Miaka Miwili ya Maajabu kwa CCM !

Miaka Miwili ya Maajabu kwa CCM !

mathcom

JF-Expert Member
Joined
Oct 13, 2012
Posts
1,396
Reaction score
519
Habari za jioni wanaJF,

Ikiwa imebaki kama miaka miwili kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, chama cha CCM inabidi
kituoneshe maajabu kwa kuhakikisha kwamba haya mambo nitakayo yataja hapa chini yanafanyika;

1. Kuwakamata na kuwachukulia hatua watuhumiwa wote wa Ufisadi bila kubagua au kupepesa midomo, adhabu kali ikiwa ni pamoja na kuwafilisi wale watakao bainika na hatia.

2. Kuwafuatilia na kuwakamata watajwa wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya (pamoja na mtandao mzima) kuwachunguza na kuwahukumu ipasavyo, huku hukumu zao zikitangazwa mbele ya Umma.

3. Kuwakamata na kuwahukumu wanaosafirisha nyara za serikali na vitendo vingine vyote vya ujangili.

4. Kupambana na wakwepa kodi wote ambao wanalitia hasara taifa huku wakizidi kuwaumiza wananchi.

Ikiwa kama haya yanaonekana ni ndoto kwa CCM nina imani kwamba yanawezekana tena kwa urahisi tu kwa baadhi ya vyama vya upinzani hasa hasa CHADEMA

MY TAKE: Kama CCM bado inahitaji ridhaa ya wananchi, basi tunaiomba ipambane na changamoto hizi

Jee ni kweli yatatokea..
 
Tukuambie mara ngapi kuwa tumeshindwa???tumeshawaambia wanajeshi wetu wawapige,wawabake,wawatandike mabomu nk!!tuseme bado tu hamuoni kuwa tunafanya kazi??basi subirini kijana wetu wa kazi @mwigulu atoke mafunzoni mutatuelewa tu!!tumewngoa kucha,meno,tumewaonyeshea mfano kwa mwangosi lakini bado tu mnatukomalia,sasa ngojeni tu mtatuelewa.
 
CCM haipo tena jamani,lazima muelewe hivyo.Tumeshawashtukia kwani hata wakifanya hivyo baada ya uchaguzi mtindo utakuwa ni ule ule.So me naona wakae tu pembeni

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Haiwezi tenda majaabu hayo hata siku moja,,maana kufanya hivyo ni sawa na kuangamiza nyoka shimoni kwa maji ya moto ingali umejificha ndani ya shimo hilo..
Mhimu kwao ni kukubali kupumzika ili watendewe iwapasavyo.
 
CCM haipo tena jamani,lazima muelewe hivyo.Tumeshawashtukia kwani hata wakifanya hivyo baada ya uchaguzi mtindo utakuwa ni ule ule.So me naona wakae tu pembeni

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
Wakiweza haya kwakweli tuseme za ukweli wana haki yakuongezewa mda, na itakua wameonesha ujasiri ule ambao watanzania wanautaka. Ngoja wazifanyie kazi hizi changamoto kwanza..!!
 
Haiwezi tenda majaabu hayo hata siku moja,,maana kufanya hivyo ni sawa na kuangamiza nyoka shimoni kwa maji ya moto ingali umejificha ndani ya shimo hilo..
Mhimu kwao ni kukubali kupumzika ili watendewe iwapasavyo.
Tuseme wamikia kiwacho hicho mkuu. Kwa nini tusiwapeni mda na msaada stahili kwanza..!!
 
Habari za jioni wanaJF,

Ikiwa imebaki kama miaka miwili kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, chama cha CCM inabidi
kituoneshe maajabu kwa kuhakikisha kwamba haya mambo nitakayo yataja hapa chini yanafanyika;

1. Kuwakamata na kuwachukulia hatua watuhumiwa wote wa Ufisadi bila kubagua au kupepesa midomo, adhabu kali ikiwa ni pamoja na kuwafilisi wale watakao bainika na hatia.

