Mfumo wetu ujifunze kuwa na mbadala ili kuzuia ya Libya na kwingineko kwani ni vigumu kuzuia Mabadiliko

Mfumo wetu ujifunze kuwa na mbadala ili kuzuia ya Libya na kwingineko kwani ni vigumu kuzuia Mabadiliko

Burkinabe

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2023
Posts
2,752
Reaction score
4,800
Asalam Aleykum wana JF.

Ama baada ya salamu hizo, niende kwenye hoja moja kwa moja.

Ndugu zangu, upo usemi usemao "Duniani, kitu pekee ambacho hakibadiliki, ni mabadiliko!".

Mabadiliko hayakwepeki kwa hali na mali.

Hivyo ni vizuri mara zote kujiandaa kukabiliana na mabadiliko katika maisha yetu. Ni sawa tu na binadamu anaanza kama mimba, mtoto, kijana (wa kike au wa kiume), mtu mzima, Mzee na hatimaye kufa.

Kuna wakati unakuwa na Afya Njema, na kuna wakati unaumwa. Hayo yote ni mabadiliko na hatuwezi kuyakwepa.

Kwa hali hiyo basi, binadamu kwa asili ni kiumbe ambaye anapenda mabadiliko. Ndiyo maana hata chakula huwa tunabadilisha badilisha.

Hatuwezi kula makande kila siku, usiku na mchana kama ambavyo pia hatuwezi kula pizza kila siku mchana na usiku.

Kwa hali hiyo pia, hata linapokuja suala la serikali ni lazima kujua kwamba ni vigumu kwa chama kimoja kuongoza serikali milele. Hakipo na hakitakuwapo.

Hivyo ninashauri mfumo wetu (wengine kitaalamu wanauita "Deep State"), kuwa na chama mbadala na ikiwezekana watu mbadala ambao "wameandaliwa" kushika jahazi la kuongoza nchi yetu endapo ikatokea wananchi walio wengi wameamua hivyo.

Mfumo wetu usitumie nguvu nyingi kuyapinga mabadiliko, kwani kufanya hivyo ni sawa na kujaribu kuzuia mafuriko kwa mikono! Haiwezekani kabisa.

Najua kwa dhati kwamba idara yetu nyeti ni moja kati ya idara bora Afrika na hata duniani kwa ujumla.

Ubora huo wa mfumo, utumike kwa weledi kutuandalia mbadala kuliko kung'ang'ania chama au mtu ambaye hakubaliki kwa wale anaowaongoza.

Idara mnapaswa kuwa wazalendo kwa nchi na wala siyo chama au mtu. Idara haipaswi kuwa na uzalendo uchwara kama alivyosema Baba Askofu fulani wakati wa maazimisho ya Misa ya sikukuu ya Pasaka.

Kwenye Biblia, kitabu cha 1 Samweli 16:1, yupo nabii mmoja aliyekuwa anaitwa Samweli ambaye alikuwa ni mhafidhina (hakuwa mpenda mabadiliko). Yeye alitamani Mfalme Sauli aendelee kuongoza licha ya madhila aliyokuwa anawafanyia watu wake na uovu wake mbele za Mungu. Lakini tunaona Mungu anamwambia Nabii Samweli kama ifuatavyo,
*1 Samweli 16:1
[1]BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.*

Ni matumaini yangu, ujumbe wangu utaeleweka vyema zaidi na wahusika kwa ubora zaidi kuliko hata nilivyouwasilisha. Maana najua wao ni watu "smart" ambao huweza kutoa kilicho bora toka kwenye kibovu.
Ahsanteni sana.
 
1 Samweli 16:1
[1]BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.
 
Umeandika Kwa Maono, Busara na Hekima. , tatizo kubwa ni kwamba hapohapo Idara, Kuna mambo yamefanyika Nchi hii chini ya macho yao na mengine wakiyafadhili yao, Tena ni mambo yalojaa Uonevu mkubwa na ukiukajibwa Hali za watu.


Sasa wanaogopa , hawajiamin, hawamwamin yoyote, walichobakiza ni "Kukomaa na CCM, kwao ,ule msemo wa Zimwi likujalo halikuli likakumaliza ". Ndio unaozunguka Vichwan kwao.


Wangekua Neutral, mawazo yako haya mazuri, wangeyafanyia kazi.

