Membe umefaulu mtihani wa kwanza, songa mbele!

Membe umefaulu mtihani wa kwanza, songa mbele!

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
16,863
Reaction score
62,390
qsUgJjdE_400x400.jpg

Ndugu Membe,

Nakusalimia kwa salamu ya uzalendo.

Nichukue nafasi hii kukupa pole kwa misukosuko na mihangaiko ya kila siku ya maisha lakini pamoja na hayo nakupa pongezi tena pongezi za dhati kabisa kwa kusimama kidete kusema ukweli na kuutetea ukweli ukiwa ndani ya chama cha mapinduzi kwa ujasiri mkubwa kabisa. Katika nyakati hizi ambazo watu ndani ya chama cha mapinduzi wamejikunyata kama vifaranga vya kuku kwa uoga kwa bwana mkubwa na wapambe wake, wewe umesimama kidete kutaka utawala bora, kutaka demokrasia nchini, kutaka pasiwepo matendo ya kunyanyasa wananchi kisiasa.

Kutokana na hayo ningependa kuzungumza na wewe yafuatayo:

1: Mahasimu wako wanakuogopa, ndiyo maana wamekuchezea faulo kukutoa mchezoni
Ndugu Membe, walioko nyuma ya faulo uliyochezewa ndani ya CCM wanajua kuwa, kama mkisimama kwa vigezo vya ubora iliwemo uadilifu kwa taifa letu, kwa uzoefu wa uongozi, kwa exposure, kwa mipango mkakati ya kupambana na umasikini, kwa imani ya demokrasia pana katika nchi, kwa kuchukia rushwa, kwa utaalamu wa kuanalyse mambo mtambuka ya kinchi kisiasa, kiuchumi na kijamii na uwezo mkubwa wa diplomasia, hawa watu wanaujua uwezo wako, wanajua kuwa wewe ni tishio katika nafasi zao kwa sababu wanajua kuwa ukichukua fomu basi bwana mkubwa hana chance.

Wewe unajua vizuri tu kuwa bwana mkubwa kukalia kile kiti ni kwa sababu ya ugomvi wako wa kisiasa na mheshimiwa Lowasa, kwa hiyo aliokota dodo chini ya mnazi. Nje ya hapo mwaka 2015 mgombea kwa tiketi ya chama cha mapinduzi alikuwa ama uwe wewe au Lowasa, hilo analijua wazi na ndo maana kambi yake imejawa hofu baada ya wewe kuonyesha msimamo, wakaamua uchezewe figisu mapema kabla hujaingia uwanjani

2: Usikubali kusikiliza kelele za kukutaka ubwage manyanga
Ndugu Membe, baada ya tukio lilitokea la kufanyiwa figisu, wamejitokeza wale wanaojiita 'watoa ushauri', wanasema eti ukae kimya, usiongee, uachane na ndoto za kugombea urais. Mimi ningependa kukwambia kuwa usiwasikilize hao, hao ni watu waoga, fear mongers, hao ni quitters, hao ni appeasers wa madhalimu, hawana utofauti na Neville Chamberlain mwanasiasa wa uingereza kipindi cha vita kuu ya dunia ya pili aliyetaka Uingereza ifanye compromise fulanifulani na kiongozi wa Third Reich ya Ujerumani na kwamba Uingereza isimpinge na wala isimconfront. Laiti Winston Churchill angeusikiliza ushauri huo, huenda kule Birmingham wangekuwa wakiongea kijerumani sasa.

Ninachotaka kusema ni kwamba usisikilize kauli za hawa wanaotaka uiache azma yako adhimu ya kugombea uraisi ili uweze kuwakomboa watanzania waondokane na utawala wa kiimla, sera mbovu za kiuchumi, diplomasia inayofeli, siasa chafu za kununua watu, watu kufunguliwa kesi za uhujumu uchumi kwa sababu za kisiasa, Matumizi mabaya ya madaraka na umasikini wa kutisha.

