Mchakato wa Katiba Mpya Chini Mutungi ni Upotevu wa Rasilimali

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,559
41,075
Upatikanaji wa katiba mpya ni utaratibu wa kisheria, na mchakato mzima ni lazima uwe wa kisheria. Process nzima, kuanzia vikao mpaka ushirikishwaji ni lazima viwe vya kisheria.

Vikao vya mchakato wa katiba siyo vikao vya kitchen party ambapo mnakutana tu mnamchagua mwenyekiti; au binti anayeolewa au mzazi wake anatamka tu kuwa fulani utakuwa mwenyekiti wa vikao vya kitchen party.

Tumesikia kuwa Jaji Mutungi, mtu ambaye hana kabisa credibility ya neutrality hata kwenye nafasi yake ya sasa, ambapo mara nyingi ametumika kama kibaraka wa wanasiasa kuhujumu vyama vya upinzani, eti ameitisha kikao cha kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya. Mambo ya kujiuliza:

1) Ni sheria gani inampa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kusimamia upatikanaj wa katiba mpya?

2) Ni sifa zipi na zimetamkwa na sheria ipi za mtu kuwa kiongozi wa mchakato wa katiba mpya? Na hizo sifa Mutungi anazo?

3) Mutungi ni kiongozi wa vyama vya saisa, ana mamlaka yapi anayoweza kuzialika taasisi na asasi ambazo hazipo chini ya ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kushiriki vikao vinavyohusiana na upatikanaji wa katiba mpya?

4) Zipi ni hadidu za rejea ambazo Mutungi amepewa katika kuhakikisha katiba mpya yenye maslahi kwa umma wa Watanzania inapatikana? Hizo hadidu za rejea nani aliziandaa, na nani alizipitisha?

5) Kwenye taarifa iliyotolewa na Mutungi ni kwamba vyama vya siasa, kila kimoja eti kitawachagua watu watakaoshiriki kwenye mchakato wa katiba. Huu ni upuuzi wa hali ya juu. Mjumbe au mtaalam aliyeteuliwa na chama fulani kuingia kwenye hiyo kamati ya katiba, kwa vile ameteuliwa na chama fulani, kwa vyovyote vile ataingia huko akiwa na fikra kuwa anatakiwa kwenda kulinda maslahi ya hicho chama kilichomteua. Hali hiyo, itageuza vikao vya katiba kuwa vikao vya kugombea maslahi ya vyama vyao. Na je, wasipokubaliana, kutatokea nini? Nani atakuwa mwamuzi wa mwisho? Chama chenye wanachama 1,000 na 1,000,0000 vitakuwa na wawakilishi sawa? Hawa wanaenda kuandaa katiba ya vyama vya siasa au katiba ya nchi?

6) Mutungi anasema eti hiyo kamati itakayoundwa na wawakilishi wa vyama vya siasa itaandaa mapendekezo. Swali: Mapendekezo yanapelekwa kwa nani? Na huyo atakayetoa uamuzi wa mwisho juu ya mapendekezo, amepewa na nani hayo mamlaka? Asipoyakubali mapendekezo yote, kutatokea nini?

Wananchi tupinge matumuzi ya hovyo ya pesa yetu kupitia mgongo wa uandaaji wa katiba. Katiba ya nchi haitengenezwi kama katiba ya vikoba. Process nzima inatakiwa kuwa ya kisheria na jumuishi.

Katiba ya mpya ya nchi siyo ya Mh. Rais Samia, siyo ya Mutungi, siyo ya CHADEMA, siyo ya CCM, wala siyo ya ACT au kakikundi fulani ka watu. Ni aheri ijulikane kuwa hatuna katiba mpya kuliko kuletewa riwaya fulani iliyoandaliwa na kakikundi ka watu, halafu tukapewa tu kuwa hii ndiyo katiba ya nchi.

Katiba inatakiwa kuwa jumuishi. Zitafutwe asasi zote zilizo rasmi na zisizo rasmi. Hata JF inatakiwa kuwakilishwa maana ni kundi kubwa la watu. Kinachotafutwa ni ushirikishwaji mpana. Makundi ya wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, vyama vya siasa na wanasiasa, vyama vya kitaaluma, makundi ya wastaafu, watetezi wa haki za binadamu, uwakilishi wa kimaeneo na kikanda,taasisi za elimu, n.k. kama ni suala la gharama, kila kundi linaweza kujigharamia lenyewe kwenye usafiri, malazi na chakula. Serikali ishughulikie ukumbi na uchapaji wa nyaraka mbalimbali. Lakini kama watu watajitegemea kwa gharama, kusiwepo hata mmoja, hata kama ni Waziri, atakayetumia pesa ya umma kwaajili ya vikao vya katiba mpya.

Kumpa Mutungi usimamizi wa jambo hili inaonekana hatupo serious, tunataka kupoteza muda na rasilimali nyingine.

Mapendekezo ya Tume ya Jaji Warioba ndiyo mapendekezo pekee yaliyojumuisha watu weng kutoka maeneo yote ya nchi, na yaliyofanyiwa uchambuzi mkubwa kitaalam. Hapo ndipo mahali pekee sahihi pa kuanzia kama kuna dhamira njema ya kuipata katiba mpya nzuri inayotokana na matakwa ya wananchi, na siyo hii ya sasa inayotakiwa kutengenezwa na akina Mutungi.

Majina huumba, tusisahau ule msemo maarufu kuwa SIRI YA MTUNGI INAIJUA KATA. Tujiukize kuna siri gani juu ya jambo hili, hata mpaka usimamizi wa jambo hili muhimu sana kwa Taifa letu, kwa kizazi cha sasa na baadaye, anapewa Mtungi, mtu ambaye iwe ni kwa sheria au hata katiba iliyopo, au kupima uadilifu wa mhusika katika utendaji wake wa kazi kwa majukumu aliyo nayo sasa, kwa vyovyote vile hakustahili.
 
Rais wetu huwa anaanza vizuri. Badae kidogo hali inabadilika. Sijui hawa washauri wake wana nia thabiti? Kwenye issue yenye mgogoro wowote, au any negotiations, jambo la credibility na integrity ya mediator ni muhimu sana. Na lazima huyo mediator angalau aaaminike na pande zote. Mbona wazee wanaoaminika na pande zote nchi hii bado wapo wengi tu?

