Mechi ya waheshimiwa wabunge

Mechi ya waheshimiwa wabunge

POMPO

JF-Expert Member
Joined
Mar 12, 2011
Posts
6,690
Reaction score
2,402
Wakuu,
kuna matangazo mbalimbali yanaendelea hapa nchini kuwa kutakuwa na mechi ya mpira wa miguu uwanja wa taifa DSM, JMosi kati ya waheshimiwa wabunge wapenzi wa YANGA dhidi ya wazao wapenzi wa SIMBA, hivyo itakuwa ni SIMBA vs YANGA.
wana JF:

Je ni sahihi kwa (wanasiasa)wawakilishi wetu kushiriki mchezo huo aliakuwa nchi inakabiliwa na mgomo wa madaktari? I mean watu wanapoteza maisha, wanateseka na ni miungoni mwa watu waliowachagua wakawawakilishe?
nimeweka uzi huu jukwaa la siasa, wanashiriki wanasiasa wetu, mbaya zaidi ni wote hata wa upinzani.
Tafakari.
 
JK LAZIMA AWE REFA MECHI YA WABUNGE

Na Haruni Sanchawa
MBUNGE wa Iramba Mashariki, Mwigulu Nchemba amesema kuwa Rais Jakaya Kikwete ni lazima awe refa wa pambano la wabunge wapenzi wa Simba na Yanga litakalopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Julai 7, mwaka huu.
Kauli ya Nchemba aliyoitoa juzi kwa mwandishi wetu inapingana na ile ya Mbunge wa Kigoma Mashariki, Zitto Kabwe ambaye ni mchezaji wa wabunge wa Simba aliyesema kuwa Rais Kikwete hafai kuwa refa wa pambano hilo kwa kuwa ni shabiki mzuri wa Yanga na anaamini kuwa atawapendelea wabunge wa timu anayoishabikia.
"Zitto ni muoga tu, wasubiri kichapo, Rais Kikwete hawezi kutupendelea sisi (Wabunge wapenzi wa Yanga) na ukweli huo utaonekana siku hiyo ya mchezo," alisema Nchemba.
Pambano la Wabunge wa Simba na Yanga linangojewa kwa hamu kubwa na wapenzi wa soka kwani ni la aina yake na kwa mujibu wa mmoja wa waratibu wa pambano hilo, Luqman Maloto, viingilio vimepangwa kuwa shilingi 10,000 kwa viti maalum (VIP) na shilingi 5,000 kwa viti vya kawaida.
Maloto alisema anaamini pambano hilo litakalofanyika siku ya Usiku wa Matumaini litakuwa kali na la kusisimua kutokana na kila upande kujiandaa vyema. Licha ya mpira wa miguu kutakuwa na burudani mbalimbali uwanjani hapo ambapo mwanamuziki Chamelione wa Uganda na Diamond wa Tanzania watatumbuiza na wapenzi wa ngumi watajionea mchezo huo.
 
Nimemkumbuka Mac vivien foe.
Kama kuongea tu huanguka na kuzimia.
Ili kutuokoa na ccm, Mungu anatuletea ukombozi bila kugoma wala kuandamana.
Mpeni kipyenga jk tuingie kwenye uchaguzi!!!!
Wabunge wa upinzani nawashauri wasitie mguu uwanjani ili kuepuka kisingiziwa wamemkata mitama kwa stail ya kigaidi
 
Hahahahahaaa!!
Akivua kibarakhashia tu Yanga wanafungwa!!!
 

Huu ndo tunauita upompompo hivi bongo timu ni Simba na Yanga tu? Hivi mnajua kinachoua soka la bongo ni usimba na uyanga? Aaa argh! Wanauzi bora wangejigawa kwa mfumo mwingine ila sio wa usimba na uyanga Sasa sisi mashabiki wa AFC, toto, nyota nyekundu, mecco, reli, mbanga FC tushabikie wapi?
 
Acheni kukurupuka, sio kila kitu mnapinga tu. Mechi ya leo, pamoja na michezo, imeandaliwa ili kukusanya fedha za kusaidi ujenzi wa mabweni ya wasichana wanafunzi sehemu mbalimbali za nchi.
 
Acha upoyoyo timu ulizo zitaja ni matawi ya Simba na Yanga na wachezaji wengi wa timu hizo utakuta ni wanazi wa ama Simba au Yanga na yanga na Simba hawajaua soka nchii.. kinachouwa soka ni mfumo mzima wa soka la tanzania kuanzia TFF...

Huu ndo tunauita upompompo hivi bongo timu ni Simba na Yanga tu? Hivi mnajua kinachoua soka la bongo ni usimba na uyanga? Aaa argh! Wanauzi bora wangejigawa kwa mfumo mwingine ila sio wa usimba na uyanga Sasa sisi mashabiki wa AFC, toto, nyota nyekundu, mecco, reli, mbanga FC tushabikie wapi?
 
wengebaki dodoma kupitisha bajeti ,hiyo mechi ina tija gani kwa taifa
 
Acha upoyoyo timu ulizo zitaja ni matawi ya Simba na Yanga na wachezaji wengi wa timu hizo utakuta ni wanazi wa ama Simba au Yanga na yanga na Simba hawajaua soka nchii.. kinachouwa soka ni mfumo mzima wa soka la tanzania kuanzia TFF...
nilijua wauwaji wa soka la bongo Simba na Yanga mtakuja juu! Hivi AFC ni tawi la Simba au Yanga? Wachezaji wa kibongo kipimo CHA mafanikio kisoka ni hizo timu ambazo mfumo, na serikali inazibeba lakini mafanikio yake ni madogo ila ni MAKUBWA ukilinganisha na vilabu vingine kwa Mara nyingine tena muhimili mwingine wa dola unazitangaza Simba na Yanga.... Huyo Nchemba anashabikia wakati Singida hamna timu ni muongo Sasa hivyo hivyo Zitto Kigoma hamna kitu anakalia usimba na uyanga
 
Ndio mech kati ya wabunge wa yanga na simba
UPDATE zitto anachezea simba ni noma kumbe na mpra anaujua . Nchemba nae yupo ft anachezea yanga
 
Back
Top Bottom