Mogambi
JF-Expert Member
- May 25, 2012
- 209
- 351
Moja
KIJIJI cha Tung’aine kinapatikana mkoani Mara katika wilaya ya Tarime mpakani kabisa na nchi jirani ya Kenya. Huko unapatikana mto mkubwa unaojulikana kama mto mesani. Ni katika bonde kubwa la mto huo kunapopatikana uwanda mkubwa wenye nyasi zilizo wanda mithili ya zulia zuri ndani ya sebule kubwa ya kisasa.
Aghalabu ni uwanda ambao umeipa wilaya ya Tarime umaarufu wa kitalii, ukivutia watalii wengi kila mwaka.
Machera akiwa na Anastazia walikuwa maeneo hayo kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka. Ulikuwa mwaka uliojaa visa na mikasa, waliona ni stahiki yao kupata mapumziko hayo kujisahaulisha matukio ya mwaka huo yaliyosumbua akili zao. Lakini wahenga walisema baada ya kisa mkasa.Ni kama mwaka huu ulitaka kuwavuta wabaki nao. Matukio ya mwaka huo yaliendelea kuwasakama.
Hali wakiendelea kujisahaulisha yaliyopita, simu ya mkononi ya Machera iliita, namba ngeni ikicheza kwenye kioo cha simu hiyo ya kisasa. Aliipokea na kusikia sauti nzito yenye mikwaruzo, haikuwa sauti ngeni, alishawahi kuisikia hapo awali katika moja ya matukio yaliyokuwa yanasisimua ya mwaka huo.
"Bila shaka hujambo bwana Machera, na sauti yangu naamini umeipata vizuri. Nilikueleza huwezi kucheza na mimi, mimi ni bomu la nuclear. Ulikuwa unaniwinda na sasa ni zamu yangu kukuwinda, tofauti ni kwamba mimi nimekupa tahadhari ili ujue unapambana na nani"
Sauti hiyo ilinyamaza ili kutoa nafasi kwa Machera kutoa maoni yake, sauti iliyowahi kumpa mhadhara juu ya kundi kubwa na hatari la siri. Kundi lililodaiwa kusambaza na kuingiza sumu na maadili potofu katika jamii zote za dunia huku wakielekeza siasa, chumi, na mifumo yote ya kijamii kuwa na mwelekeo waliotaka wao kwa kutumia maneno mazuri mazuri kama vile utandawazi, kwenda na wakati, haki za binadamu na Demokrasia. Kwa kutumia siasa na uchumi kwa msaada wa vyombo vya habari walihamasisha mmomonyoko wa maadili kote duniani.
Watu hao walijikita katika nyadhifa muhimu za uongozi na idara muhimu za dunia yakiwamo mashirika makubwa ya umoja wa mataifa. Kwa nje kundi hilo halikufahamika kwani lilikuwa moja ya makundi kadhaa yaliyofanya mambo yao kwa usiri mkubwa wakiwatumia watu maarufu na wenye ushawishi mkubwa wa kisiasa na kiuchumi ili kupitisha ajenda zao. Kwa njia hiyo kundi hilo lilifanya hila na kuhalalisha mambo haramu huku mambo halali yakiharamishwa bila umma wa dunia kutambua kwa haraka, lakini ikawa ni mambo yaliyokuwa yanatendeka kidogokidogo na hatimaye kuanza kuonekana kama ni mambo ya kawaida. Mwisho wa siku ikawa ni mambo yanayodaiwa kwa kigezo cha haki za binadamu, mataifa makubwa yaliyotawala kwa kanuni mahsusi za kundi hilo, yakashadadia na kuyafanya mataifa tegemezi yafanye uhalali wa mambo hayo kwa kigezo cha misaada.
Kwa ubabe huo wa mataifa makubwa dunia ikawa ni ishara kubwa ya utawala wa uovu usiozingatia adili. Kundi hilo likitazama vitu hivyo kama chanzo cha nuru na utajiri wa maarifa batili waliyotengeneza na kuipumbaza dunia kwa hayo. Wakiyaita Uhuru, usawa wa kijinsia na haki za binadamu.
Katika tawala za namna hiyo, mambo yaliyohusika na usafi wa mwili, roho na nafsi yalionekana kupitwa na wakati. Kundi hilo likatumia uwezo wa kifedha, ushawishi wa kisiasa na kupitia sayansi iliyopingana na uwepo wa Mungu, kuhalalisha kila aina ya uchafu katika maisha ya wanadamu, wengi wakikana uwepo wa Mungu kwa kuamini maneno na propaganda za wanasayansi wao waliowatengenezea umaarufu ulimwenguni kote!