Sasa Jaji Mutungi alishalalamikiwa mara nyingi huko nyuma kwa kutokuwa fair na kuwa biased, ila bado washauri wa Rais wanajaribu kumuaminisha Rais kuwa hakuna shida endapo Jaji Mutungi ataendelea ku-act kama mediator. Au huenda sisi ndo hatujui vizuri, labda Jaji Mutungi kaanzisha tu mchakato, ila mediator atakuwa mwingine? Hii taabu kabisa.

Utadhani washauri wa Rais hawakujifunza mambo haya darasani buana? Wakati wanajua vizuri kabisa, ila wanafanya maksudi tu. Rais yeye hatuwezi kumlaumu sana maana yeye hawezi kujua kila kitu. Hao washauri wake ndio wakulaumiwa maana wao ni wataalamu ambao tunategemea wameenda shule kujifunza mambo haya. Otherwise, tuamini kuwa hakuna nia thabiti ya kuleta KATIBA iliyo bora.
 
Upatikanaji wa katiba mpya ni utaratibu wa kisheria, na mchakato mzima ni lazima uwe wa kisheria. Process nzima, kuanzia vikao mpaka ushirikishwaji ni lazima viwe vya kisheria.

Vikao vya mchakato wa katiba siyo vikao vya kitchen party ambapo mnakutana tu mnamchagua mwenyekiti; au binti anayeolewa au mzazi wake anatamka tu kuwa fulani utakuwa mwenyekiti wa vikao vya kitchen party.

Tumesikia kuwa Jaji Mutungi, mtu ambaye hana kabisa credibility ya neutrality hata kwenye nafasi yake ya sasa, ambapo mara nyingi ametumika kama kibaraka wa wanasiasa kuhujumu vyama vya upinzani, eti ameitisha kikao cha kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya. Mambo ya kujiuliza:

1) Ni sheria gani inampa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kusimamia upatikanaj wa katiba mpya?

2) Ni sifa zipi na zimetamkwa na sheria ipi za mtu kuwa kiongozi wa mchakato wa katiba mpya? Na hizo sifa Mutungi anazo?

3) Mutungi ni kiongozi wa vyama vya saisa, ana mamlaka yapi anayoweza kuzialika taasisi na asasi ambazo hazipo chini ya ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kushiriki vikao vinavyohusiana na upatikanaji wa katiba mpya?

4) Zipi ni hadidu za rejea ambazo Mutungi amepewa katika kuhakikisha katiba mpya yenye maslahi kwa umma wa Watanzania inapatikana? Hizo hadidu za rejea nani aliziandaa, na nani alizipitisha?

5) Kwenye taarifa iliyotolewa na Mutungi ni kwamba vyama vya siasa, kila kimoja eti kitawachagua watu watakaoshiriki kwenye mchakato wa katiba. Huu ni upuuzi wa hali ya juu. Mjumbe au mtaalam aliyeteuliwa na chama fulani kuingia kwenye hiyo kamati ya katiba, kwa vile ameteuliwa na chama fulani, kwa vyovyote vile ataingia huko akiwa na fikra kuwa anatakiwa kwenda kulinda maslahi ya hicho chama kilichomteua. Hali hiyo, itageuza vikao vya katiba kuwa vikao vya kugombea maslahi ya vyama vyao. Na je, wasipokubaliana, kutatokea nini? Nani atakuwa mwamuzi wa mwisho? Chama chenye wanachama 1,000 na 1,000,0000 vitakuwa na wawakilishi sawa? Hawa wanaenda kuandaa katiba ya vyama vya siasa au katiba ya nchi?

6) Mutungi anasema eti hiyo kamati itakayoundwa na wawakilishi wa vyama vya siasa itaandaa mapendekezo. Swali: Mapendekezo yanapelekwa kwa nani? Na huyo atakayetoa uamuzi wa mwisho juu ya mapendekezo, amepewa na nani hayo mamlaka? Asipoyakubali mapendekezo yote, kutatokea nini?

Wananchi tupinge matumuzi ya hovyo ya pesa yetu kupitia mgongo wa uandaaji wa katiba. Katiba ya nchi haitengenezwi kama katiba ya vikoba. Process nzima inatakiwa kuwa ya kisheria na jumuishi.

Katiba ya mpya ya nchi siyo ya Mh. Rais Samia, siyo ya Mutungi, siyo ya CHADEMA, siyo ya CCM, wala siyo ya ACT au kakikundi fulani ka watu. Ni aheri ijulikane kuwa hatuna katiba mpya kuliko kuletewa riwaya fulani iliyoandaliwa na kakikundi ka watu, halafu tukapewa tu kuwa hii ndiyo katiba ya nchi.

Katiba inatakiwa kuwa jumuishi. Zitafutwe asasi zote zilizo rasmi na zisizo rasmi. Hata JF inatakiwa kuwakilishwa maana ni kundi kubwa la watu. Kinachotafutwa ni ushirikishwaji mpana. Makundi ya wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, vyama vya siasa na wanasiasa, vyama vya kitaaluma, makundi ya wastaafu, watetezi wa haki za binadamu, uwakilishi wa kimaeneo na kikanda,taasisi za elimu, n.k. kama ni suala la gharama, kila kundi linaweza kujigharamia lenyewe kwenye usafiri, malazi na chakula. Serikali ishughulikie ukumbi na uchapaji wa nyaraka mbalimbali. Lakini kama watu watajitegemea kwa gharama, kusiwepo hata mmoja, hata kama ni Waziri, atakayetumia pesa ya umma kwaajili ya vikao vya katiba mpya.

Kumpa Mutungi usimamizi wa jambo hili inaonekana hatupo serious, tunataka kupoteza muda na rasilimali nyingine.

Mapendekezo ya Tume ya Jaji Warioba ndiyo mapendekezo pekee yaliyojumuisha watu weng kutoka maeneo yote ya nchi, na yaliyofanyiwa uchambuzi mkubwa kitaalam. Hapo ndipo mahali pekee sahihi pa kuanzia kama kuna dhamira njema ya kuipata katiba mpya nzuri inayotokana na matakwa ya wananchi, na siyo hii ya sasa inayotakiwa kutengenezwa na akina Mutungi.

