meru

meru

Harson

New Member
Joined
Feb 22, 2012
Posts
2
Reaction score
0
Habari za kuaminika ccm imekusudia kuvuruga uchaguzi arumeru
 
Ni kweli kabisa hata mimi nimezipata hizo habari.Wamesema hata wakipata kura moja ushindi ni lazima.Tumuombe tu Mungu aweke mkono wake.
 
Habari za kuaminika ccm imekusudia kuvuruga uchaguzi arumeru

Inawezekana una hoja, lakini inawezekana ni pumba tu na kunajaribu kuleta tetesi au majungu na hapa si mahala pake. Sasa basi ni wajibu wako kutueleza ni sababu gani zimekufanya uamini hivyo, ni mbinu gani zitakazotumika, wahusika ni kina nani, unashauri nini kifanyike ili kuzuia kadhia hiyo nk nk nk

Habari hizo zitasaidia kuzuia uovu huo na hatimaye haki kutendeka Arumeru Mashariki.
 
Habari za kuaminika ccm imekusudia kuvuruga uchaguzi arumeru
Hakuna nguvu ya dola iliyowahi kuishinda nguvu ya umma mahali popote hapa duniani. Tutapambana nao hadi tone la mwisho la damu.
 
Mbona habari za vurugu ni kila upande. Mtoa uzi anasema CCM imejiandaa kufanya vurugu nami nimesikia wafuasi wa CCM wakisema CDM wamejiandaa kufanya vurugu pindi mgombea wao akishindwa. Kwamba wataifanya Meru isitawalike. Yote hayo ni tetesi hakuna kilichothibitishwa. Ila kama wahenga walivyosema lisemwalo lipo kama halipo laja; basi ni wajibu wa vyombo vya ulinzi na usalama kuhakikisha kuna ulinzi na usalama wakutosha ili Arumeru isije kuingia katika historia ya vurugu za baada ya uchaguzi - PEV isj
 
hatawavuruge kivipi ccm tayari ilishazikwa Arumeru kesho tunakwenda kuwatupia udongo.
 
warafi ccm wana wabunge wote lakini wanang'ang'ania kiti kimoja kama majita
 
Back
Top Bottom