Dini za ulimwengu, sasa zilipata wahubiri waliohalalisha maovu na kuyaweka wazi. Wahubiri wengi wakiwa ni wanachama halali wa kundi hilo huku wakikusanya makundi makubwa ya wafuasi. Mafundisho yao yakiwa ni juu ya mafanikio na juu ya kuamini uwezo wao binafsi, kwa sehemu wakiwaaminisha watu kwamba Mungu anajua udhaifu wao na ni juu yao kuamua lipi ni baya na lipi ni jema, na kwamba kama dhamiri na nafsi zao ziliona sawa, basi hakukuwa na ubaya.
Viongozi hao walifanya miujiza mikubwa kwa kutumia nguvu za giza na watu waliwafuata wakiamini ni uweza wa Mungu. Waliamini, kwani tayari kundi hilo lilikwisha waandaa kisaikolojia kuamini katika miiujiza. Wengine wakijitangaza hadharani kuwa wao ni mashoga na kutangazia ulimwengu kwamba huo ni aina mpya ya upendo miongoni mwa wanadamu.
Waliosimama kupinga walibezwa na kuulizwa wao ni nani kuwahukumu wenzao. Dunia sasa ilikuwa inazidi kuchanganyikiwa na wanadamu waliona ni kawaida tu. Uovu huo haukuishia hapo bali zinaa ilionekana ni kitu cha muhimu huku ikihamasishwa kwa kutumia vyombo vya habari vilivyofanya wanadamu waone zinaa ni suala la kawaida na la kifahari.
Sasa haikuwa ajabu tena kusikia kwamba kaka na dada wana mahusiano ya kimapenzi au mzazi na mwanae. Ile enzi ya sodoma ilikuwa imerejea, na wala haikuwa ajabu pale wanadamu waliposema ni haki yao kuishi na wanyama wawapendao kama wanandoa.
Mataifa yaliyopingana na uozo huo yalitengenezewa ajenda na sababu, yakavamiwa na kwa lazima yakaingiliwa kwa kigezo cha Demokrasia.
Sasa Machera aliitambua vema sauti ile, ilikuwa sauti ya The Don, Yule waziri aliyetoroka baada ya kutiwa mbaroni kwa mauaji ya kijana aliyejulikana kwa jina la Elinisa. Akakumbuka maneno aliyatamka baada ya kumtia mbaroni, ‘nina uwezo wa kuishi kokote kule duniani. Kokote kuliko na ushawishi wetu’ na sasa alikuwa amelithibitisha hilo.
The Don Alikuwa anaongea naye kutoka Marekani akimweleza kuchukua tahadhari kwani alikuwa anamwinda.
"Tahadhari? Kama wewe ni mtu makini bila shaka ungekuwa unafahamu kuwa mara zote nakuwa makini na wala siambiwi muda gani nichukue tahadhari. Ninakufahamu vema na watu unaowafanyia kazi, daima nipo tayari kupambana na ninyi hadi kufa". Machera alimjibu Don.
"Ha ha ha, kijana matata sana wewe. Sayansi, siasa, uchumi na hata dini za dunia zipo upande wangu, huwezi kuzima moto huu. Kwa taarifa yako tu hapo ulipo nina watu wangu wanaokutazama, kila unachofanya tunapata taarifa, kwakweli upo ndani ya box kijana. Hebu fikiri, Mimi nipo Marekani, lakini najua kwamba hapo ulipo ni chini ya kivuli kando ya mto na upo na msichana mweupe ambaye amevalia miwani, suruali ya jeans, buti za cowgirl, kofia ya sobrero na fulana ya mikono mirefu, tazama unageuka kumwangalia. Nadhani umethibitisha."
Machera alibaki kimya, kichwani mwake kulikuwa na wasiwasi.
‘Ina maana hawa watu wananitazama hapa nilipo na ninachofanya?' Wakati akitafakari hayo sauti ya The Don Ikasikika tena masikioni mwake.
"Najua unajiuliza vipi nimefahamu hayo, usipate shida, ni teknolojia. Kwa kweli ni teknolojia ambayo sasa imeanza kutumika huku Marekani na tunatarajia kuingiza Afrika hivi karibuni na Tanzania kwa upendeleo itakuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa kuipata na kuifanyia majaribio. Inaitwa microchip technology. Kazi yake ni kutuwezesha kumonita akili za walimwengu ili kuondoa dhana za kufikiri kwa ufasaha. Tunajua kwamba tumefanikiwa kwa kiwango kutengeneza akili tegemezi kwa watu wengi na nchi nyingi duniani kupitia mitandao na filamu, lakini hakuna ubishi kwamba hii programu itakuwa thabiti zaidi kwa sababu ina uwezo wa kutawala mfumo wa fikra wa mtu bila yeye mwenyewe kujua, hivyo inakuwa inarahisisha programu hii kuchakachua uwezo wa kufikiri wa mtu na kumpa machaguo ya kutekeleza amri za Komputa zetu.