Majina huumba, tusisahau ule msemo maarufu kuwa SIRI YA MTUNGI INAIJUA KATA. Tujiukize kuna siri gani juu ya jambo hili, hata mpaka usimamizi wa jambo hili muhimu sana kwa Taifa letu, kwa kizazi cha sasa na baadaye, anapewa Mtungi, mtu ambaye iwe ni kwa sheria au hata katiba iliyopo, au kupima uadilifu wa mhusika katika utendaji wake wa kazi kwa majukumu aliyo nayo sasa, kwa vyovyote vile hakustahili.
Hana lolote, ni mpuuzi tu!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Hana lolote, ni mpuuzi tu!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Huyo Mitungi sijui Litungi kama kashindwa kuiendesha ofisi yake tuu ya vyama vya siasa anapata wapi credibility ya kusimamia mambo ya nchi.
Mitungi ni kati ya majaji uchwara wa hovyo kuwahi kitokea karne ya 21.
Samia ajue hili ni taifa huru lenye watu wenye Akili asituchee na tusichezeane. Ni vizuri tukaheshimiana amepata urais kwa bahati sana ktk nchi ya kigeni.

Wenye nchi tuna wivu mkubwa sana hasa kuona watu wanao toka nchi zingine wanakuja kuichea nchi yetu tunaumia na tutukichukua maamuzi magumu tusilaumiane.
 
Rais wetu huwa anaanza vizuri. Badae kidogo hali inabadilika. Sijui hawa washauri wake wana nia thabiti? Kwenye issue yenye mgogoro wowote, au any negotiations, jambo la credibility na integrity ya mediator ni muhimu sana. Na lazima huyo mediator angalau aaaminike na pande zote. Mbona wazee wanaoaminika na pande zote nchi hii bado wapo wengi tu?

Sasa Jaji Mutungi alishalalamikiwa mara nyingi huko nyuma kwa kutokuwa fair na kuwa biased, ila bado washauri wa Rais wanajaribu kumuaminisha Rais kuwa hakuna shida endapo Jaji Mutungi ataendelea ku-act kama mediator. Au huenda sisi ndo hatujui vizuri, labda Jaji Mutungi kaanzisha tu mchakato, ila mediator atakuwa mwingine? Hii taabu kabisa.

Utadhani washauri wa Rais hawakujifunza mambo haya darasani buana? Wakati wanajua vizuri kabisa, ila wanafanya maksudi tu. Rais yeye hatuwezi kumlaumu sana maana yeye hawezi kujua kila kitu. Hao washauri wake ndio wakulaumiwa maana wao ni wataalamu ambao tunategemea wameenda shule kujifunza mambo haya. Otherwise, tuamini kuwa hakuna nia thabiti ya kuleta KATIBA iliyo bora.
Well said...
Ila tatizo lako ni Mutungi peke yake au ofisi yake kuendesha na kusimamia mchakato huo?

Maana naona watu wengi wanamlalamikia Mutungi in person kusimamia jambo hilo? Ila mleta mada kahoji ni sheria ipi inayompa mamlaka ya jambo hilo?

Kuhusu washauri,labda yawezekana wameshauri usiwalaumu bure tu..tatizo la washauri siku zote hawawezi toka hadharani waseme tumeshauri hivi na vile,ila mshauriwa amekataa,wanabaki kimya na kutupiwa lawama..na kwa kweli hivyo ndivyo inavyotakiwa kuwa.

Lakini pia imezuka tabia sasa ya kila jambo lisilowapendeza wengi,likiamriwa na mkuu,wasiopendezwa na jambo hilo utawasikia wakisema hatuwezi mlaumu mkuu,tutawalaumu washauri wake,maana mkuu hawezi jua kila kitu...ila jambo zuri utasikia mkuu anaupiga mwingi sanaa..
Kwa maoni yangu,kusema eti mkuu anapotoshwa na washauri wake kwa hata vitu vidogo vidogo,ni kumdharau mkuu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Naona huu mchakato wa kuipata Katiba Mpya bado hatujawa serious nao, kinachofanyika mpaka sasa ni muendelezo wa makosa yale yale yaliyotukwamisha wakati ule wa JK.

Ukiutazama kwa makini, utaona kuna makosa mengi sana ambayo nashindwa kuelewa kwanini yanajirudia, kosa moja kubwa kuliko yote ni kumuacha Rais ambaye nae ni mwenyekiti wa chama cha siasa, awe ndie kiongozi. Hapa tayari tumeshaanza kwa kukosea.

Na kuonesha vile tunaendelea kukosea kwenye hili jambo, ni pale ambapo baadhi yetu tunarudi kumtaka Rais huyo huyo amuondoe Mutungi tusiyemtaka kwa sababu ya rekodi yake, amuweke mwingine tutakayeridhika naye.

Hata kama hilo likifanyika, bado tutaendelea kucheza humo humo ndani ya kisima cha makosa, ambapo huyo mpya atakayeteuliwa na Rais, bado kuna uwezekano mkubwa akaenda kufanya kazi ya kumfurahisha bosi wake, kwa maslahi ya chama chao, matokeo yake tutaanza tena kupiga kelele na kuendelea kujichelewesha wenyewe.

Kwa maoni yangu, hapa kinachotakiwa kufanyika ili tuipate Katiba Mpya bora, kwanza na muhimu kabisa, Rais anatakiwa kuwekwa pembeni kwenye huu mchakato, atafutwe kiongozi/ au iundwe taasisi nyingine huru isiyo na upande wowote, isimamie huu mchakato.

Taasisi husika iachwe huru kufanya kazi zake bila vitisho vyovyote [ bunge litunge sheria ya kuiunda, na kuwalinda watendaji wake mpaka mwisho wa majukumu yao], lakini kinyume na hapo, tutaendelea kudanganyana tu.
 
Well said...
Ila tatizo lako ni Mutungi peke yake au ofisi yake kuendesha na kusimamia mchakato huo?

Maana naona watu wengi wanamlalamikia Mutungi in person kusimamia jambo hilo? Ila mleta mada kahoji ni sheria ipi inayompa mamlaka ya jambo hilo?

