beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,881
- 6,377
Jeshi la Polisi mkoani Pwani linamshikilia Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste lililopo Kongowe Wilaya ya Kibaha, Japhes Manwa (40), kwa tuhuma za kumchoma moto mwanawe.
Mchungaji huyo anadaiwa kumfanyia unyama mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miaka saba sehemu za mikononi na mgongoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, alisema, tukio hilo liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Kibaha juzi majira ya mchana.
Inadaiwa kuwa mtoto huyo mwenye ulemavu (mtindio wa ubongo) mkazi wa Vikuge Kata ya Soga, ni mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Kalabaka.
Kamanda Wankyo alisema, mtoto huyo, ambaye ni kati ya watoto wanne wa mtuhumiwa alikutwa na mkasa huo kwa madai kuwa baba yake hampendi.
Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wazazi na walezi wanaotoa adhabu kali kwa watoto kwa lengo la kuwakanya ambazo zinawasababishia majeraha na ulemavu.
Alisema, wazazi na walezi wanatakiwa kutoa adhabu kulingana na makosa na umri wa watoto.
Mchungaji huyo anadaiwa kumfanyia unyama mtoto huyo wa kiume mwenye umri wa miaka saba sehemu za mikononi na mgongoni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Wankyo Nyigesa, alisema, tukio hilo liliripotiwa katika Kituo cha Polisi Kibaha juzi majira ya mchana.
Inadaiwa kuwa mtoto huyo mwenye ulemavu (mtindio wa ubongo) mkazi wa Vikuge Kata ya Soga, ni mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Kalabaka.
Kamanda Wankyo alisema, mtoto huyo, ambaye ni kati ya watoto wanne wa mtuhumiwa alikutwa na mkasa huo kwa madai kuwa baba yake hampendi.
Kufuatia tukio hilo, Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wazazi na walezi wanaotoa adhabu kali kwa watoto kwa lengo la kuwakanya ambazo zinawasababishia majeraha na ulemavu.
Alisema, wazazi na walezi wanatakiwa kutoa adhabu kulingana na makosa na umri wa watoto.