Mgomo wa wafanyabiashara kesho

Mgomo wa wafanyabiashara kesho

Wewe ndio hujui unachoongea hakuna mfanyabiashara anayependa kulipa kodi halisi kulingana na mapato yake. Wafunge tu sisi leo tunanunua mahitaji yetu mapema,tena waambieni warefushe mgomo maana wafanyabiashara wengine wananufaika na mgomo huu. Kwanza huu mgomo hauko huru kuna vitisho na kulazimishana. Ni vizuri wafanyabiasha wakaanzisha jumuiya nyingine itakayokuwa huru wamuachie Minja na wachaga wenzie jumuiya hiyo kuwatumikia wanasiasa

Tuna miaka mingine 100 ya kuendelea kubaki hapa tulipo kwa hiyo tatizo ni Minja na uchaga wake sio fact anazotetea kuhusu huu mfumo wa kodi, mkuu piga kazi ofisini hapo subiria mwisho wa mwezi mshahara wakate PAYE nyingine wakupelekee NSSF utaichukua ukistaafu au kama utaacha au kufukuzwa, this business thing tuachie sisi
 
Tuna miaka mingine 100 ya kuendelea kubaki hapa tulipo kwa hiyo tatizo ni Minja na uchaga wake sio fact anazotetea kuhusu huu mfumo wa kodi, mkuu piga kazi ofisini hapo subiria mwisho wa mwezi mshahara wakate PAYE nyingine wakupelekee NSSF utaichukua ukistaafu au kama utaacha au kufukuzwa, this business thing tuachie sisi

Huna biashara yoyote we ni mamluki tu na ajenda zenu zilizojificha. Kwa nini wafanyabiashara wanakuwa blackmailed kushiriki mgomo? Waanzishe tu jumuia nyingine isiyotumika kisiasa
 
Issue hapa si namna kodi inavyotumika issue ni mgomo wa wafanyabiashara. Ondoa pumba hapa, anzisha thread yenye issue ya kodi inavyotumika.
Huko ulaya kodi inatumika kwa mambo ya msingi miundombinu ya kueleweka na chenchi tunapewa msaada halafu tunanunulia rada mbovu, huku kwetu kodi inatumika kununua magar ambayo hayana barabara za kupita, ambazo mvua ikinyesha dk 5 barabara zote zinapotea tunaona mito tu dar es salaam barabara ya uhuru kutoka round about mpka karume inajengwa almost miezi nane na zaid sa hiv et mkandarasi anatumia sururu kuchimba mtaro wa maji, wilaya ya ilala ambayo ndipo ikulu na wizara na idara na ofice kubwa zote zilipo, Ahsante
 
Acha kudanganya wewe. Wafanyabiashara ndio chanzo cha hayo yote unayosema wala wewe si mfanyabiashara kwa namna ulivyocomment,wala hujui mfumo wa kodi hapo bandarini na jinsi gani deal zinavyopigwa kukwepa kodi.

kwa kukusaidia mimi bandari naitumia huu ni mwaka wa 15. naifaham in an out. ndio chimbuko la pili kwa wizi kuitoa wizara ya nishati na madini. bora hata hao wanaolipia kidogo kuna wanaoiba container nzima haijalipiwa hata Mia ndio maana nikasema inawezekana wewe ni mmoja wapo wa wanufaika wa huu wizi. muulize mtu yeyote container ya nguo bei gani halafu mwambie akuonyeshe malipo yake ndio utajua
 
Kuna kundi ambalo hatujagoma.Sisi wenye nyumba mlikopanga kuweka fremu za kuuza bidhaa zenu.Kodi zetu ziko pale pale muuze msiuze mtajijua kodi zetu za pango tunazitaka hatutaki mtu acheleweshe.Hayo ya kugoma au kutogoma mnayajua nyie na hawara zenu.
 
Acha uongo dunia nzima wapi unaongelea. ucwe kama bwabwa wewe. kama hujui kaa kimya. au uliza. waambie serikali yako kwanini hawataki cc tulipe kodi. unalipia container la futi 20 nguo tshs milion 40 halafu unaletewa risiti yenye kuonyesha umelipa tshs milion 12 kwanini wasituonyeshe hiyo account tutumbukize zote 40 au ni wewe unaetetea huu ujinga.

Usiwe na jazba nimetembelea nchi za ulaya zinazotusaidia bajeti yetu kila mwaka na siku moja nikanunua zabibu mbivu nikiwa Italia nikapewa risiti ya efd yenye kodi ya serikali. Ni kweli serikali imekithiri kwa rushwa na Tra ndiyo wabaya kabisa lkn dawa kuiondoa madarakani kwa kura na kuweka nyingine. Siyo kufunga maduka. Tuungane kubadilisha serikali na sisi tufuate sheria ndivyo wanavyofanya wenzetu walioendelea.
 
Back
Top Bottom