Kuhusu washauri,labda yawezekana wameshauri usiwalaumu bure tu..tatizo la washauri siku zote hawawezi toka hadharani waseme tumeshauri hivi na vile,ila mshauriwa amekataa,wanabaki kimya na kutupiwa lawama..na kwa kweli hivyo ndivyo inavyotakiwa kuwa.

Lakini pia imezuka tabia sasa ya kila jambo lisilowapendeza wengi,likiamriwa na mkuu,wasiopendezwa na jambo hilo utawasikia wakisema hatuwezi mlaumu mkuu,tutawalaumu washauri wake,maana mkuu hawezi jua kila kitu...ila jambo zuri utasikia mkuu anaupiga mwingi sanaa..
Kwa maoni yangu,kusema eti mkuu anapotoshwa na washauri wake kwa hata vitu vidogo vidogo,ni kumdharau mkuu

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Sijagusia suala la hoja ya legal basis kwa Mutungi kuwa mediator wa jambo hili maana tumeshazoea utamaduni wa kutofuata sheria katika nchi nyingi za Africa, au developing countries. Imekuwa ni jambo la kawaida.

Mkuu yeye kulaumiwa au kutolaumiwa inategemea na maarifa yake katika hicho anachoshauriwa. Sina nia ya kutumia lugha ya maudhi ili kumdogodesha Rais, ila nachoweza kusema ni kuwa Rais hawezi kuwa na maarifa ya kitaalamu ya kila jambo ktk nchi. Maana maamuzi mengi yanategemea na utalaamu wa jambo husika endapo wataalaamu kweli watapewa nafasi katika jambo hilo na huyo Kiongozi akawa willing kufuata mawazo ya kitaalamu..

Sent from using JamiiForums mobile app
 
Naona huu mchakato wa kuipata Katiba Mpya bado hatujawa serious nao, kinachofanyika mpaka sasa ni muemdelezo wa makosa yale yale yaliyotukwamisha wakati ule wa JK.

Kuna makosa mengi sana ambayo nashindwa kuelewa kwanini yanajirudia, kosa moja kubwa kuliko yote ni kumuacha Rais ambaye nae ni mwenyekiti wa chama cha siasa, awe ndie kiongozi. Hapa tayari tumeshaanza kwa kukosea.

Na kuonesha vile tunaendelea kukosea kwenye hili jambo, ni pale ambapo baadhi yetu tunarudi kumtaka Rais huyo huyo amuondoe Mutungi tusiyemtaka kwa sababu ya rekodi yake, amuweke mwingine tutakayeridhika naye.

Hata kama hilo likifanyika, bado tutaendelea kucheza humo humo ndani ya kisima cha makosa, ambapo huyo mpya atakayeteuliwa na Rais, bado kuna uwezekano mkubwa akaenda kufanya kazi ya kumfurahisha bosi wake, kwa maslahi ya chama chao, matokeo yake tutaanza tena kupiga kelele na kuendelea kujichelewesha wenyewe.

Kwa maoni yangu, hapa kinachotakiwa kufanyika ili tuipate Katiba Mpya bora, kwanza na muhimu kabisa, Rais anatakiwa kuwekwa pembeni kwenye huu mchakato, atafutwe kiongozi/ au iundwe taasisi nyingine huru isiyo na upande wowote, isimamie huu mchakato.

Taasisi husika iachwe huru kufanya kazi zake bila vitisho vyovyote [ bunge litunge sheria ya kuiunda, na kuwalinda watendaji wake mpaka mwisho wa majukumu yao], lakini kinyume na hapo, tutaendelea kudanganyana tu.
Umezungumza jambo lenye tija sana. Ila kama nilivyosema nawe kwenye ule uzi mwingine, jambo kama hili linahitaji nia ya dhati ya ama serikali iliyopo madarakani au kwa kutumia nguvu iliyopo kwa Wananchi. Sasa hiyo nguvu mie bado siioni kama ipo. Rejea nilichosema kule kwenye ule uzi kuhusu uwekezaji wa elimu ya uraia kwa wananchi na kuwa na malengo ya badae kidogo.

Sent from using JamiiForums mobile app
 
Naona huu mchakato wa kuipata Katiba Mpya bado hatujawa serious nao, kinachofanyika mpaka sasa ni muemdelezo wa makosa yale yale yaliyotukwamisha wakati ule wa JK.

Kuna makosa mengi sana ambayo nashindwa kuelewa kwanini yanajirudia, kosa moja kubwa kuliko yote ni kumuacha Rais ambaye nae ni mwenyekiti wa chama cha siasa, awe ndie kiongozi. Hapa tayari tumeshaanza kwa kukosea.

Na kuonesha vile tunaendelea kukosea kwenye hili jambo, ni pale ambapo baadhi yetu tunarudi kumtaka Rais huyo huyo amuondoe Mutungi tusiyemtaka kwa sababu ya rekodi yake, amuweke mwingine tutakayeridhika naye.

Hata kama hilo likifanyika, bado tutaendelea kucheza humo humo ndani ya kisima cha makosa, ambapo huyo mpya atakayeteuliwa na Rais, bado kuna uwezekano mkubwa akaenda kufanya kazi ya kumfurahisha bosi wake, kwa maslahi ya chama chao, matokeo yake tutaanza tena kupiga kelele na kuendelea kujichelewesha wenyewe.

Kwa maoni yangu, hapa kinachotakiwa kufanyika ili tuipate Katiba Mpya bora, kwanza na muhimu kabisa, Rais anatakiwa kuwekwa pembeni kwenye huu mchakato, atafutwe kiongozi/ au iundwe taasisi nyingine huru isiyo na upande wowote, isimamie huu mchakato.

Taasisi husika iachwe huru kufanya kazi zake bila vitisho vyovyote [ bunge litunge sheria ya kuiunda, na kuwalinda watendaji wake mpaka mwisho wa majukumu yao], lakini kinyume na hapo, tutaendelea kudanganyana tu.
Ukweli ulio mchungu ni kuwa CCM hawawezi kuwa na nia ya dhati ya kuleta katiba bora yenye maslahi makubwa ya nchi. Maana kwa kufanya hivyo(jambo ambalo wanalifahamu wazi kabisa) ni kusababisha wao waondolewe madarakani, jambo ambalo naamini hawapo tayari hata kwa sekunde moja. Kwahiyo hoja za Tundu Lissu kuwa haya maridhiano yanaweza yasiwe na tija kwenye issue za Katiba bora zinaweza kuwa hoja za msingi kabisa.

