Mh/ Shujaa Kibanga aomba Radhi baada ya Kumpiga Mzungu

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,468
23,744
Miaka mingi iliyopita tulimsifu shujaa kibanga kwa kumpiga mkoloni aliyewaita waafrika Nyani,Mbwa na majina yote mabaya. Kibanga hakupendezwa na kauli hizo zenye kuutweza utu wa mwafrika tena nyumban kwa mwafrika kwa maneno yenye kashfa na dharau ya hali ya juu.

tunakumbuka siku ile bwana yule mzungu alipoenda kukagua mashamba na kukuta kuwa hakukuwa na mazao ya kutosha kutokana na ukosefu wa Mvua. Bwana huyo Mkoloni alianza kuporomosha matusi na kana kwamba haitoshi alitaka hata kumtandika bakora Kibanga kitu ambacho kilimkwaza sana Kibanga na kuamua kumpiga hasa mkoloni mpaka alipokuja kuomba radhi aachiwe.

Miaka mingi imepita Kibanga amegundua kuwa yale aliyokuwa akisemwa na mkoloni yule yalikuwa ni kweli. waafrika ni kama nyani,kima.mbwa n.k. wamekosa utu, wanauana wenyewe kwa wenyewe kama vile ambavyo mbwa hupigana mpaka kuuana. wamekuwa hawajali utu wanagombania madaraka na kutaka kuendelea kukaa madarakani. katika Umri huu wa uzee Kibanga amekumbuka maneno ya yule mkoloni kuwa ninyi waafrika ni wavivu, hamfanyi kazi. amekumbuka baada ya kuangalia namna ambavyo ardhi ya afrika haitumiki vizuri. rasilimali za afrika zinakuja kunyonywa na wageni.

tumeona namna ambavyo waafrika wameuana na wanauana kwa sababu ya dini,kabila,koo na rangi. tumeona namna ambavyo waafrikaw wanang'ang'ania madaraka na wapo tayari hata kuua ili waendelee kubaki madarakani. Tumeyaona ya Syria, Egypt, Burundi, Zanzibar, Kenya miaka ile, ZImbabwe na hata Afrika kusini weusi walipowaua wenzao kwa sababu ya Ajira.

Kibanga katika uzee wake huu akiwa amechoka sana ameamua kumuomba radhi mkoloni yule kwa kitendo alichofanya miaka ile kumpiga kwa kutetea waafrika wenzie. Kibanga huyu ambaye ameachwa muda huu amejilalia kwenye kibanda chake cha mbavu za Mbwa amepata nafasi hiyo aliyokuwa akiiihitaji leo hii baada ya Mkoloni yule kuwa anafungua visiwa vya maji ambayo amevichimba kama msaada baada ya Kijiji anachoishi Kibanga kukosa maji kwa miaka mingi sana hata baada ya Uhuru. Ni mkoloni yule yule aliyepigwa na Kibanga amekuja sasa kuwasaidia wana kijiji cha Kibanga. Kibanga huku akitokwa na machozi ameinama akitaka kumshika miguu mkoloni yule kumtaka radhi. Mkoloni amekataa jambo hilo akisema pia naye hakufanya jambo jema miaka ile kutamka maneno yale "mbele za watu" baada ya kumaliza kufungua mradi huo alikaa na kuongea na kibanga mamabo mawili matatu wakikumbushana habari za nyuma. na Mkoloni akauliza kama walishajenga Reli nyingine ukiacha ile waliyojenga wao. Kibanga kwa aibu aliinamisha kichwa na kujibu "bado tupo kwenye mchakato"

Mkoloni yule alisikitika na kusema wakati mwingne alikuwa anawaza kama wangekuja angalau kurekebisha mambo flan nchini halafu waondoke wawaachie tena mambo yakiwa salama. Akaulizia hata vile viwanda walivyokuwa navyo vichache miaka ile. miradi ya umeme n.k na Mkoloni yule alishangaa kuwa mbona akiwa huko kwao anawaona akina Jumbe wanaenda sana nchini kwake mkoloni wakiwa na mapesa mengi? na misafara mikubwa sana?

Baadaye yule mzungu aliondoka kuelekea kwenye kijiji kingine kuendeleza miradi ya kuwasaidia wananchi. Kibanga alirudi chumbani kwake akajilaza kitandani na kutafakari miaka ile ilivyokuwa na sasa hali ilivyo. akatokwa na machozi kwa uchungu mkubwa uliomjia rohoni kama mtu aliyekatwa na kisu kisicho na makali . akanyanyua mikono yake na kuipeleka kifuani akiugumia maumivu. akafumba macho akalala usingizi wa miele. maskini peke yake akiwa amezungukwa na kiza huku mbu na nzi wakimng'ong'a. angalau alipumzika kutokana na adha za nchi yake.
 