“Kwa maana nyingine ni kwamba chip hiyo inaruhusu computer zetu kufanya asilimia arobaini na tano ya maamuzi ya huyo mtu kwa kuulazimisha ubongo wake kufanya hivyo. Kama roboti vile. Na nimeona vema nikushirikishe hili kwani naamini vita unayopigana, ni unapigana na wewe mwenyewe. Kwa taarifa tu, kadri unavyoendelea kunisikiliza ndivyo tunavyozidi kuuvamia na kuteketeza baadhi ya mafaili ya ubongo wako."
The Don alimaliza kuongea kwa kicheko cha dhihaka. Machera akajikuta anadondosha simu toka sikioni mwake huku akishindwa kutafakari kwa muda. Mara akaisikia tena sauti ya The Don ikitamka kwa mwangwi kichwani mwake ‘unaona, hata bila simu tayari tunaweza kuwasiliana kwani ubongo wako kwa asilimia kadhaa ni mali yetu. Tutazidi kuwasiliana kijana, jiangalie sana’
Machera alinyanyuka. Kwa muda sasa Anastazia alikuwa akimwangalia kwa wasiwasi. Kadri muda ulivyozidi kusonga mbele Ana aligundua kuwa mpenzi wake huyo hakuwa sawa. Alimjua vema, haikuwahi kutokea Machera apate wasiwasi mkubwa hivyo kwa ajili ya vitisho vya wahalifu, siku zote kuna namna ambayo aliweza kuwashinda. Lakini leo…. Haikuwa kawaida. Kwa vyovyote vile, chochote alichosikia kilikuwa na kishindo kikubwa sana.
Ana alimsogelea na kumkumbatia kama mama anayejaribu kumtoa wasiwasi mwanae kipenzi, halafu kwa sauti tulivu ya kusema usijali mwanangu mama yako niko hapa kukulinda, akatamka;
"Usiumie kichwa mpenzi, chochote ulichosikia ni hila tu, hakuna jipya ni mbinu za kimafia tu ili unyong’onyee upishe wafanye mambo yao. Usiwaruhusu watuharibie muda wetu wa kufurahia penzi letu."
Machera alimtazama binti huyo mrembo kisha akasema
"Ningempata wapi mwanamke anayenifaa zaidi yako mpenzi? Si tu nina bahati, bali nimejaaliwa msaidizi hasa aliyetoka katika mbavu zangu. Naamini ulichosema ni pointi ya msingi kabisa, ya nini watuharibie fursa yetu ya kufurahia maisha, potelea mbali, nitadili nalo baadae" Alimaliza kuongea na kujaribu kumbusu mrembo wake, lakini Anastazia akamzuia kwa kidole chake cha pili baada ya gumba kwa kukiweka mshazari midomoni kwa kijana huyo na kusema;
"Sema tutadili nalo baadaye! au unadhamiria kunificha ulichoambiwa kwenye simu?"
"La hasha kichuna wangu, nisipokueleza wewe nitamweleza nani anayenifahamu vizuri zaidi yako?" Machera alijishaua na hapo akapokea busu mwororo toka kwa mrembo huyo.
Kwa pamoja walinyanyuka huku wameshikana viunoni na kumwelekea mwana punda aliyekuwa anapura majani pembeni yao. Baadae kidogo walionekana wakiwa juu ya mgongo wa mwanapunda Yule wakishuka bondeni kwenye mto mahali penye kina kirefu, mikononi wakiwa na ndoano zao zilizozamishwa kwenye maji tulivu ya mto mesani.
Mara Simu ikaita tena, mapigo ya moyo wake yakadunda kwa kasi mara mbili ya kawaida.
Hofu!
Hofu!
Hofu ya kisichojulikana ikammendea na kuutikisa mfumo wake wa fahamu, kidogo Simu idondoke mikononi mwake kwa kale kajasho ka kihoro kalikototesha viganja vyake. Ikawa hata kuinyanyua Simu yake kuiweka sikioni au basi kuitazama, ni changamoto asiyoelewa nini maana yake. Hapo, Machera akajitia ujasiri, ujasiri wa bandia kwani mapigo ya moyo wake yalieleza kitu tofauti.
Naam, sauti ya Anastazia ikamzindua toka kwenye kimuhemuhe hicho, sauti hiyo ikamkumbusha yeye ni Nani, mpelelezi maarufu nchini, mtu aliyetegemewa na taifa kwenye masuala nyeti yaliyohitaji akili na ujasiri, vitu ambavyo alijaliwa.
