Urais wa nchi ndiyo wadhifa mkubwa katika Taifa letu. Siasa kwa nijuavyo mimi, ni kitendo cha kuongoza mambo ya watu. Kwa maana hiyo, Rais anapaswa kuwa mwanasiasa mahiri ili kuliongoza taifa na watu wake katika mambo ya ndani ya nchi na yale yahusuyo medani ya kimataifa.
Wiki iliyopita nilikuwa nafuatilia hotuba ya mmoja wa wagombea urais aliyoitoa kwenye mkutano wake wa kampeni mjini Morogoro katika Uwanja wa Jamhuri unaomilikiwa na chama chake. Mkutano wake kwa hakika ulijaa watu wengi na kwa lugha ya kisasa nadiriki kusema kulikuwa na nyomi akiwamo Rais anayemaliza muda wake, Jakaya Kikwete.
Mgombea urais huyo akayatamka maneno ambayo yameniacha na tafakuri nzito kuhusu nini itakuwa hatima ya nchi yetu iwapo mgombea huyo atachaguliwa kuwa Rais. Kwa mashabiki au kwa manazi wa kisiasa na wakereketwa wa chama, maneno aliyoyatamka mgombea huyo yalipita na kutoweka katikati ya sauti za washangiliaji.
Mimi sifanyagi (sifanyi) siasa, na kwa bahati mbaya naweza nikawa si mwanasiasa mzuri. Mimi kwangu ni kazi tu yalikuwa maneno ya Dk John Magufuli. Hapa kazi ipo, kwamba rais ajaye anaweza akawa hajui siasa vizuri! Sikuamini masikio yangu kwa sababu ingekuwa ni katika nchi nyingine, kauli hii ingeweza kumkosesha urais kwa sababu wananchi wanamtegemea rais wao aijue vizuri siasa ili awaongoze vizuri.
Kama si kufanya siasa, chama cha siasa kitatawala vipi nchi? Sera za chama, ilani yao ya uchaguzi na maamuzi mbalimbali atakapokuwa madarakani yanategemea siasa kwa asilimia kubwa. Diplomasia na nchi za nje na mashirika ya kimataifa yanahitaji rais mwenye upeo mkubwa kisiasa hasa katika zama hizi za ulimwengu wa utandawazi.
Utatuzi wa masuala matatizo mengi ya wananchi kijamii, kiuchumi, kielimu na kujenga utawala bora ni mchakato wa kisiasa. Hata utekelezaji wa kauli zake kwamba anataka mabadiliko bora na si bora mabadiliko ni jambo linalotaka mchakato makini wa kisiasa.
Vinginevyo itakuwa ni ubabe wa kisiasa badala ya mabadiliko ya kisiasa. Pengine tuseme mgombea huyo alipotaja siasaalikuwa na maana ile ya mtaani yaani ujanja ujanja, hila, ghiliba, uongo au porojo?
Lakini ukiiangalia kauli mbiu yake Hapa ni kazi tu unaelewa kwamba huyu atakuwa rais mtendaji zaidi kuliko kuwa mwanafikra na mwanadiplomasia (stateman). Ikiwa hivyo, napata shaka kubwa kwamba tutashuhudia rais mwenye kutegemea kuchorewa ramani na wanasiasa kwa kuwa yeye hajui siasa.
Katika hali hiyo, anakuwa kama Waziri Mkuu badala ya kuwa Rais. Hofu yangu ni kwamba serikali yake itakuwa ya kiimla inayoongozwa na utendaji wa mtu mmoja jambo ambalo litakuwa ni hasara kwa Taifa.
Kama rais hajui vizuri siasa, ni ipi hatima ya vyama vya siasa, asasi za kijamii, vyombo vya habari na wadau wengine wa maendeleo ya nchi? Ni wazi CCM itahitaji kuwekeza vya kutosha katika kutengenezea timu yenye weledi wa siasa pale Ikulu ya Magogoni ili kuweka uwiano sawa kati ya Hapa ni kazi tu na ule upande wa rais unaohitaji weledi wake kisiasa ili kuivusha nchi salama. Vinginevyo kaulimbiu hapa kazi tu itakuja kuitokea puani hata CCM yenyewe.
Kila kitu ni siasa
Ulimwengu wa sasa karibu kila kitu ni siasa. Ili kujenga uchumi imara hahitajiki mtu kuwa mchumi mzuri pekee bali pia anahitajika kujua siasa za uchumi. Hivyo hivyo kutafsiri ilani ya uchaguzi ya chama kutoka kwenye maneno kwenda kwenye vitendo. Rais anapaswa kuijua vizuri siasa kwa sababu ilani ni tamko la kisiasa, ndiyo maana hata isipotekelezwa vizuri hakuna mtu anayefikishwa mahakamani kujibu mashitaka.
Sasa mtarajiwa wetu ambaye anakiri hadharani kuwa hajui siasa, hayo atayafanyaje? Ndiyo maana amekaririwa akilinganisha kusambaratika kwa Libya kuwa ni matokeo ya wananchi kutaka mabadiliko. Wanaojua siasa wasingeweza kulinganisha mabadiliko ya Libya na haya ya Tanzania ambayo hata yeye anakiri kutambua kuwa wananchi wana kiu ya mabadiliko.
