Mchezo mchafu wa Benki ya Dunia - Dola milioni 500

Mchezo mchafu wa Benki ya Dunia - Dola milioni 500

Abdalah Abdulrahman

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2019
Posts
223
Reaction score
202
Hivi karibuni Benki ya Dunia imehairisha kupiga kura ya kuikopesha Tanzania kiasi cha Dola za kimarekani milioni 500 kwa ajili ya sekta ya elimu nchini.

Kuhairishwa huku kwa kikao hiki kunatokana na kile kinachosadikika kuwa kampeni za wanaharakati na wanasiasa wachache wa vyama vya upinzani wanaotumika na baadhi ya nchi kuhujumu nchi ya Tanzania pamoja na serikali kwa hoja dhaifu kuwa serikali ya Tanzania inawabagua watoto wa kike wanaopata mimba mashuleni.

Ukweli ni kwamba,kamwe serikali ya Tanzania haibagui wanawake wanaopata mimba mashuleni bali inawasaidia kwa kuwapa upendeleo ambao kimsingi sio haki yao.Upendeleo huu ni ule wa serikali kuwaruhusu wakasome katika shule binafsi ili waweze kuwa na muda wa kulelea mimba zao pamoja na watoto wao kutokana na maamuzi yao. Ruhusa hii miaka ya nyuma haikuwepo kwani wazazi walikua wakiwatoa watoto wao mashuleni na huvyo kutokuendela na masomo kutokana na aibu na Changamoto zingine.

Kitendo cha mtoto wa kike kupata mimba shuleni ni kigezo pekee cha kumfanya kubadili hadhi yake ya kutoka usichana kwenda umama.Majukumu yake yanabadilika pamoja na upeo wake wa masomo darasani,hivyo kulazimika kuwa sawa na wanafunzi wengine ni kero pia kwa wanafunzi wengine.

Endapo kuhairishwa kwa kikao cha Banki ya Dunia kinatokana na sababu hii,basi ni wazi kuwa wajumbe wa Benki ya Dunia watakuwa wanashirikiana na wale wanaohujumu juhudi za serikali katika kuwaletea Watanzania maendeleo.

Zipo sababu anuai zinazothibitisha hili kama zifuatazo:-

1. Sote tunafahamu kuwa tunawapeleka watoto mashuleni wakasome na sio kwenda kufanya ngono zembe.Kitendo cha kuruhusu mkanganyiko wa wajawazito kusoma pamoja na wanafunzi wasio wajawazito kitachochea ngono zembe kwa watoto wetu.

Ni wazi kuwa ondosho la viboko mashuleni pamoja na mmomonyoko wa maadili ndani ya jamii unachochea sana masuala ya ngono katika mashule yetu. Watoto wengi wameambukizwa magonjwa ya zinaa na Virusi vya Ukimwi, na wengine wamepata mimba utotoni na kusababisha vifo vyao pamoja na watoto wanaozaliwa. Ukubwa wa tatizo hili ni zaidi ya zuio la wajawazito kurudi mashuleni na kupata elimu mbadala.

Tishio la serikali kuwapa elimu mbadala kwa wale watakaopata mimba mashuleni na kutokuwaruhusu katika shule za serikali limepunguza idadi kubwa ya wanafunzi wanapata mimba pamoja na ile ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na vifo vya mama na watoto.

2. Pili, hasara inayoweza kupatikana kwa Benki ya Dunia isipotoa huo mkopo,na serikali ikabaki na msimamo wake kuwa mwanafunzi atakayepata mimba shuleni atapata elimu mbadala ili aweze kumlelea mtoto wake vizuri pamoja na kuangalia afya ya mzazi itawalenga watoto wengi wa kike na wa kiume watakaofaidika na mkopo huu ukitolewa. Kama Benki ya Dunia hailengi kuzima juhudi za Tanzania kujiletea maendeleo, basi izingatie hili pia.