3. Taifa linakuhitaji sana
Ndugu Membe, kama ulitaka kugombea uraisi kwa ajili yako binafsi basi achana na ndoto hiyo, ila kama kwa dhati ya moyo wako kwa ndani kabisa unadhani kwa dhati kabisa kuwa unataka kugombea uraisi kwa ajili ya wananchi wa Tanzania, kwa ajili ya kutengeneza serikali inayoheshimu Katiba, kwa ajili ya kutengeneza serikali inayoheshimu haki za watu wake kwamba wananchi wana haki za kuchagua viongozi wao bila kulazimishiwa kama tulivyoshuhudia katika uchaguzi feki wa serikali za mitaa uliopita.

Kama unaamini katika umoja na mshikamano wa kitaifa kuwa nchi hii ni yetu sote na kwamba kuwa na mawazo mbadala wa mawazo ya kisiasa siyo dhambi, kama unaguswa na umasikini wa watu wetu na unaamini kabisa katika kuheshimu bunge na mahakama bila kuziingilia basi Taifa linakuhitaji sana. Na kutokana na kwamba wewe tangu ukiwa kijana ulikula viapo vizitovizito vya kuitumikia nchi yetu kwa vipahi na akili zako zote, basi nakuomba sana mheshimiwa Membe uendeleze azma yako ya kugombea Uraisi ili uweze kutumia vipawa vyako vikubwa kuinusuru nchi kutoka katika hii free fall tunayoishuhudia inayoipeleka nchi katika shimo refu lenye kiza kinene

4: Uraisi hutoka kwa Mungu, usiache kuutafuta
Ndugu Membe, Mungu akitaka kukupa uraisi anaweza kukupa ukiwa ndani ya CCM au nje ya CCM.
Kwa hiyo usiache nia yako na azma yako njema kabisa ya kugombea uraisi eti kwa sababu mahasimu wako wamekuchezea faulo, kikubwa ni kuwa unapaswa kuutaka uraisi, unapaswa kuutafuta uraisi na unapaswa kuhakikisha hubwagi manyanga chini. Kama unavyojua, vitu vyenye thamani vinahitaji juhudi na kutokata tamaa, basi nakushauri uendelee kuutafuta uraisi hata nje ya CCM kwa ajili ya kulinusuru Taifa letu. Taifa letu liko njia panda, unaliachaje achaje?. Kama ipo ipo tu.

5. Wamekutosa kwenye Tanga, Piga mbizi kapande Jingine
Mahasimu wako wamekutosa baharini kwa sababu unautaka unahodha, wasichojua masikini ni kwamba wewe ndiye unayeijua njia bora, nahodha wanayempigania anawapeleka kwenye mkondo bahari ambapo wasipokuwa makini chombo chao kitapigwa dafrao na kuzama. Laiti wangalijua.

Ndugu Membe, wewe una uzoefu wa zaidi ya miaka 45 kwenye bahari ya uongozi, umeona mengi, unajua mengi, wamekutosa lakini kupiga mbizi unajua. Sasa ni wakati wa kupiga mbizi kuliwahi Tanga jingine la watu wanaojitambua ili kwalo uweze kushirikiana ili safari iendelee salama salmini.

6. Unao uungwaji mkono
Ndugu Membe, kutokana na hali ya kinchi na kutokana na ujasiri wako wa kusimama kidete na kusema pale wengine walipoufyata, umejipatia heshima kubwa mbele ya umma. Kutokana na hilo rightfully umejikusanyia mtaji wa imani ya wananchi mkubwa sana. Na napenda nikwambie, kama utaamua kusimama kidete na kugombea, nchi hii itazizima!. Watu wamechoka kaka, watu wanaugulia maumivu braza. Njoo waziwazi utangaze nia uone nchi itakavyozizima!. Sasa hivi wananchi wanasubiri mtu mzito, jasiri wa kujitokeza na kutamka kuwa yuko tayari kusimama kwenye uchaguzi kumng'oa huyu bwana.

7. Aluta continua victory Asceta
Mwisho nimalizie, kwa kauli ya mwanaharakati aliyepotea, ndugu Ben Saanane, aliyekuwa akipenda kuitumia, akimaanisha victory is certain, na mimi napenda kukwambia, Ushindi upo basi utafute

2020 Twende na Membe

Ni mimi Missile of the Nation (Kombora hatari kabisa la Ulinzi wa Taifa)
 
Kwa binafsi yangu mimi hawa watu wa CCM naamini lao ni moja, nahisi yuko kazini huyu, kwani kama CCM wanathubutu kwenda upande wa upinzani na kuwanunua walokesha kupunguza kura za CCM na kisha wanawapa hata kazi itakuwaje ngumu CCM kumfuata membe na kumrudisha nyumbani hasa wakihisi anafanya distruction kubwa kwao?