Katiba bora itakuja kwa mashinikizo makubwa ya nguvu ya umma. Hii nguvu kwa sasa haipo nchini kwetu ila kinachoweza kufanyika sasa ni luendelea kuwekeza kwenye kutoa elimu ya uraia, kisha angalau baada ya miaka 20-30 hivi umma unaweza kuwa na nguvu ya kutosha kuushinikiza Serikali ilete katiba bora yenye maslahi ya umma wenyewe.

Sent from using JamiiForums mobile app
 
Ukweli ulio mchungu ni kuwa CCM hawawezi kuwa na nia ya dhati ya kuleta katiba bora yenye maslahi makubwa ya nchi. Maana kwa kufanya hivyo(jambo ambalo wanalifahamu wazi kabisa) ni kusababisha wao waondolewe madarakani, jambo ambalo naamini hawapo tayari hata kwa sekunde moja. Kwahiyo hoja za Tundu Lissu kuwa haya maridhiano yanaweza yasiwe na tija kwenye issue za Katiba bora zinaweza kuwa hoja za msingi kabisa.

Katiba bora itakuja kwa mashinikizo makubwa ya nguvu ya umma. Hii nguvu kwa sasa haipo nchini kwetu ila kinachoweza kufanyika sasa ni luendelea kuwekeza kwenye kutoa elimu ya uraia, kisha angalau baada ya miaka 20-30 hivi umma unaweza kuwa na nguvu ya kutosha kuushinikiza Serikali ilete katiba bora yenye maslahi ya umma wenyewe.

Sent from using JamiiForums mobile app
Hili la uwekezaji kwenye elimu ya uraia na muda unaohitajika kulifanikisha naona nao ni mlima mrefu zaidi tutakaotakiwa kuupanda, mrefu zaidi ya huu wa sasa wa kuipata hiyo Katiba Mpya.

Kutuunganisha watanzania tuanze kudai haki zetu kwa umoja, bila kutazamana itikadi zetu, rangi, na dini zetu, itakuwa ni hatua ya kwanza, halafu hapo ndipo itafuatia ile ya pili, ya kujitoa mhanga kudai haki zetu bila kuogopa vitisho vya polisi, ambao mara nyingi hutumiwa na CCM kulinda maslahi yake.

Hiyo hatua ya pili ndio imeshaonekana ngumu zaidi hata sasa, hebu tazama huko mitandaoni aina ya maoni yanayotolewa, utaona wazi kabisa wengi wetu tunajitambua, lakini tatizo letu linakuja pale ambapo tunashindwa kuchukua hatua, na badala yake kuendelea kubaki watu wa kulalamika kila siku, safari yetu bado ni ndefu sana mpaka inachosha ku-imagine!.
 
Hili la uwekezaji kwenye elimu ya uraia na muda unaohitajika kulifanikisha naona nao ni mlima mrefu zaidi tutakaotakiwa kuupanda, mrefu zaidi ya huu wa sasa wa kuipata hiyo Katiba Mpya.

Kutuunganisha watanzania tuanze kudai haki zetu kwa umoja, bila kutazamana itikadi zetu, rangi, na dini zetu, itakuwa ni hatua ya kwanza, halafu hapo ndipo itafuatia ile ya pili, ya kujitoa mhanga kudai haki zetu bila kuogopa vitisho vya polisi, ambao mara nyingi hutumiwa na CCM kulinda maslahi yake.

Hiyo hatua ya pili ndio imeshaonekana ngumu zaidi hata sasa, hebu tazama huko mitandaoni aina ya maoni yanayotolewa, utaona wazi kabisa wengi wetu tunajitambua, lakini tatizo letu linakuja pale ambapo tunashindwa kuchukua hatua, na badala yake kuendelea kubaki watu wa kulalamika kila siku, safari yetu bado ni ndefu sana mpaka inachosha ku-imagine!.
Kumbuka kundi kubwa la watu wanaotoa mawazo unayosema ni mazuri mitandaoni ni kundi la "elites". Kundi ambalo kwa bahati mbaya huwa halipo tayari kuwa front kwenye mapambano ya kudai haki.

Mapambano ya kudai haki mara nyingi hufanywa na watu wa kawaida huko mitaani. Wananchi wa kawaida kabisa kwenye mitaa yetu. Huko ndiko uwekezaji wa ushawishi unatakiwa kufanyika.

Sent from using JamiiForums mobile app
 
Rais wetu huwa anaanza vizuri. Badae kidogo hali inabadilika. Sijui hawa washauri wake wana nia thabiti? Kwenye issue yenye mgogoro wowote, au any negotiations, jambo la credibility na integrity ya mediator ni muhimu sana. Na lazima huyo mediator angalau aaaminike na pande zote. Mbona wazee wanaoaminika na pande zote nchi hii bado wapo wengi tu?

Sasa Jaji Mutungi alishalalamikiwa mara nyingi huko nyuma kwa kutokuwa fair na kuwa biased, ila bado washauri wa Rais wanajaribu kumuaminisha Rais kuwa hakuna shida endapo Jaji Mutungi ataendelea ku-act kama mediator. Au huenda sisi ndo hatujui vizuri, labda Jaji Mutungi kaanzisha tu mchakato, ila mediator atakuwa mwingine? Hii taabu kabisa.

Utadhani washauri wa Rais hawakujifunza mambo haya darasani buana? Wakati wanajua vizuri kabisa, ila wanafanya maksudi tu. Rais yeye hatuwezi kumlaumu sana maana yeye hawezi kujua kila kitu. Hao washauri wake ndio wakulaumiwa maana wao ni wataalamu ambao tunategemea wameenda shule kujifunza mambo haya. Otherwise, tuamini kuwa hakuna nia thabiti ya kuleta KATIBA iliyo bora.
Hivi huyu Jaji hajafikia umri wa kustaafu?

