Mchumi BoT: Kwanini fedha imepotea mifukoni

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
Mchumi BoT: Kwanini fedha imepotea mifukoni?
Apr 06, 2017 by Raia Mwema in Habari
MCHUMI katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Lusajo Mwankemwa, amesema muda si mrefu Watanzania wataanza kuona mzunguko wa fedha ukirejea katika hali iliyozoeleka.

Akizungumza na Raia Mwema mjini Zanzibar mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwankemwa alisema Watanzania wanalalamika kuwa fedha hazipo kwa sababu serikali imeelekeza fedha zake katika maeneo mengine muhimu kwa uzalishaji na matokeo yataonekana kabla ya mwaka 2020.

“Kwanza niseme mapema kwamba fedha ipo kwenye mzunguko lakini haipo kwenye mzunguko ambao watu walikuwa wameuzoea katika miaka iliyopita.

“Kwa mfano, labda watu walikuwa wanasafiri sana na wanalipwa masurufu ya safari zao. Au watu walikuwa wanapata posho mara kwa mara kutokana na mikutano ya kikazi.

“Ile hela ambayo mtu alikuwa anapata, labda alikuwa anaitumia kujenga nyumba yake. Akijenga maana yake fundi ujenzi anapata fedha. Fundi akipata hela ananunua vitumbua kwa mama lishe. Huyu mama akipata hela ananunua sukari kwa muuza duka. Hapo utaona namna fedha inavyozunguka. Ndivyo ilivyokuwa huko nyuma.

“Sasa siku hizi hali ni tofauti kidogo. Ile hela ya posho zisizo za lazima na matumizi mengine yasiyo na faida sana imeondolewa huko na kwenda kujenga barabara au kununua ndege.

“Sasa ukinunua ndege inawezekana hela isizunguke kwa sababu ndege inatengenezwa nje ya nchi. Lakini, ukifufua shirika la ndege, unarahisisha usafiri na kuchochea kukua kwa utalii. Vyote hivyo ni vichocheo vya uchumi.

“Kwa maana nyingine, mtu ambaye kwa sasa yuko kwenye sekta ya miundombinu anaona namna fedha inavyozunguka lakini wale wengine hawaioni,” alisema mchumi huyo.


Katika hali ya kawaida, alisema BoT huwa inafahamu kiwango chote cha fedha ambacho kiko katika mzunguko na kwamba kikiwa kimezidi mahitaji, huwa kinapunguzwa na kikiwa pungufu, benki huongeza ujazi wa fedha.

Alisema ujenzi wa viwanda unaoendelea sasa, ufufuaji wa Shirika la Ndege la ATCL, Uboreshaji wa Bandari ya Dar es Salaam na nyinginezo nchini ni mambo yanayohitaji gharama kubwa lakini yakikamilika, uchumi utaimarika na mzunguko utakuwa mzuri.

“Miundombinu ikiboreshwa, maana yake ni kwamba wakulima watakuwa jirani na masoko ya bidhaa zao. Viwanda vikikamilika, maana yake ni kwamba ajira zitaongezeka pamoja na mahitaji ya malighafi.

“Uboreshaji wa bandari zetu utaongeza ufanisi na kuchochea wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi kuitumia. Nina matumaini makubwa kwamba hali itaboreka mara viwanda vitakapoanza uzalishaji na kila uwekezaji kuanza kazi rasmi,” alisema.

Kuzimua uchumi

Mkuu wa Idara ya Uhusiano na Itifaki wa BoT, Zalia Mbeo, alisema kitendo cha taasisi hiyo kupunguza kiwango cha amana ambacho benki zilizopo nchini huweka kama dhamana (Statutory Minimum Reserve-SMR) kutoka asilimia kumi hadi asilimia nane, kina lengo la kusaidia kuboresha mzunguko wa fedha nchini.

Alisema kama benki ilitakiwa kuweka shilingi 100 kama dhamana yake BoT, sasa itaweka shilingi 80 na hivyo inaweza kuzitumia shilingi 20 zilizobaki kwa shughuli muhimu za kibenki kama vile kukopesha na kupunguza riba.