3. Sote tunafahamu majukumu ya mama kwa mtoto na adha ambayo anapata mama kipindi cha ujauzito.Je kwa mwanafunzi wa shule ambaye amepewa mimba na mhuni ambaye hayupo tayari kuchukua jukumu la kulea mimba na kumsaidia msichana huyu ambaye ndio mimba yake ya kwanza, aibu kwa jamii na familia yake, pamoja na adha zingine serikali inamtaka apate elimu mbadala ili aweze kumudu hali hii wakati wanaharakati na wanasiasa wanataka akiwa katika hali hii aendelee kusoma. Je nani kati ya serikali na wanaharakati wa kusikilizwa kama kweli Benki ya Dunia anamtendea haki mtoto wa kike?

4. Mkopo huu unawasaidia wale wanaosoma katika shule za serikali, ambao wengi wao ni wa kipato cha kati na cha chini.Watoto wa wanaharakati na wanasiasa wao wanasoma shule binafsi na zile zilizopo nje ya nchi. Serikali kukosa huu mkopo ni juhudi zao za kuendelea kufanya watawaliwa kuwa watawaliwa na watawala kuwa watawala.

Zipo sababu nyingi za kuonesha kuwa unaweza kuwa mchezo mchafu unatengenezwa na mabeberu kuhujumu serikali ya awamu ya tano ambayo inawaletea maendeleo ya kweli wananchi.
 
Hatutaki hizo pesa,tuko vzr sana.
Screenshot_2019-12-21-09-59-03-1.jpeg


dodge
 
Acha kuangaika wewe jamaa. Kwanini baada ya mkopo kuzuiliwa mnaanza kuvesha nguo katazo lenu? Ulisikia hotuba ya Mheshimiwa siku anakataza hili swala? Unajua kwanini Halima Mdee alishtakiwa juu ya hili swala?

By the way, kwanini mnahangaika na mabeberu? Si muwaache na hela zao tu?

Wewe Abdalah kwa maoni yako kama nchi inanunua ndege kwa pesa za ndani, inajenga flyovers kwa pesa za ndani, inajenga reli ya kisasa kabisa na bwawa kubwa la umeme kwa pesa za ndani, kwanini ishindwe kugharamia elimu ambayo hata ninyi mnajua ni kitu cha muhimu? Kwanini mliweka vipaumbile kwa hayo mengine mkaacha Elimu kuifanya kwa pesa za ndani? Au kwenu Elimu si kipaumbele kuliko flyover ya Mfugale?

Ujanja ujanja mwingi wa kupiga samasoti kwenye floo ya simenti kinachofuata huwa ni kuanguka tu, hakuna vinginevyo.

Mimi nashauri ili hawa mabeberu wasitupangie masharti ni bora kuachana na mamikopo yao tu. Tumeshajipambanua vya kutosha kuwa sisi ni matajiri, hebu tukomae wenyewe tuone.
 
Marekani sio kitu cha ajabu Binti wa high school kuwa na Mtoto/Watoto huku anasoma.

Yani umetengwa muda maalumu kabisa wa kunyonyesha, ukifika wanatoka wanaenda kunyonyesha kisha wanarudi darasani.

Wenzetu walipiga mahesabu wakaona kuzuia mabinti kujihusisha na mapenzi kunakowapelekea kubeba mimba ni kugumu kuliko kuwaruhusu waendelee na masomo, hata huku iko hivyo.

Tukitaka kujikomboa kiuchumi na kifikra inabidi tutumie akili sana na sio ubabe.

Unforgetable
 
Kambaku,
Serikali ina miradi mingi kwa sasa na yote ina kipaumbele,elimu ina kipaumbele kama ilivyo miundombinu,bila barabara mwanafunzi hawezi fika shule,bila hospitali akiumwa hawezi pona,nakadhalika.

Mabeberu sio pesa zao,,,hii ni WB ambao na sisi ni wadau,lakini wanataka kutumia hiki chombo kututawala,na pesa inayopatikana hapa ina umuhimu kwetu kwani ni mkopo wenye masharti nafuu na sio bure.
 
Kinachotukwamisha ni jinsi gani viongozi wetu wanapenda kujimwambafai. Kuropoka. Kwa hili la pesa za WB tusitafute mchawi. Mchawi ni sisi. Nakumbuka Mama Salma Kikwete alilishupalia hili bungeni mpaka anatoa povu kwamba hao watoto wa kike wanaopewa mimba wasiruhusiwe kurudi shule. Nilimwangalia nikajiuliza hivi hawa ndo type ya viongozi tulio nao??

