Albert Msando
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 1,019
- 171
Mh. Jakaya Kikwete,
Natanguliza samahani kama matumizi ya misemo ya taarab yatakukwaza. Sio kwamba mimi ni mmoja wa wale wanaoamini kwamba unapenda mipasho au wasaidizi wako kama Salva wanavyosemekana kutoa majibu ya kimipasho kwenye masuala nyeti yanayotugusa kila siku.
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, kumekuwa na migomo mara kwa mara, maandamano kila siku, kwa nini? Je hili ni swali unalojiuliza?
Katika hali ya kawaida ningetegemea mawaziri wako na wasaidizi wako wajiulize. Sidhani kama wanajiuliza na kama wanajiuliza sidhani kama wana majibu sahihi!
Sitashangaa wakitoa majibu kama 'ni CDM wanachochea, ni Dr Slaa anawashawishi, ni chuki za udini hizo'. Sitashangaa kamwe!
Lakini nitashangaa kiasi kama hutawashangaa kwa majibu hayo. Sitashangaa sana. Inawezekana unalitegemea hilo!
Mimi pamoja na WanaJF wenye nia njema tunajitolea kueleza sababu ni nini! Endapo utasoma hii thread chukua yale ambayo utaona ni sahihi ili uyafanyie kazi. Si dhumuni la hii thread kukurushia lawama moja kwa moja lengo ni kukueleza ukweli ambao mawaziri na wasaidizi wako hawathubutu kukueleza. Aidha wanakuogopa au hawakutakii mema! Vile vile inawezekana hawana uwezo wa kutambua na kutatua matatizo.
Hapa JF utaambiwa ukweli. Sio kwa lengo la kukudhalilisha bali kwa lengo la kuikoa nchi yetu na balaa ambalo linaweza kutokea....wewe ni shuhuda wa kilichotokea Kenya, kinachotokea Ivory Coast, kinachoendelea Misri na kilichojiri Tunisia!! Unajua vizuri sana!
Tunakoelekea hakutakuwa na muda wa kuambiana ukweli wala kupeana ushauri. Kila mmoja atakuwa anaokoa roho yake! Kila mmoja atakuwa anapigania mkate wake! Itakuwa tumechelewa sana!
Nisizunguke sana, Mheshimiwa Jakaya Kikwete, kama nilivyosema 'heshima ya suruali ni mfuko'. Watanzania mifuko yetu imetoboka! Haina kitu! Wanafunzi hawawezi kupata mahitaji yao ya kila siku, walimu, manesi, madaktari na wengineo! Wakandarasi wanaidai serikali yako Bil 700+ hawajalipwa! Dowans wanaidai tanesco Bil 94 ambazo serikali yako kupitia waziri wa fedha imesema hazina haina! Wakulima hawana fedha za kununua pembejeo na msimu wa kilimo umeanza! Wazazi hawana fedha za kuwalipia watoto wao ada na mahitaji mengine!
Kitaalamu watu wa uchumi watakushauri kuhusu mfumuko wa bei nk. Hayo mimi sina uelewa nayo! Ila na wewe ni mchumi labda utalielezea au unalielewa vizuri zaidi! Kwa mtanzania wa kawaida tatizo lililopo ni kupotea kwa heshima ya mfuko! Vijana hawana ajira! Ukame umeathiri kilimo, mishahara haitoshi kukidhi mahitaji nk! Mfuko hauna heshima yake Mheshimiwa Jakaya Kikwete!
Unatakiwa ufanye nini?
1. Kwanza jitambue. Wewe ndie kiongozi wa juu na unayo mamlaka yote kuongoza. Nafasi hiyo hukupewa na mtu yeyote zaidi ya wananchi waliokuchagua. Sio Rostam, Edward, Ngeleja wala Makamba! Ni wananchi!
2. Pili amua. Fanya maamuzi magumu. Achana na biashara za sheria ichukue mkondo wake na hadithi za 'sitaki kuingilia uhuru wa mahakama'. Kumwambia Jaji Mkuu ambaye ni mteule wako kesi zote za ubadhirifu na rushwa zisikilizwe haraka na kwa umakini mkubwa umeingiliaje uhuru wa mahakama? Mbona kesi ya yule aliyetaka kumuuza Albino Mwanza iliisha ndani ya wiki si zaidi ya tatu, akafungwa na haki itatendeka? Kinachotokea sasa hivi ni watu wanaiba fedha za serikali wanaamini wakishikwa watapewa dhamana kesi itakaa muda mrefu watahonga wataachiwa!! Watanzania huwa wanasahau! Ndio imani iliyopo!
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, ni kweli hujui kwamba kuna watu wako tayari kukaa jela miaka 7 ilii mradi fedha walizoiba zipo salama? Mfano, nikiiba Bilioni 5 nikafungwa miaka miwili kuna tatizo gani? Mshahara wa meneja wa benki ka mwezi ni milion mbili kwa mwaka ni milioni 24! Kwa miaka miwili ni Milioni 48! Kipi bora mtu aibe bil 1.3 afungwe miaka 3 abaki na Bil 1.3 au akae uraiani miaka 3 apate mil 72!!
