Mchango wa mheshimiwa Zitto Kabwe Bajeti 2010/2011

Ntemi Kazwile

JF-Expert Member
May 14, 2010
2,185
307
Ninaomba kunukuu baadhi ya vipengele kwenye hotuba ya Zito ambavyo ningependa tuvijadili:

"Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa aliyetoka kuzungumza hivi sasa [mheshimiwa Mzindakaya] alizungumza kuhusiana na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi.
Mwaka 2005 Chama cha Mapinduzi kiliwaahidi Watanzania kwamba watahakikisha kwenye ilani yao sekta ya kilimo inakua kwa asilimia 20 [!]. Kwa mujibu wa MKUKUTA wa kwanza ambao tunaumaliza sasa ilitakiwa sekta ya kilimo ikue kwa asilimia kati ya 8 mpaka 10 ili kuweza kuwaondoa nusu ya Watanzania kwenye umaskini [wa kutupwa].
Kwa masikitiko makubwa kwa taarifa ya hali ya uchumi ambayo Waziri wa Fedha ameisoma jana sekta ya kilimo ilikua kwa asilimia 3.2 tu mwaka 2009 [ukiweka na wastani wa ukuaji wa idadi ya watu pamoja na madhara ya mfumuko wa bei ukuaji huu ni hasi (negative growth)].
Katika kipindi cha miaka 5 toka Serikali ya awamu ya 4 iingie madarakani sekta ya kilimo imekua kwa wastani wa asilimia 4 peke yake. Mmeshindwa hata kufikia nusu ya malengo yenu ya ilani ya Chama cha Mapinduzi. Mmeshindwa hata kufikia nusu ya ahadi kwa mujibu wa MKUKUTA. Hii ni aibu kubwa sana na tumewapa jumla ya shilingi trilioni 26 kwa miaka 4 iliyopita na mmeshidwa kukuza kilimo angalau kufikia nusu ya mambo ambayo nyinyi mlikuwa mmeyatarajia.(Makofi)......

Mheshimiwa Naibu Spika, yaani katika kila shilingi 100 tunaitumia katika matumizi ya kawaida shilingi 23 inabidi twende tukakope, tunakopa kulipa mishahara, tunakopa kulipa posho, tunakopa kununua mafuta ya magari yetu, hii ni nchi ya namna gani? ....

Kwa sababu ni bajeti ya kuchumia tumbo, ni bajeti ya chote tunachokikusanya tunakila hatuendelei na bado tunabakia na gap ya kwenda kutafuta na kwenda kukopa na misaada kwa ajili ya kula na sio kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa sababu asilimia 65 ya bajeti ya maendeleo bado inategemea wafadhili na ukichukua recurrent na development budget asilimia 44 ya bajeti yetu na sio 33 kama Waziri alivyosema bajeti bado tunategemea wafadhili.
[Bajeti ya matumizi ya kawaida ina nakisi ya Tshs 1.8tr ambayo itazibwa na misaada ya wafadhili na mikopo kutoka ndani na nje. Inasemekana mwaka huu Serikali itafanya Deficit Financing (PRINTING MONEY!!!) ya thamani ya takribani 350bn. Katika Bajeti ya Maendeleo kuna nakisi ya Tsh 2.4tr ambayo ni sawa na asilimia 65 ya Bajeti ya Maendeleo na itazibwa na misaada na mikopo kutoka ndani na nje ya nchi]."


Tabia ya kutegemea kukopa ili ununue mahitaji yako ya muhimu ni moja ya tabia ambayo kama mtu hutaweza kuishinda ni certificate ya umasikini wa kudumu... kama hatuwezi kupunguza matumizi (safari, kualika wageni kupita uwezo wetu na ukarimu mwingine usiokuwa na tija kwa kisingizio cha kuitangaza nchi ni vitu wanavyofanya masikini na watu wenye akili za kimasikini) tunaweza tukiamua, lazima tujibane. Ninaogopa kama Kikwete atachaguliwa tena 2010 Tanzania ya 2015 itakuwa sawa na Zimbabwe ya 2005, nasema hivyo kwa sababu mtani wangu huyu Mkwere anapata faraja kwa kuonekana kwenye picha na watu maarufu, si kwa kuona watu wake wanaondokana na umasikini, kwa bahati mbaya kabisa an hulka za kimaskini, hatufai huyu!
 
Tanzania ya JK ina matatizo mawili. Moja na kubwa ni la kimfumo zaidi na la pili ni la Rais mwenyewe. Hilo la kwanza ndio kubwa zaidi na hatua ya kwanza ni ama kuitoa ccm au kuibadili ili ifanye tofauti. Kukiwa na mfumo mzuri, hilo la pili mara nyingi ni rahisi kulishughulikia.
 
