Usilitimie Neno la Mungu isivyo Halali ili kuifanya post yako kuonekana ni ya maana kumbe hakuna lolote zaidi ya Propaganda chafu na chuki binafsi dhidi ya Lowassa.
Nimeandika hii habari baada yakuona watu wanampamba Lowasa kama masiha ajaye, mkomboz na mtetezi wa wanyonge wakimsahau Mh Lowasa kwa vitendo vyake vyakinyonyaji na ukandamizaji akitumia udhaifu na ujinga wa watanzania kujitwalia umaarufu. Tufike mahali tuseme No kwa Mh Lowasa. Watanzania tumechoka.
Ningefurah kama ungenipinga kwa vipengele kuliko kusema nachuki na Mh Lowasa wakati sina ninacho mdai ama chuki nae
KWANZA:- ukitaka kututendea haki UNGEELEZA NINI MAANA YA NENO MASIHA.
PILI:- Kuna tofauti toka Mfame wa kwanza (SAUL) na wa Pili (DAUDI) namna walivyotiwa mafuta.
TATU:- Agano hilo2 la Kale mpaka kufikia mfalme wa Mwisho kutawala Agano la Kale tayari kulikuwa na namna tofauti Zimejitokeza za wafalme Kupakwa Mafuta BAADHI YAO waliingizwa kwa mtindo wa Kimapinduzi kutawala na wengine waliingia kimapinduzi.
Hamtendei haki Lowassa Je! unajua mpaka sasa ametumia Tshs ngapi Kujieneza kwa kuutaka Urais? Hizo fedha una uhakika ndio kaiba?
Ninachokijua mimi Lowassa ni mtu wa kazi ni mzalishaji.Je! fedha yake haiongezeki?
Miaka nenda rudi Lowassa atakosa kuwa na Bilioni tatu kwa uchache huo zilizo za halali?
UKWELI UNAHITAJI DARASA LA KUTOSHA LA USO KWA USO JUU YA MATUMIZI YA NENO LA MAUNGU.
Naungana na mtoa hoja na hoja yake pia. Watu humu hawaangalii amesema nini wanaanza kuelezea biblia; ni akili ndogo. Lowasa hafai kuwa kiongozi nje ya Monduli ambako nahisi watu wa huko anafanana nao.
LOWASA NI MWIZI MKUBWA. Naomba mumtafakari MEMBE
tatzo lako nimegunduwa unampends el,na ndio maana unajiitaa tumaini el,tatzo nikwamba bwana yako amelazimisha uandke yale anayotaka ila kimoyoni unamkubali
Ndungu wana jf na watanzania wote kwa ujumla napenda kuwa ambia Mh Lowasa sio Masiha ajaye.
Sisi wakristo tunajifunza ktk neno la Mungu yakuwa "MUNGU ANAWASHUSHA WENYE VIBURI NAKUWAINUA WANYENYEKEVU AMA WALIOJISHUSHA" Mh Lowasa hata kabla yakuanza safari yake yenye matumaini alisha jiaminisha kwa pesa,mali na ushawish alio nao lazima yeye ndie Rais ajaye yani Masihi, tena akamuona mwenzake kama hafanyi kitu ila yeye ndio anaweza akawa anawatisha watu serikalini huku akijuwa yeye sio msafi na wakati huo neno linasema toa kwanza boriti ndipo utoe kibanz ktk jicho la mwenzako. Mh Lowasa kwakuwa Mungu anawachukia wenye viburi, hakika hukumaliza uwaziri wako mkuu na sasa unataka kuuwaminisha umma wote wa watanzania ulijiuzulu kisiasa wakati ukijuwa kweli ulikamatwa pabaya.
Napenda kusema mh Lowasa Anapaswa kujuwa Mungu hapokei rushwa wala sadaka chafu na anasema kamwe Roho yake haitoshindana na mwanadam na wewe ni mwanadam hivyo kamwe huwezi shindana nae, imefika wakati nikwambie hufanani na Masiha yeyote amewahi tokea ktk dunia hii.
Kuna watu wanakuita Daudi. Napenda kusema hawa ni watu wasio mjuwa Daudi kijana alie kuwa shupavu na jasiri na kama wewe ungekuwa Daudi dalili ya kwanza nikukaa msituni na kondoo wa baba yako ufuwatwe na manabii kukumwagia mafuta uwe mfalme wetu, kinyume chake wewe umenunua mafuta nakujitaidi kuwaonga manabii wakupake mafuta uwe mfalme.
Sikiliza nikwambie mh Lowasa nikweli watakumwagia ndoo nzima yamafuta, ila wewe hutokuwa masihi ajaye maana Bwana anasema hakuwa nao ktk ibada zao.
Mfalme Daud aliuogopa ufalme ila wewe unautaman asubuh,mchana na usiku jambo hl limekufanya kuwa mbal na Bwana kiasi wapigana vita vyako peke yako Bwana hayupo.
Itafakari njia unapita ikiwa kama upo njia sahihi kisha upite nakusonga mbele. Asante
Nimeandika hii habari baada yakuona watu wanampamba Lowasa kama masiha ajaye, mkomboz na mtetezi wa wanyonge wakimsahau Mh Lowasa kwa vitendo vyake vyakinyonyaji na ukandamizaji akitumia udhaifu na ujinga wa watanzania kujitwalia umaarufu. Tufike mahali tuseme No kwa Mh Lowasa. Watanzania tumechoka.
Miongoni mwa watu wanaomvimbisha kichwa Lowasa mwenye uroho na urais utafikiri asipokuwa Rais basi Tanzania haitakuwa na Rais ni watu wa dini kama wewe wanao muona Lowasa ni mwizi na fisadi.Lakini ana powaletea fedha zake hizo ambazo zinasemwa kuwa ni fedha chafu munazipokea kwa kishindo huku mukitoa Amen nyingi na kusahau kuwa hizo fedha ni chafu.Utadhani kuwa wakati fedha ziko mikononi mwa Lowasa ndiyo zinakuwa chafu lakini zikiingia mikononi mwa wacha Mungu zinageuka na kuwa safi huku wakisingizia kuwa zimetolewa kwa ajili ya kuendeleza kazi ya mungu wakati wanajua kabisa hizo ni hongo kwa ajili ya urais.
hivyo cute do vyakinyonyaji unavyovizungumzia ni vipi?!
Vitaje, uthibitisho wake, tupe na maamuzi ya mahakama baada ya yeye kupelekwa mahakamani kwa kufanya vitendo hivyo.
Nimuhimu kumuhukumu mtu kwa haki, sikuendeleza maneno maneno yasio na uthibitisho dhidi ya mtu yakimchafua tu bila hakika yoyote, tena hata haki ya kusikilizwa hamumpi, nimatusi na shutuma tu.
Nasema tena na wewe unazungumza kama mtu anaelijua neno la mungu, nakuomba sana kuwa makini usijikute unamuhukumu kunyongwa mtu asiye na hatia.
Comrade
aaa na wewe utafikiri hujui si zinaombewa ili kuondoa pepo la ufisadi na wizi bwaana...