Rais Samia Suluhu ukiongeza mshahara na Madaraja Mei Mosi 2021 watumishi wataandika jina lako kwa Mhuri wa moto kwenye mioyo yao

tinkanyarwele

JF-Expert Member
Dec 30, 2016
2,017
1,940
Mh SSH ifikapo Tarehe mosi May 2021 watumishi woote wa umma wanatamani kusikia mambo mawili tuu yaani Kuongeza mishahara pamoja na kuwapandisha Madaraja.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba ni miaka karibia tano/ sita watumishi wamepuuzwa na serikali iliyokuwa ya Mh Hayati Magufuli japo maisha yanapanda kwa kasi sana.

Jambo hili limekuwa chungu sana na lenye maumivu yasiyo elezeka kwa kila mtumishi wa umma. Rais Magufuli alifanya mengi mazuri kwa Taifa hili lakini yoote hayakuwa na maana kwa watumishi wa umma, hakuna mtumishi wa umma yeyote ambaye aliyafurahia mema ya Hayati Magufuli kwa sababu tu ya uminyifu wa haki zao.

Mengine ambayo unaweza kugusia na yakachochea hisia za watumishi na kukuona wewe ndiye Joshua wa kwenye Biblia aliye mrithi Musa ni pamoja na:

3. Kufungulia uhamisho kwa awatumishi haswa walimu.

4. Kupunguza kodi kwa watumishi wa umma.

5. Kuingilia kati suala la makato ya bodi ya mikopo yaani ikiwezekana irudishwe ile 8%.

6. Kuangalia upya suala la kikotoo.

7. Fao la kujitoa kazini.

8. Kuondoa mdudu aitwaye Retention fee kwa wanufaika wa bodi ya mikopo.

9. Bima ya Afya kwa mtumishi asipangiwe aina ya wategemezi bali aweke mtu yeyote anayemtaka.

10. Kuondoa vyama nyonyaji kwa watumishi wa umma kama CWT, TALUGWA, TUGHE nk
11.
12..

Haya niongezeeni wana JF...

Hakika mama ukiyasemea haya haswa hayo mawili ya juu basi hata ukiteremka jukwaani ukakwea pipa kurudi Dar salaam tayari Mhuri wa moto wa jina lako utagongwa kwenye viunga vya moyo ya watumishi na utakumbukwa vizazi na vizazi. Pia kama utakuwa na mpango wa kusalia madarakani baada ya miaka 4= hii basi utakuwa umepata turufu yenye nguvu kubwa
 
Nani kama Mama hebu acha tuone, lakini pia aendelee kupunguza PAYEE kama JPM alivyoanza, pia jitihada ziongezeke kwenye makusanyo ya VAT kwasababu purchasing power ya watu itakuwa kubwa.

Kasheshe ni pale wafanyabiashara watakapojifanya wanauza sana exempted goods 🤣 🤣 🤣
 
Third world Dwellers bana. Wataalamu wanadai mafuta tu mgando yanasimamisha mapigo ya moyo na kufa. Ije iyo kuandika na muhuri wa moto?

Unajua wewe moyo ulivyo kiungo muhimu. Usitoe tena mfano kwa kutumia moyo bana.

City huko kashanyukwa moja na Dortmund.

Sauh'waaa!
 
Kikwete was superb, angalia vizuri kumbukumbu zako roughly 50k raw.
Niko sahihi mkuu,kwa kuwa nimekuwepo kwenye awamu zote,Nyerere-Magufuli,and now Samia,so I can compare their performance.

Nyerere was the worst.As civil servants tuliteseka sana.Mshahara "wote" with my degree,could hardly pay four loaves of bread,if you get it.Life was tough man,na ulikuwa huruhusiwi kufanya biashara yeyote kujikimu.
 
Hivi Kikwete si alikuwa anaongeza Sh.10,000,sikumbuki kama aliongeza zaidi ya hapo.Mkapa ndiye Rais peke yake aliyeheshimisha wafanyikazi.Kwa hili Marehemu Mkapa popote pale ulipo hongera sana.
Unasemaje wewe!!?

Uliza mwalimu yeyote aliyeajiriwa 2014 kwa mara ya mwisho wakati Kikwete anakabidhi kijiti ilikuwaje
 
Vip wale ambao sio watumish Mama katufanyia Nini???
Mengine nimeomba mnisaidie kuongeza hapo wana JF..nisaidie please kuongeza hapo labda maoni yetu yanaweza kumfikia huyu mamaa haswa kwa wale ambao hawaja ajiiriwa pia
 
Hiyo namba tisa inaboa sana yaani kila kukicha vigezo vimebadilishwa

Eti cheti cha ndoa mara cheti cha kuzaliwa mara... tena yote hayo ni bure tu kama hakuna namba ya nida

Yaani ndugu zetu wanaangamia ukicheki hela yako inayokatwa kila mwezi inaliwa bure nafasi zile unashindwa kuzijaza kisa wenye vigezo hawapo eti. Mbona haikuwa hivi mwanzo?
 
Unasemaje wewe!!?

Uliza mwalimu yeyote aliyeajiriwa 2014 kwa mara ya mwisho wakati Kikwete anakabidhi kijiti ilikuwaje
Mimi nilikuwa kwenye ajira ya serikali kutoka 1977-2013,kwa hiyo nina picha.Kama unazungumzia 2014,Mkapa alishaweka msingi. Mimi frankly nilipokuwepo sikuona tangible increase ya mshahara kwa Kikwete in all his 10 years in office,and mind you,I was a senior officer in government.
 
Hiyo namba tisa inaboa sana yaani kila kukicha vigezo vimebadilishwa

Eti cheti cha ndoa mara cheti cha kuzaliwa mara... tena yote hayo ni bure tu kama hakuna namba ya nida

Yaani ndugu zetu wanaangamia ukicheki hela yako inayokatwa kila mwezi inaliwa bure nafasi zile unashindwa kuzijaza kisa wenye vigezo hawapo eti. Mbona haikuwa hivi mwanzo?
Yaani hili ni janga kubwa sana sema wanaharakati hawalioni na vyama nyonyaji havilioni... kawaida sisi Waafrika haswa Watanzania tunamaisha ya kutegemeana...mtu anazaliwa analelewa na ndugu kwa mfano shangazi, mjomba, baba mdogo nk...leo wewe kwa kuwa una kazi ndiye unakuwa na mzigo wa kuwatunza walio kulea... pengine walikulea kwa sababu ulikuwa yatima...lakini nafasi ya bima wanataka baba yako mzazi, mara mama yako, mara sijui uweke cheti....upuuzi mtupu wakati pesa inakwatwa kila mwezi...inauma mno
 
Sasa wewe naona unataka serikali irudi kama ilipokuwa. Kwa mfano suala la uhamisho unataka kila mmoja apakimbie kijijini mjazane mjini nani atawafundisha madogo wa huko bush
Kwani kila mmoja anataka mjini? Wengine tunataka turudi vijijini
 
Mimi nilikuwa kwenye ajira ya serikali kutoka 1977-2013,kwa hiyo nina picha.Kama unazungumzia 2014,Mkapa alishaweka msingi. Mimi frankly nilipokuwepo sikuona tangible increase ya mshahara kwa Kikwete in all his 10 years in office,and mind you,I was a senior officer in government.
Yaani bora hata huyo aliyeweka hiyo shilingi moja kuliko ambayo hakuweka hata punje
 
Sasa wewe naona unataka serikali irudi kama ilipokuwa. Kwa mfano suala la uhamisho unataka kila mmoja apakimbie kijijini mjazane mjini nani atawafundisha madogo wa huko bush
Na wale wanaotaka kurudi vijijini unawaweka kundi lipi mkuu?
 
Back
Top Bottom