Tupo na Deep State, wenye Uzalendo Uchwara, wanaojaribu kuwaambia watu kua Upinzani ukichukua Nchi, Machafuko yanaingia.

UKWELI NI KUA, CCM IMECHOKWA, YAAN WANANCHI WAMEICHOKA TU KWA CCM KUKAA MUDA MREFU, CCM HATA WATOE HUDUMA ZA AFYA BURE, MAJI BUTE, UMEME BURE, WALIPE MISHAHARA WASOKUA NA KAZI, BADO TU WANANCHI WAMEICHOKAAAA
 
Umeandika Kwa Maono, Busara na Hekima. , tatizo kubwa ni kwamba hapohapo Idara, Kuna mambo yamefanyika Nchi hii chini ya macho yao na mengine wakiyafadhili yao, Tena ni mambo yalojaa Uonevu mkubwa na ukiukajibwa Hali za watu.


Sasa wanaogopa , hawajiamin, hawamwamin yoyote, walichobakiza ni "Kukomaa na CCM, kwao ,ule msemo wa Zimwi likujalo halikuli likakumaliza ". Ndio unaozunguka Vichwan kwao.


Wangekua Neutral, mawazo yako haya mazuri, wangeyafanyia kazi.

Tupo na Deep State, wenye Uzalendo Uchwara, wanaojaribu kuwaambia watu kua Upinzani ukichukua Nchi, Machafuko yanaingia.

UKWELI NI KUA, CCM IMECHOKWA, YAAN WANANCHI WAMEICHOKA TU KWA CCM KUKAA MUDA MREFU, CCM HATA WATOE HUDUMA ZA AFYA BURE, MAJI BUTE, UMEME BURE, WALIPE MISHAHARA WASOKUA NA KAZI, BADO TU WANANCHI WAMEICHOKAAAA
Kweli Mkuu.
Watu wengi wamechoka sana.
Ni vile tu, wengi wetu hatuna ujasiri wa kutoa maoni hadharani.
Maana hata wana CCM wenyewe wengi ukiongea nao, wamechoshwa na sera onevu za chama chao!
 
napo soma na kusikia idara ni wajuvi sana huwa nacheka mnoo

wana ujuvi gani zaidi ya umbea na kujipendekeza
 
Asalam Aleykum wana JF.

Ama baada ya salamu hizo, niende kwenye hoja moja kwa moja.

Ndugu zangu, upo usemi usemao "Duniani, kitu pekee ambacho hakibadiliki, ni mabadiliko!".

Mabadiliko hayakwepeki kwa hali na mali.

Hivyo ni vizuri mara zote kujiandaa kukabiliana na mabadiliko katika maisha yetu. Ni sawa tu na binadamu anaanza kama mimba, mtoto, kijana (wa kike au wa kiume), mtu mzima, Mzee na hatimaye kufa.

Kuna wakati unakuwa na Afya Njema, na kuna wakati unaumwa. Hayo yote ni mabadiliko na hatuwezi kuyakwepa.

Kwa hali hiyo basi, binadamu kwa asili ni kiumbe ambaye anapenda mabadiliko. Ndiyo maana hata chakula huwa tunabadilisha badilisha.

Hatuwezi kula makande kila siku, usiku na mchana kama ambavyo pia hatuwezi kula pizza kila siku mchana na usiku.

Kwa hali hiyo pia, hata linapokuja suala la serikali ni lazima kujua kwamba ni vigumu kwa chama kimoja kuongoza serikali milele. Hakipo na hakitakuwapo.

Hivyo ninashauri mfumo wetu (wengine kitaalamu wanauita "Deep State"), kuwa na chama mbadala na ikiwezekana watu mbadala ambao "wameandaliwa" kushika jahazi la kuongoza nchi yetu endapo ikatokea wananchi walio wengi wameamua hivyo.

Mfumo wetu usitumie nguvu nyingi kuyapinga mabadiliko, kwani kufanya hivyo ni sawa na kujaribu kuzuia mafuriko kwa mikono! Haiwezekani kabisa.

Najua kwa dhati kwamba idara yetu nyeti ni moja kati ya idara bora Afrika na hata duniani kwa ujumla.