Kiukweli ingawa nasikitika hawa waheshimiwa wa WB kuahirisha maamuzi, lakini bado naamini viongozi wetu lazima waamke wajue kwamba kauli zao zina uzito. Wajitafakari. Kiongozi huwezi ukaamka ukawaambia watu wako zaeeni tuu/fyatueni tuu ntasomesha! Mtoto anayezaliwa leo..by the time anakwenda shule Mh. atakuwa yuko kijijini amestaafu!

Hivi mfano issue ya ushoga. Najua kabisa wengi humu (wengi) hatuupendi ushoga. By the way hata western countries wapo ambao hawapendi hii kitu. Lakini ni nchi gani zaidi ya Makonda na wenye akili kama zake huko Lumumba, walishaenda kuutangazia ulimwengu kwamba tunakwenda kuwasaka na kuwatia jela hawa jamaa?

In all matatizo mengi ya Tanzania..ni ya kijinga na tunayatafuta wenyewe. Tunachokisahau kwa maksudi, wanaharakati wana nguvu sana kuliko hata serikali zetu. Na hata huu mkopo, nchi wanachama wa Benki ya Dunia wangependa waipe pesa Tanzania lakini..wataficha sura zao wapi? Na tusisahau...hizi pesa tunapewa za wahisani ni kodi za watu hata hao hao mashoga tunaotaka wakaozee jela! Go figure!

Kikubwa tujifunze..siyo kila mtu ni wa kugombana naye.


Viongozi wetu wanaropoka sana! Mwisho wa siku tunaoumia ni sisi wananchi.
 
Serikali ina miradi mingi kwa sasa na yote ina kipaumbele,elimu ina kipaumbele kama ilivyo miundombinu,bila barabara mwanafunzi hawezi fika shule,bila hospitali akiumwa hawezi pona,nakadhalika....Mabeberu sio pesa zao,,,hii ni WB ambao na sisi ni wadau,lakini wanataka kutumia hiki chombo kututawala,na pesa inayopatikana hapa ina umuhimu kwetu kwani ni mkopo wenye masharti nafuu na sio bure.
Wanatumia hicho chombo kututawala sababu ya njaa zetu na kwa sababu ni chao zaidi kuliko sisi. Au mkuu unaamini udau wako kwa WB ni sawa na marekani?

Unaposema mabeberu sio pesa zao hizo za WB una maana gani? Kuna tofauti ya beberu na WB?
 
Hivi karibuni Benki ya Dunia imehairisha kupiga kura ya kuikopesha Tanzania kiasi cha dola za kimarekani milioni 500 kwa ajili ya sekta ya elimu nchini.

Kuhairishwa huku kwa kikao hiki kunatokana na kile kinachosadikika kuwa kampeni za wanaharakati na wanasiasa wachache wa vyama vya upinzani wanaotumika na baadhi ya nchi kuhujumu nchi ya Tanzania pamoja na serikali kwa hoja dhaifu kuwa serikali ya Tanzania inawabagua watoto wa kike wanaopata mimba mashuleni.

Ukweli ni kwamba,kamwe serikali ya Tanzania haibagui wanawake wanaopata mimba mashuleni bali inawasaidia kwa kuwapa upendeleo ambao kimsingi sio haki yao.Upendeleo huu ni ule wa serikali kuwaruhusu wakasome katika shule binafsi ili waweze kuwa na muda wa kulelea mimba zao pamoja na watoto wao kutokana na maamuzi yao.Ruhusa hii miaka ya nyuma haikuwepo kwani wazazi walikua wakiwatoa watoto wao mashuleni na huvyo kutokuendela na masomo kutokana na aibu na Changamoto zingine.

Kitendo cha mtoto wa kike kupata mimba shuleni ni kigezo pekee cha kumfanya kubadili hadhi yake ya kutoka usichana kwenda umama.Majukumu yake yanabadilika pamoja na upeo wake wa masomo darasani,hivyo kulazimika kuwa sawa na wanafunzi wengine ni kero pia kwa wanafunzi wengine.
Endapo kuhairishwa kwa kikao cha Banki ya Dunia kinatokana na sababu hii,basi ni wazi kuwa wajumbe wa Benki ya Dunia watakua wanashirikiana na wale wanaohujumu juhudi za serikali
katika kuwaletea Watanzania maendeleo.