Pia anaweza kubanwa na vitimbi vya serikali hii kama kuzikamata mali zake, kuwanyanyasa ndugu zake, na hata kumnyoosha yeye kama yeye na kisha taratibu utamsikia, aaah mimi nimerudi nyumbani akseh, mi CCM ovyo.

Uyu ni mkazi wa CCM, kapitia tangu chipukizi, kaja UVCCM, wakampa uwaziri na vyeo kibao ni ajabu kumuamini kuwa ana nia njema nje ya CCM, ni very very mara chache akawa kama maalim Seif huyu
 
Huu mchezo tu wa kuigiza wakikutana maeneo wanagonga cheers ni swala la muda tu , Ccm wamecheza Karata Zao vizuri kuanzia kwa Lowasa na Vibaraka wake. Ndio wameufikisha upinzani hapo.
 
Huu mchezo tu wa kuigiza wakikutana maeneo wanagonga cheers ni swala la muda tu , Ccm wamecheza Karata Zao vizuri kuanzia kwa Lowasa na Vibaraka wake. Ndio wameufikisha upinzani hapo.

Hakuna cha mchezo wa kuigiza, Membe alikuwa anautaka uraisi kweli na hilo ndo lilikuwa kosa lake kubwa mbele ya bwana mkubwa.

Lowasa alifanya kweli mwaka 2015, Bwana Mkubwa anajua na Tume inajua. Na nguvu kubwa ya kuonea wapinzani na kununua wanaonunulika na wengine kuwaminyia njia zao halali za uchumi. Yote hii ni kwa sababu wana hofu ya kiluchowakuta mwaka 2015.

Itakuwa ni makosa makubwa wananchi kukubali kuaminishwa kuwa kila anayepambana na bwana mkubwa ndani ya CCM basi kisirisiri yuko naye.
 
Mkuu;
Umeandika mada ndefu bila kujua kuwa majibu ya mada yako yalishatolewa na kijana wa ''Membe''!

Mwaka 2012, Nape Nnauye aliwahi kusema kwenye kipindi cha Jambo Tanzania, TBC kuwa, "Samaki ukimtoa majini hana nguvu, CCM ni taasisi na ina nguvu, ukitaka kuwa na nguvu inabidi uwe ndani ya CCM, bila CCM mwanasiasa huwezi kuwa na nguvu, tutawatoa majini hawa samaki".

Maneno ya Nape Nnauye yalililenga kundi la Edward Lowassa na timu yake (Timu Lowassa) wakati wa vurugu za kisiasa ndani ya CCM. Maneno ya Nape yalidhihirisha ukweli baada ya Lowassa na kundi lake kuondoka CCM na kujikuta hana nguvu mpaka kuamua kurudi tena CCM.
 
kitu ambacho umesahau kuandika na kumshauri ni kwamba Membe alikuwa tishio kwenye social media na siyo ndani ya ccm, ona alivyotoswa, hana hata mfuasi mmoja wa ccm wa kumuongelea tena, tofauti nabule upande mwingine, wewe ukiwa mmoja wao wa kumuona kuwa alikuwa ni tishio, wamemwacha mwenyewe na vijana wake aliowatuma kwenye social media,

hata yale mabandiko humu jf ya twende na Membe 2020 yameishia njiani amebaki na msemaji wake tu Zitto Kabwe....usisahau ni namva five 2015, yaani ndo alikuwa wa mwisho kwa wale wagombeaji watano. Mwisho nina uhakika angepitishwa kugombea kwa tiketi ya ccm wewe ni mmoja wa watu ambao wangemkana kuwa hafai, hapa mnampamba tu kwa uongo na nyie ndo mmemharibia hadi akajiona mkubwa kuliko chama chake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bwana jela,
Tofauti ya Lowasa na Membe ni kwamba

1. Membe sasa hivi hana chama, yuko huru kwenda chama chochote wakati Lowasa alijiondoa mwenyewe CCM kwa hiyari na hivyo amerudi kwa hiyari yake

2. Pili Membe hajawahi kuwemo kwenye list of Shame ya Mafisadi. Lowasa alikuwemo kwenye List of shame iliyosomwa na CHADEMA pale Mwembeyanga.