“Unajua kama benki ina fedha kidogo, maana yake ni kwamba itakopesha watu wachache na kwa riba kubwa. Lengo la BoT katika kushusha SMR ni kuziongezea benki ukwasi na hivyo kuziwezesha kukopesha watu wengi zaidi na kwa riba nafuu.

“Kama watu wataweza kupata mikopo itawasaidia katika shughuli zao za kibiashara ambazo ndizo huchochea mzunguko wa fedha. Kama riba si kubwa sana, maana yake watu wengi wanaweza kujitokeza kukopa,” alisema Zalia.

Hali ya uchumi nchini

Wakati BoT ikitoa picha hiyo ya matumaini, kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi, wasomi, wanasiasa na wafanyabiashara kuhusu mwenendo wa hali ya uchumi nchini.

Mwezi uliopita, Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), lilitoa ripoti yake iliyosema kwamba ingawa ukuaji wa uchumi wa Tanzania ni wa kuridhisha, mambo manne yanaweza kuathiri hali hiyo.

Sababu nne kubwa zilizotolewa na IMF kuhusu hofu hiyo kwa Tanzania ni kutotabirika kwa sera zake za uchumi mpana, kutokua kwa sekta ya mikopo, kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi ya uwekezaji na kubinywa kwa sekta binafsi na serikali.

Sekta binafsi imeathiriwa na baadhi ya vitendo vya serikali ya Rais John Magufuli, likiwamo agizo la kutaka taasisi za serikali zifanye biashara zenyewe kwa zenyewe kabla ya kufikiria sekta binafsi.

Pia, agizo hilo lilitaka taasisi za serikali kufanyia mikutano yake katika kumbi zao za mikutano badala ya hoteli binafsi kama ilivyozoeleka katika miaka ya nyuma.

Hatua hiyo imeiumiza sekta binafsi kwa sababu kwa Tanzania, serikali ndiyo mhimili mkubwa wa uchumi na si sekta binafsi kama ilivyo kwa nchi zilizoendelea. Kwa maana hiyo, wakati inapofunga milango yake kwa sekta binafsi, athari zake huwa kubwa.

Wakati huo huo, serikali pia imeondoa katika benki binafsi kiasi cha shilingi bilioni 500 zilizokuwa zimehifadhiwa na taasisi zake na kwenda kuzihifadhi BoT.

Hatua hiyo imeelezwa kupunguza ujazi wa fedha katika benki za biashara zilizopo nchini; na pengine ndiyo sababu BoT imeamua sasa kupunguza kiasi hicho cha dhamana ya benki.

Mmoja wa wachumi mashuhuri nchini, Profesa Honest Ngowi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, ameliambia gazeti hili kwamba kama serikali itaendelea na utaratibu wake wa kubana matumizi hususani yale yanayozimua sekta binafsi, hali ya uchumi itaendelea kubaki kama ilivyo.

Kudhihirisha ukweli wa kauli ya Ngowi, Chama cha Wamiliki wa Hoteli hapa nchini (THA), kimetoa taarifa inayoonyesha kwamba mapato ya hoteli hapa nchini yameporomoka kwa asilimia 40 katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.

Mmoja wa viongozi wa THA, Latifa Sykes, alinukuliwa katika baadhi ya vyombo vya habari wiki hii akisema kwamba mwaka jana pekee, takribani hoteli 400 hapa nchini zilipigwa mnada kutokana na kushindwa kulipa mikopo waliyokopa benki kwa sababu ya kuyumba kwa biashara.

Pia, mwishoni mwa mwezi uliopita, Kampuni ya Konyagi ilitangaza kupunguza wafanyakazi 50 kutokana na hali mbaya ya biashara iliyosababishwa na hatua ya serikali kupiga marufuku pombe za viroba.
 
Atumbuliwe kama Mafuru!

Mafuru said the same exact thing!

Magu peke yake ndio anajua wapi kuna njaa na wapi hakuna mzunguko wa pesa.