Zipo sababu anuai zinazothibitisha hili kama zifuatazo:-

1.Sote tunafahamu kuwa tunawapeleka watoto mashuleni wakasome na sio kwenda kufanya ngono zembe.Kitendo cha kuruhusu mkanganyiko wa wajawazito kusoma pamoja na wanafunzi wasio wajawazito kitachochea ngono zembe kwa watoto wetu .

Ni wazi kuwa ondosho la viboko mashuleni pamoja na mmomonyoko wa maadili ndani ya jamii unachochea sana masuala ya ngono katika mashule yetu.Watoto wengi wameambukizwa magonjwa ya zinaa na virusi vya ukimwi,na wengine wamepata mimba utotoni na kusababisha vifo vyao pamoja na watoto wanaozaliwa.Ukubwa wa tatizo hili ni zaidi ya zuio la wajawazito kurudi mashuleni na kupata elimu mbadala.

Tishio la serikali kuwapa elimu mbadala kwa wale watakaopata mimba mashuleni na kutokuwaruhusu katika shule za serikali limepunguza idadi kubwa ya wanafunzi wanapata mimba pamoja na ile ya maambukizi ya virusi vya ukimwi na vifo vya mama na watoto.

2.Pili,hasara inayoweza kupatikana kwa Benki ya Dunia isipotoa huo mkopo,na serikali ikabaki na msimamo wake kuwa mwanafunzi atakayepata mimba shuleni atapata elimu mbadala ili aweze kumlelea mtoto wake vizuri pamoja na kuangalia afya ya mzazi itawalenga watoto wengi wa kike na wakiume watakaofaidika na mkopo huu ukitolewa.Kama Benki ya Dunia hailengi kuzima juhudi za Tanzania kujiletea maendeleo,basi izingatie hili pia.

3.Sote tunafahamu majukumu ya mama kwa mtoto na adha ambayo anapata mama kipindi cha ujauzito.Je kwa mwanafunzi wa shule ambaye amepewa mimba na mhuni ambaye hayupotayari kuchukua jukumu la kulea mimba na kumsaidia msichana huyu ambaye ndio mimba yake ya kwanza,aibu kwa jamii na familia yake,pamoja na adha zingine serikali inamtaka apate elimu mbadala ili aweze kumudu hali hii wakati wanaharakati na wanasiasa wanataka akiwa katika hali hii aendelee kusoma.Je nani kati ya serikali na wanaharakati wa kusikilizwa kama kweli Benki ya Dunia anamtendea haki mtoto wa kike ?

4.Mkopo huu unawasaidia wale wanaosoma katika shule za serikali,ambao wengi wao ni wa kipato cha kati na cha chini.Watoto wa wanaharakati na wanasiasa wao wanasoma shule binafsi na zile zilizopo nje ya nchi.Serikali kukosa huu mkopo ni juhudi zao za kuendelea kufanya watawaliwa kuwa watawaliwa na watawala kuwa watawala.

Zipo sababu nyingi za kuonesha kuwa unaweza kuwa mchezo mchafu unatengenezwa na babeberu kuhujumu serikali ya awamu ya tano ambayo inawaletea maendeleo ya kweli wananchi.

Kuahirishwa sio kuhairishwa.Tofauti na hapo umejitahidi kuandika


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kambaku,
Serikali ina miradi mingi kwa sasa na yote ina kipaumbele,elimu ina kipaumbele kama ilivyo miundombinu,bila barabara mwanafunzi hawezi fika shule,bila hospitali akiumwa hawezi pona,nakadhalika.