Membe ni mtu safi
 
Najuzeni katiba ya CCM inasemaje kama mwanachama akishafukizwa uanachama? Kuna namna yoyote ile kudai haki yake? Nina maana yeye kukata rufaa?

Kama ndivyo je ni kikao gani kinachohusika kumsikiliza? Je Mwenyekiti wa hiyo kamati ama kikao a anakuwa ni nani?

Wazo langu ni kwamba njia mwepesi ya Membe kufikia ndoto yake ni kuhakikisha anapigania haki yake within, akipigania akiwa nje ya CCM ni vigumu mno.

Kazi ya kwanza ni kupigania kuurudisha uanachama wake.
 
Yatasemwa mengi sana maana humu pia zinaonekana kua na team mbalimbali so kila upande unavutia kwake. kimsingi tusubiri kauli ama maamuzi yake bwana Membe ndio yataamua kwamba anatania au yupo serious na Mchakato Oct 2020
 
CCM ilee au ipi?
Chomoa pamba sikioni na macho uyafungue. Kama nji,hali ikoje?
Washamba ni janga
 
tuwe na kiasi, umempa sifa ambazo hajawahi kuwa nazo, wenye uelewa tushajua uko kwenye pay roll yake kujaribu kumsafisha, hiyo ni kazi ngumu ndugu, we tafuna tu mpunga wake ila hasafishiki. Hana maadili.
 
Huu mchezo tu wa kuigiza wakikutana maeneo wanagonga cheers ni swala la muda tu , Ccm wamecheza Karata Zao vizuri kuanzia kwa Lowasa na Vibaraka wake. Ndio wameufikisha upinzani hapo.
Mawazo ya kizamani haya mkuu,kipindi Cha Lowasa kwenda CHADEMA,Wana CCM Hawa kulala kupigania chama,eti unasema ni Mpango wao!

Huu .. mtifuano mkali ndani ya CCM, unafikiri JK aliposema watu hawasalimiani alitania!

Hii Vita ilianza 1995 na haitamalizika Hadi tuwe na Katiba Bora!
 
Nilipoona unamsifia Membe kwa Uadilifu na kupambana na Rushwa nikahitimisha Hili ni Moja ya ANDIKO LA KIPUMBAVU kulisoma kwa week Hii.

Senti bai yuzingi tecno T301

Kama Membe angekuwa mla rushwa na Fisadi basi angelikuwa ameshafunguliwa kesi ya ufisadi nchini, Si mnasema Ngosha anapambana na ufisadi mbona sasa anawaacha hao mafisadi mtaani?
 
kitu ambacho umesahau kuandika na kumshauri ni kwamba Membe alikuwa tishio kwenye social media na siyo ndani ya ccm, ona alivyotoswa, hana hata mfuasi mmoja wa ccm wa kumuongelea tena, tofauti nabule upande mwingine, wewe ukiwa mmoja wao wa kumuona kuwa alikuwa ni tishio, wamemwacha mwenyewe na vijana wake aliowatuma kwenye ocial media, hata yale mabandiko humu jf ya twende na Membe 2020 yameishia njiani amebaki na msemaji wake tu Zitto Kabwe....usisahau ni namva five 2015, yaani ndo alikuwa wa mwisho kwa wale wagombeaji watano. Mwisho nina uhakika angepitishwa kugombea kwa tiketi ya ccm wewe ni mmoja wa watu ambao wangemkana kuwa hafai, hapa mbamoamba tu kwa uongo ba nyie ndo mmemharibia hadu akajiona mkubwa kuliko chama chake.

Sent using Jamii Forums mobile app
Utaongeleaje mtu ukose mkate wa kila siku. Ukishakuwa muoga na muendekeza njaa huwezi simama ktk kila unachokiamini zaidi tena ukiwa sio muadilifu.

Utaugulia tu ili mradi mkono uende kinywani.

Tutabadirika pale hizo tabia nilizotaja hapo juu zitakapo koma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Membe ana ujasiri gani au kafanya jambo gani la kuungwa mkono na watanzania??
 
Back
Top Bottom