jMali
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 8,412
- 5,013
Huu mgogoro wa kipuuzi unaanza kuelekea pabaya. Ni muhimu EAC ikafanya haraka zaidi kuliko inavyofanya sasa. Ni rahisi mno kwa mgogoro kutoka kwenye siasa na kuingia kwenye ukabila. Mazingira ya Burundi yako fragile. Wananchi majority ni wahutu, watutsi ni minorities.
Serikali kwa kiasi kikubwa inaendeshwa na wahutu, lakini jeshi la burundi majority ni watutsi na wameshatoa tamko kuwa hawatakubali kuvunja katiba, ila tafsiri yao ya katiba hawajasema, sasa Nkurunzinza naye anadai yuko sahihi kikatiba, wanamaanisha hiyo hiyo ya Nkurunzinza au vipi? Watutsi wameanza kukimbilia Rwanda kutokana na vurugu za Imbonerakure, kikundi cha vijana wa chama tawala ambao wanafanya fujo dhidi ya wapinzani wa Nkurunzinza.
Ingawa hawalengi wapinzani watutsi pekee, kumbukumbu za Rwanda zinaonyesha hata Interahamwe nao walianza kisiasa vile vile. Endapo litatokea jambo kubwa dhidi ya kigogo wa kihutu mfano kama ilivyotunguliwa ndege ya Habyarimana, haitakuwa ngumu kwa hawa Imbonerakure kugeuka kuwa genociders kama Interahamwe walivyotoka kwenye siasa na kuingia genocide kule Rwanda.
Wahutu nao wanaogopa jeshi la Burundi na kiasi kidogo Imbonerakure, wanakimbilia Tanzania. Kila vurugu zikianza jeshi la burundi ambalo majority ni watutsi humalizia hasira zao kwao. Na wao wameona kabla shughuli haijawa kubwa bora waondoke mapema.
Kabla ukabila haujazidi siasa ni muhimu EAC kufanya haraka yafuatayo:
1. Kwanza wakati mazungumzo yanaendelea wazuie vikundi vya vijana kama Imbonerakure. Hawa vijana wasiachiwe kufanya shughuli zao whatever those are kwa muda huu.
2. Maongezi kati ya CNDD-FDD (chama kikuu cha wahutu na chama tawala) na UPRONA (chama kikuu cha watutsi) yawepo ili kuleta amani.
3. EAC ikusanye CNDD-FDD (chama kikuu cha wahutu na chama tawala) na UPRONA (chama kikuu cha watutsi), halafu iamue tafsiri sahihi ya mwisho ya katiba ya Burundi kuhusu Nkurunzinza ni ipi, na isimamie hapo. Kama ni against Nkurunzinza na Nkurunzinza ataleta jeuri, basi Burundi ipigwe sanctions kama wakati ule, kama ni for Nkurunzinza then mchawi anayechochea aumbuliwe. Hakuna haja ya maandamano kwa mtu yoyote asiyemtaka Nkurunzinza ili hali sio mwanachama wa CNDD-FDD. Kama uchaguzi uliopita ulikuwa huru na haki na ulitambulika kimataifa, kwa nini kuwe na wasiwasi wa kupiga kura dhidi ya Nkurunzinza? Wasiomtaka waende kwenye sanduku la kura! Kinachoonekana ni njama za makusudi za kuchochea itokee 'genocide' halafu jeshi lipindue kama linavyopinduaga kila siku, CNDD-FDD warudi tena msituni kama waasi halafu ngoma ianze moja...
Serikali kwa kiasi kikubwa inaendeshwa na wahutu, lakini jeshi la burundi majority ni watutsi na wameshatoa tamko kuwa hawatakubali kuvunja katiba, ila tafsiri yao ya katiba hawajasema, sasa Nkurunzinza naye anadai yuko sahihi kikatiba, wanamaanisha hiyo hiyo ya Nkurunzinza au vipi? Watutsi wameanza kukimbilia Rwanda kutokana na vurugu za Imbonerakure, kikundi cha vijana wa chama tawala ambao wanafanya fujo dhidi ya wapinzani wa Nkurunzinza.
Ingawa hawalengi wapinzani watutsi pekee, kumbukumbu za Rwanda zinaonyesha hata Interahamwe nao walianza kisiasa vile vile. Endapo litatokea jambo kubwa dhidi ya kigogo wa kihutu mfano kama ilivyotunguliwa ndege ya Habyarimana, haitakuwa ngumu kwa hawa Imbonerakure kugeuka kuwa genociders kama Interahamwe walivyotoka kwenye siasa na kuingia genocide kule Rwanda.
Wahutu nao wanaogopa jeshi la Burundi na kiasi kidogo Imbonerakure, wanakimbilia Tanzania. Kila vurugu zikianza jeshi la burundi ambalo majority ni watutsi humalizia hasira zao kwao. Na wao wameona kabla shughuli haijawa kubwa bora waondoke mapema.
Kabla ukabila haujazidi siasa ni muhimu EAC kufanya haraka yafuatayo:
1. Kwanza wakati mazungumzo yanaendelea wazuie vikundi vya vijana kama Imbonerakure. Hawa vijana wasiachiwe kufanya shughuli zao whatever those are kwa muda huu.
2. Maongezi kati ya CNDD-FDD (chama kikuu cha wahutu na chama tawala) na UPRONA (chama kikuu cha watutsi) yawepo ili kuleta amani.
3. EAC ikusanye CNDD-FDD (chama kikuu cha wahutu na chama tawala) na UPRONA (chama kikuu cha watutsi), halafu iamue tafsiri sahihi ya mwisho ya katiba ya Burundi kuhusu Nkurunzinza ni ipi, na isimamie hapo. Kama ni against Nkurunzinza na Nkurunzinza ataleta jeuri, basi Burundi ipigwe sanctions kama wakati ule, kama ni for Nkurunzinza then mchawi anayechochea aumbuliwe. Hakuna haja ya maandamano kwa mtu yoyote asiyemtaka Nkurunzinza ili hali sio mwanachama wa CNDD-FDD. Kama uchaguzi uliopita ulikuwa huru na haki na ulitambulika kimataifa, kwa nini kuwe na wasiwasi wa kupiga kura dhidi ya Nkurunzinza? Wasiomtaka waende kwenye sanduku la kura! Kinachoonekana ni njama za makusudi za kuchochea itokee 'genocide' halafu jeshi lipindue kama linavyopinduaga kila siku, CNDD-FDD warudi tena msituni kama waasi halafu ngoma ianze moja...