Mabeberu sio pesa zao,,,hii ni WB ambao na sisi ni wadau,lakini wanataka kutumia hiki chombo kututawala,na pesa inayopatikana hapa ina umuhimu kwetu kwani ni mkopo wenye masharti nafuu na sio bure.
WB sisi ni wadau tuna changia?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Africa kweli bado hatuna uhuru, yaani mkopo nikope mimi alafu unipangie na mambo yangu binafsi , zaidi nikwamba sio kwamba huo mkopo haurudi bila riba, Africa Africa
 
Africa kweli bado hatuna uhuru, yaani mkopo nikope mimi alafu unipangie na mambo yangu binafsi , zaidi nikwamba sio kwamba huo mkopo haurudi bila riba, Africa Africa
Sasa kama mkopo unarudi na riba na tumenyimwa si ni fresh tu wametupunguzia mizigo mzee baba.

dodge
 
Kambaku,
Serikali ina miradi mingi kwa sasa na yote ina kipaumbele,elimu ina kipaumbele kama ilivyo miundombinu,bila barabara mwanafunzi hawezi fika shule,bila hospitali akiumwa hawezi pona,nakadhalika.

Mabeberu sio pesa zao,,,hii ni WB ambao na sisi ni wadau,lakini wanataka kutumia hiki chombo kututawala,na pesa inayopatikana hapa ina umuhimu kwetu kwani ni mkopo wenye masharti nafuu na sio bure.
Hapana. Wanatumia haki ya vigezo vya uundwaji wa chombo hiki. Chombo hiki kiliundwa pamoja na mambo mengine, kilinde haki za watu;Siyo kitoe fedha kuwapa watu wenye mawazo ya kiendawazimu na uonevu dhidi ya wasio na nguvu.
Ukichunguza kwa makini sababu za mimba za watoto hasa wa shule, utagundua kuwa ni sera za hovyo za serikali yenyewe. Hivyo dhana ya "ukihere here cha watoto wa kike kupata mimba ni dhana ya watawala muflisi.
 
Hivi karibuni Benki ya Dunia imehairisha kupiga kura ya kuikopesha Tanzania kiasi cha Dola za kimarekani milioni 500 kwa ajili ya sekta ya elimu nchini.

Kuhairishwa huku kwa kikao hiki kunatokana na kile kinachosadikika kuwa kampeni za wanaharakati na wanasiasa wachache wa vyama vya upinzani wanaotumika na baadhi ya nchi kuhujumu nchi ya Tanzania pamoja na serikali kwa hoja dhaifu kuwa serikali ya Tanzania inawabagua watoto wa kike wanaopata mimba mashuleni.

Ukweli ni kwamba,kamwe serikali ya Tanzania haibagui wanawake wanaopata mimba mashuleni bali inawasaidia kwa kuwapa upendeleo ambao kimsingi sio haki yao.Upendeleo huu ni ule wa serikali kuwaruhusu wakasome katika shule binafsi ili waweze kuwa na muda wa kulelea mimba zao pamoja na watoto wao kutokana na maamuzi yao. Ruhusa hii miaka ya nyuma haikuwepo kwani wazazi walikua wakiwatoa watoto wao mashuleni na huvyo kutokuendela na masomo kutokana na aibu na Changamoto zingine.

Kitendo cha mtoto wa kike kupata mimba shuleni ni kigezo pekee cha kumfanya kubadili hadhi yake ya kutoka usichana kwenda umama.Majukumu yake yanabadilika pamoja na upeo wake wa masomo darasani,hivyo kulazimika kuwa sawa na wanafunzi wengine ni kero pia kwa wanafunzi wengine.

Endapo kuhairishwa kwa kikao cha Banki ya Dunia kinatokana na sababu hii,basi ni wazi kuwa wajumbe wa Benki ya Dunia watakuwa wanashirikiana na wale wanaohujumu juhudi za serikali katika kuwaletea Watanzania maendeleo.

Zipo sababu anuai zinazothibitisha hili kama zifuatazo:-

1. Sote tunafahamu kuwa tunawapeleka watoto mashuleni wakasome na sio kwenda kufanya ngono zembe.Kitendo cha kuruhusu mkanganyiko wa wajawazito kusoma pamoja na wanafunzi wasio wajawazito kitachochea ngono zembe kwa watoto wetu.

