Miaka 50 ya uhuru hakuna umeme wa uhakika.

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
644
Miaka 50 ya uhuru umeme tu umetushinda!ni laana,ni bahatai mbaya,ni ujinga,ni umaskini wa fikra,ni kupumbazwa au ni kitu gani hiki kinacho sababisha tusherekee miaka 50 ya uhuru wetu bila ya kuwa na vitu vya uhakika?
 
Hatuna maji y ahakika,hatuna umeme wa uhakika,hatuna barabara za uhakika,hatuna chakula cha uhakika,hatuna elimu ya uhakika,
 
Personally sidhani kama nchi hii haina uwezo wa kuwa na Umeme wa UHAKIKA.
Kuna mito kiabao Tanzania ambayo inatiririsha maji 24/7 bila kutumika either kwa kilimo ama kwa umeme. Well wengi wemeshasema kuwa tanesco ni SHAMBA LA BIBI.
Nilishawahi kusoma sehemu flani hivi kwamba ILI NCHI IENDELEE LAZIMA IWE NA UWEZO WA KUJITEGEMEA YENYEWE KWA CHAKULA. Ili linawezekana tu iwapo maji ya mvua, mito yatakuwa yanaelekezwa kwenye mashamba. Leo hii tunalia kuwa hakuna mvua za kutosha while there are rivers flowing freely to the ocean. Kuna hii Slogan ya KILIMO KWANZA, Kilimo kwanza can be possible if and only if tutaweza ku-irrigate mashamba yetu. Benefit zipo nyingi tu za kuwa na taifa lililo na chakula. Moja kati faida hizo ni KIBURI kwa masharti ya kinyonyaji unayopewa na Western countries.
Kuna usemi unasema kwamba ukitaka kumnyonya mtu zaidi basi awe na njaa. S/he will be working for food 1st, na sio kwa maendeleo mengine. Hadi aweze kutoka hapo utakuwa umeshamkamua vya kutosha.
 
Huo umeme jamani:::lakini gharama za umeme zinabebeka? Haya ndo maisha bora? Nguzo moja Tzs800,000-Tzs.1,000,000. Service charge Tzs.400,000. Pesa ya kuhonga maana list ni ndefu ya wateja( Tzs.250,000 i.e. mafundi Tzs.50,000 na meneja miradi Tzs.200,000), pesa ya kumuleta mpimaji wa kukadiria nguzo na braket Tzs.50,000/=. Pesa yako ya kuunganisha ndani Tzs.500,000/=.

Hii ndo TAnzania ya CCM. Tutafika au wajukuu zetu watafika wamechoka sana!!!!!
 
Back
Top Bottom