jogi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2010
- 25,558
- 25,323
Vijana wa CCM waliovalia kombati za chadema kuanzia wiki iliyopita wamekuwa wakipita na kugawa fedha kiasi cha shilingi 30,000 hadi 50,000 kwa vijana wenye pikipiki katika maeneo ya usa, tengeru na maji ya chai. Mpango huo wa kufitinisha ambao unaratibiwa na Mwigulu Nchemba inasemekana wamekuwa wakiwapa fedha hizo vijana wachache na hivyo kutia hasira kwa vijana wengine kuwa fedha zinatolewa kwa upendeleo na matokeo yake wenye pikipiki wengi wameanza kugoma kujitolea kama ilivyokuwa hapo awali.
Katika hila hiyo, ametajwa mhe msigwa kuwa ndiye mwenye fedha na kuwa vijana wote wenye bodaboda waende kumuona awapatie fedha jambo ambalo lilizua tafrani kubwa.
Sambamba na hilo, CCM wamekuwa wakitumia ujanja mwingine wa kutumia bendera ya chadema kufunga kwenye magari yao ili kuwavuta watu na kisha watu wakikusanyika ndio wanapojivua gamba na kusema wao ni CCM na hizo bendera wanaonyesha kuwa watu wamerudi CCM, kitu ambacho kilitafsiriwa na wenyeji wa meru kuwa ni mbinu ya kijinga.
Ukiwasikia ccm wanasema "Tutapambana" huwa wamemaanisha kurubuni, kudanganya, kupora, kutisha, kukwiba,. . . . . . . . . .
wanapambana kwani wao ndio wanapiga kura? mpiga kura ndiye hupambana kumpata mwakilishi wake!!!! this time watu wanajitambua na watawaonyesha nini maana ya kupambana.