"Mpenzi, hiyo Simu vipi? Hujaisikia?"
Sauti laini, nyororo na tamu. Sauti iliyomkumbusha ni mwanaume tegemewa wa mwanamke huyu mrembo.
"Oh, aisee sijui Nilikuwa nawaza nini!" Akazinduka na kuinyanyua Simu yake na kutazama kioo cha Simu hiyo. Kwenye kioo hicho jina la mtu mwenye mamlaka Kubwa zaidi nchini likaoneka. Mheshimiwa Raisi wa serikali ya mpito, mheshimiwa Sebastian Masebo.
Ile kuona jina la mheshimiwa Sebastian Masebo, moyo wake ukashuka, akajipata akivuta mkupuo wenye ujazo wa hewa na kutoa mkupuo mwingine nje ya mapafu yake kwa ujazo ule ule. Aliweza kupumua vema sasa, mapigo ya moyo wake yakirejea kwenye utaratibu wake wa kawaida.
"Naam mheshimiwa raisi, shikamoo Mkuu." Machera akatamka kwa uchangamfu mwingi.
"Marahabaa kijana wangu, habari za likizo bwana?" Mheshimiwa rais akasaili, sauti yake ikionekana tulivu, ikisadifu mamlaka yake.
Mamlaka ambayo kwa kiasi kikubwa aliyapata kupitia ile kamati teule isiyotambulika kisheria, kamati ya fitna wengine huiita hivyo, ikiaminiwa kuwa ni kamati ambayo ikiwa kinyume chako, hata ukafanya nini basi huwezi kuunda serikali, kinyume chake kikiwa kweli. Ukikubalika, basi unaipata nafasi hiyo.
Tetesi nyingi Mtaani zikidai kamati hiyo haikuteuliwa na mtu ila baba wa taifa. Naam, hata ingawa alikuwa ni marehemu, ilisemekana mzimu wake ulihusika kukiunda kikosi hicho cha kamati, ambapo Kila mteule alikula kiapo cha utii kwa ulinzi wa taifa, kiapo cha uzalendo, uadilifu. Ilisemekana kuwa, waliokengeuka anguko lao halikukawia na walianguka anguko la aibu. Hizo zilikuwa ni simulizi mitaani.
Kwa upande wa pili, ni Machera, Mkuu wa majeshi, Mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa na raisi mstaafu walioratibu mkakati uliompatia mheshimiwa Sebastian Masebo cheo chake kipya cha rais wa serikali ya mpito! Kamati teule!
"Sijambo Mkuu, natumaini hali inaendelea vema nchini. Hongera kwa kazi mpya Mkuu " Machera akajibu na kutia udambwi udambwi wa kumkoga mheshimiwa.
"Ah kijana wangu, uko wapi ndugu yangu, una habari huyu nduli analazimisha kutawala nchi hii kwa remote kutokea huko Marekani? Kijana, nchi inakuhitaji haraka iwezekanavyo. Fanya haraka uje tujue tunadili vipi na huyu adui ambaye sasa anaitangaza nchi kifedhuli, na kujaribu kuwachochea wananchi dhidi ya serikali yao. Ni kama amedhamiria sasa nchi iwe anarchy(isitawalike) na nikiwa kiongozi wa taifa hili siko tayari kuona mpuuzi mmoja anaigeuza Tanzania kama Rwanda ya 94" Mheshimiwa raisi akafunguka. Kwa Kila hali, Machera alihitaji kuondoka kurejea jijini kwa ajili ya kuona namna ya kulinasua taifa dhidi ya Mabruki The Don.
"Naam Mkuu, naelewa hali ilivyo, ni kweli tunahitaji kukaa tufanye maamuzi ya kujinasua kwenye makucha yake. Nitajitahidi ndani ya wiki hii niwe nimerejea jijini!" Machera akajieleza.
"Sio wiki kijana wangu, ninakuhitaji kwenye kikao kesho. Tumeshafanya mpango ambapo utasafiri kwa ndege ya kukodi ya shirika la Mogambi Empire hivi navyoongea ndege hiyo ipo njiani kuja huko na tunatarajia kwamba itaondoka huko SAA 11 alfajiri kurejea huku, ili ushiriki kikao kitakachofanyika SAA tatu asubuhi." Mkuu wa nchi alitoa agizo. Naam, pendekezo la mkubwa kawaida ni amri.
Hii ilikuwa taarifa ya ghafula, lakini ilitoka moja kwa moja kwa Mkuu wa nchi, asingeweza kukataa. Nchi ilimhitaji.