Magufuli baba, mtumbue na huyu mjuba anaejifanya katibu mwenezi wa BOT, kajiongelea bila consultation with the State House, usimcheleweshe, mchinjie baharini!
 
It is unfortunate kuwa hawa wachumi wetu hawasemi ukweli wa hali halisi ilivyo nchini; wanaposema kuwa hali itaimalika nchini mara hapo viwanda vitakapoanza uzalishaji hivyo viwanda viko wapi? Ili watu wawekeze katika ujenzi wa viwanda ni lazima kuwa na sera rafiki za uwekezaji na hakuna kitu kinakatisha tamaa uwekezaji katika nchi yeyote kama UNCERTAINTY yaani kuwa na sera zisizotabilika!! When you have an environment of uncertainty investors become hesitant in risking their investments!

Sera zisizokuwa rafiki kwa uwekezaji sio tu hazikaribishi new investments bali zinawakatisha tamaa hata wale waliokwisha wekeza such that they scale down their investments na matokeo yake ndio hayo tunayoyaona makampuni kama TBL kupunguza wafanya kazi kwani hakuna tena expansion plans!. We have to revisit our economoc policies kwani kwasasa hazisaidii wananchi walio wengi!! Tusipumbazwe na data za IMF kuwa uchumi wetu unakua lakini je wakina nani wanafaidika na ukuaji wa huo uchumi? Hilo ndio swali la kujibu.
 
Magufuli baba, mtumbue na huyu yokel usimcheleweshe huyu katibu mwenezi wa BOT, kajiongelea bila consultation with the State House, mchinjie baharini huyu!

Hawa wametumwa tu kuongea hayo mambo kama kuna mtu wa kutumbuliwa ni huyo GAVANA wa BOT!! Huyo gavana yupo au kisha tumbuliwa sisi wa vijijini taarifa hatupati kwa wakati.
 
Hawa wametumwa tu kuongea hayo mambo kama kuna mtu wa kutumbuliwa ni huyo GAVANA wa BOT!! Huyo gavana yupo au kisha tumbuliwa sisi wa vijijini taarifa hatupati kwa wakati.


I agree.

Mwalimu Ndulu ndio mzigo douche bag wa kwanza kabisa uliotakiwa kutumbuliwa... wao wamepatolea macho TRA... TRA... TRA tu...

Zinaingiaje kwa mlipa kodi ile zifike TRA hawajali...

Huku BOT wanakose set fiscal and financial policies za nchi ku regulate uchumi hawajali...
 
Mchumi anaongea kama mtu wa kijiweni..kweli awamu hii tumekula hasara
Hahahaaaa. Bora kijiweni utaskia la maana kuliko mchumi huyu. Asilimia 80 ya watu wanategemea kilimo halafu kilimo hicho unakipa asilimia 2, yet watetezi wapo tu. Dah
 
Mwankemwa ni mchumi uchwara ndiyo sababu anatoa kauli fyongo. Hongera sana kwa Profesa Honest Ngowi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe kwa siku zote kuwa mkweli kuhusu hali halisi ya uchumi nchini.
Niliwahi kuzungumza na Waziri wa Fedha Prof.Philip Mpango, yeye alitoa sababu tofauti.

Swali: "Tanzania tumekuwa tukisifiwa kwa kukua kwa uchumi kwa zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, lakini mbona ukuaji huo hauko reflected kwa watu wa kawaida?, kiwango cha umasikini kinazidi kuongezeka na fedha zimeadimika mitaani?.
Jibu: Ni kweli uchumi wetu unapaa kwa kukua kwa zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, kwa vile Tanzania inategemea kilimo ambacho kilikuwa ni 80% kimeshuka hadi 67%. Sekta zilizochangia kukua kwa hiyo 7% ni Mawasiliano, Fedha, Utalii na Madini ambayo combined ni just 5%. Sekta ya uchumi ambayo ndio tegemewa imekuwa kwa asilimia 3% tuu. Hivyo Wakulima ambao ndio wengi zaidi wamekuwa kidogo tuu, na kupata kidogo. Wafanyakazi wa Sekta ya Madini, Mawasiliano, Fedha na Utalii wanaendelea kupata pato kubwa wakati wakulima wakipata pato dogo hivyo hawana pesa.