Mbona hasemi mabadiliko yaliyotokea Tunisia ambayo ndiyo nchi ya kwanza kwa wananchi kuleta mabadiliko? Nadhani mabadiliko ya Tanzania yanafanana zaidi na yale ya Tunisia kwa kuwa yalitokana na wananchi wenyewe kuuchoka utawala wa rais Zainul Abidin. Yale ya Libya yalishinikizwa na nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani na yalitokea kwa vita kumtia adabu Muammar Gaddafi kwa tuhuma za kuunga mkono ugaidi wa kimataifa wakati haikuwa kweli.
Kwa kutokujua siasa, ndiyo maana anadhani kuondoa tatizo la rushwa ufumbuzi wake ni kuanzisha mahakama ya rushwa ambayo kwa maneno yake mwenyewe ili mafisadi na wala rushwa wafungwe haraka, Watanzania waishi kwa raha!. Tujiulize hivi kweli kuiondoa rushwa iliyokita mizizi kutafanikiwa kwa kuyafunga mafisadi na wezi tu? Mbona tulikuwa na sheria za uhujumu uchumi na bado uchumi ukahujumiwa?
Kwa mwanasiasa mweledi atatafuta chanzo na kiini cha rushwa badala ya kuanzisha mahakama ya rushwa, ambayo itaendeshwa na mahakimu na majaji walewale ambao wanahudumu katika mahakama zilizopo sasa. Kutegemea kuunda mahakama ya rushwa kumaliza tatizo la rushwa ni sawa na kutegemea kumaliza ugonjwa wa malaria kwa kugawa vyandarua vyenye dawa tu!
Bahati aliyonayo mgombea huyu wa CCM ni kwamba wananchi wengi wanaowasikiliza wagombea wa nafasi mbalimbali wana uelewa mdogo au wanafanya hivyo huku tayari wakiwa na mapenzi ya kufa kwa wagombea wao. Kibaya zaidi, katika mfumo wa kampeni wagombea hawahojiwi na hivyo hata wakisema chuya wapenzi wanajua ni mchele na watashangilia.
Ifike wakati vyombo vya habari visiishie tu kurusha matangazo ya wagombea au kuandika bali wayachambue yale yanayosemwa kujenga hoja zenye kuwafumbua macho na masikio wapigakura wawaelewe wagombea wanasema nini na kina athari gani kwa sababu kile kinachosemwa majukwaani katika kampeni wananchi wengi hawakielewi.
(Mwandishi ni mchambuzi wa masuala ya maendeleo. 0762 715311)
Wiki iliyopita nilikuwa nafuatilia hotuba ya mmoja wa wagombea urais aliyoitoa kwenye mkutano wake wa kampeni mjini Morogoro katika Uwanja wa Jamhuri unaomilikiwa na chama chake. Mkutano wake kwa hakika ulijaa watu wengi na kwa lugha ya kisasa nadiriki kusema kulikuwa na nyomi akiwamo Rais anayemaliza muda wake, Jakaya Kikwete.
Mgombea urais huyo akayatamka maneno ambayo yameniacha na tafakuri nzito kuhusu nini itakuwa hatima ya nchi yetu iwapo mgombea huyo atachaguliwa kuwa Rais. Kwa mashabiki au kwa manazi wa kisiasa na wakereketwa wa chama, maneno aliyoyatamka mgombea huyo yalipita na kutoweka katikati ya sauti za washangiliaji.
Mimi sifanyagi (sifanyi) siasa, na kwa bahati mbaya naweza nikawa si mwanasiasa mzuri. Mimi kwangu ni kazi tu yalikuwa maneno ya Dk John Magufuli. Hapa kazi ipo, kwamba rais ajaye anaweza akawa hajui siasa vizuri! Sikuamini masikio yangu kwa sababu ingekuwa ni katika nchi nyingine, kauli hii ingeweza kumkosesha urais kwa sababu wananchi wanamtegemea rais wao aijue vizuri siasa ili awaongoze vizuri.
Kama si kufanya siasa, chama cha siasa kitatawala vipi nchi? Sera za chama, ilani yao ya uchaguzi na maamuzi mbalimbali atakapokuwa madarakani yanategemea siasa kwa asilimia kubwa. Diplomasia na nchi za nje na mashirika ya kimataifa yanahitaji rais mwenye upeo mkubwa kisiasa hasa katika zama hizi za ulimwengu wa utandawazi.
Utatuzi wa masuala matatizo mengi ya wananchi kijamii, kiuchumi, kielimu na kujenga utawala bora ni mchakato wa kisiasa. Hata utekelezaji wa kauli zake kwamba anataka mabadiliko bora na si bora mabadiliko ni jambo linalotaka mchakato makini wa kisiasa.
