Pole sana dada. Kuna sababu mbalimbali za kuumwa mgongo kabla na baadaya hedhi. Ukiongea na Daktari bingwa wa matatizo ya wanawake, anaweza kukusaidia. Ila kama unataka kujaribu msaada wa kwanza "first aid', nunua unga wa majani ya mlonge, unakunywa kijiko cha chai kutwa mara tatu. Unachemsha uji kidogo, ukiiva, unauweka kwenye kikombe, ndipo unaweka mlonge na sukari, uji ukiwa wa motoooo, una mix vizuri unakunywa uji. Kama hupendi uji, unaweza ku mix na maji moto au chai ya moto, unywe ikiwa bado moto.
Vilevile angalia godoro unalolalia. Lisiwe linatumbukia au laini sana. Inafaa liwe gumu kiasi, na liwe kama la nchi 4 au 5 hivi.
Vile vile, nunua hotwater bottle, ni ya plastic, unachemsha maji ya moto, unajaza, unaizungushia kwenye taulo nyepesi, unaweka sehemu inayouma.
VILEVILE, jaribu kuwa na mazoea ya kunywa kitunguu saumu vipande vitau au vinne kutegemeana na ukubwa. Kama hupendi harufu yake, unamenya, unakatakata vidogo vidogo, unakunywa na maji asubuhi na jioni. Ni dawa nzuri sana!!
Zoezi hilo lifanye kwa miezi mitatu mfululizo. Nina hakika utapata nafuu kama sio kupona kabisa. Ila usisahau kupimwa na Daktari, kwa sbb siku hizi kuna vifaa vya hali ya juu sana, kuweza kugundua matatizo.
Natumaini utatupa majibu hapa jamvini.