Mhe. Paul Makonda, kwanini msiba huu tu?

Mhe. Paul Makonda, kwanini msiba huu tu?

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Mhe. Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni nakusalimu!

Naomba nikuulize jambo kuhusu msiba/kifo cha aliyekuwa Katibu wa Madereva Tanzania. Sote tunajua kuwa Marehemu huyu alikuwa mpigadebe mkubwa wa Dr. Magufuli na CCM kwa ujumla kwenye kampeni za uchaguzi wa Oktoba mwaka huu. Alishiriki vyema na hata 'kuwasemea' madereva kwenye mkutano wa CCM pale katika Viwanja vya Jangwani.

Mara baada ya kifo chake, Mhe. Paul Makonda umejitokeza mitandaoni na hata kwenye televisheni ya EA TV ukisema kuwa umeviagiza vyombo vya usalama vya Wilaya ya Kinondoni kufanya uchunguzi juu ya chanzo cha kifo cha Katibu huyo. Nilikuona jana kwenye kipindi cha EA TV (Kurasa) ukisema kuwa uchunguzi umeshaanza ukihusisha madaktari na hata watu wa usalama.

Sasa Mhe. Paul Makonda, kwanini ni kwa msiba huu tu? Kuna ujumbe gani unaotaka kuutuma kwa ndugu, jamaa, marafiki, madereva wenzake na watanzania kwa ujumla juu ya msiba huu? Mara ngapi umewahi kuagiza uchunguzi kwenye misiba ya viongozi wa taasisi za kijamii?
 
Mnafiki tu huyu na kutaka kujipendeza kwa mh.rais ili naye akumbukwe kwenye utawala mpya
 
Dogo anajipendekeza hadi aibu....yaani huyu yupo tayari kutoa t...go ilimradi akumbukwe na dr magufuli.
 
Funguka tu wewe ulitaka kusema nini? wacha kuzunguka, unataka kusema makonda anajua kilichomuua? makonda ni mlezi wa chama cha madereva na ndiye aliyepigania kuhakikisha kinasajiliwa hivyo huu msiba unamhusu kwa karibu.
 
Tusubulie majibu ya uchuunguzi ndipo tutapata
jibu la kile alichomaanisha PAUL makonda.
 
Last edited by a moderator:
Funguka tu wewe ulitaka kusema nini? wacha kuzunguka, unataka kusema makonda anajua kilichomuua? makonda ni mlezi wa chama cha madereva na ndiye aliyepigania kuhakikisha kinasajiliwa hivyo huu msiba unamhusu kwa karibu.

Hujaelewa mada
 
sassa na wewe mtoa mada kwa nini umemuita huyo jamaa mheshimiwa??kwanza ajieleze lile fungu alilofanya sherehe eti ya kuwapongeza polisi kwa amani ya uchaguzi alilitoa wapi,maana alialika hadi twanga pepeta.
 
Paul Makonda au CHABURUMA km anavojulikana humu ndani ni mnafiki aliekubuhu...ni mtu wa kujipendekeza kwa wakubwa ili apate fadhila!

Ingawa laana ya kumpiga makonde mzee Warioba bado inamtafuna sana na ndio maana wilaya yake ya Kinondoni haijafanikiwa kupata hata mbunge mmoja, na kata nyingi zimeenda UKAWA!
 
Last edited by a moderator:
Umeelewa mada au umekimbilia key board ?.


Funguka tu wewe ulitaka kusema nini? wacha kuzunguka, unataka kusema makonda anajua kilichomuua? makonda ni mlezi wa chama cha madereva na ndiye aliyepigania kuhakikisha kinasajiliwa hivyo huu msiba unamhusu kwa karibu.
 
makonda yuko tayari kutoa hata Tigo ili aonekane jamaa mshamba sana wa uongozi
 
Back
Top Bottom