PAYE
JF-Expert Member
- Jun 19, 2025
- 365
- 459
Mgore Miraji ameibuka mshindi kwenye kura za maoni baada ya kuwabwaga wapinzani wake watano aliokuwa akishindana nao katika mchakato wa kumpata mwakilishi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye uchaguzi mkuu ujao katika Jimbo la Musoma Mjini mkoani Mara.
Endapo Mgore atapitishwa na kamati Kuu ya chama chake kupeperusha bendera na kisha kuwa mshindi katika uchaguzi huo, basi atakuwa mwanamke wa kwanza kuwa mbunge wa jimbo hilo la Musoma Mjini.
Akitangaza matokeo ya kura za maoni kwa Wilaya ya Musoma Mjini, Katibu wa CCM wilayani humo, Burhan Ruta amesema Mgore amepata kura 2,255 huku mpinzani wake wa karibu Juma Mokili akipata kura 1,543.
Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni pamoja na Dk Eliud Esseko (115), John Bwana (43), Philbert Sasita (34) na Mashaka Biswalo (44).
“Jumla ya kura zilizopigwa ni 3,796, zilizoharibika ni 62 na halali zilikuwa 3,734, kwa hiyo namtangaza Mgore kuwa ameongeza kwenye kura za maoni,” amesema.
Ruta amesema kutokana na kanuni za chama hicho, mgombea aliyeongoza katika kura za maoni hapaswi kufanya sherehe ya aina yoyote kabla ya vikao vya uteuzi kwa maelezo kuwa kuongoza sio kigezo cha kuteuliwa na chama.
Endapo Mgore atapitishwa na kamati Kuu ya chama chake kupeperusha bendera na kisha kuwa mshindi katika uchaguzi huo, basi atakuwa mwanamke wa kwanza kuwa mbunge wa jimbo hilo la Musoma Mjini.
Akitangaza matokeo ya kura za maoni kwa Wilaya ya Musoma Mjini, Katibu wa CCM wilayani humo, Burhan Ruta amesema Mgore amepata kura 2,255 huku mpinzani wake wa karibu Juma Mokili akipata kura 1,543.
Wagombea wengine na kura zao kwenye mabano ni pamoja na Dk Eliud Esseko (115), John Bwana (43), Philbert Sasita (34) na Mashaka Biswalo (44).
“Jumla ya kura zilizopigwa ni 3,796, zilizoharibika ni 62 na halali zilikuwa 3,734, kwa hiyo namtangaza Mgore kuwa ameongeza kwenye kura za maoni,” amesema.
Ruta amesema kutokana na kanuni za chama hicho, mgombea aliyeongoza katika kura za maoni hapaswi kufanya sherehe ya aina yoyote kabla ya vikao vya uteuzi kwa maelezo kuwa kuongoza sio kigezo cha kuteuliwa na chama.