Hakuzungumzia mzunguko wa fedha wala hatua za BOT kuficha fedha.

Nitaitafuta hii clip na kuipandisha.

Paskali
 
Mie kwa maoni yangu huu ukuaji wa uchumi ambao tunaambiwa na BoT miaka nenda miaka rudi tangu za awamu ya tatu hadi awamu ya tano kwamba unakua kwa kati ya asilimia tano hadi saba kwa zaidi ya miaka 20 sasa hauko sahihi. Haiwezekani uchumi ukue kwa asilimia hizo kwa miaka yote hii na bado asilimia kubwa ya wananchi wasione ahueni yoyote ile katika huo ukuaji wa uchumi.

Wasiwasi wangu ni kwamba vigezo vinavyotumiwa na BoT kupima ukuaji wa uchumi nchini vina mushkeli mkubwa au hizo namba zinapikwa makusudi ili kuipamba Serikali iliyopo madarakani.

Tujiulize je, kuna uhuru ndani ya BoT kutwambia Watanzania ukweli kuhusu hali halisi ya uchumi wetu bila ya kuwa na hofu ya kutumbuliwa!?

Niliwahi kuzungumza na Waziri wa Fedha Prof.Philip Mpango, yeye alitoa sababu tofauti.

Swali: "Tanzania tumekuwa tukisifiwa kwa kukua kwa uchumi kwa zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, lakini mbona ukuaji huo hauko reflected kwa watu wa kawaida?, kiwango cha umasikini kinazidi kuongezeka na fedha zimeadimika mitaani?.
Jibu: Ni kweli uchumi wetu unapaa kwa kukua kwa zaidi ya asilimia 7% kwa mwaka, kwa vile Tanzania inategemea kilimo ambacho kilikuwa ni 80% kimeshuka hadi 67%. Sekta zilizochangia kukua kwa hiyo 7% ni Mawasiliano, Fedha, Utalii na Madini ambayo combined ni just 5%. Sekta ya uchumi ambayo ndio tegemewa imekuwa kwa asilimia 3% tuu. Hivyo Wakulima ambao ndio wengi zaidi wamekuwa kidogo tuu, na kupata kidogo. Wafanyakazi wa Sekta ya Madini, Mawasiliano, Fedha na Utalii wanaendelea kupata pato kubwa wakati wakulima wakipata pato dogo hivyo hawana pesa.

Hakuzungumzia mzunguko wa fedha wala hatua za BOT kuficha fedha.

Nitaitafuta hii clip na kuipandisha.

Paskali
 
Uchumi haukui kwenye sekta binafsi ndiyo maana hakuna uwiano halisi wa kipato kwa mwananchi. Kipimo chao kipo kwenye madini, usafiri hasa ufufaji wa shirika la ndege, ukusanyaji wa kodi, bandari na upanuzi wake kwa ujumla. Utalii lkn haya yote hayausaidii uchumi wa mtu mmojammoja.
Kilimo kimeachwa kila mtu aijtafutie huku serikali za mitaa zikijikusanyia kodi za kujiendesha kutoka kwa wakulima walewale. Michango ya kuendeleza shule zenye kutangaza elimu ya bure zikichota mamilioni kutoka kwenye sekta binafsi isiyosaidiwa. Ufufuaji wa mashirika mzigo yasiyo na tija kwa watu ni dhahiri sie hatujapata wanasiasa wenye nia njema na thabiti kuwakomboa maskini. Pesa iliyoelekezwa kwenye ufufaji wa shirika mzigo zinge elekezwa kwenye kilimo cha umwagiliaji miaka si mingi tungeanza kuuza chakula nje ya nchi kutokea kwa wakulima wadogo. Na uchumi wa watu binafsi ungepanda. Viwanda vinavyojadiliwa haviwekewi mpango mkakati nani ashirikishwe na kwa njia gani. Hakuna chombo chochote cha serikali chenye kutoa elimu na msaada kwa watu binafsi wenye nia ya kuanzisha viwanda, na kwakuwa wenye mitaji ni wageni hakika viwanda havitawagusa wazawa bali wageni na ijulikane kuwa hakuna mgeni anae weza kukujengea kwako. Nchi zingine huwapa mitaji wananchi wake na kujielekeza katika jambo lenye kunufaisha hali zao.
Kweli hatuwezi kufikia huko haraka lkn tunapoona tuna kopa kwa ajili ya ujenzi ya ujenzi wa daraja baharini basi tunakosa mwelekeo kwa watu wetu nini hasa cha kukopa kuwasaidia ilikuja kulipa deni hilo.
Kwa hiyo ukuaji wa uchumi tajwa na bot siyo rafiki kwa watu wadogo
 