Itaendelea
KIJIJI cha Tung’aine kinapatikana mkoani Mara katika wilaya ya Tarime mpakani kabisa na nchi jirani ya Kenya. Huko unapatikana mto mkubwa unaojulikana kama mto mesani. Ni katika bonde kubwa la mto huo kunapopatikana uwanda mkubwa wenye nyasi zilizo wanda mithili ya zulia zuri ndani ya sebule kubwa ya kisasa.
Aghalabu ni uwanda ambao umeipa wilaya ya Tarime umaarufu wa kitalii, ukivutia watalii wengi kila mwaka.
Machera akiwa na Anastazia walikuwa maeneo hayo kwa mapumziko ya mwisho wa mwaka. Ulikuwa mwaka uliojaa visa na mikasa, waliona ni stahiki yao kupata mapumziko hayo kujisahaulisha matukio ya mwaka huo yaliyosumbua akili zao. Lakini wahenga walisema baada ya kisa mkasa.Ni kama mwaka huu ulitaka kuwavuta wabaki nao. Matukio ya mwaka huo yaliendelea kuwasakama.
Hali wakiendelea kujisahaulisha yaliyopita, simu ya mkononi ya Machera iliita, namba ngeni ikicheza kwenye kioo cha simu hiyo ya kisasa. Aliipokea na kusikia sauti nzito yenye mikwaruzo, haikuwa sauti ngeni, alishawahi kuisikia hapo awali katika moja ya matukio yaliyokuwa yanasisimua ya mwaka huo.
"Bila shaka hujambo bwana Machera, na sauti yangu naamini umeipata vizuri. Nilikueleza huwezi kucheza na mimi, mimi ni bomu la nuclear. Ulikuwa unaniwinda na sasa ni zamu yangu kukuwinda, tofauti ni kwamba mimi nimekupa tahadhari ili ujue unapambana na nani"
Sauti hiyo ilinyamaza ili kutoa nafasi kwa Machera kutoa maoni yake, sauti iliyowahi kumpa mhadhara juu ya kundi kubwa na hatari la siri. Kundi lililodaiwa kusambaza na kuingiza sumu na maadili potofu katika jamii zote za dunia huku wakielekeza siasa, chumi, na mifumo yote ya kijamii kuwa na mwelekeo waliotaka wao kwa kutumia maneno mazuri mazuri kama vile utandawazi, kwenda na wakati, haki za binadamu na Demokrasia. Kwa kutumia siasa na uchumi kwa msaada wa vyombo vya habari walihamasisha mmomonyoko wa maadili kote duniani.
Watu hao walijikita katika nyadhifa muhimu za uongozi na idara muhimu za dunia yakiwamo mashirika makubwa ya umoja wa mataifa. Kwa nje kundi hilo halikufahamika kwani lilikuwa moja ya makundi kadhaa yaliyofanya mambo yao kwa usiri mkubwa wakiwatumia watu maarufu na wenye ushawishi mkubwa wa kisiasa na kiuchumi ili kupitisha ajenda zao. Kwa njia hiyo kundi hilo lilifanya hila na kuhalalisha mambo haramu huku mambo halali yakiharamishwa bila umma wa dunia kutambua kwa haraka, lakini ikawa ni mambo yaliyokuwa yanatendeka kidogokidogo na hatimaye kuanza kuonekana kama ni mambo ya kawaida. Mwisho wa siku ikawa ni mambo yanayodaiwa kwa kigezo cha haki za binadamu, mataifa makubwa yaliyotawala kwa kanuni mahsusi za kundi hilo, yakashadadia na kuyafanya mataifa tegemezi yafanye uhalali wa mambo hayo kwa kigezo cha misaada.
Kwa ubabe huo wa mataifa makubwa dunia ikawa ni ishara kubwa ya utawala wa uovu usiozingatia adili. Kundi hilo likitazama vitu hivyo kama chanzo cha nuru na utajiri wa maarifa batili waliyotengeneza na kuipumbaza dunia kwa hayo. Wakiyaita Uhuru, usawa wa kijinsia na haki za binadamu.
Katika tawala za namna hiyo, mambo yaliyohusika na usafi wa mwili, roho na nafsi yalionekana kupitwa na wakati. Kundi hilo likatumia uwezo wa kifedha, ushawishi wa kisiasa na kupitia sayansi iliyopingana na uwepo wa Mungu, kuhalalisha kila aina ya uchafu katika maisha ya wanadamu, wengi wakikana uwepo wa Mungu kwa kuamini maneno na propaganda za wanasayansi wao waliowatengenezea umaarufu ulimwenguni kote!