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Upatikanaji wa katiba mpya ni utaratibu wa kisheria, na mchakato mzima ni lazima uwe wa kisheria. Process nzima, kuanzia vikao mpaka ushirikishwaji ni lazima viwe vya kisheria.

Vikao vya mchakato wa katiba siyo vikao vya kitchen party ambapo mnakutana tu mnamchagua mwenyekiti; au binti anayeolewa au mzazi wake anatamka tu kuwa fulani utakuwa mwenyekiti wa vikao vya kitchen party.

Tumesikia kuwa Jaji Mutungi, mtu ambaye hana kabisa credibility ya neutrality hata kwenye nafasi yake ya sasa, ambapo mara nyingi ametumika kama kibaraka wa wanasiasa kuhujumu vyama vya upinzani, eti ameitisha kikao cha kuanzisha mchakato wa kupata katiba mpya. Mambo ya kujiuliza:

1) Ni sheria gani inampa mamlaka msajili wa vyama vya siasa kusimamia upatikanaj wa katiba mpya?

2) Ni sifa zipi na zimetamkwa na sheria ipi za mtu kuwa kiongozi wa mchakato wa katiba mpya? Na hizo sifa Mutungi anazo?

3) Mutungi ni kiongozi wa vyama vya saisa, ana mamlaka yapi anayoweza kuzialika taasisi na asasi ambazo hazipo chini ya ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kushiriki vikao vinavyohusiana na upatikanaji wa katiba mpya?

4) Zipi ni hadidu za rejea ambazo Mutungi amepewa katika kuhakikisha katiba mpya yenye maslahi kwa umma wa Watanzania inapatikana? Hizo hadidu za rejea nani aliziandaa, na nani alizipitisha?

5) Kwenye taarifa iliyotolewa na Mutungi ni kwamba vyama vya siasa, kila kimoja eti kitawachagua watu watakaoshiriki kwenye mchakato wa katiba. Huu ni upuuzi wa hali ya juu. Mjumbe au mtaalam aliyeteuliwa na chama fulani kuingia kwenye hiyo kamati ya katiba, kwa vile ameteuliwa na chama fulani, kwa vyovyote vile ataingia huko akiwa na fikra kuwa anatakiwa kwenda kulinda maslahi ya hicho chama kilichomteua. Hali hiyo, itageuza vikao vya katiba kuwa vikao vya kugombea maslahi ya vyama vyao. Na je, wasipokubaliana, kutatokea nini? Nani atakuwa mwamuzi wa mwisho? Chama chenye wanachama 1,000 na 1,000,0000 vitakuwa na wawakilishi sawa? Hawa wanaenda kuandaa katiba ya vyama vya siasa au katiba ya nchi?

6) Mutungi anasema eti hiyo kamati itakayoundwa na wawakilishi wa vyama vya siasa itaandaa mapendekezo. Swali: Mapendekezo yanapelekwa kwa nani? Na huyo atakayetoa uamuzi wa mwisho juu ya mapendekezo, amepewa na nani hayo mamlaka? Asipoyakubali mapendekezo yote, kutatokea nini?

Wananchi tupinge matumuzi ya hovyo ya pesa yetu kupitia mgongo wa uandaaji wa katiba. Katiba ya nchi haitengenezwi kama katiba ya vikoba. Process nzima inatakiwa kuwa ya kisheria na jumuishi.

Katiba ya mpya ya nchi siyo ya Mh. Rais Samia, siyo ya Mutungi, siyo ya CHADEMA, siyo ya CCM, wala siyo ya ACT au kakikundi fulani ka watu. Ni aheri ijulikane kuwa hatuna katiba mpya kuliko kuletewa riwaya fulani iliyoandaliwa na kakikundi ka watu, halafu tukapewa tu kuwa hii ndiyo katiba ya nchi.

Katiba inatakiwa kuwa jumuishi. Zitafutwe asasi zote zilizo rasmi na zisizo rasmi. Hata JF inatakiwa kuwakilishwa maana ni kundi kubwa la watu. Kinachotafutwa ni ushirikishwaji mpana. Makundi ya wakulima, wafanyabiashara, wafanyakazi, vyama vya siasa na wanasiasa, vyama vya kitaaluma, makundi ya wastaafu, watetezi wa haki za binadamu, uwakilishi wa kimaeneo na kikanda,taasisi za elimu, n.k. kama ni suala la gharama, kila kundi linaweza kujigharamia lenyewe kwenye usafiri, malazi na chakula. Serikali ishughulikie ukumbi na uchapaji wa nyaraka mbalimbali. Lakini kama watu watajitegemea kwa gharama, kusiwepo hata mmoja, hata kama ni Waziri, atakayetumia pesa ya umma kwaajili ya vikao vya katiba mpya.

Kumpa Mutungi usimamizi wa jambo hili inaonekana hatupo serious, tunataka kupoteza muda na rasilimali nyingine.

Mapendekezo ya Tume ya Jaji Warioba ndiyo mapendekezo pekee yaliyojumuisha watu weng kutoka maeneo yote ya nchi, na yaliyofanyiwa uchambuzi mkubwa kitaalam. Hapo ndipo mahali pekee sahihi pa kuanzia kama kuna dhamira njema ya kuipata katiba mpya nzuri inayotokana na matakwa ya wananchi, na siyo hii ya sasa inayotakiwa kutengenezwa na akina Mutungi.

Majina huumba, tusisahau ule msemo maarufu kuwa SIRI YA MTUNGI INAIJUA KATA. Tujiukize kuna siri gani juu ya jambo hili, hata mpaka usimamizi wa jambo hili muhimu sana kwa Taifa letu, kwa kizazi cha sasa na baadaye, anapewa Mtungi, mtu ambaye iwe ni kwa sheria au hata katiba iliyopo, au kupima uadilifu wa mhusika katika utendaji wake wa kazi kwa majukumu aliyo nayo sasa, kwa vyovyote vile hakustahili.
Huyu mtungi anajulikana kwa ukosefu wa uadilifu tangu akiwa hakimu kisutu. Alikuwa mtu wa rushwa na kama system ningekuwa inafanya kazi vizuri asingepewa ujaji
 
Naona huu mchakato wa kuipata Katiba Mpya bado hatujawa serious nao, kinachofanyika mpaka sasa ni muemdelezo wa makosa yale yale yaliyotukwamisha wakati ule wa JK.

