Mch. Rwakatare avunjiwa nyumba

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,143
Rungu la Sheria limetua kwa Mch.Gertrude Rwakatare,Mchungaji Kiongozi wa 'Mlima wa Moto'.Ni nyumba yake iliyokuwa Mbezi Beach. Alijenga katika eneo la mjane alilolivamia. Hatimaye sheria imechukua mkondo wake. Mjane alilia kwa furaha. Nyumba hiyo ilisajiliwa kwa jina la mtoto wa Mch.Rwakatare. Uboboaji huo ulifanywa chini ya ulinzi mkali wa askari waliokuwa wamesheheni silaha za moto.

Wakati wa ubomoaji,alijitokeza mtu mmoja aliyedai kuwa ni Wakili wa mwenye nyumba akiwa na nyaraka za kimahakama zinazodaiwa kuweka zuio la kubobolewa kwa nyumba hiyo.Hatahivyo,alipuuzwa na ubomoaji kuendelea kama ulivyopangwa. Kweli sheria ni msumeno!

Chanzo: ITV


CHANZO: Mwananchi
 
kwa mujibu wa ufuo Saro nyumba ni za mbunge viti maalumu Mama Rwakatare ila kaandika majina ya mtoto wake.
 
Mbona hatukuelewi,andika vizuri basi
 
ikiwa hivyo basi haki imetendeka....
 
Hongera sana serikali yangu. Mkosaji ni mkosaji tu. haijalishi hadhi yake
 
Nyumba nne eneo la mbezi beach ikiwamo no. 314 zilizopo ufukweni mwa bahari ya hindi zimebomolewa leo na serikali

Kwa mujibu wa Eng.wa manispaa ya kinondoni kila nyumba ina thamani ya million 30.siku nyingine uwe mchunguzi ili kuitetea serikali.Serikali hii hii inadai kupitia NHC inajenga nyumba za bei nafuu na kupitia habari iliyowekwa hapa JF nyumba ya bei ya chini Ni million 40.huo ufahari unautoa wapi mkuu
 
Hatimaye.......maana hili sakata nililisikia muda mrefu sana mama akawa anatumia njia anazojua yeye kuzima hii issue, hongera Tibaijuka hongera Mdee maana najua lazima kuna nguvu zako mpaka hilo zoezi limefanikiwa.
 
Hapa ndipo ninapoipendea serikali yetu, haijali cheo, hadhi wa fedha za mtu linapokuja suala la kufuata sheria!
 
Nyumba nne eneo la mbezi beach ikiwamo no. 314 zilizopo ufukweni mwa bahari ya hindi zimebomolewa leo na serikali
.....mbona umemumunya maneno????..ungesema tu ni nyumba zinazohusishwa na lile limama Lwakatare.....ambaye tayari anahusishwa na dhuluma na ufisadi....pasipokusahau biashara haramu ya watoto....Alafu anajiita mchungaji......Unafiki wa wanasiasa wetu huu..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…