Ni wazi kuwa ondosho la viboko mashuleni pamoja na mmomonyoko wa maadili ndani ya jamii unachochea sana masuala ya ngono katika mashule yetu. Watoto wengi wameambukizwa magonjwa ya zinaa na Virusi vya Ukimwi, na wengine wamepata mimba utotoni na kusababisha vifo vyao pamoja na watoto wanaozaliwa. Ukubwa wa tatizo hili ni zaidi ya zuio la wajawazito kurudi mashuleni na kupata elimu mbadala.

Tishio la serikali kuwapa elimu mbadala kwa wale watakaopata mimba mashuleni na kutokuwaruhusu katika shule za serikali limepunguza idadi kubwa ya wanafunzi wanapata mimba pamoja na ile ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi na vifo vya mama na watoto.

2. Pili, hasara inayoweza kupatikana kwa Benki ya Dunia isipotoa huo mkopo,na serikali ikabaki na msimamo wake kuwa mwanafunzi atakayepata mimba shuleni atapata elimu mbadala ili aweze kumlelea mtoto wake vizuri pamoja na kuangalia afya ya mzazi itawalenga watoto wengi wa kike na wa kiume watakaofaidika na mkopo huu ukitolewa. Kama Benki ya Dunia hailengi kuzima juhudi za Tanzania kujiletea maendeleo, basi izingatie hili pia.

3. Sote tunafahamu majukumu ya mama kwa mtoto na adha ambayo anapata mama kipindi cha ujauzito.Je kwa mwanafunzi wa shule ambaye amepewa mimba na mhuni ambaye hayupo tayari kuchukua jukumu la kulea mimba na kumsaidia msichana huyu ambaye ndio mimba yake ya kwanza, aibu kwa jamii na familia yake, pamoja na adha zingine serikali inamtaka apate elimu mbadala ili aweze kumudu hali hii wakati wanaharakati na wanasiasa wanataka akiwa katika hali hii aendelee kusoma. Je nani kati ya serikali na wanaharakati wa kusikilizwa kama kweli Benki ya Dunia anamtendea haki mtoto wa kike?

4. Mkopo huu unawasaidia wale wanaosoma katika shule za serikali, ambao wengi wao ni wa kipato cha kati na cha chini.Watoto wa wanaharakati na wanasiasa wao wanasoma shule binafsi na zile zilizopo nje ya nchi. Serikali kukosa huu mkopo ni juhudi zao za kuendelea kufanya watawaliwa kuwa watawaliwa na watawala kuwa watawala.

Zipo sababu nyingi za kuonesha kuwa unaweza kuwa mchezo mchafu unatengenezwa na mabeberu kuhujumu serikali ya awamu ya tano ambayo inawaletea maendeleo ya kweli wananchi.
Mdomo umekiponza kichwa jpm anaongea sana kumbe ni kapuku tu
 
Africa kweli bado hatuna uhuru, yaani mkopo nikope mimi alafu unipangie na mambo yangu binafsi , zaidi nikwamba sio kwamba huo mkopo haurudi bila riba, Africa Africa
Wewe ni maskini wa kipato hadi wa akili, unaonekana hujawahi miliki hata milioni 10 mkupuo. Maswala ya fedha yanaendeshw kwa masharti hasa biasahara za kibenki. Nenda hata NMB ikakope watahakikisha wanajua unakopa kwa sababu gani na wanaweza kukwambia mkopo unaochukua haukufai kutokana na biashara unayoenda kufanya. Hawatoi pesa ukafanyie biashara ya pilipili.
 
Personally sikubaliani na Mama kurudi shule, Mama aende college kwenye uhuru wa kufanya aliyokuwa anayataka pia kupata muda wa kulea mtoto.

Shule ni sehemu ya kupata elimu, ukihitaji kuolewa mwambie mzazi akuozeshe upate wasaa wa kuzaa utakavyo.

Women Empowers msizibe nafasi za watu wanaokwenda kusoma.
 
Personally sikubaliani na Mama kurudi shule, Mama aende college kwenye uhuru wa kufanya aliyokuwa anayataka pia kupata muda wa kulea mtoto.

Shule ni sehemu ya kupata elimu, ukihitaji kuolewa mwambie mzazi akuozeshe upate wasaa wa kuzaa utakavyo.

Women Empowers msizibe nafasi za watu wanaokwenda kusoma.
Nafikiri akipata wigo mpana zaidi itamsaidia zaidi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom