Mchengerwa: Maafisa Utumishi walioshindwa kuwapandisha vyeo waliostahili washushwe vyeo

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amewaelekeza watendaji wa ofisi yake kufanya ufuatiliaji ili kuwashusha vyeo Maafisa Utumishi katika Taasisi za Umma walioshindwa kutekeleza agizo la Mhe. Rais Samia Suluhu Hasssan la kuwapandisha vyeo watumishi wenye sifa za kupanda madaraja.

Mhe. Mchengerwa ametoa maelekezo hayo leo wakati akifungua kikao kazi cha Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali chenye lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watendaji hao kilichofanyika katika Ukumbi wa Hazina jijini Dodoma.

Mhe. Mchengerwa amesema, Afisa Utumishi yeyote aliyezembea na kusababisha Watumishi wa Umma kutopandishwa madaraja achukuliwe hatua kwa kushushwa cheo na kuhamishwa kituo cha kazi ili iwe ni fundisho kwa wengine wanaoshindwa kuwajibika ipasavyo.

“Fanyeni upembuzi na kuwaondoa Maafisa Utumishi wote waliobainika kutotekeleza wajibu wa kuwapandisha madaraja watumishi wenye sifa stahiki, kwani nimekuwa nikipokea malalamiko toka kwa watumishi wa taasisi mbalimbali,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Ameongeza kuwa, ofisi yake ilifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha taarifa za kiutumishi zilizotumwa na waajiri zinafanyiwa kazi kwa lengo la kuwapandisha vyeo watumishi husika, hivyo amewapongeza watendaji wa ofisi yake kwa kutekeleza vema wajibu wao.

Mhe. Mchengerwa ameeleza kuwa, Mhe. Rais anawajali sana Watumishi wa Umma na ndio maana alitoa agizo la kuwapandisha vyeo katika kipindi ambacho mijadala ya bajeti Bungeni ilikuwa ikiendelea jambo ambalo katika hali ya kawaida isingekuwa rahisi kutekelezeka.

“Mhe. Rais anatambua kuwa nguzo ya Serikali kiutendaji ni Watumishi wa Umma hivyo haiwezi kufanya vizuri iwapo haitowajali watumishi wake na ndio maana aliagiza wapandishwe madaraja,” Mhe. Mchengerwa amefafanua.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki wa kikao kazi hicho, Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma, Dkt. Emmanuel Shindika amemshukuru Mhe. Waziri kwa kukubali wito wa kukutana na Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali na kumuahidi kutekeleza maelekezo yote aliyoyatoa.

Dkt. Shindika amemhakikishia Mhe. Mchengerwa kuwa Watendaji Wakuu hao wa Wakala za Serikali watahakikisha wanahimiza uwajibikaji kwa Maafisa Utumishi wao ili waendane na kasi ya kiutendaji ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amehimiza uwajibikaji kwa Watendaji Wakuu wa Wakala za Serikali ili waweze kuendana na Kaulimbiu ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya KAZI IENDELEE.
 
Kasema amepokea malalamiko ya watumishi wengi, kayashughurikiaje? yeye kama yeye kawashusha maafsa utumishi wangapi?
 
Nani ataratibu mpango huo mzuri kuwabaini maafisa utumishi wazembe? Wengi wao Mh.Waziri piga jicho kwenye ofisi za halmashauri za wilaya kuna uonevu wa hali juu mno, eti baadhi wameambiwa wasubiri awamu ya mwakani??
 
Wa 2027 hawakupangwa licha ya wengine kutakiwa kupanda 2016 lakini walichelewa huwa hadi 2017 hii ni haki?
 
Chonde chonde Rais wetu mpendwa mrejeshe huyu jembe, kumbuka Mambo ya vikokotoo mwasisi na mtetezi wa kikokotoo!!!! Huyu jamaa ataleta Imani kubwa Sana mrejeshe
 
Back
Top Bottom