Mimi nadhani uchumi wetu umetegemea spending ya serikali kwa mda mrefu. Kwamba uchumi unakua...Hilo in kawaida maana wananchi wengi kipato chetu in informal. Wengi tunaumia kwa sababu tunategemea mzunguko wa pesa ya serikali directly. Mfano mahotel mengi ya mjini yanategemea workshops za serikali. It's normal lazima suppliers na wengine waliotegemea hiyo sector waumie. Sasa unategemea hii sector itafanyaje kusurvive?

Yes mzunguko upo. Lakini kwenye sector ipi? Ndege? Ujenzi? Hizo sectors ziko dominated na foreigners ambao ndo wanafaida. Tujitahidi individually na collectively tuone Kama Watu wetu wanaweza kuongeza uwezo WA kubenefit from these sectors.

Otherwise sioni Kama hali itabadilika Leo wala kesho. All I can say sina uhakika Kama atakayekuja baadala ya Magufuli....will do continuation of Magufuli or return to the old days.

Ushauri; people have to reinvent to survive. Simple.
 
Msinitupia mawe tafadhali!!

Tatizo la mzunguko wa pesa Tanzania ni kuwa unategemea sana pesa za serikali, ambazo nyingi ni za kutoka nje ya nchi. Tanzania siyo nchi ambayo serikali inategemea pesa za kodi kutoka kwenye mzunguko. Kwa hali hiyo serikali ikithibiti matumizi ya pesa zake tu au isipopata msaada kutoka nje na kuutumia msaada huo katika mzunguko, basi mzunguko huo unaporomoka kama jiwe linaloanguka kutoka mlimani!

Ni uhusiano wa kuku na yai - vicious circle.
 
Huu uchumi wa makaratasi wanaoutamka kila siku lakini kumbe kiuahilisia hamna kitu.
Yaaan waachie free flow ya pesa... co wanakaa nazo tu BOT alaf wanakuja kutangaza uchumi utakuwa sawa.
 
Hata atumbuliwe Gavana aliyepo na kuweka malaika haitasaidia kitu katika mazingira yetu. Monetary policy inafanya kazi sambamba na fiscal policy. Kazi ya BoT ni kupanga na kusimamia monetary policy. Fiscal policy inapangwa zaidi na treasury... hazina. Kwa Tanzania tuna gap kubwa kati ya hivi vyombo viwili. Kimoja kinavuta kulia kingine kinavuta kushoto. Kumbuka mvutano wa BoT na hazina kuhusu kodi kwenye miamala ya fedha. Hakuna uratibu. Isitoshee, monetary policy inafanya kazi kwenye mazingira ambapo budget ya serikali inaheshimiwa. Kuna kila dalili kuwa kuna matumizi yanafanywa nje ya budget. Mfano mzuri ni bombadier. Pesa za bunge, n.k. Katika mazingira hayo hata uwe na monetary policy nzuri bado haitafanya kazi.
 