Dini za ulimwengu, sasa zilipata wahubiri waliohalalisha maovu na kuyaweka wazi. Wahubiri wengi wakiwa ni wanachama halali wa kundi hilo huku wakikusanya makundi makubwa ya wafuasi. Mafundisho yao yakiwa ni juu ya mafanikio na juu ya kuamini uwezo wao binafsi, kwa sehemu wakiwaaminisha watu kwamba Mungu anajua udhaifu wao na ni juu yao kuamua lipi ni baya na lipi ni jema, na kwamba kama dhamiri na nafsi zao ziliona sawa, basi hakukuwa na ubaya.
Viongozi hao walifanya miujiza mikubwa kwa kutumia nguvu za giza na watu waliwafuata wakiamini ni uweza wa Mungu. Waliamini, kwani tayari kundi hilo lilikwisha waandaa kisaikolojia kuamini katika miiujiza. Wengine wakijitangaza hadharani kuwa wao ni mashoga na kutangazia ulimwengu kwamba huo ni aina mpya ya upendo miongoni mwa wanadamu.
Waliosimama kupinga walibezwa na kuulizwa wao ni nani kuwahukumu wenzao. Dunia sasa ilikuwa inazidi kuchanganyikiwa na wanadamu waliona ni kawaida tu. Uovu huo haukuishia hapo bali zinaa ilionekana ni kitu cha muhimu huku ikihamasishwa kwa kutumia vyombo vya habari vilivyofanya wanadamu waone zinaa ni suala la kawaida na la kifahari.
Sasa haikuwa ajabu tena kusikia kwamba kaka na dada wana mahusiano ya kimapenzi au mzazi na mwanae. Ile enzi ya sodoma ilikuwa imerejea, na wala haikuwa ajabu pale wanadamu waliposema ni haki yao kuishi na wanyama wawapendao kama wanandoa.
Mataifa yaliyopingana na uozo huo yalitengenezewa ajenda na sababu, yakavamiwa na kwa lazima yakaingiliwa kwa kigezo cha Demokrasia.
Sasa Machera aliitambua vema sauti ile, ilikuwa sauti ya The Don, Yule waziri aliyetoroka baada ya kutiwa mbaroni kwa mauaji ya kijana aliyejulikana kwa jina la Elinisa. Akakumbuka maneno aliyatamka baada ya kumtia mbaroni, ‘nina uwezo wa kuishi kokote kule duniani. Kokote kuliko na ushawishi wetu’ na sasa alikuwa amelithibitisha hilo.
The Don Alikuwa anaongea naye kutoka Marekani akimweleza kuchukua tahadhari kwani alikuwa anamwinda.
"Tahadhari? Kama wewe ni mtu makini bila shaka ungekuwa unafahamu kuwa mara zote nakuwa makini na wala siambiwi muda gani nichukue tahadhari. Ninakufahamu vema na watu unaowafanyia kazi, daima nipo tayari kupambana na ninyi hadi kufa". Machera alimjibu Don.
"Ha ha ha, kijana matata sana wewe. Sayansi, siasa, uchumi na hata dini za dunia zipo upande wangu, huwezi kuzima moto huu. Kwa taarifa yako tu hapo ulipo nina watu wangu wanaokutazama, kila unachofanya tunapata taarifa, kwakweli upo ndani ya box kijana. Hebu fikiri, Mimi nipo Marekani, lakini najua kwamba hapo ulipo ni chini ya kivuli kando ya mto na upo na msichana mweupe ambaye amevalia miwani, suruali ya jeans, buti za cowgirl, kofia ya sobrero na fulana ya mikono mirefu, tazama unageuka kumwangalia. Nadhani umethibitisha."
Machera alibaki kimya, kichwani mwake kulikuwa na wasiwasi.
‘Ina maana hawa watu wananitazama hapa nilipo na ninachofanya?' Wakati akitafakari hayo sauti ya The Don Ikasikika tena masikioni mwake.
"Najua unajiuliza vipi nimefahamu hayo, usipate shida, ni teknolojia. Kwa kweli ni teknolojia ambayo sasa imeanza kutumika huku Marekani na tunatarajia kuingiza Afrika hivi karibuni na Tanzania kwa upendeleo itakuwa miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa kuipata na kuifanyia majaribio. Inaitwa microchip technology. Kazi yake ni kutuwezesha kumonita akili za walimwengu ili kuondoa dhana za kufikiri kwa ufasaha. Tunajua kwamba tumefanikiwa kwa kiwango kutengeneza akili tegemezi kwa watu wengi na nchi nyingi duniani kupitia mitandao na filamu, lakini hakuna ubishi kwamba hii programu itakuwa thabiti zaidi kwa sababu ina uwezo wa kutawala mfumo wa fikra wa mtu bila yeye mwenyewe kujua, hivyo inakuwa inarahisisha programu hii kuchakachua uwezo wa kufikiri wa mtu na kumpa machaguo ya kutekeleza amri za Komputa zetu.
