Mchumba hataki tufunge ndoa

Mchumba hataki tufunge ndoa

mama pita

Member
Joined
Jul 20, 2012
Posts
97
Reaction score
140
Habarin za jion wapendwa
Naomben mnisaidie mawazo
Ninamchumba wangu tuna mwaka na nusu tumeshamaliza taratibu zote mpaka mahari ameshatoa....mwanzo tulipanga tufunge ndoa mwezi wa 10nimekaaa nimeona kimya hata maandalizi hakuna ikabidi niulize VP utaratibu ....

Ndio akaniambia kwa sasa anaujenzi wa nyumban kwao anichukue tu hivyo hivyo mwaka kesho ndio tutafunga ndoa......mi nimemwambia kufunga ndoa haitaji gharama kubwa kama mkiamua mnafanya simple tu kwa gharama kidogo
Kwanza RC hua haina mambo mengi mnaweza nenda na wasimamizi wenu tu mkitoka mnaandaa chakula kidogo badae mnarudi kwenu
Anadai hili tendon halijirudii Mara 2 ni bora tuchukuane tu sasa hv badae akusanye kama mil 7 HV mwaka kesho afanye ya kifahari
...naomben mnishauri niende tu au nibane mpaka ndoa?
 
Msikilize anachosema maana yeye ndio muoaji...
 
Kwa maelezo naona yeye anakwepa gharama ila hapo hapo naona anataka iwe ya gharama pia.

sijaelewa.

Wewe hutaki harusi na sherehe? kama hautaki mbona hii wanaume wengi hatuna shida mnaenda kanisani tu na wazazi wa pande mbili na baba paroko yanaisha.

Siku hiyo hiyo upo kwako.
 
Hapo mmekutana Mpenda sherehe(Jamaa) na Mnapenda Ndoa(wewe)

Bas ngoma mbichi ...... Sema nn, usihadaike na nyimbo zake, kufunga ndoa yenye mahudhurio kidogo inathaman kubwa kuliko "Njoo tuishi wote"
 
Honestly we can never know kama anachosema anamaanisha kweli, au ndo imetoka hiyo. Ila I'll advice you to wait. Usiende kwake.
 
kikubwa msikilize yeye na tena kama mahari kashatoa siyo mbaya,mana hata mimi cjafunga ndoa ila niliambiwa hili jambo la kufanya sherehe ndogo baada ya kupata baraka za ndoa ila mm nikaona nisubr nijipange nije nifanye tu kwa nafasi nzuri kuliko kujibana sana na siku izi kama unavyojua vipato vya watu vilivyo,lazima ujipange ili nao waone jitihada zako ww muoaji.nazani yupo sahihi kama hatakuwa na shabaha nje ya hiyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo mmetofautiana kidogo tu.. Wewe unawaza NDOA ila mwenzio anawaza HARUSI. Anyway Jaribu kumuelewesha kwa unyenyekevu atakuelewa tu. Hofu yake hataki kuonekana masikini mbele ya watu wanaomzunguka.
 
Kwa maelezo naona yeye anakwepa gharama ila hapo hapo naona anataka iwe ya gharama pia.

sijaelewa.

Wewe hutaki harusi na sherehe? kama hautaki mbona hii wanaume wengi hatuna shida mnaenda kanisani tu na wazazi wa pande mbili na baba paroko yanaisha.

Siku hiyo hiyo upo kwako.
Mimi nilichomwambia kama uwezo hauruhusu tufanye kitu simple tu hataki,,,, binafsi sina tatizo hata tumalize kufunga ndoa tuje nyumbani tulale
Yeye ndio hataki kufanya hivyo anataka tuishi tu sasa hv ajipange taratibu afanye babu kubwa
 
Mimi nilichomwambia kama uwezo hauruhusu tufanye kitu simple tu hataki,,,, binafsi sina tatizo hata tumalize kufunga ndoa tuje nyumbani tulale
Yeye ndio hataki kufanya hivyo anataka tuishi tu sasa hv ajipange taratibu afanye babu kubwa
Mchunguze vizuri.
 
Mchunguze vizuri.
kiaje daby?
mi nawaza kama kipaumbele chake nikuoa angesitisha ujenzi kwanza sababu nyumba yakuishi nzuri tu IPO angesitisha baada ya kumaliza swala la ndoa anaendelea na ujenzi
hataki yeye anataka tukubaliane aje na gali abebe vitu vyangi nihamie kwake
 
kiaje daby?
mi nawaza kama kioaumbele chake nikuoa angesitisha ujenzi kwanza sababu nyumba yakuishi nzuri tu IPO angesitisha baada ya kumaliza swala la ndoa anaendelea na ujenzi
hataki yeye anataka tukubaliane aje na gali abebe vitu vyangi nihamie kwake
Wazazi wanasemaje kwa hili?

mlishawahi kuishi pamoja! mna mtoto?
 
Tangu lini RC hawana mambo mengi. Tena mara nyingi mnaotaka mambo mengi ni nyinyi mnaoolewa.

Anyway jamaa atakuwa kashapata mbadala wako.
 
ndoa makaratasi ndugu,kama uko happy,mko wote happy...karatasi ndio ikusumbue..?? .akikuona uko desperate na ndoa ndio kwanza atahairisha hata kukuoa lol
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom