Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 55,028
- 59,657
Huu utakuwa wa nchi nzima, TABOA wamekataa na hawakubaliani na nauli mpya iliyowekwa na SUMATRA
Leo mpaka sa sita wasipopata jibu hawatakata ticket. Na mgomo kesho utakuwepo kama kawa.
Mkurugenzi wa sumatra yeye kasema kuwa Taboa hawajui taratibu kwani taratibu zipo badala ya kugoma.
=============================
KUNA kila dalili ya kutokea mgomo mwingine wa madereva wa mabasi yanayoofanya safari zake kati ya mikoa na mikoa pamoja na daladala nchi nzima, kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo kile kinachoelezwa kuwa ni kiburi cha Serikali.
Aprili 10, 2015, madereva wa mabasi ya abiria yanafanya safari zake mikoani pamoja na madereva wa daladala walifanya mgomo nchi nzima, ambao ulitikisa kwa kiasi kikubwa sekta hiyo ya usafiri na usafirishaji kabla ya viongozi wa Serikali kuingilia kati ili kunusulu hali mbaya kwa abiria iliyokuwepo.
Katika mgomo huo uliochukua takriban saa tisa, ulioanza asubuhi saa 12:00 hadi saa 9:00 alasiri ambapo mabasi ya mikoani na daladala yaliporejesha huduma, mawaziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka walilazimika kutoka maofisini mwao na kwenda kusikiliza madai ya madereva hao, ingawa awali kabla ya mgomo huo, walikuwa wamewapuuza.
Habari za uhakika zilizoifikia FikraPevu na baadaye kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Muungano wa Vyama Vya Madereva nchini, Clement Masanja, zinasema mgomo huo mwingine wa madereva wa mabasi unaweza kuanza muda na siku yoyote kuanzia sasa.
Sababu zinazotajwa na madereva hao kutaka kurejea kwenye mgomo wao mwingine huo, zimetajwa kwamba ni...
Habari zaidi, soma=>: FikraPevu: Mgomo mwingine wa Madereva wa Mabasi ya Abiria na Daladala wanukia kuanzia Sasa
Leo mpaka sa sita wasipopata jibu hawatakata ticket. Na mgomo kesho utakuwepo kama kawa.
Mkurugenzi wa sumatra yeye kasema kuwa Taboa hawajui taratibu kwani taratibu zipo badala ya kugoma.
=============================
KUNA kila dalili ya kutokea mgomo mwingine wa madereva wa mabasi yanayoofanya safari zake kati ya mikoa na mikoa pamoja na daladala nchi nzima, kutokana na sababu mbalimbali, ikiwemo kile kinachoelezwa kuwa ni kiburi cha Serikali.
Aprili 10, 2015, madereva wa mabasi ya abiria yanafanya safari zake mikoani pamoja na madereva wa daladala walifanya mgomo nchi nzima, ambao ulitikisa kwa kiasi kikubwa sekta hiyo ya usafiri na usafirishaji kabla ya viongozi wa Serikali kuingilia kati ili kunusulu hali mbaya kwa abiria iliyokuwepo.
Katika mgomo huo uliochukua takriban saa tisa, ulioanza asubuhi saa 12:00 hadi saa 9:00 alasiri ambapo mabasi ya mikoani na daladala yaliporejesha huduma, mawaziri wa Uchukuzi, Samuel Sitta na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka walilazimika kutoka maofisini mwao na kwenda kusikiliza madai ya madereva hao, ingawa awali kabla ya mgomo huo, walikuwa wamewapuuza.
Habari za uhakika zilizoifikia FikraPevu na baadaye kuthibitishwa na Mwenyekiti wa Muungano wa Vyama Vya Madereva nchini, Clement Masanja, zinasema mgomo huo mwingine wa madereva wa mabasi unaweza kuanza muda na siku yoyote kuanzia sasa.
Sababu zinazotajwa na madereva hao kutaka kurejea kwenye mgomo wao mwingine huo, zimetajwa kwamba ni...
Habari zaidi, soma=>: FikraPevu: Mgomo mwingine wa Madereva wa Mabasi ya Abiria na Daladala wanukia kuanzia Sasa