“Kwa maana nyingine ni kwamba chip hiyo inaruhusu computer zetu kufanya asilimia arobaini na tano ya maamuzi ya huyo mtu kwa kuulazimisha ubongo wake kufanya hivyo. Kama roboti vile. Na nimeona vema nikushirikishe hili kwani naamini vita unayopigana, ni unapigana na wewe mwenyewe. Kwa taarifa tu, kadri unavyoendelea kunisikiliza ndivyo tunavyozidi kuuvamia na kuteketeza baadhi ya mafaili ya ubongo wako."
The Don alimaliza kuongea kwa kicheko cha dhihaka. Machera akajikuta anadondosha simu toka sikioni mwake huku akishindwa kutafakari kwa muda. Mara akaisikia tena sauti ya The Don ikitamka kwa mwangwi kichwani mwake ‘unaona, hata bila simu tayari tunaweza kuwasiliana kwani ubongo wako kwa asilimia kadhaa ni mali yetu. Tutazidi kuwasiliana kijana, jiangalie sana’
Machera alinyanyuka. Kwa muda sasa Anastazia alikuwa akimwangalia kwa wasiwasi. Kadri muda ulivyozidi kusonga mbele Ana aligundua kuwa mpenzi wake huyo hakuwa sawa. Alimjua vema, haikuwahi kutokea Machera apate wasiwasi mkubwa hivyo kwa ajili ya vitisho vya wahalifu, siku zote kuna namna ambayo aliweza kuwashinda. Lakini leo…. Haikuwa kawaida. Kwa vyovyote vile, chochote alichosikia kilikuwa na kishindo kikubwa sana.
Ana alimsogelea na kumkumbatia kama mama anayejaribu kumtoa wasiwasi mwanae kipenzi, halafu kwa sauti tulivu ya kusema usijali mwanangu mama yako niko hapa kukulinda, akatamka;
"Usiumie kichwa mpenzi, chochote ulichosikia ni hila tu, hakuna jipya ni mbinu za kimafia tu ili unyong’onyee upishe wafanye mambo yao. Usiwaruhusu watuharibie muda wetu wa kufurahia penzi letu."
Machera alimtazama binti huyo mrembo kisha akasema
"Ningempata wapi mwanamke anayenifaa zaidi yako mpenzi? Si tu nina bahati, bali nimejaaliwa msaidizi hasa aliyetoka katika mbavu zangu. Naamini ulichosema ni pointi ya msingi kabisa, ya nini watuharibie fursa yetu ya kufurahia maisha, potelea mbali, nitadili nalo baadae" Alimaliza kuongea na kujaribu kumbusu mrembo wake, lakini Anastazia akamzuia kwa kidole chake cha pili baada ya gumba kwa kukiweka mshazari midomoni kwa kijana huyo na kusema;
"Sema tutadili nalo baadaye! au unadhamiria kunificha ulichoambiwa kwenye simu?"
"La hasha kichuna wangu, nisipokueleza wewe nitamweleza nani anayenifahamu vizuri zaidi yako?" Machera alijishaua na hapo akapokea busu mwororo toka kwa mrembo huyo.
Kwa pamoja walinyanyuka huku wameshikana viunoni na kumwelekea mwana punda aliyekuwa anapura majani pembeni yao. Baadae kidogo walionekana wakiwa juu ya mgongo wa mwanapunda Yule wakishuka bondeni kwenye mto mahali penye kina kirefu, mikononi wakiwa na ndoano zao zilizozamishwa kwenye maji tulivu ya mto mesani.
Mara Simu ikaita tena, mapigo ya moyo wake yakadunda kwa kasi mara mbili ya kawaida.
Hofu!
Hofu!
Hofu ya kisichojulikana ikammendea na kuutikisa mfumo wake wa fahamu, kidogo Simu idondoke mikononi mwake kwa kale kajasho ka kihoro kalikototesha viganja vyake. Ikawa hata kuinyanyua Simu yake kuiweka sikioni au basi kuitazama, ni changamoto asiyoelewa nini maana yake. Hapo, Machera akajitia ujasiri, ujasiri wa bandia kwani mapigo ya moyo wake yalieleza kitu tofauti.
Naam, sauti ya Anastazia ikamzindua toka kwenye kimuhemuhe hicho, sauti hiyo ikamkumbusha yeye ni Nani, mpelelezi maarufu nchini, mtu aliyetegemewa na taifa kwenye masuala nyeti yaliyohitaji akili na ujasiri, vitu ambavyo alijaliwa.