Hizi ni "facts" zinazohitaji suluhisho la kuondoa tatizo hili la umaskini uliokithiri. Sasa hivi mtu mwenye kipato kidogo wategemezi walionyuma ni wengi kuliko huko nyuma mfano miaka ya 90 rudi nyuma mzee wa kichaga alikuwa na pato la kitosha kutokana na kahawa leo hii wazee wale na wake zao na watoto wao walioko vijijini na wajukuu na vituu vyao wote wanaishi kwa kutegemea misaada toka kwa watoto walio mjini. Siku hizi kwenda likizo kijijini si kheri tena maana kule mahitaji yote ni ya kununua - wakulima hawana hata akiba ya chakula chao
 
Unakopa ili ule, unakopa ili ulipe kibarua wa pale nyumbani hivi kweli utaendelea? siku zote mkopo unatakiwa uwe wa kufanya jambo/mradi wa maendeleo. Hapa nimepata picha kamili ya umasikini wa Taifa letu licha ya utajiri tuliobarikiwa na mwenyezi Mungu.
 
Hizi ni "facts" zinazohitaji suluhisho la kuondoa tatizo hili la umaskini uliokithiri. Sasa hivi mtu mwenye kipato kidogo wategemezi walionyuma ni wengi kuliko huko nyuma mfano miaka ya 90 rudi nyuma mzee wa kichaga alikuwa na pato la kitosha kutokana na kahawa leo hii wazee wale na wake zao na watoto wao walioko vijijini na wajukuu na vituu vyao wote wanaishi kwa kutegemea misaada toka kwa watoto walio mjini. Siku hizi kwenda likizo kijijini si kheri tena maana kule mahitaji yote ni ya kununua - wakulima hawana hata akiba ya chakula chao

Kwa kweli inatisha. Siku za nyuma mgeni kutoka kijijina alikuja angalau na hata maharagwe leo wanakuja empty handed.

Tunakopa ili tuvae
tunakopa ili tule
tunakopa ili tulipe ada za watoto
tunakopa ili tujiendeleze kielimu
tunakopa ili tupate nauli za kwenda kazini maana mishahara ya wengi inaisha baada ya siku kumi.
maendelea na hiyo MIKUKUTA sahauni
 
Ninaomba kunukuu baadhi ya vipengele kwenye hotuba ya Zito ambavyo ningependa tuvijadili:

"Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa aliyetoka kuzungumza hivi sasa [mheshimiwa Mzindakaya] alizungumza kuhusiana na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi.
Mwaka 2005 Chama cha Mapinduzi kiliwaahidi Watanzania kwamba ...........


Na huo ndio ukweli wenyewe mkubali au msikubali. Nchi ya kukopa!!!!
:embarrassed1:
 
watanzania wengi hawaelewi kua iyo ''DEFICIT FINANCING - PRINTING MONEY'' ndio chanzo cha mfumuko wa bei, na ndio chanzo cha mafuta kupanda, bei za chakula kupanda na garama za maisha kiujumla! hakuna kitu kibaya kama icho, ila serikali inakifanya kwani inajua umma mkubwa hawatajua kua shida wanazopata ni sababu ya matendo ya kishetani kama ayo ya kuchapisha pesa zaidi! tunabaki tunamlaumu mchuuzi kua wanapandisha bei, tunagombana wananchi wa kawaida eti muuza bidhaa fulani amepandisha bei na kuiomba eti serikali iwabane! kumbe serikali kwao ni kicheko wakijua ubaya wao haujajulikana! na ii serikali ya awamu ya nne ndio maarufu kwenye mchezo uo ndio maana kwa mfano bei za chakula zimepanda mara 3 hadi 4 ya zaidi alivyozikuta!

na chanzo cha yote haya ni uwezo mdogo wa ii serikali kushindwa kutafuta vyanzo vya mapato kwa hili nampongeza sana rais wa awamu ya tatu kwa kutojihusihsa na ushetani huu wa kuumiza wananchi! hata kama ufisadi ulikua ktk pesa alizozalisha na mtanzania wa kawaida alilindwa katika mahitaji yake!
 
watanzania wengi hawaelewi kua iyo ''DEFICIT FINANCING - PRINTING MONEY'' ndio chanzo cha mfumuko wa bei, na ndio chanzo cha mafuta kupanda, bei za chakula kupanda na garama za maisha kiujumla! hakuna kitu kibaya kama icho, ila serikali inakifanya kwani inajua umma mkubwa hawatajua kua shida wanazopata ni sababu ya matendo ya kishetani kama ayo ya kuchapisha pesa zaidi! tunabaki tunamlaumu mchuuzi kua wanapandisha bei, tunagombana wananchi wa kawaida eti muuza bidhaa fulani amepandisha bei na kuiomba eti serikali iwabane! kumbe serikali kwao ni kicheko wakijua ubaya wao haujajulikana! na ii serikali ya awamu ya nne ndio maarufu kwenye mchezo uo ndio maana kwa mfano bei za chakula zimepanda mara 3 hadi 4 ya zaidi alivyozikuta!

na chanzo cha yote haya ni uwezo mdogo wa ii serikali kushindwa kutafuta vyanzo vya mapato kwa hili nampongeza sana rais wa awamu ya tatu kwa kutojihusihsa na ushetani huu wa kuumiza wananchi! hata kama ufisadi ulikua ktk pesa alizozalisha na mtanzania wa kawaida alilindwa katika mahitaji yake!

