Mfumo wa elimu Tanzania

MLA PANYA SWANGA

JF-Expert Member
Jul 31, 2015
5,184
5,435
Wanasema kuishi na kuwa na pesa ni ujanja tu.

Hapa Tanzania wale waliosoma shule wakawa wanashika nafasi za kwanza na za pili darasani hupelekwa kusomea mambo ya engineer wakavumbua na vitu.

Hawa wanaoshika nafasi za tatu wanaenda kusomea sheria na kuja kuwa mameneja wa hawa maelite wanasayansi.

Kuna hawa wanaoshika nafasi za nne wao hujiingiza kwenye siasa na kisha kuja kuwa mabosi na kuwatawala wote wanasheria na wanasayansi.

Kuna hawa waliofeli hawa wengi hujiingiza katika jeshi na kushika nyazifa kubwa na kumiliki njia za ulinzi hawa wote wakizingua jamaa wanapindua nchi na kutawala wote.

Lakini kuna huyu mtoro wa shule aliyekimbia shule yeye hujiingiza ktk jadi na kuwa mganga wa jadi kwa hiyo mwanasayansi, meneja mwanasheria, mwanajeshi humiminika kwake kama msafara wa kikombe cha babu wakapate kinga na watatue matatizo yao kwa njia za jadi na kumwachia mapesa mengi.

Hii ndiyo ecosystem ya elimu Tanzania yetu ndiyo maana unawaona mawaziri wanamwaga vitu vya ajabu ajabu bungeni tena wakiwa wanasheria huulizi wamevitoa wapi gamba laishia kiunoni.

Kutwa kucha mtaala wa elimu haueleweki yaani taifa halijajua linaenda wapi kielimu.
Ndiyo maana ubashite hauishi Tanzania elimu ndogo inaiongoza elimu kubwa.

Tufikie hatua tuishi kisayansi siyo kwa ramli za kitamaduni zisizo na evidential fact or data.
Mbunge anapeleka mswada wa kutaka sayansi ya usafiri wa ungo ihalalishwe aliyajulia wapi yote hayo?

8a12bf6175716c3993f94340074c67e3.jpg
65f14a529eeb5333bb2dcfa4d9c3ea2a.jpg
d8e54da3519c8677c43d821a4e95916e.jpg
4960d3fa0c4cabab4c25f6813bb9f947.jpg
cee2ab4baf3ca2651fc4e7783b92c8b3.jpg
c027ea86d499c7f1d5a191aef7a570b2.jpg

Tusipobadili mtaala wetu wa elimu tutaendelea na matukio zaidi ya ajabu kuliko hata haya.
 
Elimu yetu iliasisiwa na wakoloni walioitumia kwa manufaa yao, haikuwa ya faida kwa mwafrika.

Kibaya zaidi hata sisi wenyewe tumeshindwa kuibadilisha ili iendane na mazingira pamoja na mahitaji yetu.

Elimu ya TZ haiendani na mazingira yaliyopo na ndio maana wahitimu hawawezi kutumia elimu yao ili kukabiliana na changamoto zinazowazunguka kwenye mazingira. Kwa Tanzania ni vigumu sana kuona tofauti kati ya msomi na asiye msomi.

Kwa ufupi elimu yetu inatumia rasilimali nyingi lakini ipo off-target.

NB:Huyo anayejaza maji kwenye galoni ana fanana na Paul Makonda.
 
Elimu yetu iliasisiwa na wakoloni walioitumia kwa manufaa yao, haikuwa ya faida kwa mwafrika.

Kibaya zaidi hata sisi wenyewe tumeshindwa kuibadilisha ili iendane na mazingira pamoja na mahitaji yetu.

Elimu ya TZ haiendani na mazingira yaliyopo na ndio maana wahitimu hawawezi kutumia elimu yao ili kukabiliana na changamoto zinazowazunguka kwenye mazingira. Kwa Tanzania ni vigumu sana kuona tofauti kati ya msomi na asiye msomi.

Kwa ufupi elimu yetu inatumia rasilimali nyingi lakini ipo off-target.

NB:Huyo anayejaza maji kwenye galoni ana fanana na Paul Makonda.
Haahaahaahaaaaaa, weee noma.
 
Mafails wameamua kufanya biashara ya kununua watu. Nasikia mwingine kawajibu kuwa yeye hana bei hanunuliki. Tutaona mengi nchi hii.
 
Back
Top Bottom