"Mpenzi, hiyo Simu vipi? Hujaisikia?"
Sauti laini, nyororo na tamu. Sauti iliyomkumbusha ni mwanaume tegemewa wa mwanamke huyu mrembo.
"Oh, aisee sijui Nilikuwa nawaza nini!" Akazinduka na kuinyanyua Simu yake na kutazama kioo cha Simu hiyo. Kwenye kioo hicho jina la mtu mwenye mamlaka Kubwa zaidi nchini likaoneka. Mheshimiwa Raisi wa serikali ya mpito, mheshimiwa Sebastian Masebo.
Ile kuona jina la mheshimiwa Sebastian Masebo, moyo wake ukashuka, akajipata akivuta mkupuo wenye ujazo wa hewa na kutoa mkupuo mwingine nje ya mapafu yake kwa ujazo ule ule. Aliweza kupumua vema sasa, mapigo ya moyo wake yakirejea kwenye utaratibu wake wa kawaida.
"Naam mheshimiwa raisi, shikamoo Mkuu." Machera akatamka kwa uchangamfu mwingi.
"Marahabaa kijana wangu, habari za likizo bwana?" Mheshimiwa rais akasaili, sauti yake ikionekana tulivu, ikisadifu mamlaka yake.
Mamlaka ambayo kwa kiasi kikubwa aliyapata kupitia ile kamati teule isiyotambulika kisheria, kamati ya fitna wengine huiita hivyo, ikiaminiwa kuwa ni kamati ambayo ikiwa kinyume chako, hata ukafanya nini basi huwezi kuunda serikali, kinyume chake kikiwa kweli. Ukikubalika, basi unaipata nafasi hiyo.
Tetesi nyingi Mtaani zikidai kamati hiyo haikuteuliwa na mtu ila baba wa taifa. Naam, hata ingawa alikuwa ni marehemu, ilisemekana mzimu wake ulihusika kukiunda kikosi hicho cha kamati, ambapo Kila mteule alikula kiapo cha utii kwa ulinzi wa taifa, kiapo cha uzalendo, uadilifu. Ilisemekana kuwa, waliokengeuka anguko lao halikukawia na walianguka anguko la aibu. Hizo zilikuwa ni simulizi mitaani.
Kwa upande wa pili, ni Machera, Mkuu wa majeshi, Mkuu wa kitengo cha usalama wa taifa na raisi mstaafu walioratibu mkakati uliompatia mheshimiwa Sebastian Masebo cheo chake kipya cha rais wa serikali ya mpito! Kamati teule!
"Sijambo Mkuu, natumaini hali inaendelea vema nchini. Hongera kwa kazi mpya Mkuu " Machera akajibu na kutia udambwi udambwi wa kumkoga mheshimiwa.
"Ah kijana wangu, uko wapi ndugu yangu, una habari huyu nduli analazimisha kutawala nchi hii kwa remote kutokea huko Marekani? Kijana, nchi inakuhitaji haraka iwezekanavyo. Fanya haraka uje tujue tunadili vipi na huyu adui ambaye sasa anaitangaza nchi kifedhuli, na kujaribu kuwachochea wananchi dhidi ya serikali yao. Ni kama amedhamiria sasa nchi iwe anarchy(isitawalike) na nikiwa kiongozi wa taifa hili siko tayari kuona mpuuzi mmoja anaigeuza Tanzania kama Rwanda ya 94" Mheshimiwa raisi akafunguka. Kwa Kila hali, Machera alihitaji kuondoka kurejea jijini kwa ajili ya kuona namna ya kulinasua taifa dhidi ya Mabruki The Don.
"Naam Mkuu, naelewa hali ilivyo, ni kweli tunahitaji kukaa tufanye maamuzi ya kujinasua kwenye makucha yake. Nitajitahidi ndani ya wiki hii niwe nimerejea jijini!" Machera akajieleza.
"Sio wiki kijana wangu, ninakuhitaji kwenye kikao kesho. Tumeshafanya mpango ambapo utasafiri kwa ndege ya kukodi ya shirika la Mogambi Empire hivi navyoongea ndege hiyo ipo njiani kuja huko na tunatarajia kwamba itaondoka huko SAA 11 alfajiri kurejea huku, ili ushiriki kikao kitakachofanyika SAA tatu asubuhi." Mkuu wa nchi alitoa agizo. Naam, pendekezo la mkubwa kawaida ni amri.
Hii ilikuwa taarifa ya ghafula, lakini ilitoka moja kwa moja kwa Mkuu wa nchi, asingeweza kukataa. Nchi ilimhitaji.
Itaendelea