Kuna makosa mengi sana ambayo nashindwa kuelewa kwanini yanajirudia, kosa moja kubwa kuliko yote ni kumuacha Rais ambaye nae ni mwenyekiti wa chama cha siasa, awe ndie kiongozi. Hapa tayari tumeshaanza kwa kukosea.

Na kuonesha vile tunaendelea kukosea kwenye hili jambo, ni pale ambapo baadhi yetu tunarudi kumtaka Rais huyo huyo amuondoe Mutungi tusiyemtaka kwa sababu ya rekodi yake, amuweke mwingine tutakayeridhika naye.

Hata kama hilo likifanyika, bado tutaendelea kucheza humo humo ndani ya kisima cha makosa, ambapo huyo mpya atakayeteuliwa na Rais, bado kuna uwezekano mkubwa akaenda kufanya kazi ya kumfurahisha bosi wake, kwa maslahi ya chama chao, matokeo yake tutaanza tena kupiga kelele na kuendelea kujichelewesha wenyewe.

Kwa maoni yangu, hapa kinachotakiwa kufanyika ili tuipate Katiba Mpya bora, kwanza na muhimu kabisa, Rais anatakiwa kuwekwa pembeni kwenye huu mchakato, atafutwe kiongozi/ au iundwe taasisi nyingine huru isiyo na upande wowote, isimamie huu mchakato.

Taasisi husika iachwe huru kufanya kazi zake bila vitisho vyovyote [ bunge litunge sheria ya kuiunda, na kuwalinda watendaji wake mpaka mwisho wa majukumu yao], lakini kinyume na hapo, tutaendelea kudanganyana tu.

Umenena vizuri kabisa.

Katiba siyo ya Rais, Rais ni zao la katiba. Mzaliwa hawezi kujizaa.

Mapendekezo yangu hayatofautiani nawe kimsimamo. Jambo amblo lingefanyika, kwanza ingekuwa ni kuzitambua taasisi za umma, za Serikali, asasi za kirai, asasi za kidini, vyama vya siasa, taasisi za kielimu, makundi mbalimbali yaliyo rasmi na yasiyo rasmi.

Hawa wote wapewe nafasi ya kuwateua wawakilishi wao.

Timu ya majaji iandae hadidu za rejea za Tume ya katiba.

Wawakilishi wa makundi yote wakutane kupitia hadidu za rejea na kuzipitisha.

Wawakilishi wa makundi yote wapendekeze majina matatu kwa kila nafasi kwenye kamati ya katiba. Majina hayo yaliyopendekezwa kutika kwenye orodha ya watu wenye sifa kama zitakavyokuwa zimeanishwa, na yakawa yamepiguwa kura na wawakikishi wa makundi yote, yapelekwe kwa Rais ambaye atachukua jina mojawapo kutoka kwa waliopendekezwa, na kulitangaza kwa nafasi husika, kisha wajumbe hao waapishwe na jaji mkuu kuwa wajumbe wa kamati ya katiba.

Kamati ya katiba ipitie mapendekezo ya kamati ya katiba ya jaji Warioba, kisha kufanyia marekebisho maeneo ambayo itaonekana kuna haja. Kisha waandae version ya mwisho ya katiba pendekezwa ambayo itapigiwa kura na wajumbe wawakilishi wa makundi yote.

Baada ya hapo, kazi.iwe imekwisha. Sioni umuhimu wa kuandaa uchaguzi wa wananchi wote kuipigia kura katiba. Jambo la muhimu ni uwakilishi wa wananchi kupitia makundi mbalimbali uwe mpana sana.
 
Huyo Mitungi sijui Litungi kama kashindwa kuiendesha ofisi yake tuu ya vyama vya siasa anapata wapi credibility ya kusimamia mambo ya nchi.
Mitungi ni kati ya majaji uchwara wa hovyo kuwahi kitokea karne ya 21.
Samia ajue hili ni taifa huru lenye watu wenye Akili asituchee na tusichezeane. Ni vizuri tukaheshimiana amepata urais kwa bahati sana ktk nchi ya kigeni.

Wenye nchi tuna wivu mkubwa sana hasa kuona watu wanao toka nchi zingine wanakuja kuichea nchi yetu tunaumia na tutukichukua maamuzi magumu tusilaumiane.
we kawahi mirembe hutakiwi kuendelea kuishi nasi uraiani. Unajua maana ya Tanzania? We ndiyo mgeni maana huwajui hata wenyeji
 
Utadhani washauri wa Rais hawakujifunza mambo haya darasani buana? Wakati wanajua vizuri kabisa, ila wanafanya maksudi tu. Rais yeye hatuwezi kumlaumu sana maana yeye hawezi kujua kila kitu. Hao washauri wake ndio wakulaumiwa maana wao ni wataalamu ambao tunategemea wameenda shule kujifunza mambo haya. Otherwise, tuamini kuwa hakuna nia thabiti ya kuleta KATIBA iliyo bora.
Washauri mara zote hubebeshwa lawama tu Ila pongezi atapewa boss.
JokaKuu zitto junior
 
Washauri mara zote hubebeshwa lawama tu Ila pongezi atapewa boss.
JokaKuu zitto junior
Tunajaribu ku-assume kuwa Rais ana nia ya dhati ya mabadiliko kama anavyojinasibu kwenye majukwaa. Kisha Wataalamu wanahitajika ku-play role yao kuwezesha hayo mabadiliko kwa kumshauri Rais. Endapo Rais anashauriwa vizuri ila yeye mwenyewe akakaidi na kufuata njia zake, basi hilo ni tatizo la kiongozi mwenyewe. Kwa bahati mbaya huwa hatuambiwi kuwa wataalaamu wamemshauri nini Kiongozi kuhusiana na maamuzi yanayofanyika kila siku ili tujue exactly ni nani wa kumtupia lawama.

Sent using JamiiForums mobile app
 
Kumbuka kundi kubwa la watu wanaotoa mawazo unayosema ni mazuri mitandaoni ni kundi la "elites". Kundi ambalo kwa bahati mbaya huwa halipo tayari kuwa front kwenye mapambano ya kudai haki.

