Mhe Zitto. HOJA YA FEDHA ZA USWISS BUNGENI DODOMA.

Mhe Zitto. HOJA YA FEDHA ZA USWISS BUNGENI DODOMA.

Karibuni masijala

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2012
Posts
409
Reaction score
135
Wanajamvi, heshima kwenu kisima cha mjadala wenye Afya.

Hoja ya kuficha fedha USWISS ilipojadiliwa ili himitishwa pia kwa hoja Serikali ishughulikie, watu wenye ushahidi akiwemo mtoa hoja Mhe. Zitto kuwasilisha nyakara au ushaidi ili kuipa serikali muda wafuatilie Bunge hili ijadiliwe.

Je? Mhe. Zitto, CHADEMA, WANAKAMATI- BUNGE na Wana JF kwa Itelejinsia hoja imepangwa kwenye RATIBA ya Bunge hili?

Je Wasiopenda kitendo hicho akiwemo mtoa hoja, CHADEMA, Wanaharakati na Wana Jamvi Tumejipanga kwa namna hoja haitakosa mashiko kwa kufifishwa na wahusika kwa kutumia serikali kama wanaweza na Refa wa Bunge kama haridhii, " Speedi na Viwango" kuizima.

Je Majina ya wahusika yatawekwa wazi na mtoa hoja au hata kutajwa na Mzalendo mwingine huko Bungeni kama Dr Slaa aliyetupa kufahamu List of shame na Mhe Mabere aliyetaja watu 10 wanaohusika na kinachoendelea akaahidi ku deal nao kukomesha vitendo vyao;

Au awamu hii mtoa hoja na Wanaomunga mkono watasema, "MAJINA SIO ISSUE" kutupa kazi ni wakina nani?

TUJADILI
 
Karibuni wote mtoa hoja, Wanachama wa vyama wanaopenda na wasiopenda mambo ya USWISS na mzee Mwanakijiji mtuongoze kujadili CD ya USWISS itaimba au itabuma na wote mawazo yako ya hoja ni ya muhimu kwa Tanzania tuitakayo usisite kutupia ili Bungeni kieleweke.
 
Nasikitika kukwambia kuwa ule msemo wa JK "upepo tu huu utapita" ni wakweli kabisa!

Dowans=Richmond wanalipwa chao! Habari ya Mwagosi kwisha sahaulika! Singo ya Mwakyembe na CCM ndio imepigwa kidogo nayo chali! UDA muulize Mwanakijiji!

Aah unauliza fweza za Uswisi? Keshajifia huyo! hivi wale form 4 failure imeishia wapi? Maandamano ya kumtoa Mulugo?

Maumivu ya kichwa huanza pole pole!
 
Wewe ndugu yangu achana na mambo ya Tanzania kama hutaki kung'olewa kucha na meno bila ganzi
 
Wewe ndugu yangu achana na mambo ya Tanzania kama hutaki kung'olewa kucha na meno bila ganzi

Nimekuelewa mkuu kuonea huruma meno yangu.
Eee Mungu epushia Mbali meno, kucha na afya uliyotujalia kudhuriwa kwa kuhoji kama haki yetu dhidi ya watawala na watawaliwa
 
Chezeya ccm weye! Alijifanya 6 kuhoji hoji mambo almanusra akabadilishwe jinsia!
 
hii ndo Tanzania, aje Zitto kwanza atuambie ana mpango gani na yale majina, je aliyakabizi kwa tume? na kwa sababu yeye ndo alikuwa mtoa hoja ana haki ya kujua kama tume imemaliza kazi yake, hivyo hapaswi kuwa haelewi kitu
 
Last edited by a moderator:
Toka mwaka jana naona unamwandama huyu dogo! Je, ile orodha ya magwiji wa mihadarati ambayo tuliambiwa ipo mezani mbona huishupalii!
 
Toka mwaka jana naona unamwandama huyu dogo! Je, ile orodha ya magwiji wa mihadarati ambayo tuliambiwa ipo mezani mbona huishupalii!
Orodha ya magwiji wa mihadarati ni noumaa,pesa hiyo ya mihadarati ndo imetuweka madarakani,tunawataja vipi?
 
Back
Top Bottom