Membe alitupeleka china kutuandaa na 2015

Membe alitupeleka china kutuandaa na 2015

Andrew123

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2012
Posts
8,405
Reaction score
11,196
Sisi marais wa vyama vya wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania tumelipiwa safari(nauli &pesaya kujikimu) ya kwenda na kurud China kwa gharama za mhe. kama njia ya kutaka support yetu wakati ukifika kutafuta kura 2015. CDM mtajibeba 2015 mmezidi ubahili.
 
hivi membe yupo serious kweli eeh! kimchezo mchezo anaweza kuchukua nchi hii 2015.
 
mmmhhhh wewe ndo raisi ya chuo kweli unaongea maneno kama hayo,,,,,,na kama mtu anaongozwa na wewe basi wote mtakuwa vilaza
 
duuh nchi hii ni ya ajabu full fitna. membe ameanza na kasi ya ajabu
 
Sisi marais wa vyama vya wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania tumelipiwa safari(nauli &pesaya kujikimu) ya kwenda na kurud China kwa gharama za mhe. kama njia ya kutaka support yetu wakati ukifika kutafuta kura 2015. CDM mtajibeba 2015 mmezidi ubahili.

We ni Mtanzania wa aina yake. Zandiki, Jambawazi, fisadi kabisa weye!
Yaani unaona sifa kutangaza kununuliwa kwa kisafari cha China na ukakubali. Kwani wote wanaoenda China wanpelekwa na Membe? What was so special mpaka mmepoteza akili zenu? Hivi nyie ndiyo wasomi tunaowangojea? Naomba niwe nimekufa wakati kizazi chako kinapofikia kutoa hata Mkuu wa wilaya.

Hii ni tabia ya kukemewa, kwani siyo tu inaonyesha ujinga wa mtu hadharani,bali pia inahamasisha rushwa. Kwamba na CHADEMA waje nyie mko tayari kupokea! I feel like throwing out.
 
Elly B hata ungekuwa wewe unaletewa tiketi ya kwenda na kurudi China na hela ya matumizi utakataaa kisa nini?
 
Mkapa alipewa nchi AKAISHIA kuuza Madini, Mashamba, hifadhi za Taifa, Viwanda hadi TANESCO...Mnataka kuturudisha kusini ili muuze Chuma kilichogundulika Tanga au? Huyo Membe mnae jitahidi kumnadi mpaka sasa amedeliver nini kwa Watanzania? Kama Criteria ya kumpata Rais wa Tanzania itakuwa Majungu na Fitna BASI Joka la Mdimu ataongoza kwa mbaliiiiii ... I wish CCM wamsimamishe Membe ili unabii utimie!!! "Mpasuko wa Kudumu ndani ya CCM"...
 
Kumbe we uko kipesa zaidi na si kutetea wananchi,nenda india uulizie hbr ya chama tawala kilivyoshindwa japo kilitoa pesa.
 
CCM IKO KWENYE AMBULACE KUELEKEA ICU.
Membe from no where anataka Urais kwa kuwalaghai vijana kwa ajira na scholarship.
Membe hajawahi kukutana na mikikimikiki na matatizo magumu ya watanzania na akaonyesha hata njia ya kutokea,leo hii anataka Urais wa nchi .Angalau urais wa Club ya Simba ungeweza ukamtosha.

Hehu tujiulize kama sio kubebwa na Familia ya Kikwete,kuanzia mwaka 2000 mpaka 2005 nani aliwahi kumsikia Membe bungeni hata tu akiishauri serikali au kuikosoa achilia mbali hata kuisifia basi.

UKAWA kazeni buti CCM mwaka 2015 inapeleka Mhitimu wa Chekechea chuo kikuu badala ya kuanza darasa la kwanza.
 
Elly B hata ungekuwa wewe unaletewa tiketi ya kwenda na kurudi China na hela ya matumizi utakataaa kisa nini?

Kuchukua ama kutochukua, hayo ni matashi binafsi. Kuna anayeweza kuchukua na akafanya anavyojua yeye, wengine wana dhamiri nyepesi. Wakishachukua dhamiri zao zinawasuta kwa usaliti na kwa hiyo ili wawe na amani japo kidogo inabidi wafanye kama walivyokubaliana.

Kwa mimi binafsi, nakuhakikishia kuwa sihitaji kupewa chochote ili nifanye mtu yeyote anavyotaka. Napenda sana hali ya kuwa in control of everything around me. Kwa hiyo siwezi kujiuza halafu nipoteze uwezo wangu wakusema na kufanya kama ninavoamini na kujisikia. ukifuatilia michango yangu hata humu JF utagundua mimi ni mtu wa aina gani.

Sijawahi kununuliwa, sihitaji kununuliwa na sitegemei kununuliwa. Nakuhakikishia kuwa kama ni safari nitaenda popote, wakati mimi nataka kwenda huko,na nitakwenda kufanya ninachotaka kufanya mimi! That's me.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Tuondolee utoto wako mada hata haieleweki inazungumzia nini.
 
Ingekuwa kweli ungekuja kuropoka hapa! China? Ungedanganya London,Dubai, New York hivi and other western world ni bora kwa shopping and vacation. China pollution tu huko! ACHENI KUCHAFUANA
 
Nyie ndio mnajiita wasomi tena viongozi wa wasomi......kama mpaka membe kaweza kuwashika akili no wonders hata shamba boy wangu anaweza kuwashika akili.....poleni sana kwa fedheha na kadhia hii
 
Sisi marais wa vyama vya wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania tumelipiwa safari(nauli &pesaya kujikimu) ya kwenda na kurud China kwa gharama za mhe. kama njia ya kutaka support yetu wakati ukifika kutafuta kura 2015. CDM mtajibeba 2015 mmezidi ubahili.
Rais wa chuo ndiyo anaandika hovyo kiasi hiki kazi tunayo.
Haya twambie china mlikuwa mnafanya biashara gani make china zipo biashara nyingi mkuu.
 
Nyie ndio mnajiita wasomi tena viongozi wa wasomi......kama mpaka membe kaweza kuwashika akili no wonders hata shamba boy wangu anaweza kuwashika akili.....poleni sana kwa fedheha na kadhia hii
Mkuu huyu hana usomi wala uongozi wowote katika taifa hili ila ni bavicha wa kawaida tu.
 
Back
Top Bottom