Vinginevyo itakuwa ni ubabe wa kisiasa badala ya mabadiliko ya kisiasa. Pengine tuseme mgombea huyo alipotaja siasaalikuwa na maana ile ya mtaani yaani ujanja ujanja, hila, ghiliba, uongo au porojo?
Lakini ukiiangalia kauli mbiu yake Hapa ni kazi tu unaelewa kwamba huyu atakuwa rais mtendaji zaidi kuliko kuwa mwanafikra na mwanadiplomasia (stateman). Ikiwa hivyo, napata shaka kubwa kwamba tutashuhudia rais mwenye kutegemea kuchorewa ramani na wanasiasa kwa kuwa yeye hajui siasa.
Katika hali hiyo, anakuwa kama Waziri Mkuu badala ya kuwa Rais. Hofu yangu ni kwamba serikali yake itakuwa ya kiimla inayoongozwa na utendaji wa mtu mmoja jambo ambalo litakuwa ni hasara kwa Taifa.
Kama rais hajui vizuri siasa, ni ipi hatima ya vyama vya siasa, asasi za kijamii, vyombo vya habari na wadau wengine wa maendeleo ya nchi? Ni wazi CCM itahitaji kuwekeza vya kutosha katika kutengenezea timu yenye weledi wa siasa pale Ikulu ya Magogoni ili kuweka uwiano sawa kati ya Hapa ni kazi tu na ule upande wa rais unaohitaji weledi wake kisiasa ili kuivusha nchi salama. Vinginevyo kaulimbiu hapa kazi tu itakuja kuitokea puani hata CCM yenyewe.
Kila kitu ni siasa
Ulimwengu wa sasa karibu kila kitu ni siasa. Ili kujenga uchumi imara hahitajiki mtu kuwa mchumi mzuri pekee bali pia anahitajika kujua siasa za uchumi. Hivyo hivyo kutafsiri ilani ya uchaguzi ya chama kutoka kwenye maneno kwenda kwenye vitendo. Rais anapaswa kuijua vizuri siasa kwa sababu ilani ni tamko la kisiasa, ndiyo maana hata isipotekelezwa vizuri hakuna mtu anayefikishwa mahakamani kujibu mashitaka.
Sasa mtarajiwa wetu ambaye anakiri hadharani kuwa hajui siasa, hayo atayafanyaje? Ndiyo maana amekaririwa akilinganisha kusambaratika kwa Libya kuwa ni matokeo ya wananchi kutaka mabadiliko. Wanaojua siasa wasingeweza kulinganisha mabadiliko ya Libya na haya ya Tanzania ambayo hata yeye anakiri kutambua kuwa wananchi wana kiu ya mabadiliko.
Mbona hasemi mabadiliko yaliyotokea Tunisia ambayo ndiyo nchi ya kwanza kwa wananchi kuleta mabadiliko? Nadhani mabadiliko ya Tanzania yanafanana zaidi na yale ya Tunisia kwa kuwa yalitokana na wananchi wenyewe kuuchoka utawala wa rais Zainul Abidin. Yale ya Libya yalishinikizwa na nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani na yalitokea kwa vita kumtia adabu Muammar Gaddafi kwa tuhuma za kuunga mkono ugaidi wa kimataifa wakati haikuwa kweli.
Kwa kutokujua siasa, ndiyo maana anadhani kuondoa tatizo la rushwa ufumbuzi wake ni kuanzisha mahakama ya rushwa ambayo kwa maneno yake mwenyewe ili mafisadi na wala rushwa wafungwe haraka, Watanzania waishi kwa raha!. Tujiulize hivi kweli kuiondoa rushwa iliyokita mizizi kutafanikiwa kwa kuyafunga mafisadi na wezi tu? Mbona tulikuwa na sheria za uhujumu uchumi na bado uchumi ukahujumiwa?
Kwa mwanasiasa mweledi atatafuta chanzo na kiini cha rushwa badala ya kuanzisha mahakama ya rushwa, ambayo itaendeshwa na mahakimu na majaji walewale ambao wanahudumu katika mahakama zilizopo sasa. Kutegemea kuunda mahakama ya rushwa kumaliza tatizo la rushwa ni sawa na kutegemea kumaliza ugonjwa wa malaria kwa kugawa vyandarua vyenye dawa tu!
Bahati aliyonayo mgombea huyu wa CCM ni kwamba wananchi wengi wanaowasikiliza wagombea wa nafasi mbalimbali wana uelewa mdogo au wanafanya hivyo huku tayari wakiwa na mapenzi ya kufa kwa wagombea wao. Kibaya zaidi, katika mfumo wa kampeni wagombea hawahojiwi na hivyo hata wakisema chuya wapenzi wanajua ni mchele na watashangilia.
Ifike wakati vyombo vya habari visiishie tu kurusha matangazo ya wagombea au kuandika bali wayachambue yale yanayosemwa kujenga hoja zenye kuwafumbua macho na masikio wapigakura wawaelewe wagombea wanasema nini na kina athari gani kwa sababu kile kinachosemwa majukwaani katika kampeni wananchi wengi hawakielewi.
(Mwandishi ni mchambuzi wa masuala ya maendeleo. 0762 715311)