliowekwa wa kamati hiyo kukamilisha
jukumu lake, huku kukiwa na kimya kimetanda. Kulikoni Tenga na kamati yake? Bado inakusanya maoni?

Au imekuwa vigumu kupata suluhisho? Naomba jambo hili lifanyiwe kazi haraka iwezekanavyo. Suala la udhibiti wa mapato linatia shaka ni wakati sasa wa kamati iliyokuwa ikifanya kazi hiyo kumaliza jambo hili mapema iwezekanavyo na kutoka na ufumbuzi wa
jambo hilo.

" Ni lazima tutafute njia ya kuondoa tatizo hilo, kwani klabu zinahitaji fedha kwa ajili ya kuendesha mpira, TFF pia inahitaji fedha na hakuna sehemu nyingine ya kupata fedha na wenye viwanja wanataka za kuboreshea viwanja kwa sababu TFF haimiliki viwanja,"
nakumbuka kauli ya Tenga wakati akiizungumzia kamati yake.

Kwa mujibu wa Tenga kamati hiyo imepewa hadidu mbalimbali za rejea, ambazo inatakiwa izifanyie kazi kwa kupata taarifa na maoni kutoka kwa wadau wa soka juu ya nini kifanyike kupambana na hujuma ya mapato milangoni.

"Kuyafanyia kazi maoni hayo na kutoa mapendekezo juu ya utaratibu mzuri wa udhibiti na
uboreshaji wa mapato," anasema Tenga na kuongeza kuwa kamati hiyo itatathmini na kufanyia kazi mambo mbalimbali ikiwemo mfumo wa udhibiti wa mapato ulivyo sasa.

" Pia tumewapa kazi ya kuangalia suala la miundombinu ya viwanja vyetu kama vina mashine za kutambua tiketi na je, tuna uwezo wa kuzipata na nini kifanyike kwa wakati huu.

" Na pia suala la rasilimali watu inayohusika na usimamizi wa mapato ya milangoni ni suala lingine ambalo tumeipa kamati hiyo. Tunatakiwa kuona watu tunaowatumia kudhibiti
mapato wana uwezo huo na wameonekana katika jamii kama ni waaminifu?" anakumbuka Tenga.

Eneo lingine ambalo anasema wamelitaka kamati hiyo kutilia mkazo ni suala la kuangalia mchakato wa upatikanaji, usambazi, uuzaji na uhakiki wa tiketi na utaratibu wa ukusanyaji na uhakiki wa mapato. Hayo yapo wapi?
 
Jumamosi Desemba 04, 2010 Makala

Makocha Kenya, Somalia, wachekelea kampeni ya Malaria
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 3rd December 2010 @ 21:00 Imesomwa na watu: 45; Jumla ya maoni: 0


12_10_buaqc5.jpg

Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na wachezaji wa Zambia katika mechi ya ufunguzi wa Kombe la Chalenji, Zambia ilicheza na Kilimanjaro Stars.



HAKUNA asiyefahamu kwamba ugonjwa wa Malaria ndio unaoongoza kwa kuua Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Kwa mujibu wa takwimu, Afrika watu takriban milioni 38.9 huugua malaria ambapo wengi wao ni watoto na mama wajawazito. Kana kwamba hiyo haitoshi takribani watu zaidi ya 209,000 hufa kila mwaka kwa ugonjwa huo.

Inaaminika kuwa kila sekunde 45 hufariki mtoto mmoja kwa malaria. Kwa vile ugonjwa huo sasa umesambaa kila mahala mpaka kwa wanamichezo, ndio maana kampeni ya kutokomeza malaria imeingia kwenye michuano ya Kombe la Chalenji inayoendelea Dar es Salaam kwa kushirikisha timu kutoka nchi 12.

Lengo kubwa la kampeni hiyo kuingia kwenye michuano ya Kombe la Chalenji ni kufikisha ujumbe na kuwataka wanasoka kuungana na wanamichezo wengine, watu mbalimbali kutokomeza malaria.

Katika uzinduzi wa kampeni ya Tuungane kutokomeza malaria (UAM) kabla ya kuanza kwa Kombe la Chalenji Ijumaa iliyopita, Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga anasema ni jambo bora kwa kampeni hizo kuingia kwenye michuano hiyo kwani soka inapendwa na watu wengi hivyo itakuwa ni njia rahisi kwa nyota wa mchezo huo kufikisha ujumbe na namna ya kujikinga na malaria kwa mashabiki wao.

"Ni jambo sahihi kabisa kuwa kwenye kampeni za kutokomeza malaria soka ina nguvu sana, watu wanapenda soka, wanapenda nyota wao, makocha wao, hivyo kama watapeleka ujumbe wa namna ya kupiga vita malaria, mashabiki wao watawasikiliza," anasema.

"Mchezo wa soka unataka jamii yenye afya ili uendelee na kukua. Wanahitajika makocha, wachezaji, wasimamizi, waamuzi na hata mashabiki wenye afya, bila hivyo hatuwezi kuendeleza soka.

Jamii yenye malaria haina afya, ndio maana tunaunga mkono juhudi za kutokomeza malaria zinazofanywa na kampeni ya United Against Malaria," anasema.

"UAM imepata ushirikiano wa hali ya juu kutoka CECAFA, hii inadhihirisha dhamira yao ya kushiriki katika vita dhidi ya Malaria."

Anasema David Kyne, Meneja wa kampeni ya UAM. Naye Katibu Mkuu wa Cecafa, Nicholas Musonye anasema: "Tuunganishe nguvu zetu kutokomeza malaria na kuthibitisha hilo, wanachama wa Cecafa wote wameungana kutekeleza hilo".