Mapambano ya kudai haki mara nyingi hufanywa na watu wa kawaida huko mitaani. Wananchi wa kawaida kabisa kwenye mitaa yetu. Huko ndiko uwekezaji wa ushawishi unatakiwa kufanyika.

Sent from using JamiiForums mobile app
Kwanini hawa elites hawapo tayari kwenda front kudai haki zao kama nao wanapitia matatizo yale yale wanayopitia wale wengine?

Upandaji wa gharama za maisha ni mfano mzuri, hili linawagusa wote, elites na wasio elites, naona hapa tuambizane ukweli tu, hawa elites wetu ni wajinga tu. Tena ni wajinga na wabinafsi hasa bora hata wale wengine wasio na elimu yoyote, na hawa ndio kwa kiasi kikubwa wanarudisha nyuma harakati za kuikomboa hii nchi.

Hawa ukiwatazama kwa makini utaona nao wanasubiri tu wapate nafasi serikalini nao wageuke waitwe mafisadi, wengi wao hawana nia yoyote ya dhati kuunganisha nguvu zao ili kujikomboa.

Tazama tatizo la ukosefu wa ajira linavyowatafuna kwa mfano, lakini wapo kimya tu, kila mmoja wao anachungulia nafasi yake akapate pakujibanza awaache wenzie mtaani, matokeo yake wote wanaendelea kusota mitaani!.
 
Umenena vizuri kabisa.

Katiba siyo ya Rais, Rais ni zao la katiba. Mzaliwa hawezi kujizaa.

Mapendekezo yangu hayatofautiani nawe kimsimamo. Jambo amblo lingefanyika, kwanza ingekuwa ni kuzitambua taasisi za umma, za Serikali, asasi za kirai, asasi za kidini, vyama vya siasa, taasisi za kielimu, makundi mbalimbali yaliyo rasmi na yasiyo rasmi.

Hawa wote wapewe nafasi ya kuwateua wawakilishi wao.

Timu ya majaji iandae hadidu za rejea za Tume ya katiba.

Wawakilishi wa makundi yote wakutane kupitia hadidu za rejea na kuzipitisha.

Wawakilishi wa makundi yote wapendekeze majina matatu kwa kila nafasi kwenye kamati ya katiba. Majina hayo yaliyopendekezwa kutika kwenye orodha ya watu wenye sifa kama zitakavyokuwa zimeanishwa, na yakawa yamepiguwa kura na wawakikishi wa makundi yote, yapelekwe kwa Rais ambaye atachukua jina mojawapo kutoka kwa waliopendekezwa, na kulitangaza kwa nafasi husika, kisha wajumbe hao waapishwe na jaji mkuu kuwa wajumbe wa kamati ya katiba.

Kamati ya katiba ipitie mapendekezo ya kamati ya katiba ya jaji Warioba, kisha kufanyia marekebisho maeneo ambayo itaonekana kuna haja. Kisha waandae version ya mwisho ya katiba pendekezwa ambayo itapigiwa kura na wajumbe wawakilishi wa makundi yote.

Baada ya hapo, kazi.iwe imekwisha. Sioni umuhimu wa kuandaa uchaguzi wa wananchi wote kuipigia kura katiba. Jambo la muhimu ni uwakilishi wa wananchi kupitia makundi mbalimbali uwe mpana sana.
Mbona tena hapo kwenye mapendekezo ya majina matatu yapelekwe kwa Rais, naona tena umerudisha mamlaka ya hii issue kwa Rais, tofauti na msimamo wako wa mwanzo uliposema Rais ni zao la Katiba hivyo mzaliwa hawezi kujizaa?

Hivi tunataka kukubaliana kwamba Rais akiwa kama mwenyekiti wa chama cha siasa, ambaye kimsingi anatakiwa awe na nguvu sawa na wenyeviti wa vyama vingine, hawezi kabisa kuachwa pembeni kwenye hili?

Basi kama ni hivyo, napendekeza Rais ashirikishwe kwenye huu mchakato kwa namna ambayo atakuwa na kofia ya uenyekiti wa chama chake, sawa na wenyeviti wengine kwa nafasi itakayowahitaji kutoa maoni yao, lakini asiwe kama Rais ambapo anaweza kuingilia utendaji aa tume kwa namna moja au nyingine.
 
Naona huu mchakato wa kuipata Katiba Mpya bado hatujawa serious nao, kinachofanyika mpaka sasa ni muemdelezo wa makosa yale yale yaliyotukwamisha wakati ule wa JK.

Kuna makosa mengi sana ambayo nashindwa kuelewa kwanini yanajirudia, kosa moja kubwa kuliko yote ni kumuacha Rais ambaye nae ni mwenyekiti wa chama cha siasa, awe ndie kiongozi. Hapa tayari tumeshaanza kwa kukosea.

Na kuonesha vile tunaendelea kukosea kwenye hili jambo, ni pale ambapo baadhi yetu tunarudi kumtaka Rais huyo huyo amuondoe Mutungi tusiyemtaka kwa sababu ya rekodi yake, amuweke mwingine tutakayeridhika naye.

Hata kama hilo likifanyika, bado tutaendelea kucheza humo humo ndani ya kisima cha makosa, ambapo huyo mpya atakayeteuliwa na Rais, bado kuna uwezekano mkubwa akaenda kufanya kazi ya kumfurahisha bosi wake, kwa maslahi ya chama chao, matokeo yake tutaanza tena kupiga kelele na kuendelea kujichelewesha wenyewe.

Kwa maoni yangu, hapa kinachotakiwa kufanyika ili tuipate Katiba Mpya bora, kwanza na muhimu kabisa, Rais anatakiwa kuwekwa pembeni kwenye huu mchakato, atafutwe kiongozi/ au iundwe taasisi nyingine huru isiyo na upande wowote, isimamie huu mchakato.

Taasisi husika iachwe huru kufanya kazi zake bila vitisho vyovyote [ bunge litunge sheria ya kuiunda, na kuwalinda watendaji wake mpaka mwisho wa majukumu yao], lakini kinyume na hapo, tutaendelea kudanganyana tu.
Bunge gani? La Tulia au?
 
Back
Top Bottom