nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
[h=1]
[/h]
Na John Maduhu,Mwanza
Akizungumza na MTANZANIA Mjini Mwanza jana, Mgeja alisema ameshangazwa na taarifa zilizochapishwa na gazeti moja (siyo MTANZANIA), kuwa yeye na Wenyeviti na Makatibu wa Mikoa wako hatarini kutimuliwa kutokana na kuwa karibu na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowasa.
Alisema kinachowaunganisha wana CCM ni itikadi bila kujali rangi, dini au ukabila na kusisitiza kuwa urafiki wa mtu binafsi siyo suala la chama.
Suala la urafiki siyo suala la chama hata siku moja, hawa ni wanasiasa ucharwa jamani ambao wamekuwa wakipotosha umma kwa maslahi yao binafsi.
Kila mwanachama ana haki sawa na mwanachama mwenzake, lakini nashangaa baadhi ya wanasiasa ndani ya CCM wanapanga mikakati maalumu kwa ajili ya kuwashughurikia wenzao.
Sina kosa la kimaadili ndani ya chama na sijawahi kuitwa katika kikao chochote kwa kuvunja maadili, siogopi kufukuzwa kama itatokea nimefanya kosa la kimaadili na usaliti ndani ya CCM, lakini sitokubali kuchaguliwa rafiki.
Nina imani na Sekretarieti ya chama inayoongozwa na Katibu Mkuu, Wilson Mukama na kamwe haitoweza kupokea ushauri wenye nia ya kukiangamiza chama chetu.
Kwa hiyo, wana CCM mkoani Shinyanga, wapuuze maneno hayo na waendelee kuchapa kazi za kuimarisha chama chetu.
Wasisikilize hizi porojo za vibaka wa kisiasa ambazo hazisaidii bali zimelenga kukichafua chama, hoja zao hazina mashiko yoyote, mimi niko imara siku zote na nitaendelea kupigania haki ndani ya chama,alisema Mgeja kwa kujiamini.
[/h]
- Monday, November 14, 2011, 6:04
- Mtanzania-Habarihttp://www.newhabari.com/category/mtanzania-habari/
Na John Maduhu,Mwanza
Akizungumza na MTANZANIA Mjini Mwanza jana, Mgeja alisema ameshangazwa na taarifa zilizochapishwa na gazeti moja (siyo MTANZANIA), kuwa yeye na Wenyeviti na Makatibu wa Mikoa wako hatarini kutimuliwa kutokana na kuwa karibu na Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowasa.
Alisema kinachowaunganisha wana CCM ni itikadi bila kujali rangi, dini au ukabila na kusisitiza kuwa urafiki wa mtu binafsi siyo suala la chama.
Suala la urafiki siyo suala la chama hata siku moja, hawa ni wanasiasa ucharwa jamani ambao wamekuwa wakipotosha umma kwa maslahi yao binafsi.
Kila mwanachama ana haki sawa na mwanachama mwenzake, lakini nashangaa baadhi ya wanasiasa ndani ya CCM wanapanga mikakati maalumu kwa ajili ya kuwashughurikia wenzao.
Sina kosa la kimaadili ndani ya chama na sijawahi kuitwa katika kikao chochote kwa kuvunja maadili, siogopi kufukuzwa kama itatokea nimefanya kosa la kimaadili na usaliti ndani ya CCM, lakini sitokubali kuchaguliwa rafiki.
Nina imani na Sekretarieti ya chama inayoongozwa na Katibu Mkuu, Wilson Mukama na kamwe haitoweza kupokea ushauri wenye nia ya kukiangamiza chama chetu.
Kwa hiyo, wana CCM mkoani Shinyanga, wapuuze maneno hayo na waendelee kuchapa kazi za kuimarisha chama chetu.
Wasisikilize hizi porojo za vibaka wa kisiasa ambazo hazisaidii bali zimelenga kukichafua chama, hoja zao hazina mashiko yoyote, mimi niko imara siku zote na nitaendelea kupigania haki ndani ya chama,alisema Mgeja kwa kujiamini.