Pungezeni maigizo! Wanasiasa bwana. Simjui huyo Jasmine kabisa lakini wanasiasa wana tabia ya kuingia kwenye siasa na unyenyekevu halafu tunakiona cha mtema kuni -- wakishanyonya nchi wanajiona miungu midogo. Hata hayo magenge tunayosikia sasa hivi ya ufisadi na utekaji walianza na kujifanya wanajali wananchi sana -- kwenye kampeni kujifanya wana umoja na wananyonge kukaa chini, kunywa kahawa magengeni, lakini wakishapata madaraka -- watetezi wanageuka kuwa watesaji.