Timu 12 zinazoshiriki michuano ya Kombe la Chalenji ni Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars', Zanzibar Heroes, Ivory Coast, Malawi, Zambia, Rwanda, Ethiopia, Kenya, Burundi, Sudan, Somalia na Uganda.

Kati ya timu hizo zinazoshiriki, karibu zote zilishaingia kwenye kampeni ya UAM isipokuwa Kenya, Burundi, Sudan na Somalia ambazo ndizo zimeingia kwenye kampeni hizo katika michuano ya Chalenji ya mwaka huu. Makocha wa timu hizo walipata nafasi ya kuzungumzia hatua hiyo kwenye gazeti hili.

Kocha wa Kenya, Jacob ‘Ghost' Mulee anasema hana wasiwasi na kampeni hizo na kwamba yeye na kikosi chake watashiriki kikamilifu kusambaza ujumbe kwa wananchi wa Kenya na kuwapa elimu jinsi ya kujikinga na ugonjwa huo.

"Ni jambo zuri si baya kwa sababu hakuna asiyeufahamu ugonjwa wa malaria Afrika kwa jinsi unavyoua watu, hata wanamichezo, wanasoka wapo waliokufa kwa ugonjwa huu… "Ni mara ngapi makocha tunapoteza wachezaji wetu kwenye mechi muhimu kwasababu tu wanaugua malaria, tutaungana kutokomeza malaria nina hakika wananchi wa Kenya watatusikia katika kulifanikisha hilo,"anasema.

Kocha wa Somalia, Yousuf Adam anakiri ugonjwa wa malaria unatesa wanamichezo na hata wachezaji wake wa Somalia walishawahi kuugua ugonjwa huo si mara moja mara mbili.

"Ni kama vile watu wameuchukulia mazoea, lakini ni ugonjwa mbaya sana, haupaswi kuachiwa, tumeridhika kabisa kutumika katika kampeni hizi za kupambana na ugonjwa wa malaria, wengine tuna ndugu zetu jamaa, watoto wamekufa kwa ugonjwa huu,"anasema.

Naye Kocha wa Sudan, Nasir Beshir Award anasema anawapongeza wahusika wa kampeni za kutokomeza malaria (UAM) kwa kuamua kuingiza kampeni hizo kwenye michuano hiyo.

"Kwa kufanya hivyo wanatufanya wapenzi wa soka katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati kuamka na kutambua kuwa malaria ipo na inaua.

"Mimi kama kocha nikiondoka hapa kwenye mashindano nitakwenda na ujumbe huo wa Tuungane kutokomeza malaria, naamini nitaeleweka katika jamii inayonizungumza, vivyo hivyo hata kwa wachezaji wangu,"anasema.
 
Friday, 03 December 2010 19:50

kocha%20poulsen2.jpg
Andrew Kingamkono
TANZANIA yenye idadi ya watu wanaokadiliwa kufikia milioni 43,739,051 kwa mujibu wa ripoti ya Benki ya Dunia ya mwaka 2009 leo watakuwa na kibarua kizito mbele ya Burundi yenye wakazi 8,303,330 katika kusaka tiketi ya kufuzu kwa hatua ya pili ya michuano ya Tusker Chalenji.
Tanzania inayosifika kwa amani, utulivu na nguvu za kijeshi katika nchi za maziwa makuu ilitwaa kwa mara ya mwisho ubingwa wa Kombe la Tusker Chalenji mwaka 1994, nchini Kenya wakati Burundi ikiingia kwenye vita ya kikabila zilizosababisha mauaji ya kimbari na uvunjwa wa amani.

Burundi pamoja na kuwa na idadi ndogo ya watu kuandamwa na vita ya wenye kwa wenye kwa zaidi ya miaka 16, michuano ya mwaka huu imeonyesha kubadilika zaidi na kufanikiwa kupata pointi nne na sasa wanahitaji sare tu kufuzu kwa hatua ya pili kama mshindi wa pili kutoka Kundi A nyuma ya Zambia iliyoichakaza Somalia kwa mabao 6-0.

Wachezaji wa Kilimanjaro Stars waliobeba dhamana ya Tanzania milioni 40 wenye sifa ya amani ya leo itakuwa si kitu mbele ya mashabiki wao wenye hamu ya kuona nchini yao ikipata ushindi na kuthibisha nguvu zake za kisiasa katika ukanda huu kwa kuichapa Burundi na kusonga mbele si kusubili nafasi ya upendeleo ya Cecafa wakiwa washindi wa tatu.

Kilimanjaro Stars inashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa kundi A inayoongozwa na Chipolopolo yenye pointi 7, wakati Burundi inashika nafasi ya pili ikiwa na pointi nne na Somalia ya mwisho.

Timu hizo zimekutana mara tano kwenye michuano ya chalenji tangu mwaka 2004 ambapo Stars ilishinda mechi tatu miaka tofauti, suluhu moja huku Burundi ikiikung'uta mabao 2-0 jijini Addis Ababa Ethiopia 2004 ambao ndio ushindi pekee wa timu hiyo hadi leo zinapokutana.

Wachezaji wa Kili Stars watakuwa kwenye kibarua kigumu cha kuthibisha uzalendo wao mbele ya Watanzania walionekana kuchoshwa na uchezaji wa kutojituma kwa nyota hao.

Kocha Jan Poulsen anajua matokeo yasiyoridhia kwenye mchezo huo yatamweka kiti moto mbele ya mashabiki wake kama ilivyokuwa kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Zambia na kulazimika kubadilisha nyota wake wawili alipocheza dhidi ya Somalia.