Siamini kwamba Mheshimiwa Jakaya Kikwete haujui kwamba wafanyakazi wa serikali na hata mawaziri wako ni wezi! Wanaandaa risiti za uongo, wanaongeza bei za vitu, wanatumia vyombo vya serikali vibaya nk! Mambo haya ndio yanasababisha matumizi ya serikali kuongezeka na wananchi kupata hasira zaidi! Fanya maamuzi na washughulikie wahusika!
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, ulikuwa na list ya wanaokwepa ushuru ukasema unampa Kamisha Mkuu wa TRA!! Kwa nini usiifanyie kazi wewe mwenyewe?
3. Tatu mfukuze Makamba. Hana msaada kwako! Sina la zaidi.
4. Nne ongoza nchi na wananchi wako. Serikali yako imejitenga sana na wananchi walioiweka madarakani. Hata nyumbani kwako usipomwambia mke na watoto wako unapata mshahara kaisi gani, unadaiwa sh ngapi na matumizi ni yapi usilalamike wala kushangaa mkeo akita ummnunulie Audi zawadi ya birthday na mtoto akitaka ML 500 ampe girlfriend wake zawadi karudi kutoka UK! Hawajui shida na mahangaiko yako! Mbaya zaidi wakiona wewe unatapanya! Unakunywa bia kila siku! Unasafiri kila siku hawajui unaenda wapi na kufanya nini! Wanaona jirani analima shamba lao anavuna anasafirisha mazao wao wapo tu! Wanasubiri ahadi yako utawapa Audi na ML 500 kama zawadi! Watachoka kusubiri watadai kwa nguvu utahama nyumba!
Jaribu kuwashirikisha, ni nchi yao! Mbona ni watu waelewa sana wananchi wako?
5. Washauri wako hawana manufaa kwako! Inawezekana wachache ni wazuri lakini kuna mambo mengi yanayoenda sivyo yanasababisha tuamini kwamba timu yako ya ushauri ina walakini! Mfano, wanashindwaje kuona tatizo kabla halijatokea? Mbona wanaweza kuona vurugu za CHADEMA kabla hazijatokea hata kama kwa kuona huko watu wanakufa?
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, wanaJF watasema zaidi! Watakusaidia ili kuokoa nchi yao! Wasikilize! Kuwa mvumilivu kwani utakayoyasikia ndio mawazo yao! Wana haki ya kusema na watasema!
Heshima ya suruali mfuko Mheshimiwa Jakaya Kikwete!!
Natanguliza samahani kama matumizi ya misemo ya taarab yatakukwaza. Sio kwamba mimi ni mmoja wa wale wanaoamini kwamba unapenda mipasho au wasaidizi wako kama Salva wanavyosemekana kutoa majibu ya kimipasho kwenye masuala nyeti yanayotugusa kila siku.
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, kumekuwa na migomo mara kwa mara, maandamano kila siku, kwa nini? Je hili ni swali unalojiuliza?
Katika hali ya kawaida ningetegemea mawaziri wako na wasaidizi wako wajiulize. Sidhani kama wanajiuliza na kama wanajiuliza sidhani kama wana majibu sahihi!
Sitashangaa wakitoa majibu kama 'ni CDM wanachochea, ni Dr Slaa anawashawishi, ni chuki za udini hizo'. Sitashangaa kamwe!
Lakini nitashangaa kiasi kama hutawashangaa kwa majibu hayo. Sitashangaa sana. Inawezekana unalitegemea hilo!
Mimi pamoja na WanaJF wenye nia njema tunajitolea kueleza sababu ni nini! Endapo utasoma hii thread chukua yale ambayo utaona ni sahihi ili uyafanyie kazi. Si dhumuni la hii thread kukurushia lawama moja kwa moja lengo ni kukueleza ukweli ambao mawaziri na wasaidizi wako hawathubutu kukueleza. Aidha wanakuogopa au hawakutakii mema! Vile vile inawezekana hawana uwezo wa kutambua na kutatua matatizo.
Hapa JF utaambiwa ukweli. Sio kwa lengo la kukudhalilisha bali kwa lengo la kuikoa nchi yetu na balaa ambalo linaweza kutokea....wewe ni shuhuda wa kilichotokea Kenya, kinachotokea Ivory Coast, kinachoendelea Misri na kilichojiri Tunisia!! Unajua vizuri sana!
Tunakoelekea hakutakuwa na muda wa kuambiana ukweli wala kupeana ushauri. Kila mmoja atakuwa anaokoa roho yake! Kila mmoja atakuwa anapigania mkate wake! Itakuwa tumechelewa sana!
Nisizunguke sana, Mheshimiwa Jakaya Kikwete, kama nilivyosema 'heshima ya suruali ni mfuko'. Watanzania mifuko yetu imetoboka! Haina kitu! Wanafunzi hawawezi kupata mahitaji yao ya kila siku, walimu, manesi, madaktari na wengineo! Wakandarasi wanaidai serikali yako Bil 700+ hawajalipwa! Dowans wanaidai tanesco Bil 94 ambazo serikali yako kupitia waziri wa fedha imesema hazina haina! Wakulima hawana fedha za kununua pembejeo na msimu wa kilimo umeanza! Wazazi hawana fedha za kuwalipia watoto wao ada na mahitaji mengine!