Kipindi kile cha kodi ya kichwa wananchi walikuwa wanahoji matumizi ya serikali na kudai maendeleo kwa kuwa walikuwa wanajua, serikali kagundua namna ya kumuibia kipofu ni kuhakikisha humgusi wakaleta indirect tax na sasa wanatumia mbinu hiyo hiyo. Tutafuta mchawi wa ukosefu wa maendeleo yetu na tutampata kuwa ni mwenyekiti wa mtaa wetu, mtendaji wa kijiji chetu,etc (kwa sababu ndiye tunaogusana nao), kumbe matatizo yote yanaanzia Magogoni, kwa sera za kifukara kwa kuendekeza maisha ya kifahari tusiyostahili. kila kitu kopa.
 
Kijana kazungumza.Sipati picha kama angekua ameyazungumza hayo maneno bolded (baada ya quotation mark) bungeni ingekuaje. Nadhani imefika wakati kila mtanzania kwa nafasi yake ajifunze kuwajibika na si kusubiri kulaumu.

Mimi na wewe twaweza wajibika kuleta mabadiliko na mabadiliko haya tutayapata pitia sanduku la kura Oct 31 Jumapili 2010. Tujitokeze tulete mabadiliko. Tuweweke kina Zito wengi zaidi tuwapeleke kina Silaa tuone wapi watachomokea.
 
Hili swala ni gumu sana.

Ningependa kujua wanapo tayarisha Hii Budget ya mwaka wa fedha wana tizama nini esp? maana kama wanatayarisha budget muda wote huo na wanapofika wakati wa uchangiaji unaikuta hiyo Budget ina makosa rukuki, inamaaana huwa waandaaji wa budget huwa hawajiridhishi kwa kuipitia na kuhusisha wachumi wengine wenye esperience ya budget ya nchi au huwa kuna lao jambo kutowahusicha wasomi wa uchumi?

Maana kuan mapungufu fulani Zitto aliyasema "
Mheshimiwa Naibu Spika, Waziri wa Fedha amezungumza kuhusu kuuzwa kwa hisa za NBC na Serikali kupata zaidi ya shilingi bilioni 30. Lakini nimeangalia kitabu namba moja Revenue Book hiyo source of revenue haimo. Kwa hiyo nilikuwa naomba Waziri wa Fedha aweze kutoa ufafanuzi ? [Kila shilingi inayotarajiwa kukusanywa na Serikali ni lazima ionyeshwe katika Kitabu Na 1 cha Mapato ya Serikali. Tshs 30bn zimetajwa katika Hotuba ya Bajeti lakini haimo katika kitabu hicho.....!!!!]. " na Waziri wa fedha aliyasoma kwa budget ambavyo hivyo alivyo visema havipo hii si kuwadanganya wananchi twalipeleka wapi taifa jamani??

Naye mbuge mwingine wa CCM Mzindakaya akema Takwimu za WB 2007 kuwa sie ni maskini 89% na bado watanzani wengi tu wavivu ......????

Wavivu in what sence ?Kama nchi yenyewe haina MUSTAKABIRI wa jinsi gani kuiongoza nchi na mapendekezo muhimu yafanyiwe kiupaumbele sishangai kuona wanchi wakiwa wavivu wao hawaoni Serikali na CCM yake inavyojipanga hovyo hovyo kila kitu kikifanyika hiyo ilikuwa ni ILANI ya CCM na kumbe hakuna inamaana hatuko makini kati kuiongoza nchi twa rashia rashia tuuu,

Nini nachotaka kusema ni kuwa lazima tujiulize na huo usemi kuwa watanzania wengi sie ni wavivu?
1: Mikakati mibovu ya maendeleo nchini kwetu lazima tu itatufanya sie tuonekane ni wavivu
2: Viongozi wasio kuwa ni wazalendo na viongozi wasio taka kuona mbali
3: Budget hazina mikakati ya kuinua watu walio maskini yaaani kutengeneza mifumo bora ya kuinua uchumi kwa watu wa kipato chachini na mengineyo
 
Nasikitishwa sana na wabunge wa Tanzania akiwemo Zitto na Slaa wanavyojikita sana kwenye current budget badala ile ya 3 years.... ile inasomwa asubuhi... haiwezekani kila mtu anazungumzia kodi ya bia na sigara kila siku we must have serious people who are challenging our stragetic goals, objectives etc.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom