Mhe. Mbunge wa singida mashariki.

Mhe. Mbunge wa singida mashariki.

msambaru

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2011
Posts
245
Reaction score
109
Wanajamvi salamuni.
Kwa heshima kubwa napenda kuchukua fursa hii kumkumbusha mbunge wetu akumbuke akipotoka, tunajivunia weledi, werevu, umakini na uelewa mpana alionaona kwa maslahi mapana ya kitaifa.
Katika kutimiza wajibu wako fahamu kuwa jimbo lako ni kati ya majimbo ambayo yanafanyiwa fitna wabunge wake muonekane hamfai, na kwa mbali naona umeshaanza kupikia majungu na kuchonganishwa na wapiga kura wako, pamoja,na hayo yasemwayo yapo anbayo ni ya kweli japo mengine wanakuchafua.
Hata kama kazi ya mbunge sio kuleta pesa jimbo ila uhamasishaji na usimamizi bora wa maendeleo jimboni ni kati ya majukumu yako kama mbunge, ila ukweli uliopo sasahivi haueleweki na sisi makada, makamanda, wafuasi na wapenzi wa CDM unatupa kazi ngumu jimboni japo kitaifa na kimataifa unafanya vizuri.
Sahivi umekomaa na makanikia ya maccm wakati kuna shanta gold mine wanafanya uchimbaji miaka 10+ na wanasema wapo katika utafiti ilihali wachimbaji wadogo wakiendelea kufukuzwa kila wanapogusa.
Suala la umeme, shahidi ni wewe mwenyewe nguzo zenye unconnected wires zimeishia kijijini kwako bila kua na tija.
Jimbo zima hakuna josho ht moja functional.
Wanufaika wa fedha za mfuko wa jimbo ni walewale miaka yote.
Wananchi chini ya usimamizi wako vijiji vya taru na mang'onyi walifanyiwa tathimini na shanta gold mine ila waliolipwa ni wachache na isivyo kwa mujibu wa tathimini halisi.
Hakuna miradi ya maji jimboni mpaka zama hizi tunachimba maji ya kunywa kwenye mchanga mitoni.
Ushauri na ombi langu kwako, tafadhali jipange kumobilize wapiga kura wako kupitia ofisi yako kidogo upewacho na serikali na nguvu zao kujiletea maendeleo hata kupitia mtandao wako mpana kimataifa upate hata ufadhili ili mambo yaende.
Unakubalika kitaifa ila umetokana na watu wachache watendee haki ya wakilishi, ni hayo tu.
 
ushauri ni ushauri. ila wabunge wengi hawaendi majimboni kamwe. kwa mfano kule kusini kuna jimbo la mbinga vijijini mbunge wake haonekani jimboni kamwe.
 
Ujumbe murua ila tegemea majibu ya kichawi ya akina palampa fundikila na wenzao wa giningi
 
Ujumbe murua ila tegemea majibu ya kichawi ya akina palampa fundikila na wenzao wa giningi
Ujumbe una umurua gani?
It is like umpuuze Tomas ulimwengu kwa kuwa tumefungwa na malawi na kupendekeza kutomtumia tena kwenye kikosi cha kifafa stars.

Angetuambia mbunge akienda jimboni huwa mgawa pesa kama Rugemalila wa enzi ile tungepata uelewa mpya.

Lakini hizi ni akadablaa za ccm tu!
Ccm Wanacheza ngoma ya mahepe.
 
Hajielewi huyo mbinge mpk uchaguzi ukikaribia.msaidieni maana ni msaada mzuri ki taifa.asiporudi kama taifa tutaumia ila nyie mtafaidika kwa mabadiliko.mtayoyaamua
 
Upumbavu wa 4G kulala sebuleni kwa dada,lumumba akili zao huwa wanaziacha msalani kma haja kubwa...wote wamejazana dar kusubiria migao ya pesa chakavu na bungeni ni kusema ndiyooo tunaibiwa sana.
Wakti wao ndio majizi ya karne bila rushwa maisha hayaedi
 
wacheni kuwa na mawazo finyu na kuleta nyuzi za kitoto hapa, lissu analifanyia kazi taifa zima,na pia msijenge imani kuwa mbunge ndio analeta maendeo ya majimbo, kama unafuatilia bunge tazama hizo kelele wabunge wanapiga kila mwaka na hayo yanayotekelezwa na serikali,
pia kila jimbo lina viongozi wengi sana wakuu wa mikoa,wilaya wenye viti na kila aina ya viongozi na hamna tafauti yeyote ikiwa mbunge hayupo. hii kuwa na wabunge 400 nchi nzima ni formality tu cha muhumi ingekuwa shida zinatekelezwa hata wabunge 10 wangetosha nchi nzima

kama lissu ni mbunge wangu ningemuomba asije hasa jimboni kwa kazi anazofanya zinatosha,
 
ushauri ni ushauri. ila wabunge wengi hawaendi majimboni kamwe. kwa mfano kule kusini kuna jimbo la mbinga vijijini mbunge wake haonekani jimboni kamwe.
Hata mwakyembe huwa haonekani jimboni hapa amekuwa ni mbunge wa huko Dodoma na Dsm
 
Bwana Msambaru, hao Shanta Gold Mine wapo hapo kwa mkataba wa serikali ya CCM na kubarikiwa na wazee wa "ndiyooo" kama ilivyo kwingine hawakuletwa na Tundu Lissu labda nikukumbushe kuna mradi wa maji na upanuzi wa shule vilifanywa na Shanta Mine je nani alilazimisha mpaka mradi huo ukafanyika? Je wale FFU waliopo pale shanta mine wapo kwa kuletwa na nani hapo? Mwisho kama wewe ni msema kweli si msema ovyo je ni nani aliweka zuio madini yasichimbwe mpaka wananchi wamelipwa haki na stahiki zao?
Nimewasilisha
 
Back
Top Bottom