Ubora huo wa mfumo, utumike kwa weledi kutuandalia mbadala kuliko kung'ang'ania chama au mtu ambaye hakubaliki kwa wale anaowaongoza.

Idara mnapaswa kuwa wazalendo kwa nchi na wala siyo chama au mtu. Idara haipaswi kuwa na uzalendo uchwara kama alivyosema Baba Askofu fulani wakati wa maazimisho ya Misa ya sikukuu ya Pasaka.

Kwenye Biblia, kitabu cha 1 Samweli 16:1, yupo nabii mmoja aliyekuwa anaitwa Samweli ambaye alikuwa ni mhafidhina (hakuwa mpenda mabadiliko). Yeye alitamani Mfalme Sauli aendelee kuongoza licha ya madhila aliyokuwa anawafanyia watu wake na uovu wake mbele za Mungu. Lakini tunaona Mungu anamwambia Nabii Samweli kama ifuatavyo,
*1 Samweli 16:1
[1]BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.*

Ni matumaini yangu, ujumbe wangu utaeleweka vyema zaidi na wahusika kwa ubora zaidi kuliko hata nilivyouwasilisha. Maana najua wao ni watu "smart" ambao huweza kutoa kilicho bora toka kwenye kibovu.
Ahsanteni sana.
Hiyo Idara sijui wizara maalum ipo compromised.

Inalinda CCM na viongozi wake ndio maana Nchi ipo dormant miaka 60 ya uhuru.
 
Wakuu wa Idara wanaongoza kwa kukwepa kodi, wengine wana makampuni feki alafu unasema wako smart!! Lissu aliwahi kusema nchi hii inahitaji kuanza upya, yaani unashangaa mkuu wa Usalama amepiga dili ya 12bilioni wanaenda kugawana na wahujumu uchumi.

Kipindi kile kwenye uongozi wa Marehemu Magu alikamata magari zaidi 50 V8 bandarini walioshindwa kulipiwa kodi then wanyang'aji wa hao unaowaita usalama wakazitapeli na kuwagawia na michepuko.
 
Umeandika Kwa Maono, Busara na Hekima. , tatizo kubwa ni kwamba hapohapo Idara, Kuna mambo yamefanyika Nchi hii chini ya macho yao na mengine wakiyafadhili yao, Tena ni mambo yalojaa Uonevu mkubwa na ukiukajibwa Hali za watu.


Sasa wanaogopa , hawajiamin, hawamwamin yoyote, walichobakiza ni "Kukomaa na CCM, kwao ,ule msemo wa Zimwi likujalo halikuli likakumaliza ". Ndio unaozunguka Vichwan kwao.


Wangekua Neutral, mawazo yako haya mazuri, wangeyafanyia kazi.

Tupo na Deep State, wenye Uzalendo Uchwara, wanaojaribu kuwaambia watu kua Upinzani ukichukua Nchi, Machafuko yanaingia.

UKWELI NI KUA, CCM IMECHOKWA, YAAN WANANCHI WAMEICHOKA TU KWA CCM KUKAA MUDA MREFU, CCM HATA WATOE HUDUMA ZA AFYA BURE, MAJI BUTE, UMEME BURE, WALIPE MISHAHARA WASOKUA NA KAZI, BADO TU WANANCHI WAMEICHOKAAAA
Kama dirisha la udahili la idara ni UVCCM si mwendo wa kupewa maelekezo ya kulinda chama milele na milele amina
 
Asalam Aleykum wana JF.

Ama baada ya salamu hizo, niende kwenye hoja moja kwa moja.

Ndugu zangu, upo usemi usemao "Duniani, kitu pekee ambacho hakibadiliki, ni mabadiliko!".

Mabadiliko hayakwepeki kwa hali na mali.

Hivyo ni vizuri mara zote kujiandaa kukabiliana na mabadiliko katika maisha yetu. Ni sawa tu na binadamu anaanza kama mimba, mtoto, kijana (wa kike au wa kiume), mtu mzima, Mzee na hatimaye kufa.

Kuna wakati unakuwa na Afya Njema, na kuna wakati unaumwa. Hayo yote ni mabadiliko na hatuwezi kuyakwepa.

Kwa hali hiyo basi, binadamu kwa asili ni kiumbe ambaye anapenda mabadiliko. Ndiyo maana hata chakula huwa tunabadilisha badilisha.