Daaah Zile dawa unazokunywa zimekusaidia sana maana umeleta madini kwa lugha ambayo wenye akili tu ndo wanaweza kukuelewa. wengine wanachungulia tu wanaondoka. wanakosa cha kuchangia. hii ni fasihi mzee mwenzangu. upo vizuri unaweza andika kitabu kwa fasihi hii na watu wenye akili tu ndo tukakuelewa.
unachosema ni kweli. kwa sasa wakoloni ndio wanaotusaidia .ukiangalia kwa makini mambo tunayofanyiana ni yale yale maneno ya kuwa SISI NI MANYANI. donald trump huwa anaongea ukweli kabisa.sema watu hawamwelewi tu lakini ukiangalia issue ya zanzibar ndo utaona kuwa sisi waafrika ni manyani tu.

bado mpaka leo suala la huduma bora ni tatizo kama hata net tunaomba toka usa sisi ni watu wa ajabu sana. madawa hosp tunategemea ya msaada na yaliyopo tunayapata kwa rushwa au ni shida kuyapata. nadhani haya ni mambo yaliyomuumiza sana kibanga. akikumbuka miaka ile alipompiga mkoloni alionekana shujaa.akipigania watu wake ambao mwishowe walikuja kumtelekeza. tizama amekufa peke yake akiwa amezungukwa na nzi na mbu. hakuna mtu aliyemjali.
 
Babu umeua sana kwa hii story. umeua mbaya. ningeshauri story hii uiandike isomwe tena darasani. ni ya kusisimua hasa nimesoma mpaka mwishoni machozi yalianza kunitoka nikikumbuka haya unayoyasema. kiukweli bado tuna safari ndefu. na uzi kama huu ni wachache wanaweza uelewa na kutoa comments zao. maana wanatakiwa kutumia akili kukuelewa unazungumzia nini. kuna haja nadhan ya kuwaleta tena wakoloni watutawale ili kuifanya afrika iendelee. nasikia Mugabe ameanza kurudisha mashamba kwa wazungu. kwa kuwa hali imekuwa mbaya kwake kiuchumia na chakula hamna kwa wazimbambwe. huyu mzee alikuwa kama kibanga sasa ameona umuhimu wa kushirikiana na wakoloni ambao kipindi kile walipokuwa wakisema tuliwaona kama ni wanyama kumbe sisi ndo wanyama sana.
 
Daaah Zile dawa unazokunywa zimekusaidia sana maana umeleta madini kwa lugha ambayo wenye akili tu ndo wanaweza kukuelewa. wengine wanachungulia tu wanaondoka. wanakosa cha kuchangia. hii ni fasihi mzee mwenzangu. upo vizuri unaweza andika kitabu kwa fasihi hii na watu wenye akili tu ndo tukakuelewa.
unachosema ni kweli. kwa sasa wakoloni ndio wanaotusaidia .ukiangalia kwa makini mambo tunayofanyiana ni yale yale maneno ya kuwa SISI NI MANYANI. donald trump huwa anaongea ukweli kabisa.sema watu hawamwelewi tu lakini ukiangalia issue ya zanzibar ndo utaona kuwa sisi waafrika ni manyani tu.

bado mpaka leo suala la huduma bora ni tatizo kama hata net tunaomba toka usa sisi ni watu wa ajabu sana. madawa hosp tunategemea ya msaada na yaliyopo tunayapata kwa rushwa au ni shida kuyapata. nadhani haya ni mambo yaliyomuumiza sana kibanga. akikumbuka miaka ile alipompiga mkoloni alionekana shujaa.akipigania watu wake ambao mwishowe walikuja kumtelekeza. tizama amekufa peke yake akiwa amezungukwa na nzi na mbu. hakuna mtu aliyemjali.

Mkuu kuna memba kibao humu ambao hawakusoma mtaala wenye hiyo story ya Kibanga Ampiga Mkoloni, kwa hiyo uwasamehe bure.

Ingawa mleta story amejaribu kuoanisha kwa kiasi kikubwa sana, Big Up kwa mleta mada.
 
Ni ukweli unaoumma.Hata hakuna sababu ya kujiita Taifa huru ikiwa hata panadol zenye ubora tunategemea kutoka kwa Mkoloni.Ni kweli hata hospitali ni zile zile toka enzi za Mkoloni.Ni aibu kubwa,halafu kuna watu wanakuja na eti tunatumbua majipu,majipu yenyewe ni wao wameyatengeneza.

Tunawapa Uenyeviti wa Bunge akina Jumbe wanaokwenda Ulaya na mifuko ya sandarusi iliyojaa fedha za jasho la Mtanzania.Hakika Kibanga anahaki ya kufa kwa kihoro
 
Miaka mingi iliyopita tulimsifu shujaa kibanga kwa kumpiga mkoloni aliyewaita waafrika Nyani,Mbwa na majina yote mabaya. Kibanga hakupendezwa na kauli hizo zenye kuutweza utu wa mwafrika tena nyumban kwa mwafrika kwa maneno yenye kashfa na dharau ya hali ya juu.

tunakumbuka siku ile bwana yule mzungu alipoenda kukagua mashamba na kukuta kuwa hakukuwa na mazao ya kutosha kutokana na ukosefu wa Mvua. Bwana huyo Mkoloni alianza kuporomosha matusi na kana kwamba haitoshi alitaka hata kumtandika bakora Kibanga kitu ambacho kilimkwaza sana Kibanga na kuamua kumpiga hasa mkoloni mpaka alipokuja kuomba radhi aachiwe.