"Nimekuwa nao kambini, mazoezini kila dakika wana morali ya kutosha na kila mmoja ana ari ya kushinda anataka kuona timu ikicheza fainali, makosa waliyofanya kwenye mchezo wa Zambia wameyaelewa na wamejirekebisha ndio maana wakacheza mpira mzuri na Somalia na hata mechi ya Burundi itakuwa hivyo, tumejianda kushinda si vinginevyo na naomba watu waamini wachezaji wao,watashinda."

Safu ya ushambuliaji wa Kili Stars itaongozwa na mchezaji ghali wa Ligi Kuu ya Tanzania, Mrisho Ngassa kwa kushirikiana na Thomas Ulimwengu au John Boko mfungaji wa bao la pili dhidi ya Somalia.

Viungo watakuwa chini ya Henry Joseph na Shabaan Nditi wataiunganisha timu hiyo na kuhakikisha watibua mipango yote ya Waburundi hao wenye sifa ya kufanya mashabulizi ya kushitukiza.

Katika mchezo wake wa pili beki wa Stars, Kelvin Yondani na Juma Nyoso walifanya makosa mengi ambayo leo hayapaswi kurudiwa na tayari kocha Poulsen amehaidi kulifanyia kazi tatizo hilo.

Mechi nyingine itakayochezwa leo ni Malawi dhidi ya Ethiopia, Malawi inaongoza msimamo wa kundi C ikiwa na pointi nne baada ya kushinda mechi yake ya awali iliifunga Kenya mabao 3-2 kabla ya kutoka sare na Uganda ya bao 1-1 wakati kwa upande wa Ethiopia wana pointi tatu sawa na Uganda wakati na tofauti ya bao.

Wakati huo huo; Hussein Kauli anaripoti kuwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, ACP Suleimani Kova, amewatahadharisha mashabiki wanaotarajiwa kuushuhudia mchezo wa kati ya Kilimanjaro Stars na Burundi leo, kuwa hakuna atakayeruhusiwa kusimama ili kuepuka madhara yaliyowakumba Kenya hivi karibuni.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, ACP Kova alisema wasingependa kuingia kwenye tukio kama lile lilitokea Kenya ambapo mashabiki saba walifariki baada ya kukanyagana kutokana na uwanja wa Nyayo kujaa kupita uwezo wake.

Alisema kwa kuwa mashabiki wengi wanatarajiwa kushuhudia mchezo huo, suala la usalama wa mashabiki litapewa kipaumbele kwa kuhakikisha mashabiki hawajai kupita uwezo wa uwanja huo wa watu 60,000.

Hivyo aliwataka mashabiki wawahi kuingia uwanjani kabla ya mchezo huo kuanza na iwapo itatokea uwanja huo ukajaa, hawataruhusu mashabiki kusimama ili kuepuka maafa.

"Tunachowaomba mashabiki wanatakiwa kuwahi mapema na kila mmoja achukue nafasi yake kwa sababu uwanja una viti vingi, itakapofikia uwanja umejaa tutafunga milango na mtu atakayeruhusiwa kuingia" alionya Kova.

Alisema jeshi hilo litahakikisha kuwa usalama wa mashabiki unazingatiwa, hivyo pamoja na mashabiki kuruhusiwa kuinga bure lakini sio holela kiasi cha kuhatarisha usalama wao.
 
Saturday December 04, 2010 Sports
Local girls beat Kenya in cricket


By DAILY NEWS Reporter, 2nd December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 52

TANZANIA launched their East Africa under-19 Cricket Women tournament title campaign with a strong note by comprehensively whitewashing Kenya by 86 runs at the Annadil Burhani grounds in Dar es Salaam on Thursday.

The local ladies have vowed to win the trophy and they simply made a statement of intent with a determined display. Tanzania won the toss and went to bat first hitting 104 runs. Jessica Elili hit 20 runs, while Asha Ibrahim scored 19 runs. Other contribution came from Mariam Said who hit 14 runs.

In replay to Tanzania's target Kenya failed to chase, ending their inning with meagre 18 runs for all. Asha Ibrahim and Mariam Said claimed four and three wickets each.

In the second match of the day Uganda thrashed Rwanda by 108 runs. Shellan Atoulla and Rebecca Mirembe scored 26 and 17 runs respectively to steer Uganda to a comfortable victory.

Uganda's Janet Mbabazi took four wickets, while Juliana Asimwe managed three wickets. The 30 overs tournament continues today where Tanzania will play host to Rwanda at the University of Dar es Salaam grounds in the first match, while the second match to be played at the same venue would see Uganda taking on Kenya.

On Saturday, Kenya will confront Rwanda in the first match to be played at the Annadil Burhani grounds, while Tanzania will have an encounter with Uganda in the second match.

The tournament co-ordinator Kazeem Nasser said the two top teams will face off in the final to be preceded by a play off match that will pit third and fourth placed teams. Both matches will be played at the Annadil Burhani grounds on Sunday
 
Saturday December 04, 2010 Sports
National Stadium gets supervisor


By DAILY NEWS Reporter, 2nd December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 84

THE Permanent Secretary in the Ministry of Information, Youth, Culture and Sports Sethi Kamuhanda, has appointed Rishiankira Urio to supervise the running of the National Stadium in Dar es Salaam.

According to a statement released by the ministry on Thursday, the appointment was effective from November 11 this year.

Urio, who is the Senior Distribution and Procurement Officer at the ministry, is also in charge of the construction of proposed phase two of the National Sports Complex.

The statement said Urio will be in charge of the day to day activities at the FIFA/ IAAF standard stadium, until the government contracts out the management of the facility to a qualified properity and sports management company.

Two years ago, the government advertised bid, inviting experienced and qualified companies to submit letters of expression of interest to provide service of the stadium's management.