Kitaalamu watu wa uchumi watakushauri kuhusu mfumuko wa bei nk. Hayo mimi sina uelewa nayo! Ila na wewe ni mchumi labda utalielezea au unalielewa vizuri zaidi! Kwa mtanzania wa kawaida tatizo lililopo ni kupotea kwa heshima ya mfuko! Vijana hawana ajira! Ukame umeathiri kilimo, mishahara haitoshi kukidhi mahitaji nk! Mfuko hauna heshima yake Mheshimiwa Jakaya Kikwete!
Unatakiwa ufanye nini?
1. Kwanza jitambue. Wewe ndie kiongozi wa juu na unayo mamlaka yote kuongoza. Nafasi hiyo hukupewa na mtu yeyote zaidi ya wananchi waliokuchagua. Sio Rostam, Edward, Ngeleja wala Makamba! Ni wananchi!
2. Pili amua. Fanya maamuzi magumu. Achana na biashara za sheria ichukue mkondo wake na hadithi za 'sitaki kuingilia uhuru wa mahakama'. Kumwambia Jaji Mkuu ambaye ni mteule wako kesi zote za ubadhirifu na rushwa zisikilizwe haraka na kwa umakini mkubwa umeingiliaje uhuru wa mahakama? Mbona kesi ya yule aliyetaka kumuuza Albino Mwanza iliisha ndani ya wiki si zaidi ya tatu, akafungwa na haki itatendeka? Kinachotokea sasa hivi ni watu wanaiba fedha za serikali wanaamini wakishikwa watapewa dhamana kesi itakaa muda mrefu watahonga wataachiwa!! Watanzania huwa wanasahau! Ndio imani iliyopo!
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, ni kweli hujui kwamba kuna watu wako tayari kukaa jela miaka 7 ilii mradi fedha walizoiba zipo salama? Mfano, nikiiba Bilioni 5 nikafungwa miaka miwili kuna tatizo gani? Mshahara wa meneja wa benki ka mwezi ni milion mbili kwa mwaka ni milioni 24! Kwa miaka miwili ni Milioni 48! Kipi bora mtu aibe bil 1.3 afungwe miaka 3 abaki na Bil 1.3 au akae uraiani miaka 3 apate mil 72!!
Siamini kwamba Mheshimiwa Jakaya Kikwete haujui kwamba wafanyakazi wa serikali na hata mawaziri wako ni wezi! Wanaandaa risiti za uongo, wanaongeza bei za vitu, wanatumia vyombo vya serikali vibaya nk! Mambo haya ndio yanasababisha matumizi ya serikali kuongezeka na wananchi kupata hasira zaidi! Fanya maamuzi na washughulikie wahusika!
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, ulikuwa na list ya wanaokwepa ushuru ukasema unampa Kamisha Mkuu wa TRA!! Kwa nini usiifanyie kazi wewe mwenyewe?
3. Tatu mfukuze Makamba. Hana msaada kwako! Sina la zaidi.
4. Nne ongoza nchi na wananchi wako. Serikali yako imejitenga sana na wananchi walioiweka madarakani. Hata nyumbani kwako usipomwambia mke na watoto wako unapata mshahara kaisi gani, unadaiwa sh ngapi na matumizi ni yapi usilalamike wala kushangaa mkeo akita ummnunulie Audi zawadi ya birthday na mtoto akitaka ML 500 ampe girlfriend wake zawadi karudi kutoka UK! Hawajui shida na mahangaiko yako! Mbaya zaidi wakiona wewe unatapanya! Unakunywa bia kila siku! Unasafiri kila siku hawajui unaenda wapi na kufanya nini! Wanaona jirani analima shamba lao anavuna anasafirisha mazao wao wapo tu! Wanasubiri ahadi yako utawapa Audi na ML 500 kama zawadi! Watachoka kusubiri watadai kwa nguvu utahama nyumba!
Jaribu kuwashirikisha, ni nchi yao! Mbona ni watu waelewa sana wananchi wako?
5. Washauri wako hawana manufaa kwako! Inawezekana wachache ni wazuri lakini kuna mambo mengi yanayoenda sivyo yanasababisha tuamini kwamba timu yako ya ushauri ina walakini! Mfano, wanashindwaje kuona tatizo kabla halijatokea? Mbona wanaweza kuona vurugu za CHADEMA kabla hazijatokea hata kama kwa kuona huko watu wanakufa?
Mheshimiwa Jakaya Kikwete, wanaJF watasema zaidi! Watakusaidia ili kuokoa nchi yao! Wasikilize! Kuwa mvumilivu kwani utakayoyasikia ndio mawazo yao! Wana haki ya kusema na watasema!
Heshima ya suruali mfuko Mheshimiwa Jakaya Kikwete!!