Slim5
JF-Expert Member
- Jan 7, 2014
- 28,433
- 38,401
Ukiwa Dar es Salaam maduka ya mchele huwa yanajinadi kwa mbwembwe MCHELE SAFI KUTOKA MBEYA
Ukishafika Mbeya unakutana na maduka ya mchele yakijinadi
PATA MCHELE SAFI KUTOKA KYELA
Ukifika zako hapo mjini Kyela unakutana na maduka ya mchele nayo yakijinadi TUNAUZA MCHELE SUPER KUTOKA IPINDA
Unakufahamu Ipinda wewe? Ukishafika unakwenda zako duka la mchele. Mwuzaji anakwambia HUU NI MCHELE SUPER KABISA KUTOKA BONDE LA TENENDE
Halafu ikitokea ukazurura hadi Tenende wenyeji wanakwambia MCHELE SUPER NI ULE WA SHAMBA LA MZEE MANJOLI.
Ukifika kwa Mzee Manjoli anakwambia mchele super ni ule wa shamba la MKE MKUBWA
Unashangaa?
Kila kizuri kina kizuri zaidi yake usituletee maringo kwa uzur wako kuna wazuri zaidi Yako .......[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ukishafika Mbeya unakutana na maduka ya mchele yakijinadi
PATA MCHELE SAFI KUTOKA KYELA
Ukifika zako hapo mjini Kyela unakutana na maduka ya mchele nayo yakijinadi TUNAUZA MCHELE SUPER KUTOKA IPINDA
Unakufahamu Ipinda wewe? Ukishafika unakwenda zako duka la mchele. Mwuzaji anakwambia HUU NI MCHELE SUPER KABISA KUTOKA BONDE LA TENENDE
Halafu ikitokea ukazurura hadi Tenende wenyeji wanakwambia MCHELE SUPER NI ULE WA SHAMBA LA MZEE MANJOLI.
Ukifika kwa Mzee Manjoli anakwambia mchele super ni ule wa shamba la MKE MKUBWA
Unashangaa?
Kila kizuri kina kizuri zaidi yake usituletee maringo kwa uzur wako kuna wazuri zaidi Yako .......[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]