The interested firms were required to submit relevant and comprehensive information and documentations, indicating their core competencies and qualification in managing similar stadium.

Built, by Beijing Construction and Engineering Group Company Limited to the tune of US$ 56.4 million (72.756b/-), the 60, 000 seating capacity stadium designed and built to FIFA and IAAF Standard was funded by Chinese and Tanzania governments.

The stadium's outstanding features include a roof that extends inwards to cover seats up to the halfway line, 114 close-circuit television cameras, a scoreboard and five main entrances, a lavish VIP lounge, 600 indoor car parking bays and 2,000 car parking outside the stadium.

Kamuhanda has also appointed Josephine Mutahiwa as the new Manager of the historic Uhuru Stadium, just a stone throw away from the National Stadium. Mutahiwa's appointment was effective from October15. Her appointment follows the death of former manager Charles Masanja, who passed away last year.

Prior to her appointment, Mutahiwa was Chief Sports Officer, Department Sports Development in the ministry.
 
Saturday December 04, 2010 Sports
‘Arusha Wazees' soccer team now to build own club house


From MARC NKWAME in Arusha, 30th November 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 124

THE Wazee Sports Club of Arusha have started efforts to construct their ‘Club House' at a recently acquired plot within the Nane-Nane grounds in Themi Hill area of Njiro.

The Wazee SC has for years been pitching camp on the General Tyre (EA) grounds, the closed down vehicles' tire manufacturing factory which is also based in Njiro.

Now oldies club have been provided with land by the Tanzania Agricultural Society (TASO) on which to set up their club house.

TASO have in the course of this week, allocated the ‘Wazees' (oldies) a vacant plot inside the Nanenane grounds, where they will soon erect their Club House with sporting facilities, an office as well as provisions for community services.

Reports from the team have revealed that the designs for the same are ready and that financial and material contributions towards the project have already started flowing in.

The Wazee Club is essentially a football team made up of ageing individuals.

Meanwhile, members of the Arusha Wazee Sports Club during their recently held general elections have unanimously retained Danford Mpumilwa a veteran journalist as their Chairman for the coming three years.

His term will end in 2013. The members also elected Aatsa Atogo from Cameroon, Vice-Chairman; Ally Mamuya (Tanzania), Secretary; Saidou Guindo (Mali), Assistant Secretary; Ernest Olomi (Tanzania), Treasurer; Ms Sophia Burra (Tanzania), Assistant Treasurer; Emmanuel Ntoko (Cameroon), Public Relations and Liaison Officer and Francis Kiwanga (Tanzania ), Legal Advisor.

The Wazee Club, which has more than 150 members, brings together diplomats, academicians, businessmen, government and non-government organisations as well as company executives, who are in the middle or advanced ages for sporting activities in Arusha.
 
Saturday December 04, 2010 Sports
Dodoma to host cycling race
By DAILY NEWS Reporter, 1st December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 78

DODOMA region will on this Saturday host a bicycle race as part of activities to mark the World AIDS Day (WAD), which is marked on December 1st every year.

The event organised by Massimo Cycling Club of Dodoma (MCC), is expected to attract participants from Dodoma, Mwanza, Shinyanga, Arusha, Zanzibar, Tanga and Dar es Salaam.

Team leader Louis Musisi said in a statement that: "MCC is committed in the fight against HIV-AIDS and organises every year a competition and related awareness activities."

He said the race for men will start from the Jamhuri Stadium at 07:00 a.m through Dar es Salaam road, up to Mbande and back. The race he said, will cover 135 kilometres.

Musisi said the race for women will start at Jamhuri Stadium at 07:15 am through Dar es Salaam road, up to Chamwino and back and will cover 60 km.

He said the finishing point will be in front of the Parliament. First prize for men is 250,000/-. The same amount will be awarded to women.

The team leader said registration of participants will start at Jamhuri Stadium tomorrow.

The event is sponsored by DSI – quality tyres, A-SANTE drinking water, Yashnas Mini Supermarket, KMJ Telecommunications Ltd, Victory Bookshop and Dodoma Travel Café
 
Saturday December 04, 2010 Sports
Poulsen lauds 12th player for victory
By DAILY NEWS Reporter, 1st December 2010 @ 12:00, Total Comments: 1, Hits: 399

KILIMANJARO Stars' head coach, Jan Poulsen applauded local football fans for the support shown during the 3-0 victory over Somalia at the National Stadium in Dar es Salaam on Tuesday.

"The crowd was fantastic today; they were truly fantastic in the way they got behind us," Poulsen told the post match press conference.

"I come from Denmark where everybody knows that playing in Copenhagen is very, very difficult because everybody is behind the team," he added.

Thousands of enthusiastic fans flocked at the 60,000-seater arena and were strongly backing the home team, inspiring Stars to the crucial victory over the Horn-of-Africa nation.

Cecafa's decision to make entry free after they experienced a low turnout of fans in the opening three days effective from the Tuesday games, with the aim of restoring the excitements of the event, paid dividends as fans almost packed the venue to the brim.

Henry Joseph, John Boco and Nurdin Bakari scored a goal apiece to give the home team a perfect response to a 1-0 defeat against Zambia in their opening match last Saturday.

The win revived Kilimanjaro Stars hopes of reaching the quarterfinals of the regional championship and the Danish tactician believes victory would restore confidence in his squad as they prepare to face Burundi in a must win match on Saturday.

"I thought we could have scored at least as many goals, but I am very satisfied with the attitude and commitment of my players, but I think there is a room for improvement," said Poulsen.

Poulsen's side rest third in their group on three points, one behind first and second placed Zambia and Burundi respectively.

They must beat Burundi in their last match to seal book their place in the quarterfinals. Pouslen apparently suggested that he would field a team that he believes can get good results, "You always put your team and try to win, but whether you succeed or not, you never know."

His Somali counterpart Yousuf Adam conceded that they were lucky not to concede more goals.

"We're very lucky today, I think we could have lost by bigger a margin," Adam admitted. He said his team played with determination but said, the problems that dogged them since their arrival here could not help them play better.

The Somali team only arrived from their Djibouti base on Saturday night, hours after their scheduled match against Burundi.

They were thus forced to play on Sunday afternoon.

A day later, the team's bus was involved in a road accident on the way to training leaving three players injured.

The two-week tournament sponsored by East African Breweries through its Tusker brand continues today with Group C matches that will see defending champions Uganda play Malawi at 2pm and Kenya take on Ethiopia at 4pm.

Uganda beat Ethiopia 2-1 while Malawi defeated Kenya 3-2 in their opening matches on Monday.
 
Saturday December 04, 2010 Sports
Tanzania, Norway to enhance social-cultural ties


By DAILY NEWS Reporter, 30th November 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 114

AS Tanzania and Norway celebrate over 40 years of partnership, the Norwegian government has promised on further collaboration in socio-cultural co-operation with Tanzanians.

Norwegian Ambassador Designate Ingunn Klepsvik told reporters in Dar es Salaam that her country will continue to partner with Tanzania in all areas, saying the socio-cultural ties were unbreakable.

The Ambassador Designate was speaking at the Msasani Lutheran Church during the just concluded Christmas Gospel Concert that featured lead gospel group Kijitonyama Upendo Choir and the Garness Gospel Group from Oslo Gospel Choir, Norway.

Gospel revelers in their tens, including the US Ambassador to Tanzania Alfonso Lenhardt attended the two-hour fascinating gospel music feat that extended to the St Peter's Church.

There were hearty claps and ululations from the congregation after every presentation, but the biggest attraction was when the two groups hit a popular hit ‘Oh Holy Night', where everybody in the packed Msasani Church hummed along.

More fascination came when the two groups interactively performed in different languages with the visiting twin Norwegian sisters Ingelin and Hildegunn Reigstad stealing the show owing to their surprise mastery of the Swahili hits on display.

The Norwegian Embassy supports three main cultural projects in Tanzania namely Tanzania Culture Trust Fund (Mfuko wa Utamaduni), the Dhow Countries Music Academy at Zanzibar and the Norway-Tanzania Project, as well as support to some small projects, such as the ‘Sauti za Busara' Festival held in Zanzibar.

This year's support to the Christmas Gospel Concert, where the embassy collaborated with Msasani Lutheran Church, marked a huge milestone in the long and undying partnership.

In 2009, the embassy hosted a successful Food and Dance Festival that drew artists from Norway, Mozambique and Tanzania to a shared stage of thrilling performance.

The Ambassador Designate said: "We are happy that our strong collaboration has extended to gospel music.

This is basically coined to strengthen our over 40 years of partnership. We are, however, exploring areas for more cultural collaboration."
 
Saturday December 04, 2010 Sports
Seven locals for zonal ITF tennis championships 2011





By PAUL JOHN, 2nd December 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 41

SEVEN junior tennis athletes have been named to make up the national team that will compete for Tanzania in the 2011 edition of ITF / CAT East African Tennis Championships, slated for Bujumbura, Burundi early next year.

The seven include three players from Dar es Salaam namely Sarah Bura, John Njau and Salum Msafiri while the rest are Arusha based Shabani Ibrahim, Tumaini Martin, Edna John and Lydia Lucas.

Tanzania Tennis Association (TTA) Secretary General Inger Njau told the ‘Daily News' that players from nine countries will be lining up for the zonal championship and that the players' discipline and level of respective game were highly considered in the selection for the event that will see top players qualify for next year's African Junior Championships (AJC).

Inger said the named players have expressed good attitude during local events over the year and their level of play was more than impressive considering the available resources and infrastructure.

The secretary general said: "Good attitude and the players' self discipline were highly considered. The intention was to send the most disciplined players for regional events, considering the fact that participants will be competing for a place in the African Junior Championships.The named players have been improving in their level of play and we are confident for a good performance on their visit to Burundi for the 2011 AJC qualifier." Send your Comments First name : Last Name: Email: Your comment: Total Comments on the above stories (0)
 
Saturday December 04, 2010 Sports
Arusha Gymkhana aim to develop snooker


By DAILY NEWS Reporter, 30th November 2010 @ 12:00, Total Comments: 0, Hits: 83

THE Arusha Gymkhana Club has organised a fund-raising dance on Saturday, aimed at mount up resources for the development of snookers section at the club.

The Snooker Captain at the club Shakir Bandali said on Monday that the night dubbed ‘Snooker Night' would see people enjoying music by one of the regions top DJ Satty.

During the day, he said, dinner will be on sale with choices of Indian, African and Chinese cuisine.

"All funds raised will be used towards the rehabilitation and movement of the section to the newly developed Club House area," he said.

Bandali said sponsorship in cash or items that can be donated for the silent auctions for the event, whereas the names of all sponsors together with value of items donated will be announced to all members and visitors during the event.

Moreover, he said, companies and institutions with any branding they wish to display during the night have been asked to contact the organizing committee for logistics.
 
Stewart awaweka chini 'Cannavaro', Morris Saturday, 27 November 2010 21:58

Jessca Nangawe
KOCHA wa timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes, Hall Stewart ameanza kuweka mikakati ya kuujenga ukuta wake, amewaita mabeki Nadir Haroub 'Cannavaro' na Aggrey Morris na kuwaeleza nini cha kufanya.

Zanzibar Heroes, moja ya timu za Tanzania, itakuwa na kibarua leo kwa itakapoivaa Sudan katika mchezo wa Kundi B wa michuano hiyo.

Stewart alisema: "Nataka muhakikishe mnakabiliana na wapinzani wenu mpaka hatua ya mwisho...kushinda mchezo wa kesho (leo) ni muhimu, najua tuko kundi gumu hasa ukiangalia timu kama Ivory Coast, tutapigana lakini hawa watatupa wakati mgumu kidogo."

Cannavaro na Morris ni mabeki wa kati tegemeo la timu hiyo. Cannavaro aliyekuwa akimsubiri Victor Costa, ndiye mkoba wa Taifa Stars aliyemnyang'anya namba beki huyo wa zamani wa Simba na kumpoteza kabisa katika medani ya soka nchini.

Stewart alisema licha ya kuwa ni mara yake ya kwanza kuwa na timu katika michuano hiyo, hana hofu na kuwataka vijana wake kuwa na ushirikiano wa kutosha ili kuanza vyema michuano hiyo.

Alisema pamoja na uchanga wa timu yake katika mashindano makubwa kama hayo lakini anaamini kikosi hicho kikiongozwa na wachezaji wake mahiri kama Cannavaro na Morris kitaweza kushinda mchezo huo wa kwanza na kusonga mbele.

Stewart alisema anatambua ushindani uliopo katika mashindano haya ambayo yanashirikisha nchi mbalimbali za Afrika Mashariki na kati hivyo watatumia vema kuonyesha uwezo wao kwani walijiandaa ili kuhakikisha wanaacha historia nzuri katika michuano hiyo.

"Tunakutana na Sudan natarajia kuwepo kwa ushindani mkubwa,tayari nimepanga kikosi changu kikamilifu dhidi ya wapinzani wetu na jukumu kubwa nimeliacha kwa wachezaji wangu," alisema Stewart. Mbali ya mchezo huo, Somalia na Burundi zitaonyeshana kazi.
 
Somalia yaipa ahueni CECAFA Saturday, 27 November 2010 21:57

Sosthenes Nyoni
KUCHELEWA kwa Somalia na hata kuahirishwa kwa mchezo kati yake na Burundi, kumelipa ahueni Baraza la vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati, CECAFA, kutokana na kutingwa na ratiba ya ufunguzi.

Akizungumza jana asubuhi, Katibu Mkuu wa CECAFA, Nicholaus Musonye alisema kutokufika mapema kwa Somalia kwa upande mwingine kumesaidia kupunguza msongamano wa ratiba. Mechi hiyo iliyokuwa ichezwe jana, sasa itachezwa leo baada ya Somalia kuwasili jana usiku.

Katika taarifa yake, CECAFA ilisema kuwa Somalia ilishindwa kuwasili mapema kama ilivyotarajiwa baada ya kukosa usafiri wa moja kwa moja wa ndege.

"Unajua wale jamaaa hawakai pale Mogadishu kutokana na masuala ya kiusalama na kule walikokuwa hakuna usafiri wa ndege ya moja kwa moja hadi Dar es Salaam, lakini kwa kushirikiana na wadhamini wetu tumelitatua hilo na sasa watatua leo na kesho watacheza,"alisema Musonye

Musonye alisema kuwa hatua ya mchezo huo kuchezwa leo utawasaidia pia kufanikisha ufunguzi wa michuano hiyo kwa ufanisi kwavile siku hiyo kulitarajiwa kuwa na mambo mengi.
 
Kili Stars robo fainali kombe la tusker
Imeandikwa na Mwandishi Wetu; Tarehe: 4th December 2010 @ 23:59 Imesomwa na watu: 948; Jumla ya maoni: 0


12_10_u7rtxj.jpg

Mchezaji wa timu ya Kilimanjaro Stars,Mrisho Ngasa,(kushoto) akimruka Nzeyimana Hussein wa timu ya taifa ya Burundi wakati wa mchezo wa kombe la Chalenji uliochezwa katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam jana. Kilimanjaro ilishinda mabao 2-0. (Picha na Yusuf Badi)


HATIMAYE wawakilishi wa Tanzania Bara kwenye michuano ya Kombe la Chalenji, Kilimanjaro Stars jana walishusha ‘presha' za mashabiki wao baada ya kuifunga Burundi mabao 2-0 na kutinga hatua ya robo fainali za michuano hiyo.

Kili Stars ilipata ushindi huo mbele ya maelfu ya mashabiki waliojaa uwanjani ambapo ilionesha soka safi tofauti na ilivyokuwa katika mechi zake mbili zilizopita.

Aidha, shabiki mmoja alijeruhiwa baada ya kutokea vurugu zilizotokana na mashabiki waliokuwa wanalazimisha kuingia uwanjani huku kukiwa kumejaa.

Kwa vurugu hizo, moja ya mageti ya kuingilia uwanjani hapo lilivunjika. Shujaa aliyefunga mabao hayo ya ushindi alikuwa Nurdin Bakari ambapo sasa amefikisha mabao matatu katika michuano hiyo baada ya kufunga bao moja katika ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Somalia.

Bakari alifunga bao la kwanza katika dakika ya 20 baada ya kuunganisha krosi ya Mrisho Ngassa kabla ya kuujaza mpira wavuni kwa kichwa.

Kuingia kwa bao hilo kuliamsha ari kwa wachezaji wa Kili Stars ambapo sasa walianza kulishambulia lango la Burundi mithili ya nyuki, lakini juhudi zao hazikuzaa matunda kwani ilibidi wasubiri hadi kipindi cha pili kuandika bao la ushindi.

