Bi dentamol
JF-Expert Member
- Feb 1, 2014
- 987
- 1,912
I hope mko poa guys
Naitaji ushauri hapa serious kabisa
Mimi ni mwanamke nina miaka 30 nina mchumba ambaye wazazi walishatupa ruhusa ya kuishi pamoja
Mwaka 2016 nilipata kazi ya muda mfupi katika kampuni fulani nilifanya kazi ndani ya miezi minne nilikutana na kaka ana 33 kwa a
Huyu Kaka nilimpenda sana alikuwa mtu fulan mpole hana Mambo ya ajabu ukweli nilitokea tu kuvutiwa nae. Nikafanya juhudi tukawa marafiki wa karibu, kusaidiana mambo mbalimbali haikupita muda tukawa tumeanza mahusiano ya kimapenzi
Uzuri jamaa alikuwa hayupo katika mahusiano serious, alikua na mwanamke ambae walikua hawafahamiani aliunganishiwa na jamaa tu so wakawa na mapenzi ya kwenye simu
Baada ya miezi 6 jamaa akanipeleka kwao kunitambulisha ilikua Desemba mwaka jana, Februaru mwaka huu alihamishwa mkoa mwingine kikazi nami nikaacha pale nikaanza biashara zangu binafsi. March akaja nyumbani kwetu kujitambulisha, Juni kupanga na kutoa mahari.
Oktoba Wazazi pande zote mbili walikutana kupanga mambo ya ndoa, wazazi wake wakaomba tuchukuane tu kwa sasa hawana uwezo tutafunga ndoa mwaka kesho. Hii ni sawa kwa jamii ya wasukuma wa kijijin kwani huamini ukishamtolea mahari mwanamke tayari wanakuja kumchukua. Familia yangu ikakubali
Kilichonileta kwenu
Baada ya kukaa kiuchumba na jamaa nilikua nahisi hanipendi tangu kabla hajanipeleka kwao nikawa najiondoa kwake ajabu nikikaa nae nikimwambia tuachane hakubali kabisa anaweza hata jitupa chini akibembeleza nisimuache
Nikimuangalia ni mtu ambae haoneshi kama ananipenda anaweza kaa siku 1 au 2 bila kunipigia. Ninaweza pata shida kunisaidia akawa mzito mno. Ni mtu ambaye hajali unaumwa, umepata matatizo unaishi vipi haelewi
Mwanzo nilihisi labda anamahusiano mengine lakini nilifanya uchunguzi sikubaini hicho. Mi nampenda najikuta naumia nahitaji kupata attention yake, muda wake, nilishaongea nae sana. Ni mtu ambae hata kuniambia nakupenda au nimekumiss au kuniita tu mpenzi wangu ni ngumu labda muwe kitandani kapandwa na hisia anaweza fanya hivyo au muwe mna ugomvi anakubembeleza au ndio mmeelewana
Atafanya hivyo for 2 days then anarudi katika hali yake
Nilishaongea nae kama hanipendi nimeshamuomba aniache niumie badae nitazoea hataki. Kuna kipindi nilimwambia aniache tu atafute mwanamke anaempenda na nikamchunia kweli
Aliteseka sana alinitafutia washauri sio ndugu zake, rafiki zake na zangu. Nashindwa kuelewa nitaishije na huyu mtu jamani. Sielewi ni maumbile yake yuko hivi, makuzi au tu hanipendi!
Amekulia kijijini hasa tena hasa nashindwa kuelewa labda ndivyo alivyo. Nawaza labda yupo kwangu kimaisha tu sababu yeye ana kazi nzuri mshahara mkubwa lakini familia ya kwao inamuelemea ukoo mzima unamtegemea yeye
Mimi kipato changu kidogo kwake lakini nina maendeleo kidogo namzidi na ninafanya vitu vya msingi. Nahisi labda jamaa amefata maisha!
Wadau samahani kwa kuwachosha naombeni mawazo yenu
Naitaji ushauri hapa serious kabisa
Mimi ni mwanamke nina miaka 30 nina mchumba ambaye wazazi walishatupa ruhusa ya kuishi pamoja
Mwaka 2016 nilipata kazi ya muda mfupi katika kampuni fulani nilifanya kazi ndani ya miezi minne nilikutana na kaka ana 33 kwa a
Huyu Kaka nilimpenda sana alikuwa mtu fulan mpole hana Mambo ya ajabu ukweli nilitokea tu kuvutiwa nae. Nikafanya juhudi tukawa marafiki wa karibu, kusaidiana mambo mbalimbali haikupita muda tukawa tumeanza mahusiano ya kimapenzi
Uzuri jamaa alikuwa hayupo katika mahusiano serious, alikua na mwanamke ambae walikua hawafahamiani aliunganishiwa na jamaa tu so wakawa na mapenzi ya kwenye simu
Baada ya miezi 6 jamaa akanipeleka kwao kunitambulisha ilikua Desemba mwaka jana, Februaru mwaka huu alihamishwa mkoa mwingine kikazi nami nikaacha pale nikaanza biashara zangu binafsi. March akaja nyumbani kwetu kujitambulisha, Juni kupanga na kutoa mahari.
Oktoba Wazazi pande zote mbili walikutana kupanga mambo ya ndoa, wazazi wake wakaomba tuchukuane tu kwa sasa hawana uwezo tutafunga ndoa mwaka kesho. Hii ni sawa kwa jamii ya wasukuma wa kijijin kwani huamini ukishamtolea mahari mwanamke tayari wanakuja kumchukua. Familia yangu ikakubali
Kilichonileta kwenu
Baada ya kukaa kiuchumba na jamaa nilikua nahisi hanipendi tangu kabla hajanipeleka kwao nikawa najiondoa kwake ajabu nikikaa nae nikimwambia tuachane hakubali kabisa anaweza hata jitupa chini akibembeleza nisimuache
Nikimuangalia ni mtu ambae haoneshi kama ananipenda anaweza kaa siku 1 au 2 bila kunipigia. Ninaweza pata shida kunisaidia akawa mzito mno. Ni mtu ambaye hajali unaumwa, umepata matatizo unaishi vipi haelewi
Mwanzo nilihisi labda anamahusiano mengine lakini nilifanya uchunguzi sikubaini hicho. Mi nampenda najikuta naumia nahitaji kupata attention yake, muda wake, nilishaongea nae sana. Ni mtu ambae hata kuniambia nakupenda au nimekumiss au kuniita tu mpenzi wangu ni ngumu labda muwe kitandani kapandwa na hisia anaweza fanya hivyo au muwe mna ugomvi anakubembeleza au ndio mmeelewana
Atafanya hivyo for 2 days then anarudi katika hali yake
Nilishaongea nae kama hanipendi nimeshamuomba aniache niumie badae nitazoea hataki. Kuna kipindi nilimwambia aniache tu atafute mwanamke anaempenda na nikamchunia kweli
Aliteseka sana alinitafutia washauri sio ndugu zake, rafiki zake na zangu. Nashindwa kuelewa nitaishije na huyu mtu jamani. Sielewi ni maumbile yake yuko hivi, makuzi au tu hanipendi!
Amekulia kijijini hasa tena hasa nashindwa kuelewa labda ndivyo alivyo. Nawaza labda yupo kwangu kimaisha tu sababu yeye ana kazi nzuri mshahara mkubwa lakini familia ya kwao inamuelemea ukoo mzima unamtegemea yeye
Mimi kipato changu kidogo kwake lakini nina maendeleo kidogo namzidi na ninafanya vitu vya msingi. Nahisi labda jamaa amefata maisha!
Wadau samahani kwa kuwachosha naombeni mawazo yenu