Mie kwa maoni yangu huu ukuaji wa uchumi ambao tunaambiwa na BoT miaka nenda miaka rudi tangu za awamu ya tatu hadi awamu ya tano kwamba unakua kwa kati ya asilimia tano hadi saba kwa zaidi ya miaka 20 sasa hauko sahihi. Haiwezekani uchumi ukue kwa asilimia hizo kwa miaka yote hii na bado asilimia kubwa ya wananchi wasione ahueni yoyote ile katika huo ukuaji wa uchumi.

Wasiwasi wangu ni kwamba vigezo vinavyotumiwa na BoT kupima ukuaji wa uchumi nchini vina mushkeli mkubwa au hizo namba zinapikwa makusudi ili kuipamba Serikali iliyopo madarakani.

Tujiulize je, kuna uhuru ndani ya BoT kutwambia Watanzania ukweli kuhusu hali halisi ya uchumi wetu bila ya kuwa na hofu ya kutumbuliwa!?
Uchumi unakuwa lakini njia za usambazi wa utajiri wa nchi sio nzuri. Kwa miaka mingi, serikali imetumia utoaji wa elimu kuwa ndio njia ya pekee ya kugawa utajiri wa nchi. Tatizo linalokuja ni kuwa elimu yenyewe ni duni na isiyo na manufaa kwa wengi.

Viwanda vinaweza kutumika katika usambazi wa utajiri. Lakini, serikali ya Tanzania haiendeshi vitu kwa ufanisi. Hivyo sidhani kama mtu wa chini atafaidika.

Kuhusu hoja ya mchumi wa benki kuu, naona anatoa hoja za serikali. Yeye kama mfanyakazi wa benki kuu alitakiwa atoe hoja za kibenki. Serikali inaangalia fiscal policies na benki inaanzalia monetary policies.
 
Mimi nadhani uchumi wetu umetegemea spending ya serikali kwa mda mrefu. Kwamba uchumi unakua...Hilo in kawaida maana wananchi wengi kipato chetu in informal. Wengi tunaumia kwa sababu tunategemea mzunguko wa pesa ya serikali directly. Mfano mahotel mengi ya mjini yanategemea workshops za serikali. It's normal lazima suppliers na wengine waliotegemea hiyo sector waumie. Sasa unategemea hii sector itafanyaje kusurvive?

Yes mzunguko upo. Lakini kwenye sector ipi? Ndege? Ujenzi? Hizo sectors ziko dominated na foreigners ambao ndo wanafaida. Tujitahidi individually na collectively tuone Kama Watu wetu wanaweza kuongeza uwezo WA kubenefit from these sectors.

Otherwise sioni Kama hali itabadilika Leo wala kesho. All I can say sina uhakika Kama atakayekuja baadala ya Magufuli....will do continuation of Magufuli or return to the old days.

Ushauri; people have to reinvent to survive. Simple.
Uchumi unakuwa lakini kukua kwa uchumi na distribution of wealth ni vitu viwili tofauti.

Uchumi unaweza kukua lakini wamiliki wakawa ni wachache, this is the case of Tanzania.

Kwa miaka mingi, serikali nyingi zimeamini kuwa elimu ni ufunguo wa maisha. Hivyo serikali zimetumia elimu kama njia ya kugawa utajiri. Lakini data zilizopo sasa zinaonyesha kuwa elimu duni kama inayotolewa kwa watanzania wengi doesnt make the cut.

Imefika wakati serikali iangalie upya sera zake. Inawezekana decentrization ikawafanya kazi
 
Kama hawa wachumi nyoko ndo tunawategemea haki ya nani maendeleo tutaendelea kuyasikia kwa Kagame tu! Pumbavvv kabisa huyu mchumi wa BOT eti unasema posho zisizo za lazima, jinga kabisa hili! Ooooh, God have mercy on us! Eti anasema tusubiri viwanda, tusubiri maboresho ya bandari nyoko kabisa! Anashindwa kutueleza kwamba bandari haifanyi vizuri kwa sababu tumeweka vikodi vya kijinga kijinga watu wametukimbia malori hayafanyi kazi ajira imepungua. Hivyo viwanda tunavyoambiwa tuvisubiri vinajengwa wapi?
 
Back
Top Bottom