Bakari alifunga bao hilo la pili katika dakika ya 75 baada ya kuunganisha pasi ya Shadrack Nsajigwa iliyotokana na kazi nzuri ya Ngassa ambapo mpira ulimgonga beki wa Burundi begani kabla ya kumfikia mfungaji aliyefunga bao kwa kichwa tena.

Matokeo hayo yanaifanya Kilimanjaro Stars kushika nafasi ya pili katika kundi A ikiwa na pointi sita nyuma ya Zambia inayoongoza ikiwa na pointi saba.

Wapinzani wa Kili Stars na Zambia ‘Chipolopolo' kwenye robo fainali watajulikana leo baada ya mechi ya mwisho ya kundi hilo kati ya Ivory Coast na Sudan.

Kwa mujibu wa ratiba ya Cecafa, mshindi wa pili wa kundi A ambaye ni Kilimanjaro atacheza na mshindi wa pili wa kundi B, hivyo endapo Ivory Coast yenye pointi tatu ikishinda leo itafikisha Pointi sita na kufanya Kilimanjaro Stars kucheza na Rwanda kwa vile timu hiyo ‘Amavubi' itakuwa nafasi ya pili ikiwa na pointi tano.

Na endapo Ivory Coast ikifungwa na Sudan, Stars itacheza na Zanzibar kwa vile ndio itakayoshika nafasi ya pili kundi B kwa kuwa na pointi nne.

Akizungumza baada ya mechi hiyo, Kocha Mkuu wa Stars Jan Poulsen alisema amefurahi kupata ushindi na kuwapongeza wachezaji wake kwa kucheza vizuri hasa katika kipindi cha kwanza na kuongezeka wingi wa mashabiki kulichangia kwa kiasi kikubwa ushindi wa timu yake.

Naye kocha msaidizi wa Burundi, Niyongabo Amars alisema timu yake ilicheza vizuri lakini makosa kidogo yaliyofanywa na wachezaji wake ndiyo yaliyowagharimu.

Mechi nyingine iliyochezwa mapema jana ni kati ya Malawi na Ethiopia ambapo zilitoka sare ya bao 1-1.

Leo mbali na mechi ya Ivory Coast na Sudan, pia bingwa mtetezi Uganda inatarajiwa kucheza na Kenya kama itasitisha mgomo. Kenya ilitangaza kujitoa kwenye michuano hiyo kutokana na ukata.
 
Msanii aumwa na nyoka wake

Imeandikwa na John Nditi, Morogoro; Tarehe: 4th December 2010 @ 23:55 Imesomwa na watu: 265;


NYOKA si rafiki wa binadamu, hali hiyo imejidhihirisha kwa Msanii wa Kikundi cha Sanaa cha Towero cha Manispaa ya Morogoro, Rajabu Athuman ( 24) ' Roja' baada ya kuumwa na nyoka wake aina ya chatu aliyekuwa akicheza naye wakati wa maonesho ya sanaa za ngoma za utamaduni wa asili ya makabila mbalimbali kwenye mahafali ya 17 ya Wahitimu wa Ualimu wa Ufundi Stadi ( VETA ) Morogoro.

Tukio la kuumwa na nyoka wanaocheza nao mbali na kujitokeza siku za nyuma, hali hiyo imejitokeza juzi wakati msanii huyo alipokumbwa na dhahama hiyo wakati wa kuhitimisha onesho la kikundi hicho mbele ya mgeni rasmi Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo.

Naibu Waziri huyo alikuwa mjini hapa kuhudhuria mahafali ya 17 ya wahitimu wa Ualimu wa Ufundi Stadi ngazi ya Stashahada na cheti kutoka Chuo cha Ualimu Veta Morogoro sambamba na viongozi wengine wa Serikali.

Bila kutarajiwa na wengi msanii huyo mzaliwa wa Kijiji cha Matuli Tarafa ya Ngerengere na makazi yake kuwepo Manispaa ya Morogoro, aliumwa na nyoka huyo muda mfupi kabla ya kumaliza kuonesha umahiri wa kucheza na naye wakati akicheza ngoma ya asili ya makabila ya watanzania.

Baada ya kuumwa na nyoka huyo wasanii wenzake walimchukua nyoka huyo na kumhifadhi kwenye kisanduku maalumu na kuanza kumtibia mwenzao kwa kutumia dawa za asili zinazosadikika kuua sumu ya nyoka.

"Ni kweli niliumwa na nyoka wangu muda mfupi kabla ya kumaliza onesho mbele ya mgeni rasmi…lakini nimejitibia kwa kutumia dawa zetu za kuua sumu ya nyoka…hata hivyo huyu Chatu hana sumu, licha ya kutomwondoa meno yake," alisema.

Alisema kuumwa na nyoka akiwa mchezoni haikuwa ni mara yake ya kwanza kwa vile siku kadhaa za nyuma aliwahi pia kuumwa na nyoka akiwa kwenye maonesho ya burudani za sanaa ya kucheza ngoma za makabila ya Tanzania.

"Leo (juzi) nyoka ameniuma sehemu ya nyuma ya kiganja cha mkono wangu wa kushoto…na kitendo hiki watu wengi hawakuweza kukiona ila mimi mwenyewe na wasanii wenzangu kwa vile dalili waliziona kwenye uchezaji wangu," alisema Athumani.

Naye Msanii wa Kikundi hicho, Saidi Omary alisema kuwa aliwahi kuumwa sehemu ya karibu na sikio lake la kushoto wakati akicheza na nyoka kwenye moja ya onesho lililofanyika mjini hapa.

