singsong
Member
- May 7, 2014
- 77
- 9
Nimekuwa nafuatilia mikutano yako mingi nitaje michache ya hivi karibuni wa Kivule moshibar , Kitunda na Ukonga .Ni mara chache wabunge , madiwani wa CCM wanaruhusu maswali kwa wananchi katika mikutano ya hadhara lakini mikutano ya mwanamama huyu yote anatoa nafasi kubwa kwa wananchi kuuliza maswali na kinachonivutia ni namna unavyoyapangua kwa ujasiri inaonyesha kweli unalifahamu jimbo na changamoto zetu.Kwa hilo nakupongeza na kura yangu kama utagombea tena hesabu unayo.