'MESEJI' ya HUJUMA...

We jamaa hebu acha fitna..haiwezekani uifute hiyo namba. Kwa azingira yetu tulivyo tunafowadi SMS zenye muelelekeo km huu kwa ndugu jamaa na marafiki iweje wewe ulie kisha uifute. Sasa kama umeifuta hatuna haja ya kukuamini..
Mkuu kilichoniliza ni hiki.Kwanza nani kawapa nambari yangu? Kwanini wafanye mchezo kama huo? Nioneni mjinga,mzandiki,muongo,mwoga na kadhalika lakini huo ndio ukweli. Ni humu humu jamvini nilipotukanwa kwa kusema kuwa Madaktari wangegoma tena.Yalipotimia sikuombwa msamaha. Ngoja niwe msahimilivu tu Wakuu wangu...
 
mi nafikili jamaa hajielewi huyu
 
Kwa CCM yote yanawezekana.....naunga hoja mkono mia kwa mia mbili
 
wewe ulioleta hii issue nafikiri haujajipanga vizuri...utoto huu ulioandika kama kweki kuna kitu kama hicho unajua taratibu.
 
Mambo mengine ni kupotezeana mda tu!

Utanilipa kwakufanya niingie kwenye huu uzi mkuu!
 
Lete namba zako za cm watu tufanyie kazi, la sivyo tumia muda huu kabla MOD hajachukua hatua za kukurekebisha. Hapa Kazi tu mengine peleka MabweP.
 
Mkuu ni ngumu mtu kukuamini kwasababu hujaleta ushahidi.
 

wewe ni ME au KE??
 
Acha kutuhadaa wewe na MAGAMBA wenzio tutatoa maoni kama kawaida tena jana DODOMA wametoa maoni DHAIFU apunguziwe madaraka ole wake JAJI WARIOBA asizingatie hilo.
 
Ila umechemka sema "NDIO" umepokeaje sms na ukaifuta gafla hapo umeonyesha uzaifu na woga kama mtanzania halisi.Ungetupa iyo number na ss wenzako wa jf ili tuwe makini na tukipata sms iyo tusishtuke natujue ni yule yule anaeneza izo habari.
 
Wewe siyo mvivu wa kufikiria bali mzembe wa kufikiria
 

We unaota! vivid dreams
 

sidhani kama wangekutumia msg, kwa upeo wangu, na kwa jinsi vile issue yenyewe ilivyo sensitive, wange kupigia ili usiwe na ushahidi pindi utakapo kataa, na binafsi sijaona kilicho kuliza ni nini, wewe ulikua na hamu tu ya kulia,jipange kijana, hili ni jukwaa la watu makini, kuleta habari zisizo na ushahidi ukome, make sure unachoandika una ushahidi nacho,
 

Mkuu suluhisho ni kulia? kama kulia basi wapinzani leo tungekuwa tumekufa kwa kulia. Kama uko seriuos basi hakikisha unapambana sio kulia. Hapa tunapambana na uozo wa system hatulii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…