Kwa mujibu wa msanii huyo, kikundi chao kimekuwa kikijihusisha kwa baadhi ya wasani wake kucheza na nyoka ambapo kwa zaidi ya miaka mitano wamekuwa wakiwaburudisha wananchi kwa kutumia nyoka hasa chatu.

Alisema nyoka hao wanawapata maeneo ya porini na mashambani kwa kushirikisha wakazi wa maeneo hayo kwa kuwaonesha mashimo yao na hatimaye kuwatega kwa kutumia unga maalumu.

Alisema kuwa baada ya kuwakamata hasa nyoka aina chatu ambaye hana sumu kali wanawatunza na kufanya nao mazoezi ili kuwazoea kabla ya kushiriki nao kwenye maonesho mbalimbali.

Baadhi ya wananchi walihudhuria mahafali hayo wakizungumzia kitendo cha wasanii hao kucheza na nyoka ambaye hajaondolewa meno yake kuwa ni cha hatari mbele ya watu endapo atamuuma mtu mwingine.

Hivyo ameiomba mamlaka husika kuandaa utaratibu maalumu utakaowaongoza wasanii wanaocheza na nyoka kuhakikisha wanachukua tahadhari kwa watu wengine iwapo nyoka hao kuwateleza wasanii na kuwauma watu.
 
Waombwa kuendeleza Taekwondo kwa watoto
Imeandikwa na Evance Ng'ingo; Tarehe: 4th December 2010 @ 23:30 Imesomwa na watu: 32;

WAZAZI, walezi, serikali pamoja na jamii kwa ujumla wameombwa kuwaendeleza watoto wao katika mchezo wa Taekwondo kwa maendeleo wa afya zao.

Wito huo ulitolewa na Athuman Musa ambaye ni mshindi wa medali ya shaba katika mchezo wa Taekwondo alipozungumza na HABARILEO muda mfupi baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akitokea Libya alipokwenda kushiriki mashindano ya dunia ya mchezo huo.

Musa alisema kutokana na mchango wa familia pamoja na uongozi wa chama cha Taekwondo nchini amefanikiwa kupata ushindi huo ambao ni wa faida kwa taifa.

Musa alisema kuwa alifanikiwa kufika katika hatua ya nusu fainali ambapo katika nchi 15 zilizocheza hakuna wachezaji wengine walishindwa kufikia hatua hiyo muhimu.

Musa alicheza katika hatua ya uzito wa kilo 35 ambapo alishindwa nusu fainali na mchezaji kutoka nchini Tunisia ambaye ndiye aliibuka mshindi.

Kocha wa Musa, Richard Kitolo aliliambia gazeti hili kuwa nyota ya Musa ilianza kung'ara katika michuano ya kitaifa ambayo iliendeshwa na chama hicho mwaka huu ambapo watoto wengi walishiriki na kuchujwa.

Alisema kuwa Musa alionesha uwezo wa juu katika kumudu mchezo huo ambapo aliwachakaza washindani wake bila ya huruma mpaka kufikia hatua ya nusu fainali.

Katika hatua nyingine, Kitolo alisema kuwa mchezaji mwingine Marik Juma alishindwa kupigana kutokana na kuchelewa kuwasili nchini Libya.

Alisema kuwa Juma alitakiwa kucheza mchezo huo wa Taekwondo kwa uzito wa kilo 59 ambapo kutokana na kuchelewa alikuta wenzake wa uzito wake wameshacheza.

" Ndio kama nilivyosema kuwa iwapo tungewahi basi tungecheza na huyu kijana ndio angekuja na medali ya dhahabu kabisa kwa kuwa ninamwamini sana, ila ndio kushindwa kuwahi basi tumekuta kila kitu kimeshafanyika," alisema Kitolo.
 
Pinda ataka siku ya Mtanzania Kitaifa
Imeandikwa na Mwandishi Maalumu; Tarehe: 4th December 2010 @ 23:00 Imesomwa na watu: 84;

WAZIRI Mkuu Mizengo Pinda ameiagiza Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo kuanzisha Siku ya Mtanzania kuadhimisha mambo mbalimbali ya kijamii katika ngazi ya Wilaya hadi ya Taifa ili kuuenzi utamaduni wa nchi yetu.

Alikuwa akizungumza katika sherehe za miaka 10 ya Usiku wa Mtanzania zilizoandaliwa na Hoteli ya Peacock ya Dar es Salaam kwenye viwanja vya Karimjee juzi.

Usiku wa Mtanzania ya Chakula hufanywa na Hoteli ya Peacock kila Jumatano kwa kuandaa na kuuza vyakula vya asili vinavyopikwa kwa kutumia vyombo na majengo ya kisasa na wataalamu waliosomea mapishi, tangu mwaka 2000.

Waziri Mkuu alisema kuna haja ya kuiadhimisha Siku ya Mtanzania kiwilaya, kimkoa na kitaifa na kupanua maudhui yake ili kuhusisha masuala mengine ya kijamii na burudani kama vile mavazi, ngoma, utawala na harusi.

"Bwana Mfugale (Joseph, Mkurugenzi Mkuu wa Peacock) amebuni Usiku wa Mtanzania wa Chakula… Natoa wito kwa Watanzania wengine kufuata nyayo na ningependa wenzagu Serikalini wafikirie namna ya kufanya Siku ya Mtanzania kitaifa katika maeneo haya yote," alisema.

Katika sherehe hiyo, viliandaliwa vyakula vya asili kwa kanda za mikoa mbalimbali nchini. Kulikuwa pia na burudani mbalimbali ikiwa pamoja na muziki wa asili, wa dansi na sarakasi.

Miongoni mwa viongozi walioshiriki ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Emmanuel Nchimbi na Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo na baadhi ya Wabunge.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom