Mh.Kamanda J.Mnyika mbunge wa Ubungo, Nimesikiliza WAPO RADIO kipindi cha yaliyotokea ambapo msaidizi wa mbunge akitoa tamko kuhusiana na kuwepo maandamano ya kesho kinyume na tangazo la jana la kamanda wa polisi mkoa Kindoni kusitisha maandamano hayo.
Mimi nadhani itakuwa sio busara tena kuwashawishi wananchi kuendelea na maandamano ilhali tayari mamlaka zinazohusika kusimamia usalama wa waandamaji zimekunyima kibali cha kufanya hivyo.
Lazima tujifunze kuepuka majeruhi na vifo visivyo na lazima kwa walala hoi kwani maandamano haya hayataleta maji bali mbunge kaa chini na makamanda wenzako kwa kutumia influence yako.
Ninaimani ufumbuzi uko mikononi mwenu bila gharama ya damu ya watanzania.
Ninafahamu nguvu ya harakati katka kulinda heshima na utu wa mtu ila busara ikitawala kiasi cha damu ya kumwagika kitapungua.
Mimi nadhani itakuwa sio busara tena kuwashawishi wananchi kuendelea na maandamano ilhali tayari mamlaka zinazohusika kusimamia usalama wa waandamaji zimekunyima kibali cha kufanya hivyo.
Lazima tujifunze kuepuka majeruhi na vifo visivyo na lazima kwa walala hoi kwani maandamano haya hayataleta maji bali mbunge kaa chini na makamanda wenzako kwa kutumia influence yako.
Ninaimani ufumbuzi uko mikononi mwenu bila gharama ya damu ya watanzania.
Ninafahamu nguvu ya harakati katka kulinda heshima na utu wa mtu ila busara ikitawala kiasi cha damu ya kumwagika kitapungua.