Membe anatumika kuua upinzani?

technically

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2016
Posts
13,647
Reaction score
58,452
Mwaka 2010 waliotaka kumchallenge Kikwete ilikuwaje? mwaka 2000 je kwa Mkapa ilikuwaje? Membe kugombea urais mwaka huu anatumwa na nani? hata angekuwa yeye ndiye rais angekubali mtu mwingine apewe form? Sikubaliani Na Magufuli kwa mambo mengi ila kuna ajenda ya siri anayo Membe.

Membe anatumika kupoteza tension ya uchaguzi ndani ya vyama vya upinzani na kuteka social media ili wagombea wa upinzani wakose platform.

Membe ni mtu hatari kwa upinzani kuliko hata ccm kwenyewe mimi binafsi kama kuna chama cha upinzani hasa CHADEMA AU ACT watamkaribisha Membe nitamchagua Magufuli hatuwezi kurudisha nchi kwa hizi ngedere.
 
Unafikiri taratibu sana mkuu...
Kwahiyo mtu akitaka kufanya kitu kwenye nchi huru kama hii lazima atumike?
BTW upinzani ushindwe kushine kisa Membe katangaza nia kwel?
Wanasiasa waoga sana ...
Magufuli ana system ya kutosha kum discipline Membe wala sioni kama kuna haja ya kuzungumza mambo mengi na conspiracy theory za kubuni..
Acha nature ifanye kaz yake ...
 
Duh hivi mwaka 2000 na 2005 kina nani walijitokeza kuchukua Fomu za Urais bara?

Wajuvi tupeni kumbukumbu
 
Hahaaa naona homa kali hapo imeanza kuingia kwa ccm, sumbukeni na Membe kwanza halafu mje mkutane na chama dume CDM.
 
Kwa hili sikukubaliani na wewe,mengi umeandika humu nimerespond positively lkn kwa hili hapana
 
Itajulikana June hadi October
 
[emoji28][emoji28][emoji28]

Membe ni kamanda tumuamini

Membe mkombozi wetu sisi chadema

Membe akigombea tutadeki barabara kuanzia Mbagala hadi Nanyumbu
Membe ndiye mgombea wa kiti cha Urais kupitia CCM mwaka huu ni suala la muda tu
 
Mkuu mbona kama utabiri huu sioni kama unamatumaini ya kuweza kutokea?
Yeye mwenyewe ametamka kuwa between June and October, maajabu yatatokea...........

Kwa kuwa hatujafika hiyo October, hebu tuwe na subira na kuyashuhudia hayo maajabu ya dunia yakijitokeza hapa TZ
 
Tumeshaanza maandalizi, kamanda membe anatosha 2020.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…