Hatuwezi kula makande kila siku, usiku na mchana kama ambavyo pia hatuwezi kula pizza kila siku mchana na usiku.

Kwa hali hiyo pia, hata linapokuja suala la serikali ni lazima kujua kwamba ni vigumu kwa chama kimoja kuongoza serikali milele. Hakipo na hakitakuwapo.

Hivyo ninashauri mfumo wetu (wengine kitaalamu wanauita "Deep State"), kuwa na chama mbadala na ikiwezekana watu mbadala ambao "wameandaliwa" kushika jahazi la kuongoza nchi yetu endapo ikatokea wananchi walio wengi wameamua hivyo.

Mfumo wetu usitumie nguvu nyingi kuyapinga mabadiliko, kwani kufanya hivyo ni sawa na kujaribu kuzuia mafuriko kwa mikono! Haiwezekani kabisa.

Najua kwa dhati kwamba idara yetu nyeti ni moja kati ya idara bora Afrika na hata duniani kwa ujumla.

Ubora huo wa mfumo, utumike kwa weledi kutuandalia mbadala kuliko kung'ang'ania chama au mtu ambaye hakubaliki kwa wale anaowaongoza.

Idara mnapaswa kuwa wazalendo kwa nchi na wala siyo chama au mtu. Idara haipaswi kuwa na uzalendo uchwara kama alivyosema Baba Askofu fulani wakati wa maazimisho ya Misa ya sikukuu ya Pasaka.

Kwenye Biblia, kitabu cha 1 Samweli 16:1, yupo nabii mmoja aliyekuwa anaitwa Samweli ambaye alikuwa ni mhafidhina (hakuwa mpenda mabadiliko). Yeye alitamani Mfalme Sauli aendelee kuongoza licha ya madhila aliyokuwa anawafanyia watu wake na uovu wake mbele za Mungu. Lakini tunaona Mungu anamwambia Nabii Samweli kama ifuatavyo,
*1 Samweli 16:1
[1]BWANA akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe.*

Ni matumaini yangu, ujumbe wangu utaeleweka vyema zaidi na wahusika kwa ubora zaidi kuliko hata nilivyouwasilisha. Maana najua wao ni watu "smart" ambao huweza kutoa kilicho bora toka kwenye kibovu.
Ahsanteni sana.
CCM wanataka kuzuia mafuriko kwa mikono eti wakisema.............. hoyee!
 
Umeandika Kwa Maono, Busara na Hekima. , tatizo kubwa ni kwamba hapohapo Idara, Kuna mambo yamefanyika Nchi hii chini ya macho yao na mengine wakiyafadhili yao, Tena ni mambo yalojaa Uonevu mkubwa na ukiukajibwa Hali za watu.


Sasa wanaogopa , hawajiamin, hawamwamin yoyote, walichobakiza ni "Kukomaa na CCM, kwao ,ule msemo wa Zimwi likujalo halikuli likakumaliza ". Ndio unaozunguka Vichwan kwao.


Wangekua Neutral, mawazo yako haya mazuri, wangeyafanyia kazi.

Tupo na Deep State, wenye Uzalendo Uchwara, wanaojaribu kuwaambia watu kua Upinzani ukichukua Nchi, Machafuko yanaingia.

UKWELI NI KUA, CCM IMECHOKWA, YAAN WANANCHI WAMEICHOKA TU KWA CCM KUKAA MUDA MREFU, CCM HATA WATOE HUDUMA ZA AFYA BURE, MAJI BUTE, UMEME BURE, WALIPE MISHAHARA WASOKUA NA KAZI, BADO TU WANANCHI WAMEICHOKAAAA
Ccm naifanananisha na mwanamke mzee anayejipaka mkorogo ili avutie vijana. Lakini unakuta vijana hawampendi bali wanafuata hela zake, na yeye akiona humtaki anaamua kukuloga. Ccm ielewe kizazi kikichoka kimechoka, hakuna namna kitakukubali, sana sana itaishia kuumiza wanaoipinga, kupora chaguzi, na ni rahisi sana kuingiza nchi kwenye machafuko. Utaratibu mzuri ilikuwa na kuwa na vyama viwili vyenye nguvu, ambavyo vingekuwa vinabadilishana kwa ajili ya kupata ladha mpya.
 
Back
Top Bottom