Miaka mingi imepita Kibanga amegundua kuwa yale aliyokuwa akisemwa na mkoloni yule yalikuwa ni kweli. waafrika ni kama nyani,kima.mbwa n.k. wamekosa utu, wanauana wenyewe kwa wenyewe kama vile ambavyo mbwa hupigana mpaka kuuana. wamekuwa hawajali utu wanagombania madaraka na kutaka kuendelea kukaa madarakani. katika Umri huu wa uzee Kibanga amekumbuka maneno ya yule mkoloni kuwa ninyi waafrika ni wavivu, hamfanyi kazi. amekumbuka baada ya kuangalia namna ambavyo ardhi ya afrika haitumiki vizuri. rasilimali za afrika zinakuja kunyonywa na wageni.

tumeona namna ambavyo waafrika wameuana na wanauana kwa sababu ya dini,kabila,koo na rangi. tumeona namna ambavyo waafrikaw wanang'ang'ania madaraka na wapo tayari hata kuua ili waendelee kubaki madarakani. Tumeyaona ya Syria, Egypt, Burundi, Zanzibar, Kenya miaka ile, ZImbabwe na hata Afrika kusini weusi walipowaua wenzao kwa sababu ya Ajira.

Kibanga katika uzee wake huu akiwa amechoka sana ameamua kumuomba radhi mkoloni yule kwa kitendo alichofanya miaka ile kumpiga kwa kutetea waafrika wenzie. Kibanga huyu ambaye ameachwa muda huu amejilalia kwenye kibanda chake cha mbavu za Mbwa amepata nafasi hiyo aliyokuwa akiiihitaji leo hii baada ya Mkoloni yule kuwa anafungua visiwa vya maji ambayo amevichimba kama msaada baada ya Kijiji anachoishi Kibanga kukosa maji kwa miaka mingi sana hata baada ya Uhuru. Ni mkoloni yule yule aliyepigwa na Kibanga amekuja sasa kuwasaidia wana kijiji cha Kibanga. Kibanga huku akitokwa na machozi ameinama akitaka kumshika miguu mkoloni yule kumtaka radhi. Mkoloni amekataa jambo hilo akisema pia naye hakufanya jambo jema miaka ile kutamka maneno yale "mbele za watu" baada ya kumaliza kufungua mradi huo alikaa na kuongea na kibanga mamabo mawili matatu wakikumbushana habari za nyuma. na Mkoloni akauliza kama walishajenga Reli nyingine ukiacha ile waliyojenga wao. Kibanga kwa aibu aliinamisha kichwa na kujibu "bado tupo kwenye mchakato"

Mkoloni yule alisikitika na kusema wakati mwingne alikuwa anawaza kama wangekuja angalau kurekebisha mambo flan nchini halafu waondoke wawaachie tena mambo yakiwa salama. Akaulizia hata vile viwanda walivyokuwa navyo vichache miaka ile. miradi ya umeme n.k na Mkoloni yule alishangaa kuwa mbona akiwa huko kwao anawaona akina Jumbe wanaenda sana nchini kwake mkoloni wakiwa na mapesa mengi? na misafara mikubwa sana?

Baadaye yule mzungu aliondoka kuelekea kwenye kijiji kingine kuendeleza miradi ya kuwasaidia wananchi. Kibanga alirudi chumbani kwake akajilaza kitandani na kutafakari miaka ile ilivyokuwa na sasa hali ilivyo. akatokwa na machozi kwa uchungu mkubwa uliomjia rohoni kama mtu aliyekatwa na kisu kisicho na makali . akanyanyua mikono yake na kuipeleka kifuani akiugumia maumivu. akafumba macho akalala usingizi wa miele. maskini peke yake akiwa amezungukwa na kiza huku mbu na nzi wakimng'ong'a. angalau alipumzika kutokana na adha za nchi yake.
Mkuu Good narration but Syria is Asia and not Africa
 
Umewasilisha ujumbe vizuri sana, jambo moja nililojifunza hapa ni kuwa vitabu vingi vya historia viliandaliwa kujenga mind za watu kuwa ukoloni lilikuwa ni jambo halikupaswa kuvumiliwa kabisa,inawezakana ndo maana wazungu baada ya kujua hilo wakawa na ubaguz sana kwa weusi. Fine, inawekana history ilikuwa na lengo zuri, ila sasa utandawazi na muda ndo vinasema ukweli kama namna ulivyowasilisha.
 
Kibanga ni shujaa asiyeimbwa... Ajabu wanaimbwa wasiotaka watoke madarakani japo wananchi hatuwataki

Bravo Kibanga ni mazingira tu yalikukwamisha
 
Kwa sisis wazee tumeelewa ni nin unachomaanisha. umetumia fasihi vizuri na ninataman nijue mwalimu wako wa fasihi ni nani. pia kama unapata muda andika kitabu.
 
Back
Top Bottom