2. Kuwafuatilia na kuwakamata watajwa wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya (pamoja na mtandao mzima) kuwachunguza na kuwahukumu ipasavyo, huku hukumu zao zikitangazwa mbele ya Umma.

3. Kuwakamata na kuwahukumu wanaosafirisha nyara za serikali na vitendo vingine vyote vya ujangili.

4. Kupambana na wakwepa kodi wote ambao wanalitia hasara taifa huku wakizidi kuwaumiza wananchi.

Ikiwa kama haya yanaonekana ni ndoto kwa CCM nina imani kwamba yanawezekana tena kwa urahisi tu kwa baadhi ya vyama vya upinzani hasa hasa CHADEMA

MY TAKE: Kama CCM bado inahitaji ridhaa ya wananchi, basi tunaiomba ipambane na changamoto hizi

Jee ni kweli yatatokea..

Umesau
Kuwachukilia hatua polisi wote walioshiriki kuua raia wanaodai haki zao kwa maandamano,
Pia kuwachukulia hatua viongozi wote wa usalama wanaongoa watu kucha na meno kuilinda ccm
 
Kumruhusu ama kumwongezea mtu aliyechoka na kukata tamaa katika shughuli za umma ni kumpa mwanya wa kupora zaidi kwa maslai binafsi,,na kufanya ivyo ni kusaliti jamii yako.
 
Huu ushaur ni mzito kwa hali ilivyo hakuna hata mmoja mwenye ubavu wa kumfyolea mwingne kidole ccm ni ukoo wa panya wote wez,nachelea kusema jambo hli ni gumu sana kwao labda Yesu ashuke.
 
Umesau
Kuwachukilia hatua polisi wote walioshiriki kuua raia wanaodai haki zao kwa maandamano,
Pia kuwachukulia hatua viongozi wote wa usalama wanaongoa watu kucha na meno kuilinda ccm
Mambo ni mengi mkuu, sijui watafanya lipi waache lipi..??
 
Habari za jioni wanaJF,

Ikiwa imebaki kama miaka miwili kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, chama cha CCM inabidi
kituoneshe maajabu kwa kuhakikisha kwamba haya mambo nitakayo yataja hapa chini yanafanyika;

1. Kuwakamata na kuwachukulia hatua watuhumiwa wote wa Ufisadi bila kubagua au kupepesa midomo, adhabu kali ikiwa ni pamoja na kuwafilisi wale watakao bainika na hatia.

2. Kuwafuatilia na kuwakamata watajwa wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya (pamoja na mtandao mzima) kuwachunguza na kuwahukumu ipasavyo, huku hukumu zao zikitangazwa mbele ya Umma.

3. Kuwakamata na kuwahukumu wanaosafirisha nyara za serikali na vitendo vingine vyote vya ujangili.

4. Kupambana na wakwepa kodi wote ambao wanalitia hasara taifa huku wakizidi kuwaumiza wananchi.

Ikiwa kama haya yanaonekana ni ndoto kwa CCM nina imani kwamba yanawezekana tena kwa urahisi tu kwa baadhi ya vyama vya upinzani hasa hasa CHADEMA

MY TAKE: Kama CCM bado inahitaji ridhaa ya wananchi, basi tunaiomba ipambane na changamoto hizi

Jee ni kweli yatatokea..
Mkamateni kwanza dr slaa wa ufisadi anaofanya ndani ya chama chenu
 
Mkamateni kwanza dr slaa wa ufisadi anaofanya ndani ya chama chenu
Ni moja ya majukumu ya vyombo vya dola inayoongoza nchi kwa kupitia CCM. Sisi tunataka kazi ifanyike, bila kuangalia sura mkuu.
 
Bado wanapiga akili kuleta Meli kubwa kuliko MV Bukoba!!!!!
 
Back
Top Bottom